Hivi inakuwaje mtu anajua kusoma Quran ila lugha ya kiarabu haijui?

Hivi inakuwaje mtu anajua kusoma Quran ila lugha ya kiarabu haijui?

The Arabic Language (Its Amazing History and Features)


This video is all about the Arabic language, from its early origins on the Arabian peninsula, to its current status as the 5th most spoken language on Earth. I also examine a number of features of Arabic
Source : Langfocus

That guy is FIRE! I have known him for quite sometime
 
Lugha ina siri nyingi, ni Tanzania tu ambapo magazeti hayatumii KiSwahili sanifu.

Gazeti la Taifa Leo la Kenya linaweza kutumiwa na mgeni anayejifunza lugha ya kiSwahili lakini magazeti pendwa ya Tanzania kiswahili chake ni cha "mtaa fulani mdogo'.

Lugha ya Kiarabu sanifu classical Arabic hufundishwa mashuleni na kutumiwa katika magazeti makubwa, riwaya na pia ndicho kinachotumiwa ktk kufundishia ktk madrasa.

Tatizo sisi waTanzania hatuheshimu lugha ya kiSwahili, huwezi kutofautisha nani ni mwanzuoni yaani msomi wakati watanzania wakioongea.

Lakini watu wa jamii nyingine wanaotumia lugha kama za Kiarabu au Kingereza ukisikia mtu anaongea unaweza kwa haraka kutambua kuwa mtu huyu ni msomi au kakulia katika mazingira ambayo watu wanauelewa mpana wa lugha ya Kiarabu classical au Kiingereza classical.

Media za Tanzania zinatakiwa kuwa mbele kwa kuchapisha magazeti kwa lugha sanifu haijalishi ukubwa au udogo wa gazeti, kituo cha radio au kituo cha televisheni.

Ndiyo maana hapa jamiiforums tunaona tunasahihisha kuhusu matumizi ya herufi mfano H katika maneno kama atakuja au hatakuja maneno haya mawili ya kiSwahili yana maana tofauti, lakini media zetu utakuta watangazaji au waandishi wa katika media kubwa hata kutamka au kuandika kwa usahihi tunashindwa.
waKenya, waTanzania, waIngereza, mwIngereza, mBongo, mSwahili 🙂 🙂 🙂

Huu uandishi ni sheeeeidaa
 
Naomba kueleweshwa, binafsi huwa naona Quran ni maandishi ya kiarabu.

Sasa kuna maustadhi kama wanne hivi kwa nyakati tofauti nimewahi kuwapa gazeti lenye maandishi ya kiarabu wanisomee na kunitafsiria ila cha ajabu wameshindwa.

Je kuna tofauti ya lugha iliyotumika kuandika Quran na lugha ya kiarabu cha kawaida?
Quaran haisomwi.

Wanakariri maneno kama yalivyo.
 
So lugha iliyotumika kwenye kuandika Quran ni tofauti na kiarabu chenyewe?
Kuna tofauti lugha inaongelewa ni tofauti kwa maana ina maneno asilimia labda 90 huko hayako kwenye quraan kwa maana hayatumiki katika kuongea kila siku kumbuka ila ukijuwa kiarabu utaelewa ni kama biblia lugha iliyoko ndani unaweza kusoma na usielewe au msamiati wa bible huwezi kukuta mtu anaongea huku mitaani utaonekana hujui lugha. Kwa ufupi kujuwa kusoma quraan haina maana unajuwa kuongea lugha ya kiarabu ndio maana katika vyuo vya dini unasoma somo la quraan na unasoma somo la lugha ni vitu viwili tofauti.
 
Naomba kueleweshwa, binafsi huwa naona Quran ni maandishi ya kiarabu.

Sasa kuna maustadhi kama wanne hivi kwa nyakati tofauti nimewahi kuwapa gazeti lenye maandishi ya kiarabu wanisomee na kunitafsiria ila cha ajabu wameshindwa.

Je kuna tofauti ya lugha iliyotumika kuandika Quran na lugha ya kiarabu cha kawaida?
Ni hivi,
Kule kwenye vitabu vya dini kuna aya (tuite sentensi) ambazo ni muunganiko wa maneno mbalimbali. Sasa maneno haya ni ya kiarabu na ukiyaunga unapata sentensi/aya/verse kuhusu jambo fulani.

Lakini maneno haya yakiunganishwa na maneno mengine ambayo msomaji wa Quraan hakujifunza yataleta maana ingine ambayo msomaji anaweza asiielewe.

Mfano mtu anaweza kujifunza kwenye Quraan tafsiri ya aya iliyoandikwa kwa kiarabu inayosema "Alipofika kwenye SOKO alihubiri dini". Mtu huyo ukimpa gazeti la kiarabu linalosema "SOKO linaungua" hatoelewa tafsiri yake sababu neno KUUNGUA haliko kwenye Quraan so hajawahi kujifunza tafsiri yake.
 
