Hivi Rais Samia amewahi kuandika Makala au Paper ya utatuzi wa changamoto za jamii?

Hivi Rais Samia amewahi kuandika Makala au Paper ya utatuzi wa changamoto za jamii?

Nyerere hakufilisi uchumi wa nchi. Nyerere alianzisha mashirika na viwanda vingi tu lakini hakujua watanzania ni wezi na wavivu wa kutupwa. Enzi za Nyerere watu waliokuwa wanasoma bure. Hospital bure. Kulikuwa mpaka na kupewa warrant wa kusafiri kwa wanafunzi na watu wengine kama wanamuziki. Kwa kifupi watu wa kawaida ndiyo walikuwa wana-enjoy keki ya Taifa. Hebu nionyeshe katika hizi nchi za sub-Sahara African countries ni nchi ipi wananchi wake walikuwa wanaishi vizuri kama Tanzania kipindi cha Nyerere! Nyerere mpaka raslimali aliziacha kwa matumizi ya baadae. Sasa hizi wanashindana kuzipiga bei.
Alipaswa kujua watanzania ni wavivu kabla ya kutaifisha mashirika na viwanda binafsi na kuvifanya vya serikali, matokeo yake vikawa, vinajiendesha kwa hasara hadi kujifia

Serikali kutoa vitu bure sio ujanja, serikali sio baba au mama yako, serikali inatakiwa kuweka miundombinu sahihi na sera sahihi kwa ajili ya wananchi kuzalisha na kipato na kujilipia huduma wenyewe, nchi zilizoendelea ndio zilifanya hivyo, ujamaa ni kulea uvivu
Kipindi cha Nyerere ndio kipindi wananchi waliishi maisha magumu kuliko vipindi vyote, kwa mgao wa bidhaa, udikteta, njaa
 
Magufuli alifoji elimu ndiyo maana wakamuua Ben Saanane. Vinginevyo, duniani hakuna msomi wa kweli atakayekasirika kwa mtu kuhoji elimu yake. Yaani eti sasa hivi uanze kumshambulia Pro. Shivji kwa kuhoji uprofesa wake halafu akasirike? Kwanza wewe unayehoji utaonekana ni mwehu!
Nakubaliana na ujumbe wako kuanzia hapo kwenye 'vinginevyo' upo sahihi kabisa.

Hapo kwenye sentensi ya kwanza, Mungu naomba anipe uwezo wa kunyamaza, kuna vitu vinauma sana!
 
Nakubaliana na ujumbe wako kuanzia hapo kwenye 'vinginevyo' upo sahihi kabisa.

Hapo kwenye sentensi ya kwanza, Mungu naomba anipe uwezo wa kunyamaza, kuna vitu vinauma sana!
Huo ndio ukweli mchungu
 
😅😅😅Tuache sie na mwanamke Rais wetu

Kazi iendeleee...
 
Nimelazimika kuuliza hii kitu, ni muhimu sana kujua. Makala nzito iliyojaa critical analysis na ikapatikana kwenye national au International journals. Paper fulani hivi ya kuzungumzia changamoto mtambuka za jamii yetu ya Kitanzania.

Mambo haya yanaakisi sana uwezo wa mtu. Nafikiri ana Degree na Masters, ziko wapo Research reports zake tuzifanyie Literature Review.

Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi chungu mzima. Lakini hatuoni hatuoni hata moja ikipatiwa majibu ya utatuzi. Nchi ni kama mgonjwa anayesubiri muujiza wa Baba wa Mbinguni tu.
Kaka huo ubongo Hana. Ni mwepesi kichwani. Watanzania mkataeni kwa nguvu zote 2025 kama atajileta kwa faida ya kesho ya taifa letu.
 
..Nchi ilifilisika wakati wa awamu ya kwanza.

..baadhi ya matatizo yalisababishwa na sera za kijamaa alizoziamini Mwalimu Nyerere.

..kibaya zaidi Mwalimu alikataa ushauri wa kuchukua hatua za kurekebisha uchumi mapema.

..nashauri msome vitabu vilivyoandikwa na Edwin Mtei, na Andy Chande, mtapata picha ya nini ilisababisha uchumi wetu kuanguka miaka ya 1980.

..Kwenye kitabu cha Andy Chande anaelezea jinsi Mwalimu alivyotaifisha mali za kina Chande na kuanzisha shirika la National Milling.

..tatizo ni kwamba waliopewa kuendesha hizo mali za kina Chande / National Milling hawakuwa na uzoefu wa uendeshaji wa biashara hiyo.

..Matokeo yake shirika la umma kukawa likiendeshwa kwa hasara. Serikali ya Mwalimu iliendelea kutupa fedha ktk mashirika mengi ya aina hiyo.

