Hivi kuna perfume ya kiume yenye kunukia vizuri kuliko hii?

Nadhani kilichokuwa kinataka kukuliza ni laki 8. 😂 Ungemwambia hiyo huwa inanikataa, huwa natoka vibarango, naomba tu hiyo hela ninunue huku. Laki nane inaendaje na upepo kirahisi hivo!? 😂
Yaani kujipulizia perfume ya laki naneba huku unadaiwa ada ya ntoto,kodi imeisha,ndani hakuna unga wala mchele lazima ulie
 
Inapunguza nguvu za kiume na kufanya uume ulegee kuwa makini nayo
 
Ila nayo bei mmhh.
Mie nnacho cha mls 30 nimeletewa. Nmeuliza bei dukani 110,000
Tafuta fake mkuu, usijitese.

Mimi nilikua mdau mkubwa sana wa perfume OG. Nilikuaga naagiza mwenyewe nje kupitia ebay ma Creed Aventus, Lacoste, Armani Code, 1 million etc hata mke wangu nilikua namuagizia ma Issey Miyake, JPG nk. Siku moja perfume niliyokua natumia ikawa imeisha na sijaagiza nyingine, nikapita sehemu nikachukua fake 35k.

Kesho yake nimeingia ofisini kila mtu ananiuliza aisee perfume gani hiyo inanukia vizuri ivyo.. mademu wanaulizia niwaagizie niliponunua wakawachukulie waume zao! Wakati ile OG hamna mtu ata amewahi kuniuliza. 😄

Huo ndio ukawa mwisho wa OG saiz ni mwendo wa fekero tu
 
Mbonamwandiko buu haufanani na perfume ya 345,000?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…