Arabic ya kwenye qur'an ni old, pia haibadiliki miaka yote ni hiyo na ofcourse mlemle t kuna maneno ni kuntu kam huyo sheikh hajafanya mapitio hawez kukupa tafsiri. Lakin tuje kwen hoja yako ya gazeti...kwen lugha ya kiarabu kuna kitu kinaitwa shakli ..hizi shakli zinakazi ya kumuongoza msomaji namna ya kutamka maneno..sasa misahaf mingi inayosomwa imeandikwa kwa izo shakli..ni vialama tu ambavyo kwen lugha yetu ni kama vile irabu kasoro (o na e) sasa magazeti hayana izi alama muongozo kwaio kama shee wako aliishia njiani hataweza kusoma gazeti la mwarabu...pili lugha inayotumiwa kwen qur an ni tofauti na ya gazeti kulingana na nyakati,na maendleo ya teknolojia....na hapo kwen gazeti unaweza kuokoteza ukitaka shee wako aliekataa shule akukimbie nenda chukua manual guide ya kiarabu af mwambie asome uone...hahah
 
Mbona ni swali jepesi sana,
Lugha ya Kiarabu iliyotumika kwenye Qur'an ni ile original yaani ya kizamani (kumbuka Qur'an haija chakachukuliwa kama vitabu vyengine) ndio maana unaweza kupata mzungumza Kiarabu asiweze kusoma Lugha iliyopo kwenye Qur'an kutokana na Kiarabu cha sasa kimelainishwa,

Hao Maustaadh walioshindwa kusoma lugha ya gazetini ni vice versa na hicho hapo juu,

Ukisoma historia ya Lugha zote Duniani utaelewa hayo, kadri ya kizazi na kizazi Lugha inaenda inabadilishwa,

Kiswahili hiki hiki tunachokiongea sie sio kiswahili sanifu na ukiwekewa kiswahili kile original huwezi kuelewa mwishowe udhanie ni Kimakonde kumbe ni Kiswahili kilicho Sanifu.
 
Ni hivi,
Kule kwenye vitabu vya dini kuna aya (tuite sentensi) ambazo ni muunganiko wa maneno mbalimbali. Sasa maneno haya ni ya kiarabu na ukiyaunga unapata sentensi/aya/verse kuhusu jambo fulani.

Lakini maneno haya yakiunganishwa na maneno mengine ambayo msomaji wa Quraan hakujifunza yataleta maana ingine ambayo msomaji anaweza asiielewe.

Mfano mtu anaweza kujifunza kwenye Quraan tafsiri ya aya iliyoandikwa kwa kiarabu inayosema "Alipofika kwenye SOKO alihubiri dini". Mtu huyo ukimpa gazeti la kiarabu linalosema "SOKO linaungua" hatoelewa tafsiri yake sababu neno KUUNGUA haliko kwenye Quraan so hajawahi kujifunza tafsiri yake.
Kweli kabisa najivunia Mimi siyo muislamu sijawahi na sitawahi Yani hiki kitu namshukuru Mungu wa kweli.

Yesu ni Mungu


STRUGGLE MAN Mlolongo
 
Ni hivi,
Kule kwenye vitabu vya dini kuna aya (tuite sentensi) ambazo ni muunganiko wa maneno mbalimbali. Sasa maneno haya ni ya kiarabu na ukiyaunga unapata sentensi/aya/verse kuhusu jambo fulani.

Lakini maneno haya yakiunganishwa na maneno mengine ambayo msomaji wa Quraan hakujifunza yataleta maana ingine ambayo msomaji anaweza asiielewe.

Mfano mtu anaweza kujifunza kwenye Quraan tafsiri ya aya iliyoandikwa kwa kiarabu inayosema "Alipofika kwenye SOKO alihubiri dini". Mtu huyo ukimpa gazeti la kiarabu linalosema "SOKO linaungua" hatoelewa tafsiri yake sababu neno KUUNGUA haliko kwenye Quraan so hajawahi kujifunza tafsiri yake
with all that being true yawezekana usieleweke pia..watoto wengi wanapokuwa wanajifunza hiki kitabu huwa wanameza kama kilivyo bila kuelewa maana yake..sasa mtoto wa namna hii ukija kumpa gazeti lazma ajambe...madrasa zote kuna somo la qur an na somo la kiarabu..,ukilielewa vema somo la kiarabu kama mimi hahaha utaweza kutafsir qur an bila shida the same to gazeti ingawaje utapata changamoto ya vocabularies
 
Naomba kueleweshwa, binafsi huwa naona Quran ni maandishi ya kiarabu.

Sasa kuna maustadhi kama wanne hivi kwa nyakati tofauti nimewahi kuwapa gazeti lenye maandishi ya kiarabu wanisomee na kunitafsiria ila cha ajabu wameshindwa.

Je kuna tofauti ya lugha iliyotumika kuandika Quran na lugha ya kiarabu cha kawaida?
Mkuu kunantofauti kubwa kati ya lugha ya kiarabu na Quran:
1.lugha ya kiarabu haina alama zinazotumika kwwnye kusoma
2.ili uweze kujua kiarabu lazima ukasomee lugha ya kiarabu
3.lakini QUran ukifundishwa hata na mzazi wako unajua .
 
Naomba kueleweshwa, binafsi huwa naona Quran ni maandishi ya kiarabu.

Sasa kuna maustadhi kama wanne hivi kwa nyakati tofauti nimewahi kuwapa gazeti lenye maandishi ya kiarabu wanisomee na kunitafsiria ila cha ajabu wameshindwa.

Je kuna tofauti ya lugha iliyotumika kuandika Quran na lugha ya kiarabu cha kawaida?
Hata mi nimesoma shule ya kiislam nikiwa mkristu.Niliwauliza rana lakini hawakuwahi kunipa majibu yakueleweka.
 
Naomba kueleweshwa, binafsi huwa naona Quran ni maandishi ya kiarabu.

Sasa kuna maustadhi kama wanne hivi kwa nyakati tofauti nimewahi kuwapa gazeti lenye maandishi ya kiarabu wanisomee na kunitafsiria ila cha ajabu wameshindwa.

Je kuna tofauti ya lugha iliyotumika kuandika Quran na lugha ya kiarabu cha kawaida?
Ile lugha ya Majini kiarabu ni lugha ya kabila ila likitamkwa jina la Yesu yanaogopa na kukimbia yaani yaja Yesu Kristo kwa lugha yeyote lazima majini ya kwenye quran yake kona
 
Back
Top Bottom