Hizi ni stori za kwenye Biblia ambazo zimeniacha na maswali sana

Hizi ni stori za kwenye Biblia ambazo zimeniacha na maswali sana

Sikia mkuu, Quran kariim ipo clearly, haiitaji roho mtakatifu bali akili, ulichoweka hapo si ulicho kisema, alafu kila siku mna sahihishwa lakini wapi, hakuna swali ambalo Quran kariim haija jibu, Quran kariim ni maneno ya Allah, ipo wazi, jibril ni malaika wa ALLAH na Shetani ni adui wa wanaadamu, je Quran kariim haija sema hivo?, (ndio hoja yako ipo hapo?
Huajaeleweka
 
Mungu hayupo, hizo ni stories za watu tu za kuungaunga.

Ndiyo maana ukakasi mwingi.
Kama Mungu hayupo basi ka lale na mamayo, vinginevyo Mungu yupo, hiyo sayansi haijui lolote kuhusu mwamke ispokua ni mzalishaji, sasa kamzalishe mama yako, Mark My words, only Mungu tu kamzungumzia mama kwa hadhi ya juu siyo hyo sayansi yako ya kijinga
 
Angalau kwa biblia ila Kuna kitabu hiko Kuna Aya hadi leo inanifikirisha sana na sielewi kwanini wafuasi wake wanakaza shingo kukiamini

Qu'ran 2:97
Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.

Nani ni adui wa Jibril? Jibu ni shetani
Kwanini shetani ateremshe Quran na tunaambiwa kuran ni tukufu?

Hili swali haitatakea nikapata jibu la kuridhika
Unahakika gani kuwa shetani ni adui wa jibril mkuu?
 
1. Kwenye Mwanzo 1:26 imeandikwa kuwa Mungu alisema tuumbe mtu kwa mfano wetu. Nimejiuliza ina maana uumbaji ulifanywa nae kwa kushirikiana na wengine? Hakuwa peke yake? Hao wengine kina nani?

Ukisoma Yohana 1: 1 - 18

Utaona inatoa majibu ya kwamba wakati wa uumbaji wa ulimwengu na vitu vyake, utaona ulimwengu ulifanywa na Mungu baba na mwana, huyu mwana katajwa kama Nuru au Neno aliyekuja kufanyika mwili (Yesu Kristo)...
 
Mimi ni mkristo na ninaamini Mungu yupo na anatenda. Ila kuna mambo ukisoma kwenye biblia lazima ujiulize maswali mengi sana yanayokosa majibu. Leo nitashea nanyi mambo ambayo naona kama yana ukakasi;

1. Kwenye Mwanzo 1:26 imeandikwa kuwa Mungu alisema tuumbe mtu kwa mfano wetu. Nimejiuliza ina maana uumbaji ulifanywa nae kwa kushirikiana na wengine? Hakuwa peke yake? Hao wengine kina nani?

2. Mwanzo 6 - 10 kuna stori maarufu ya Nuhu. Hii ni stori ina ukakasi zaidi. Nikiandika maswali yote niliyojiuliza uzi utakuwa mrefu. Ninashauri mkaisome ili tuifungulie uzi wake.

3. Kutoka 11:5-6 kuna maandiko yanayosema kuwa wazaliwa wa kwanza wote wa wamisri kwa upande wa binadamu hadi wanyama watauwawa na Mungu mwenyewe ili waisraeli wapewe ruhusa ya kwenda nchi ya ahadi. Kiukweli haya yalikuwa ni mauaji ya halaiki kwa wasio na hatia. Unaambiwa hadi mzaliwa wa kwanza wa mbuzi, kuku, ng'ombe, mbwa na farasi waliuwawa. Kwanini isingetumika njia nyingine hao waisraeli wakaondoka?

4. Kitabu kizima cha Joshua kimejaa stori za mauaji matupu. Ikumbukwe Joshua alichukua nafasi ya Musa kwenye kuwaingiza waisraeli nchi ya ahadi baada ya kifo cha Musa. Nchi waliyoahidiwa ilikuwa tayari ina wakazi wake ambao ilibidi wauwawe wote ili kuwapisha waisraeli. Hivi ilishindikana vipi kufanya kama alivyofanya Mama Samia kuwatoa wamasai Ngorongoro na kuwapeleka Msomera kwa amani kabisa bila kumwaga damu? Kama leo 2024 bado kuna maeneo duniani hayajakaliwa na binadamu ilikuwaje enzi za Joshua? Ukisoma kitabu cha Joshua utaona kila sehemu waliyopita walikuwa wakiua wenyeji watakaowakuta. Kulikuwa na sababu zipi za msingi za mauaji haya yote?

