Hizi ndizo sehemu zilizopigwa na makombora ya Iran huko Israel siku ya jana!

Simple arithmetic unashindwa kuing'amua bro!?
Juzi Iran alirusha makombora mangapi katika kila!?
Alirusha ballistic na hypersonic kwa wakati mmoja katika duru 3+ za mashambulizi.
Iron dome zipo ngapi!?
Pia inachukua muda gani hadi ku reload missile interceptors ndani ya iron dome!?
Iran alirusha ballistics kwaajili ya kuzi overwhelm iron dome kesha akafyatua na strategic hypersonic missiles kulenga target.
 
Sawa hapo unataka tuingie kwenye specification za hiyo mitambo kitu ambacho sikutaka maana ingekua unamlisha maneno mwandishi. Mfano wewe hapo mwenyewe umeshindwa kuweka jibu la swali ulilojiuliza na mimi nimepigia mstari hapo juu.

Sasa tuambie wewe unafikiri iron dome ina uwezo gan katika ku reload interceptors.
Na ukumbuke pia kuwa ziko mashine za kutosha ku fire intercepting missiles.

Nilitaka tu stick kwenye literal concept ya mleta mada bila kuongeza maneno yetu, maana huko sasa tutakwenda deep T14 Armata njoo utie neno
 
Mbona mleta mada kaeleweka na ameongea kiwepesi tu!?
Ni wapi mkuu hujaelewa??
 
50 yote hayo? Jibu lake itawachukua siku mbili kujua kama mashambulizi yametokea humohumo Iran au nje ya Iran
 
Uwezo wa Israel kujilinda Iran anataka kuchukua credit kwamba ameepuka kuua raia.
 
Mbona mleta mada kaeleweka na ameongea kiwepesi tu!?
Ni wapi mkuu hujaelewa??
Nikuulize swali ,je wewe unajua kuwa mtambo mmoja wa Iron dome,una weza ku intercept missiles ngapi na ndani ya muda gani??
Maana hapo mleta uzi kasema out of 10, the iron dome takes out 1, how far can you go to provide us with a proof?
 
Kambi sawa zitarekebishwa
Hezbollah command centre hairekebishiki. Maofisa wa Iran hawarudi, maofisa wa Hezbollah hawarudi, Hamas haivamii tena.

Bado yajayo kwa Iran hanafurahisha.
F-35 zitaletwa mpya kutoka USA hilo linafahamika na makao makuu yatajengwa upya.
Makao makuu gani yalipigwa? Kila kilichopigwa na Israel picha zipo, nipe evidence makao makuu yamepigwa. Makombora yalikuwa yanajidondokea bila shabaha halisi.

F-35 Israel inanunua, au onyesha ni fighter jets gani "zililetwa Israel" bila Israel kutoa hela. Na zinaletwa za nini wakati hamna zilizoharibika.

Kwanza F-35 za Israel ni za kipekee kuliko F-35 nyinginezo, ni 'Adir'. Haubebi ndege from nowhere ukaleta Israel zikatumika. Na nani atazitoa, na Lockheed Martin hawazifyatui bila order kama gari.

Utaona kama Israel itanunua ndege yeyote kabla haijaijibu Iran.
Ila wewe jamaa huwa hukosi sababu,si wewe juzi ulisema Iran na makombora yake yasiyo na madhara haina cha kufanya!?
Makombora hayana mashara ndio. Cha kufanya ilikuwa nacho, ni kufyatua makombora yasiyo na madhara. Siku ile shambulizi la magaidi wawili kwa bunduki lilileta madhara makubwa kuliko shambulizi la makombora 200.
Mkuu huwa napendaga kujadiliana na wewe kwasababu una accuracy kubwa ya kujadili hoja,Iran sio Hizbollah na wala sio Hamas.
Iran ni nchi kamili na ina jeshi kamili na ina kila aina ya silaha ambayo Israel anayo.
Iran haina fighter jets, haina refuering tanks, haina airlifters, haina air defence systems covering the vast country, haina nukes, haina subs.

