#COVID19 Hizi dawa za COVID-19 ni siasa au tuna malengo gani? SUA hiki kitu gani?

Wabongo bwana mmeshazoea vya kuletewa, mtaletewa hata mavirus muyaite vaccines, hata hizo vaccines za ulaya hazina accuracy 100% ndio mana na wao wanapukutika kama kawaida. Tafiti nyingi zilifanikiwa kwa majaribio je Kuna ulazima gani wa kuwakatisha tamaa wataalam wetu!
 
Hiyo NIMRCAF sisi wengine tunaitumia kutenderize steak kabla ya kubarbecue...inafanya nyama iwe laiiiini
 
Ile mashine yenu ya kijifukiza bado inafanya kazi?
 
Tuliotumia hiyo dawa tukapona tunakushangaa. Kuna mambo mawili, maana yenyewe ipo kwenye kopo la brown, labda umepata feki.
Au labda uliifungua muda mrefu hukuitunza Kwa usafi.
Kwa hiyo dawa, labda useme lingine
 
Utapeli mtupu kupitia migongo ya wajinga
 
Iyo bobo Iko kama ya sumu yakupulizia wadudu
 
mtu mweusi ni janga la dunia, hapa ungetumia za mzungu na zikakupa madhara usingebeza wala kujudge.
 
ile ndio funga kazi, nasikia wiki hii imeanza tena kufuka moshi, wateja watakuwa wameanza kupatikana🤣
“Kufuka moshi”
Itakua wakina kanjibahi wanaogelea humo nmaana ndo mitaa yao😅
 
Tulizoea kuona matone ya macho, hapa CHUO KIKUU kikaleta matone ya koo! Dah! Ningekuwa na uwezo watu kama hawa wote wangezuiliwa kufundisha vijana wetu. Hwa ni waharibifu kabisa. Bora waanzishe makanisa
 
mtu mweusi ni janga la dunia, hapa ungetumia za mzungu na zikakupa madhara usingebeza wala kujudge.
Ninayo hisia moja tu, kwamba ukinipa dawa inayoonesha umahili wako lazima nikupe hongera. Lakini ukinipa majani na mizizi ya kuchemsha na mchanganyiko wa kachumbali kama mimi ninavyoweza kuchemsha, hapo unajitukanisha kichwa chako.
 
Hapa mkuu unazungumzia dawa gani.. Panadol yenyewe inatushinda halafu iwe dawa ya Corona...!? Unless Wanazungumzia muarobaini.....!!
 
Ombi langu ni moja tu! Hawa wanaouza madawa kama haya wajiheshimu. Wanatumia umaarufu wa vyuo vikuu kutapeli wananchi na kuonesha ujinga wao. Na wanasiasa kwa kutaka huruma ya wananchi kwamba kuna jambo la maana linafanyika, wanaunga mkono utapeli huu. Hii ni kulisha watu uchafu.

Na inavyoonekana, tumekuwa wazoefu tangu mzee wa Loliondo.
 
Wewe ndiye mjinga kwa kuziamini dawa zinazofanana na ndumba badala ya kuamini katika sayansi.
 
Bosi na wewe una kipaji cha ujinga! Unategemea nchi hii upate mwanasayansi wa kukupa dawa ya Corona? Hawa wapayukaji ndo wajue sayansi?
Hata uandishi wake unaonyesha kuwa, kweli anakipaji Cha ujinga!
 
Wewe ndiye mjinga kwa kuziamini dawa zinazofanana na ndumba badala ya kuamini katika sayansi.
Huo unaoita utapeli ndio umesaidia kuponya wengi kwa ushahidi kabisa...sasa wewe unaowakosoa wasomi waliotumia sayansi kupima mimea yenye kusaidia matatizo ya kupumua una msaada gani kwa jamii...matusi haya huwatukani Mlimani,Sua bali unatukana mpk mamlaka ya mkemia mkuu wa serikali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…