5. Ayubu 1:6-12 utaona stori ya shetani alipojiunga na wana wa Mungu kupita mbele ya Mungu kumwabudu hadi Mungu akashangaa imekuwaje shetani akawa eneo lile? Baada ya hapo Mungu na Shetani wakakubaliana kwenda kumjaribu Ayubu kwa sharti la kutogusa mwili wa ajabu (kumuua). Katika yale majaribu watoto wa Ayubu waliuwawa na shetani. Naweza kusema ni mauaji yaliyokuwa na approval toka juu. Ilikuwa kazi maalum. Je, sio kwamba wawili hawa hukutana na kukubaliana baadhi ya mambo? Sio kwamba kuna kazi za shetani zina kibali maalum?
Mungu na Shetani ni marafiki wazuri sana na wanaelewana. Sisi wanandamu
 
Unahakika gani kuwa shetani ni adui wa jibril mkuu?
Nipe uhakika juu ya adui wa Jibril, ni nani hasa adui wa Jibril?
Jibril ni malaika mwema, je malaika mwema anaweza kuwa na uaudui na malaika mwema mwenzie? Au wewe tuambie ni nani adui wa Jibril pengine sisi tumekurupuka kuthibitisha kuwa ni shetani
 
Nipe uhakika juu ya adui wa Jibril, ni nani hasa adui wa Jibril?
Jibril ni malaika mwema, je malaika mwema anaweza kuwa na uaudui na malaika mwema mwenzie? Au wewe tuambie ni nani adui wa Jibril pengine sisi tumekurupuka kuthibitisha kuwa ni shetani
Mimi siwezi thibitisha huo uadui maana wote shetani na jibril sina hakika nao as well. Nilikuwa nakuuliza wewe uliyekuwa unaongelea huo uadui mkuu labda unaweza kunisaidia katika hilo
 
3. Kutoka 11:5-6 kuna maandiko yanayosema kuwa wazaliwa wa kwanza wote wa wamisri kwa upande wa binadamu hadi wanyama watauwawa na Mungu mwenyewe ili waisraeli wapewe ruhusa ya kwenda nchi ya ahadi. Kiukweli haya yalikuwa ni mauaji ya halaiki kwa wasio na hatia. Unaambiwa hadi mzaliwa wa kwanza wa mbuzi, kuku, ng'ombe, mbwa na farasi waliuwawa. Kwanini isingetumika njia nyingine hao waisraeli wakaondoka?

Mungu ndiye atoaye na kuuchukua uhai wa mwanadamu...

Ayubu 1
21 akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe.

Zaidi Biblia inaonesha kwamba kizazi hubeba dhambi za baba zao (watawala ni baba wa taifa)...

Maombolezo 5
7 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.

Hesabu 14
18 Bwana ni mpole wa hasira, mwingi wa rehema, mwenye kusamehe uovu na makosa, naye hatamfanya mwenye hatia kuwa hana makosa kwa njia yo yote; mwenye kuwapatiliza wana kwa uovu wa baba zao, katika kizazi cha tatu na cha nne.

Ezekieli 7
8 Basi hivi karibu nitamwaga ghadhabu yangu juu yako, nitazitimiza hasira zangu juu yako, nami nitakuhukumu sawasawa na njia zako; nami nitakupatiliza machukizo yako yote.
 
Na Kwa kukuchanganya zaidi kwenye Hiyo Aya ya 3...!

Mungu alikua analeta mapigo Kwa farao, HALAFU TENA ANAMWINGIA FARAO KIROHO NA KUUFANYA MOYO WAKE KUWA MGUMU, Yani kifupi ni hivi, kama Mungu asingeufanya Moyo wa Farao kuwa Mgumu, basi Farao angeshawaruhu Wana Israel kitambo na yote ya kuuliwa Kwa Uzao wa kwanza kuanzia Sungura, Ng'ombe, Mbuzi mpaka Binadamu yasingetokea.

Tatizo lako unatumia Akili Yako ya Kibinadamu kuelewa Mambo ya Kiroho, Utakua na Maswali mpaka Yesu anarudi....!

GOD IS THE SPIRIT.
Acha upuuzi wewe. Ulitaka nitumie akili gani?
 
Mimi ni mkristo na ninaamini Mungu yupo na anatenda. Ila kuna mambo ukisoma kwenye biblia lazima ujiulize maswali mengi sana yanayokosa majibu. Leo nitashea nanyi mambo ambayo naona kama yana ukakasi;

1. Kwenye Mwanzo 1:26 imeandikwa kuwa Mungu alisema tuumbe mtu kwa mfano wetu. Nimejiuliza ina maana uumbaji ulifanywa nae kwa kushirikiana na wengine? Hakuwa peke yake? Hao wengine kina nani?

2. Mwanzo 6 - 10 kuna stori maarufu ya Nuhu. Hii ni stori ina ukakasi zaidi. Nikiandika maswali yote niliyojiuliza uzi utakuwa mrefu. Ninashauri mkaisome ili tuifungulie uzi wake.

