Hizi ndio nchi ambazo Marekani na Israel hawawezi kuthubutu kuingiza pua zao kushambulia kijeshi

Hizi ndio nchi ambazo Marekani na Israel hawawezi kuthubutu kuingiza pua zao kushambulia kijeshi

Hili hata mimi silipingi mkuu, japo kuna wale wenzangu na mimi walipoona kambi za Marekani zinashambuliwa kule Iraq na Syria wakaanza kufikiri kwamba jibu la Marekani itakuwa ni kuivamia Iran kijeshi kitu ambacho ni dhahiri kuwa wanaota mchana kweupe huku wanatembea.
Wengi hawajui bali ushabiki tu na hata chuki ila vita mkuu sio rahisi kulianzisha watapiga pembeni tu
 
Iran juzi amepigwa na Pakistani tena ndani ya ardhi yake, akakimbilia kuomba msamaha.
Pakistan hii hii ambayo haina uwezo wa kutengeneza hata risasi, inayotegemea kununua silaha kutoka katika nchi zingine ndo iwe na uwezo wa kupambana na nchi inayounda silaha zake yenyewe na haitegemei badget ya kijeshi itoke Marekani na Ulaya kila mwaka kama Israel!

Pakistan ishukuru Iran haikutaka kuingia vitani na Pakistan kwa sababu ya mazingira ya vita katika eneo. Kwa sababu kulikuwa na mazingira ya kuchangiwa na nchi tatu zikiwemo Israel, Marekani na Pakistani yenyewe.

But hata hivyo Pakistan ni nchi, tofauti na Israel inashambuliwa kila siku na wanamgambo tu wa hezbulla ambao hawana silaha za maana, hawana jeshi wala mamlaka yoyote ya nchi na bado hajaweza kuwadhibiti kwa chochote.
 
Ni Iran pekee pale Mashariki ya kati ndo vijana wake wana uwezo wa kushambulia kambi za jeshi za Marekani na wakati huo huo wakashambulia ardhi ya Israel. Nchi moja tu ambayo haina backup yoyote ya badget ya kijeshi kutoka popote ila inadhibiti ujinga wote unaoendelea pale Mashariki ya kati.
Na ndio ukweli tena inashambulia bila kuogopa yaaani
 
Mkuu si Iran inataka kuifuta Israel kwenye Ramani ya dunia. Nini kimemshinda?
Mkuu lengo la Iran sio kuifuta Israel kwa sababu haipeani mpaka na Israel na pia haina masilahi yoyote kutoka huko ilipo Israel. Lengo kuu la Iran ni kuizuia Israel isijitanue mpaka ije iifikie Iran kidogo kidogo.

Ukipata muda ucheki huu uzi niliokuwekea hapo chini utaelewa kila kitu. Israel ni kama inatumiwa na nchi zenye nguvu kwa malengo yao ya baadae. So huu ujinga ndo Iran kama taifa lenye kujitambua miaka na miaka haitaki kuusikia.
 

Attachments

  • Screenshot_20240125-152920.jpg
    Screenshot_20240125-152920.jpg
    84.8 KB · Views: 2
Unazungumzia Israel hii inayotumia jeshi lote la nchi nzima hadi askari wa akiba, midege ya kijeshi, meli na vifaru kupambana na vijana wasiozidi elf 20 tu ambao wanatumia silaha za kienyeji na bado wameshindwa kukomboa mateka wao?

Ni kama vile jwtz iingie mzigoni na silaha zake zote kupambana na kakikundi ka vijana wa panya road pale Manzese na bado washindwe kuwadhibiti alafu wewe bado ulione jwtz kuwa ni jeshi bora [emoji23][emoji23][emoji23]
Kwa hiyo vita ili ushinde ukomboe mateka,akili za kikobazi hizi!
 
Niaje waungwana

Hapo chini naorodhesha nchi ambazo si Marekani wala Israel itaweza kuthubutu kuingiza pua yake kuzivamia kijeshi kwa namna yoyote ile. Hii ni kutokana na uwezo mkubwa wa kijeshi, kiintelejensia, kiteknolojia ni kiuwezo zilizo nazo nchi hizo katika kulikalisha chini na kulihenyesha taifa lolote litakalothubutu kuvamia ardhi zao.

