Hivi inakuwaje mzazi anakua tegemezi Kwa mtoto ambaye amejitafuta Kwa jasho lake bila kumrithisha hata mbuzi mmoja

Hivi inakuwaje mzazi anakua tegemezi Kwa mtoto ambaye amejitafuta Kwa jasho lake bila kumrithisha hata mbuzi mmoja

Kwa maana hiyo unataka kusema ww ukiwa mzazi ; mtoto akililia wembe utampa? Mtoto wako anayetambaa akiufuata moto utamwacha afanye kama atakavyo? Unatakiwa ujifunze kufanya maamuzi kwa mambo makubwa kutokana na uzoefu unaopatikana katika mambo madogo. Kwa akili ya kawaida huwezi kuridhia kumpa mtoto m5 hata kama unajua ni haki yake huku ukijua fika kwamba kwa hizo m5 ndo umempa mwanao Umauti kwa mikono yako mwenyewe wewe mzazi. Asikudanganye mtu. Huo sio upendo.
Kwahiyo ukimnyima hiyo pesa ndio hatokufa
 
Fanya lile unaloliweza kumsaidia mzazi wako! Lile usiloliweza liache.
Kwa mfano usiache kutunza familia yako kwa sababu ya Wazazi wako.
Kama bado wana nguvu wafanye lile wanaoliweza kujikimu na maisha.
Maandiko yanasema,Mtu atamwacha Baba na Mama naye ataambatana na mkewe,na si wawili tena bali ni Mwili mmoja,Mwanzo2:21-24
Lakini,
(Kutoka20:12)-Waheshimu baba yako na mama; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.
Amri ya Nne ya Mungu: Waheshimu baba yako na mama yako upate miaka mingi na heri duniani (Biblia; Kutoka 20: 12; Katekisimu jimbo Katoliki Moshi)
Ni kweli haijaandikwa "Uwatunze wazazi ......... ......" Lakini katika Kuwaheshimu wazazi utajikuta kwa Ufahamu wako, Busara na Akili zako na pia katika Nafsi yako; hutaridhika kuwaacha wazazi wako Wadhalilike kutokana na kupungukiwa. Lazima nafsi yako ikuume kama vile unapomwona mtu anampiga mama yako mzazi tena hadharani. Utachukua hatua.
 
Huna akili watoto wako wamekula hasara
Kivipi mkuu? Yan ninamwepushia balaa, madhila na umauti mwanangu halafu ww unaniambia eti nimekula hasara? Dah! Kazaae wakwako halafu ifike mahali wakudai urithi wao ilhali ww ukingali hai then uwape kwa sababu una akili.
 
Kivipi mkuu? Yan ninamwepushia balaa, madhila na umauti mwanangu halafu ww unaniambia eti nimekula hasara? Dah! Kazaae wakwako halafu ifike mahali wakudai urithi wao ilhali ww ukingali hai then uwape kwa sababu una akili.
Sio nikazae ninao na nawapa uhuru wote ikiwemo pesa hizo akili za mtu mweusi Mimi sina
 
Sio nikazae ninao na nawapa uhuru wote ikiwemo pesa
Kuwapa uhuru na pesa huo ni msaada kama inavyotakiwa mzazi afanye kuwatunza watoto wake. Nimezungumzia mwanao kukudai Urithi wakati ww upo hai.
 
Mimi sio muumini mzuri wa kutoa sadaka kanisani ,lakin kila nikipata huwa nawapa wazaz wang kama sadaka na haipiti mwezi bila kupata dili lingine.
 
Usingekuwepo duniani fikiria furaha zote zile ambazo unazo bila kuzaliwa usingezipata.
Dah! Nasi hapa Jf tungelikosa michango yake iliyotukuka ya ushiriki wake kama asingelizaliwa. Anatakiwa awashukuru waliomzaa kwani ni kwa kuzaliwa kwake tumenufaika naye.
 
Kuna furaha gani Tanzania mkuu?? Dhiki kila mahali, CCM inazidi kuitafuna nchi wanakula na kisaza wao na watoto wao ilhali Mlalahoi anakula mara 2 tena kwa tabu sana..
Usikwazike wala kukereheka mno kupita kiasi kwani hayo ni ya muda tu - yatapita.
 
Kuna furaha gani Tanzania mkuu?? Dhiki kila mahali, CCM inazidi kuitafuna nchi wanakula na kusaza wao na watoto wao ilhali Mlalahoi anakula mara 2 tena kwa tabu sana..
Changamoto ndio maisha ya binadamu aliye hai it mean kama hauna changamoto you are dead.ndio maana umepewa utashi(akili),hekima ya kuyatatua hayo.
 
Back
Top Bottom