Iran haifanani kwa lolote na Israel kijeshi. Iran ina jeshi limekazania kujihami, kujilinda. Israel ina jeshi linalosisitiza kushambulia. Kwa sera za Israel ni bora iwe na attack jets kuliko kuwa na interceptor jets.

Iran ina idadi ya wanajeshi wengi ambayo haina maana kwa mantiki hii sababu haipakani na Israel, sasa watapita wapi?
Pia ina makombora mengi na drones.

Kumbuka Israel haijawahi tumia ballistic missile wala ICBM labda cruise tu. Wote hawa watatumia anga kushambuliana na Iran haina air dominance.
Askari 14 kwenye vita serious ni idadi ndogo sana labda uzungumzie vita njaa kama Vita ya Kagera. Hujaona casualties za Hezbollah na wala sio kila siku Israel itapoteza 14. Na kawaida ya invading forces inatarajiwa kupata casualties 3:1 kwa defending forces kama zina nguvu sawa. Ila sababu Israel ina nguvu, Hezbollah ndio watachakaa zaidi.
 
Yaani wabongo vita mnachukulia kama mechi ya watani wa Jadi.. vita sikieni tu ni si ya kufurahia
 
Iran wao hawana shida na raia japo raia wapo kwenye mahandaki mda huu ila wale jamaa wana roho nzuri sana huwezi sikia raia kafa kwenye shambulio lao
🤣🤣🤣wana roho nzuri maajabu duniani hayaishi.Ww sema hao jamaa kila wakijitahidi kurusha vi manati vyao vinaishia juu havitui chini.Hivi kuna muislam anampenda muislaeli mtoa roho...yaan hao wanatamani hako ka nchi wakafute ww unasema wana roho nzuri😂😂
 
Iran wao hawana shida na raia japo raia wapo kwenye mahandaki mda huu ila wale jamaa wana roho nzuri sana huwezi sikia raia kafa kwenye shambulio lao
Unanipiga risasi nikiwa nimevaa bulletproof vest, vest inazuia alafu unasema una roho nzuri?
 
Mashambulizi ya juzi air defense systems zote zilikuwa activated.
Naona mnaishabulia Iron dome pekee ambayo ni short range.
Vipi ufanisi wa David & Arrow 3?
 
Sawa wamepiga,ila majibu ya myahudi huwa mabaya na yanaogofya sana.
Turned watamfanyaje muajemi,walimtaka na sasa amekuja bila kuogopa
 
Iran ina BMs(Fattah-2, mach 20) zaidi ya 4000, zingine zinazalishwa na hawajui waziweke wapi
Urusi alimaliza robo ya stock, chap kesho yake pipa likajaa tena
mkijibu, tunarusha 1500
Kumbe unaandika ushabiki.
Uzalishaji wake uko juu kwa sababu anafadhili makundi mengi so anatakiwa kuwa na mzigo mkubwa.
Nimeuliza wapinzani wake hawana siraha hatari kwa Iran? Au iran ndie mwenye siraha hatari zaidi duniani?
 
Kumbe unaandika ushabiki.
Uzalishaji wake uko juu kwa sababu anafadhili makundi mengi so anatakiwa kuwa na mzigo mkubwa.
Nimeuliza wapinzani wake hawana siraha hatari kwa Iran? Au iran ndie mwenye siraha hatari zaidi duniani?
Usimchukulie serious huyu dronedrake maana yeye anafikiri kurusha missiles ni kama kushika uboo na kupiga nyeto. Ndio kitu pekee anakijua.
 
Kumbe unaandika ushabiki.
Uzalishaji wake uko juu kwa sababu anafadhili makundi mengi so anatakiwa kuwa na mzigo mkubwa.
Nimeuliza wapinzani wake hawana siraha hatari kwa Iran? Au iran ndie mwenye siraha hatari zaidi duniani?
Iran ana BMs nyingi Middle East, Israel analijua hilo ndiyo maana hawezi jibu
anajua Iron Dome haifui dafu tena kwa Fattah, anajua akijibu, Tel Aviv inakuwa Gaza-2
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…