Hata Mmarekani anajua ndomaana akitaka ku deal nao kiaina huwa anatuma tu silaha huku yeye akiwa nje ya mapambano, au anaishia kushambulia vidagaa vilivyowekwa na hao wababe wasiopenda kuendeshwa kijinga jinga na nchi za magharibi. Kuna wazungu wa buhambwe walikuwa wanaota huku wanatembea kwamba eti Marekani itaivamia Iran kutokana na mashambulizi yaliofanywa na vijana kadhaa huko Iraq.

Wazungu hawa wa buhambwe wengi waliendeshwa na mihemko kuliko uhalisia kamili wa kile wanachokiota. Wenye akili tulipinga kwamba mbabe huyo wa mchongo hawezi kutia pua uajemi kufanya shambulizi, ila hawakutuelewa. Sasa leo wameona wenyewe jinsi mbabe wao alivyokwepa jukumu la kuthubutu kuivamia uajemi. Anachotaka kufanya ni kupambana tu na vijana waliowekwa na waajemi washughulike nae.

Nchi zenyewe ni...ga

1. Russia
2. Iran
3. China
4. North Korea.
Tanganyika umeiacha
 
Kwa hiyo vita ili ushinde ukomboe mateka,akili za kikobazi hizi!
Lengo la kuingia vitani ilikuwa ni kuwamaliza Hamas na kuokoa mateka kwa muda wa wiki 1.

Leo tuna miezi minne Hamas hawajamalizwa na mateka hawajaokolewa. Endelea kujazwa matango pori kijana.
 
Iran haimo kivipi mbona haueleweki?

Kati ya hizo nchi nilizotaja, ni nani ana mdindia Mmarekani live live na kupiga mabomu kambi zake kila siku.

Unafikiri Iran ingekuwa Libya, Iraq au Venezuela ndo zinashambulia kambi hata moja au mbili tu za Marekani hali ingekuwaje
Iraq hakuitindia us tena huku russia akimsspoti?
 
Israel tunaipa sifa kwa sababu ya biblia tu na dini. Lakini kiuhalisia tukiacha kuendekeza unafki na hisia za dini. Israel haina nguvu yoyote ya kuwa super power katika dunia hii ya leo. Kwa sababu inategemea kila kitu kutoka nje mpaka badget yake ya kijeshi inatoka Marekani, UK na Ulaya.

Hizo nchi zikijitoa kuisaidia au kuiwekea vikwazo kama Iran au North Korea kwa miaka mitano tu itakuwa nyang'a nyang'a kama chapati ya maji iliyowekwa maji mengi.

Tukiweka mihemko pembeni kusema ukweli wanaume ni Iran na North Korea maana pamoja na vikwazo vya nchi kubwa za magharibi kwa zaidi ya miaka 70 lakini bado zinatengeneza silaha zao zenyewe tena zile kubwa kubwa, hatari na za kisasa, nafikiri umeona ndege zisizo na ruban za Iran zilizobadilisha hali ya vita kule Ukraine hadi nchi za magharibi na Ukraine yenyewe zilikuwa zinalalamika kuwa vita imebadilika ghafla na kuwa ngumu kwa Ukraine baada ya Iran kumpa mrusi zile ndege zake, hapo sijazungumzia silah zingine ambazo anaziweka kwa ajili ya matumizi yake binafsi, hizo nchi hazitegemei msaada wa kifedha wala wa kijeshi kutoka kwa nchi nyingine yoyote, zina intelejensia yao, teknolojia zao, na juzi wao.

Iran juzi karusha satellite zake tatu. Jiulize kama hizo nchi zisingewekewa vikwazo kama Israel, Japan au Uk leo hii zingekuwa wapi kijeshi na kiuchumi. Israel haina vikwazo, inapewa misaada, na inafadhiliwa badget ya jeshi kila mwaka, lakini cha kushangaza juzi waliposhambuliwa na vijana elf 20 tu wanaotumia silaha duni, yeye kakimbilia kuomba msaada mungine wa kijeshi kutoka Marekani, kaita mpaka jeshi la akiba na wale wastafu ili kuja kupambana na vijana wanaotumia silaha za kienyeji, hawana jeshi wala uwezo wa kununua silaha. Alafu cha kushangaza zaidi na Marekani akamuongezea na ile meli yake ya kijeshi kupambana na wana mgambo elfu 20 ambao idadi yao haifiki hata ya raia wanaoishi kata ya manzese.