..Mwalimu pia alitaifisha mashamba ya mkonge. Mkonge ilikuwa moja ya mazao yanayoingiza fedha nyingi za kigeni. Matokeo ya hatua za utaifishaji za Mwalimu Nyerere ni kuanguka kwa sekta ya mkonge.

..kulikuwa na harakati nyingi za kuyasimamisha mashirika yaliyokuwa yametaifishwa, pamoja na kuanzisha mengine mengi mapya ambayo hayakuweza kusimama yenyewe.

..Mwalimu alishauriwa atafute wabia kwa mashirika na makampuni yaliyokuwa wakifanya vibaya, lakini ushauri huo haukutekelezwa.

..Watanzania waliokuwa wakitoa ushauri, au kuunga mkono mabadiliko ya sera za uchumi waliitwa WASALITI / VIBARAKA ndani ya Ccm, na walishindwa ktk chaguzi za ndani ya chama.

..Mfumo wa uendeshaji uchumi wa Mwalimu uliwakera nchi wafadhili na taasisi zilizokuwa zikitukopesha. Matokeo yake ni wafadhili na wakopeshaji kugoma kutupa fedha mpaka pale tutakapobadili sera zetu za uchumi.

..Hali hiyo ndio chanzo cha mgogoro kati ya Mwalimu Nyerere na taasisi za fedha kama IMF na WB. Mwisho wa yote Mwalimu aliamua kung'atuka na kupisha wengine wake waendesha nchi.

..Tofauti ya Mwalimu Nyerere na waliomfuatia ni kwamba yeye hakuna au hakunufaiki ktk lindi la matatizo ya kiuchumi tuliyokuwa tukikabiliana nayo. Mwalimu aliachia madaraka akiwa hana hata pensheni ya Uraisi.
Mimi bado nitaendelea kusimamia hoja zangu. Nakubali ni kweli alifanya makosa ila ni makosa yaliyotokana na mtu kufanya mambo kwa nia njema kabisa. Baada yake, marais wote waliofuatia wamekuwa wanafanya mambo kibinafsi zaidi. BTW kuna nchi gani Afrika, kusini ya jangwa la Sahara ambayo rais wake anaweza kupigiwa mfano kuwa alifanya vizuri kuliko Tanzania? Labda Botswana kwa mbali. Baada ya kubahatika kutoka na ku-experince nchi za Scandinavia nitaendelea kusema kosa kubwa la mwalim ni kuwaamini watanzania. Hizo nchi nimekuta mashirika na kampuni nyingi tu zinaendeshwa na serikali na zinafanya vizuri. Tofauti ni kwamba wananchi wa kule ni wachapakazi wa waaminifu sana.
 
Mimi bado nitaendelea kusimamia hoja zangu. Nakubali ni kweli alifanya makosa ila ni makosa yaliyotokana na mtu kufanya mambo kwa nia njema kabisa. Baada yake, marais wote waliofuatia wamekuwa wanafanya mambo kibinafsi zaidi. BTW kuna nchi gani Afrika, kusini ya jangwa la Sahara ambayo rais wake anaweza kupigiwa mfano kuwa alifanya vizuri kuliko Tanzania? Labda Botswana kwa mbali. Baada ya kubahatika kutoka na ku-experince nchi za Scandinavia nitaendelea kusema kosa kubwa la mwalim ni kuwaamini watanzania. Hizo nchi nimekuta mashirika na kampuni nyingi tu zinaendeshwa na serikali na zinafanya vizuri. Tofauti ni kwamba wananchi wa kule ni wachapakazi wa waaminifu sana.

..tafuta vitabu vya Edwin Mtei, na Andy Chande.

..naamini ukichanganya na uzoefu wako utapata full picture ya nini kiliangusha uchumi wetu.
 
Nimelazimika kuuliza hii kitu, ni muhimu sana kujua. Makala nzito iliyojaa critical analysis na ikapatikana kwenye national au International journals. Paper fulani hivi ya kuzungumzia changamoto mtambuka za jamii yetu ya Kitanzania.

Mambo haya yanaakisi sana uwezo wa mtu. Nafikiri ana Degree na Masters, ziko wapo Research reports zake tuzifanyie Literature Review.

Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi chungu mzima. Lakini hatuoni hatuoni hata moja ikipatiwa majibu ya utatuzi. Nchi ni kama mgonjwa anayesubiri muujiza wa Baba wa Mbinguni tu.
Aliandika kwa mkono wake mwenyewe makala ya miaka 30 ya vyama vingi vya Siasa na mtazamo wake juu ya mustakabali wa siasa za vyama vingi nchini Tanzania na lilikuwa andiko lililoshiba haswa.

Natumai siku za usoni ataandika makala nyingine
 
Nimelazimika kuuliza hii kitu, ni muhimu sana kujua. Makala nzito iliyojaa critical analysis na ikapatikana kwenye national au International journals. Paper fulani hivi ya kuzungumzia changamoto mtambuka za jamii yetu ya Kitanzania.

