Hivi haya majina ya vitu vipya kwa Kiswahili nani huwa anatunga?

Hivi haya majina ya vitu vipya kwa Kiswahili nani huwa anatunga?

Kila lugha duniani ina maneno mepesi na maneno magumu (Kiswahili, Kilatini, Kigiriki, Kihadzabe, n.k).

Labda muwe na hoja nyingine, ila hii ya kutaka kiswahili kiwe na maneno yote mepesi mepesi (kwa kutohoa toka lugha zingine) mimi sioni kama lina mashiko.

Na ukipenda sana vitu laini laini, tepetepe au ndembendembe, utaanza kuamini hata neno "MFUNGWA" ni gumu mno, utapendekeza watu waliohukumiwa kutumikia adhabu gerezani waitwe "PRIZONA."

Sio sawa.

Kishkwambi daima, Kishkwambi milele.
Sawa 🙏
Aya chukua sharubati glass mbili ntakuja kulipia 🙂
 
Ni kama wanafanya makusudi
Mpwiloka
IMG-20220629-WA0004~2.jpeg
 
Computer keyboard- kicharazio
Memory card- kadi sakima
Toothpick- kichokonoo
Covid 19- uviko- 19( kumi na Tisa)
Spy- shushushu

Mie Ni mkenya wakuu,je mwalimu wangu wa kiswahili alipatia ama alichemka?
 
Nini tasfiri ya neno" serious" kwa kiswahili? Watz naomba mnijuze tafadhali
Hilo neno halina tafsiri moja, ila itategemea limetumikaje katika sentensi.
Maelezo:
1. Serious = Hasa/Haswa.
Mfano: Serious problem = Tatizo hasa.

2. Serious = Maanisha
Are you serious? = Je, unamaanisha?
 
Hilo neno halina tafsiri moja, ila itategemea limetumikaje katika sentensi.
Maelezo:
1. Serious = Hasa/Haswa.
Mfano: Serious problem = Tatizo hasa.

2. Serious = Maanisha
Are you serious? = Je, unamaanisha?
Nimekuelewa Sana mkuu
 
Wawe wanashirikisha wadau bana.

Na hata kama hawashirikishi wengine watunge basi majina ama maneno mazuri. Sasa kama hili kishkwambi Yani unaltamka huku umekunja uso. Angalau wangeita tu tableti.

Mengine yanayokera jokofu wangeacha tu friji. Smart phone Eti simu janja. Eti password nywila unabaki kushangaa WTF?! Angalau wangeita tu paswedi.

Nahisi ni wakenya Hawa kwasababu juice eti kinywaji tamu unabaki kukasirika tu afadhali bongo tumekomaa na juisi. Shirikisheni wadau mnapotunga nakuita vitu kwa majina ya ajabu ajabu.

Sijui drones wanaziitaje?
Uundaji wa maneno hukuza lugha na zipo njia 8 za uundaji wa maneno mampya ikiwe hii uliyoipendekeza ya kutohosha... ingawa ni njia dhahifu haizingatii mabadiliko ya isitalahi, pia hudumaza ubunifu wa uundaji wa misamiati mipya ...kama we muuandishi umedumaa na unaona usumbufu kuunda misamiati kwa njia ya unyumbuaji na fasiri ya maana na uunganishaji wa maneno....
Neno.. mfano wa maneno tuliyo tohoa... redio, data, programu, eroplaini, dukani, ikulu nk... ukitohoa kazi inakuwa ni kusanifisha muundo wa lugha kisha neno hutumika.
 
Kishkwambi neno limekaa, ki udaku ki kiherehere ki kimbele mbele.

Ni zuri kwa kwel limeendana na siye Watz
 
Back
Top Bottom