Nsikuchoshe na Usinchoshe,tusichoshane!
Ukiona viongozi wa Serikali wana wang'ang'ania wazee kwenye nafasi nyeti tambua ya kwamba vijana watakuwa na matatizo ya kiakili,Vijana wengi waliopewa nafasi ili waonyeshe uwezo wao wamekuwa wapumbavu kuliko hata wazee waliochokaa!.
Hili Taifa la Tanzania ndilo Taifa linaloongoza duniani kwakuwa na Vijana wapumbavu kuliko Mataifa yote yanayotambulika na Umoja wa Mataifa (UN).
Hebu fikiria kijana anatoka nyumbani au kibaruani kwake kuelekea Airport (JKNIA) kumpokea msanii wa muziki wa kizazi kipya kisa kachukua tuzo huko Marekani,na kibaya zaidi huyo kijana anakimbiza gari lililombeba huyo msanii kitokea Airport hadi Kawe!.
Zaidi ya Km 22 huyu kijana anakimbiza gari kutoka JULIUS KAMBARAGE NYERERE INTERNATIONAL AIRPOT (JKNIA) hadi Kawe huku akitokwa jasho na kunuka kama mbuzi wakati huo huo huyo msanii akiwa anapigwa na AC (Air Condition)!.
Nimetafakari sana namna vijana wa nchi hii (Wengi) walivyo wapumbavu hadi nimekosa majibu!.
Hebu fikiria muda ambao huyo kijana kapoteza katika shughuli za uzalishaji mali!.
Kwanini vijana wasitumie muda kama walioutumia leo wakaandamana kuihoji serikali kuhusu ripoti ya CAG? Nilitamani kuona vijana wanahoji wezi wa mali na
wafuja rasilimali zilizotajwa kwenye ripoti ya CAG lakini hakuna anayehoji zaidi ya kushiriki kwenye mambo ya kipumbavu!.
Hili Taifa bila Vijana kubadilika sidhani kama twaweza kupiga hatua zaidi ya kila siku kuishia kuimba nyimbo za mapambio za kina
Lucas mwashambwa mama anaupiga mwingi!
Hebu fikiria jitu lililokuwa linapewa heshima hapa jf kama liokota makopo maarufu la JF
Chizi Maarifa nalo limekuwa sehemu ya ujinga huo leo pale Airport to Kawe!
Mdeki vyoo wa pale lugalo
GENTAMYCINE yeye alishituka mapema hakwenda huko ila alimuachia mwehu mwenzie
Chizi Maarifa amuwakilishe!
Vijana wa hili Taifa wengi ni wapumbavu sana!