Mambo haya yanaakisi sana uwezo wa mtu. Nafikiri ana Degree na Masters, ziko wapo Research reports zake tuzifanyie Literature Review.

Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi chungu mzima. Lakini hatuoni hatuoni hata moja ikipatiwa majibu ya utatuzi. Nchi ni kama mgonjwa anayesubiri muujiza wa Baba wa Mbinguni tu.
Magu na jakaya waiandika nyingi sana wakifuatiwa na Mwinyi
 
Rais Samia alivyokuwa anaanza urais alikuwa idealist fulani hivi, maridhiano, demokrasia, 4R , Rule of law n.k
Baadae akaja kuona upuuzi wa siasa za Afrika, akaamua kuwa pragmatic kama Magufuli
True, na sisi pia tulimpoozea sasa ni spana za kimtindo!.
P
Siyo kwamba alipoanza tu kulewa madaraka (yaani pale tu madaraka yalipo mnogea/alipoanza tu kutukuzwa kupitiliza, na kuanza kuchukuliwa na wasaidizi wake kama mungu mtu) ndipo mambo sasa yaliponza kubadilika!!
 
Nimelazimika kuuliza hii kitu, ni muhimu sana kujua. Makala nzito iliyojaa critical analysis na ikapatikana kwenye national au International journals. Paper fulani hivi ya kuzungumzia changamoto mtambuka za jamii yetu ya Kitanzania.

Mambo haya yanaakisi sana uwezo wa mtu. Nafikiri ana Degree na Masters, ziko wapo Research reports zake tuzifanyie Literature Review.

Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi chungu mzima. Lakini hatuoni hatuoni hata moja ikipatiwa majibu ya utatuzi. Nchi ni kama mgonjwa anayesubiri muujiza wa Baba wa Mbinguni tu.
Karatasi pekee anayo itumia mara kwa mara ni toilet paper [emoji3474][emoji3474][emoji3474] tu
 
Nimelazimika kuuliza hii kitu, ni muhimu sana kujua. Makala nzito iliyojaa critical analysis na ikapatikana kwenye national au International journals. Paper fulani hivi ya kuzungumzia changamoto mtambuka za jamii yetu ya Kitanzania.

Mambo haya yanaakisi sana uwezo wa mtu. Nafikiri ana Degree na Masters, ziko wapo Research reports zake tuzifanyie Literature Review.

Tanzania inakabiliwa na changamoto nyingi chungu mzima. Lakini hatuoni hatuoni hata moja ikipatiwa majibu ya utatuzi. Nchi ni kama mgonjwa anayesubiri muujiza wa Baba wa Mbinguni tu.
Makala au pepa ndio inatatua Changamoto zako au za jamii?

Pili Kauli yake ,miongozo,maagizo ni makala tosha.

Kwa mfano Wizara ya Elimu ilikuwa na proposal ya mradi wa HEET(Mageuzi ya Elimu ya Juu) na ililenga kuongeza uwezo wa Miundombinu,utafiti,kuongeza wakufunzi nk kwenye existing universities and other higher Learning institutions.(Mkopo kutoka WB).

Samia akasema Kaeni Upya na WB Ili kwamba badala ya kurundikaaendeleo maeneo hayo hayo Kila siku tusambaze Nchi nzima ndipo Sasa WB wakakubari na Sasa Vinajengwa vyuo Vikuu na Matawi ya Vyuo Vikuu kwenye Mikoa yote ambayo haikuwa na vyuo.

Huu ni mfano mmja kati ya mambo mengi ambayo Rais ameweka interventions na yametatua Changamoto.

Umeelewa wewe nyumbu wa Chadema?
 
Paper ya nini wewe mapepa yamejaa kibao mtaani yanafungia chapati? Matatizo ya nchi hii yanafahamika na utatuzi unajulikana hakuna haja ya pepa.
 
Namna tu anavopitia mikataba kabla ya kui sign ni sawa na feitoto alivokuwa anafanya kwenye mikataba na Yanga halafu utegemee mtu wa namna hiyo aandike paper tena ya utatuzi wa changamoto, sidhani
Nanga mkono hoja yako ila raisi ni taasisi achana na mbwembwe za yule mwalimu kukariri notice
 
Magu na jakaya waiandika nyingi sana wakifuatiwa na Mwinyi

..kama Magufuli aliandika itakuwa ni ktk majarida ya wakemia wenzake.

..Magufuli hakuwahi kuandika makala yoyote akiwa kiongozi na mwanasiasa ktk masuala ya kijamii, kisiasa, na kiuchumi.

..Hata hotuba alizokuwa akitoa hazikuwa zikiwekwa ktk tovuti ya Ikulu kama alivyofanya Mkapa na Kikwete.
 
Back
Top Bottom