Hivi Tanzania kuna taasisi inayojishighurisja na haki za wanyama? Kama ipo mnijuze kabla sijafanya ukatili mbaya

Usimuue mchukue kwa gari yako nenda nae mbali kidogo mrushie nje then chomoka na faster …imeisha hiyo
 
Kwa hiyo ww ni Shoga? Unapofananyisha wenzako kama ww?
 
Umewahi kula nyama ya paka? Usiue msosi huo , mchinje ule paka rost
Unakulaje Paka,hiyo ni njaa iliyopitiliza.
Kuku,ng'ombe,nguruwe,mbuzi,samaki,kondoo vyote vipo daily.
Uanze kula hao wanyama au wadudu we utakua chizi tu.
Kwanza naweza kula wali maharage mwezi mzima au ugali mchicha au mlenda bila tabu.
Nyama kwangu sio kipaumbele
 
fulani na fulani ni paka na panya, ebu tuanzie hapo.
 
Wananusa sana hao hata sumu hawali
 
Mbwa anakula Paka'
Paka anakula Panya

SULUHISHO: Fuga Mbwa huyo Paka' atahama mwenyewe bila kupenda

Usimtie kwenye kiroba
Usimtie Rungu
Usimpige na bullet
Usimsafirishe

Paka hakai na Mbwa nyumba moja ukimuingiza Mbwa Paka' lazima atahaga mpambano
sio kweli mkuu nenda kwa wazungu ambapo mbwa ni sehemu ya familia anaweza kukaa barazani na wamiliki basi mbwa wao wakiwa na paka wote wanakaa ndani na wanakuwa marafiki
 
Wananusa sana hao hata sumu hawali
Usiweke kwenye bakuli nje au sufuria.
Weka palepale anapofungua friji kuiba mboga.
Ataangusha sufuria ale badae chali.
Nimefuga sana hiyo mifugo,na mbwa wangu Obbi hajawai hata siku moja kufanya ujinga.
Mbwa nikikusakizia atarara na wewe mbere labda nimwambie stop.
Hili paka sasa
 
Ningekuwa Dar es salaam ,ningekuomba daktari unipe huyo jamaaa ,nawapenda sana hawa wadudu japo ukishawafuga kubali kuwa mtumwa maana wanaanzaga kutuona sisi ni wafanyakazi wao
 

Kuna chama kinaitwa Tanzania Animals Protection Organisation makao makuu yake yako Dar na Shinyanga hiki chama ni NGO kiko chini ya SPCA Society for Protection of Cruelty to Animals chama cha New York Marekana.
Ofisi za TAPO ziko hapo karibu na Muhimbili nahisi kile chama cha zamani TASPC wamebadili jina.
Wanyama wote mbele za MUNGU ni viumbe wake japo kwenye vitabu vya dini wapo walioharamishwa.Mfano Nguruwe waslam kutokula Nguruwe haiamanishi waislam wanakubali Nguruwe afanyiwe ukatili.

Wanyama MUNGU amewaleta kwa makusudio maalum kwenye sayansi tunasema Ecosystem.Mfano unaweza ukaangamiza wanyama aina flani jamii nyingine ya wanyama wakaangamia hatimaye binadamu naye akaangamia.Nitoe mfano mbu ni kero kwa binadamu lakini ndio wanafanya popo aishi popo naye akipotea kuna wanyama kwenye food chaini watakufa mfano nyota na baadhi ya ndege.

Wanyama hata wenyewe wanapata maumivu binadamu unayoyapata wewe ukisulubiwa.
Habari za Paka ni antena ya wachawi ni imani za kishirikina zilizopo Africa huku sisi wajinga wajinga mbona wazungu hawana hizo imani na hawadhuriki.Bundi wamemuweka kundi la mlozi lakini ukweli bundi sio mlozi kinachotokea ni kwamba ukiwa na mgonjwa nyumbani kwako akianza kufa taratibu zile cell za mwili bundi ana kipaji cha kujua hivyo anapata hisia kuwa kuna mzoga uko karibu ndio maana akilia juu ya paa lako mgonjwa akifa utasema ndio aliyeleta mkosi.

Wazungu wao mbona hawapati haya madhara?

Kutumia risasi ajili ya kumuua paka msumbufu ni uharibifu wa pesa.Ukitaka kumuondoa paka wako mkorofi hakuna haja ya kumpiga rungu wewe mchukue muweke kwenye mfuko na usiwe unageuka nyuma nenda kilomita za kutosha mfungulie rudi nyumbani kwako atakuwa paka shume ila utakuwa hujatenda dhambi.

Wenzetu wazungu paka anaweza fungiwa hata Chip ya signals asipotee na hata mtu akipotelewa na paka au mbwa anaweza andika kwenye gazeti au kutangaza kwenye TV.pia wenzetu unavyoona kuna vituo vya kutunza watoto Yatima pia kuna sanatorium ajili ya kutunza wanyama waliotelekezwa.

Kuna mawazo yasiyo rasmi yasiyo na ushahidi nawaza kuwa waafrica tulivyo nyuma sana kimaendeleo sometimes ni laana MUNGU ametuachia kutokana na roho mbaya tulizo nazo
 
huna haja ya kufanya yote hayo , mpake rangi ya madoa doa alaf wapigie tanapa waambie umeokota mtoto wa chui watakuja mbio kumchukua
 
Paka nawapenda hasa wale wente rangi kuna mmoja nilikuwa nae alikuwa muda mwingi ananifuata ,paka akianza kuwa wizi hakai karibu na watu we mvizie akiiba mtandike pia kwani dagaa sh ngap changanya na chakula kisagie umo anakua hawi mwizi au mbebe kamptupe wilaya ingine
 
Paka hafi kwa sumu ya panya, labda binadamu ndio anakufa kwa sumu ya panya.

Waliosema paka ana roho saba usidhani huo msemo ni wa bure.
 
Mkuu hapa unazungumzia wale paka wanaotumwa dukani na pesa na wanarudi nyumbani na bidhaa siyo hawa ukila tonge la ugali anameza yeye huku kakukodolea macho.
 
Yani sometime sipendi kubishana na kina mama, nina kibali cha kunuwa risasi 500 kwa mwaka, nisipopata watu husika huyu namnyoosha kwa bullet.
Risas 500 kwa mwakaaa??? Thubutuuu yako,! Au mwenzetu unamiliki silaha gani?
 
Siwezi kubishana na mtu unayebisha kitu usichokijuwa.
Wewe ndo hujui. Kukusaidia tu kiwango cha kibali cha Risas unachoruhusiwa kununua/kumiliki katika kila mwaka kimeoanishwa kwenye Sect 22 of the firearms and ammunition Control act ya mwaka 2015.
Sasa tueleze wewe una silaha gani tu tukuwekee specific limit ya Risas unazoruhusiwa kumiliki in that particular year. Otherwise endelea na porojo zako kwa wasiojua. Wanaojua wanakutizama tuuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…