Alafu mtu useme eti nchi hiyo ikipigana dunia itatingishika. Ipigane mara ngapi na wakati leo ipo vitani kwa zaidi ya miezi minne kupambana na vijana duni elfu 20 bila kufikia malengo ya kuokoa mateka hata mmoja.

Huu ni unafiki wa hali ya juu ambao moyoni kwako mwenyewe unakataa [emoji23][emoji23][emoji23]

Ukiniambia Russia na Marekani, Japan na China au Iran na Uturuki hapo nitaelewa.
Toa Iran toa udini unakupofusha.
 
Wewe ni mnafiki. Unasema hawakufanya retaliation zozote za maana, wakati shambulizi lilileta madhara makubwa katika kambi ya Marekani nchini Iraq!

Israel hiyo ndo inashambuliwa kila siku katika ardhi yake, so yenyewe ilibahatisha kuuwa afisa mmoja au wawili ni tofauti na yeye anaeshambuliwa kila siku katika ardhi yake na kusababisha maafa makubwa kama Oktoba 7.

China geographia yake inasababisha asikutane na changamoto hizi. Kama na yeye angeishi Mashariki ya kati kwenye misukosuko ya kila siku pengine na yeye angejaribiwa japo naamini na yeye angekuwa kama Iran asingesubiri kufanywa mnyonge.

Israel akikatiwa misaada na ufadhili wa kijeshi anaopewa na nchi za magharibi kila mwaka ni mwepesi mno. anaweza kuchakazwa hata na hezbulla kama walivyomchakaza mwaka 2006 pamoja na misaada yake ya kijeshi.
Akatiwe msaada ili iweje mbona mnaowaita panya road(hamas)hadi msikitini kwenu kule kilanjelanje mnachangia.Russia hachangiwi na Iran?kwa hiyo Iran yuko juu kuliko Russia?akili za bikra 72 hizi!
 
Lengo la kuingia vitani ilikuwa ni kuwamaliza Hamas na kuokoa mateka kwa muda wa wiki 1.

Leo tuna miezi minne Hamas hawajamalizwa na mateka hawajaokolewa. Endelea kujazwa matango pori kijana.
Ila kwa russia kutoka siku 3 hadi miaka kashinda vita,kobazi wanafiki sana!
 
Russia alijiapiza eti yeyote atakaye ingilia vita kati yake na Ukraine kwa kuipa chochote Ukraine atapata kichapo ambacho hatakuja kukisahau. Sasa najiuliza Je Marekani anaisaidia Ukraine silaha kwa kificho?
Ila kuna ukakasi flani yani mimi napigana nawewe lakini wanaonisaidia kukupiga wanatangaza siraha za kukupiga huu ni uzoba na woga kwa siraha walizotangaza kuzipeleka ukrein basi mrusi angesumbuka mno ila sasa mh
 
Taiwan ipo katika mikono ya China, ikiamua kuangamizwa na China ni sekunde tu.

Ila inachokataa China ni kwa vile inaamini kuwa wataiwani ni ndugu zake, hivyo kuiangamiza Taiwan ni sawa na kuwangamiza raia wake wa kesho. Marekani pale ingeishia kutuma silaha tu kama inavyofanya kwa Ukraine hadi mwisho ingechoka na kuwaachia wataiwani zigo lao wanamalizane nalo wenyewe.
Kabisa madhara wangebaki nayo wenyewe taiwan kama kievu tu
 
Iraq hakuitindia us tena huku russia akimsspoti?
Imdindie wakati Marekani ana kambi zake tayari katika ardhi yao na amekataa kuzitoa?

Hivi unaweza kusema unamdindia adui yako na wakati anajimilikisha chumba katika nyumba yako?
 
Back
Top Bottom