3. Kutoka 11:5-6 kuna maandiko yanayosema kuwa wazaliwa wa kwanza wote wa wamisri kwa upande wa binadamu hadi wanyama watauwawa na Mungu mwenyewe ili waisraeli wapewe ruhusa ya kwenda nchi ya ahadi. Kiukweli haya yalikuwa ni mauaji ya halaiki kwa wasio na hatia. Unaambiwa hadi mzaliwa wa kwanza wa mbuzi, kuku, ng'ombe, mbwa na farasi waliuwawa. Kwanini isingetumika njia nyingine hao waisraeli wakaondoka?

4. Kitabu kizima cha Joshua kimejaa stori za mauaji matupu. Ikumbukwe Joshua alichukua nafasi ya Musa kwenye kuwaingiza waisraeli nchi ya ahadi baada ya kifo cha Musa. Nchi waliyoahidiwa ilikuwa tayari ina wakazi wake ambao ilibidi wauwawe wote ili kuwapisha waisraeli. Hivi ilishindikana vipi kufanya kama alivyofanya Mama Samia kuwatoa wamasai Ngorongoro na kuwapeleka Msomera kwa amani kabisa bila kumwaga damu? Kama leo 2024 bado kuna maeneo duniani hayajakaliwa na binadamu ilikuwaje enzi za Joshua? Ukisoma kitabu cha Joshua utaona kila sehemu waliyopita walikuwa wakiua wenyeji watakaowakuta. Kulikuwa na sababu zipi za msingi za mauaji haya yote?

5. Ayubu 1:6-12 utaona stori ya shetani alipojiunga na wana wa Mungu kupita mbele ya Mungu kumwabudu hadi Mungu akashangaa imekuwaje shetani akawa eneo lile? Baada ya hapo Mungu na Shetani wakakubaliana kwenda kumjaribu Ayubu kwa sharti la kutogusa mwili wa ajabu (kumuua). Katika yale majaribu watoto wa Ayubu waliuwawa na shetani. Naweza kusema ni mauaji yaliyokuwa na approval toka juu. Ilikuwa kazi maalum. Je, sio kwamba wawili hawa hukutana na kukubaliana baadhi ya mambo? Sio kwamba kuna kazi za shetani zina kibali maalum?
Biblia ipo kiroho zaidi. Huwezi elewa baadhi ya maandiko mpaka umaanishe kumfuata Kristo.
“ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa.

— Marko 4:12

Kwa kukusaidia machache:
1. Tumfanye mtu kwa sura na mfano wetu: kumbe yupo Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu

3. Hapo kwa wazaliwa wa kwanza, kibinadamu ni wazaliwa wa kwanza ndiyo, lakini Mungu alikuwa anashughulikia miungu ya Wamisri inayompa kiburi farao. Hapo ilikuwa vita ya Mungu na miungu. Kumbuka Waisraeli walikuwa ni wazaliwa wa kwanza kwa Mungu kabla ya mataifa mengine yote.

4. Hapo kwa Joshua, kumbuka huko nyuma aliangamiza wanadamu wote na kubaki Nuhu tu sababu ya maovu mengi ya wanadamu. Kumbuka Sodoma na Gomora. Kumbuka Ninawi. Toka Adam atende dhambi, ndiyo mwanzo wa mauaji, mwanzo wa kuondoka amani duniani. Biblia inasema hakuna amani kwa wabaya. Na Yesu hakuja kuleta amani duniani bali upanga ili mtu achukiane na ndugu yake. Halafu akaleta amani yake ya kipekee tofauti na hizi amani za kidunia. Joshua aliwaua wote waliokataa kufanya shirika na Israel, na waisrael walikatazwa kuoana na watu wa maraifa mengine kwani wangewafanya Israel waabudu miungu mingine. Hata sasa tunaishi duniani Mungu akiwa na huruma lakini huruma ya Mungu haipo kwa wafu. Aliyekufa katika dhambi hakuna msamaha tena, ukomo wa huruma ya Mungu.

5. Kuhusu Ayubu. Kwani kwanin Mungu kamwacha shetani kwa muda. Hapo mwanzo Shetani alitaka kuabudiwa kwa kushawishi malaika wenzake kuwa Mungu ni dikteta. Mungu akamwacha ili kudhihirisha je, madai ya Shetani ni kweli au uongo. Akamwacha kila malaika na kila mwanadamu afanye machaguzi aidha ya kusimama na Mungu au kumwamini Shetani. Leo watu wote tunaoana Shetani ni mwongo. Tafuta kitabu cha Yashari (the book of jashar) na kitabu cha henoko (The book of enock). Utaona mengi humo
 
Kama Mungu hayupo basi ka lale na mamayo, vinginevyo Mungu yupo, hiyo sayansi haijui lolote kuhusu mwamke ispokua ni mzalishaji, sasa kamzalishe mama yako, Mark My words, only Mungu tu kamzungumzia mama kwa hadhi ya juu siyo hyo sayansi yako ya kijinga
Hujathibitisha Mungu yupo.

Umeleta logical non sequitur fallacy.

Inayoonesha ujinga wako.

Ujinga unaothibitisha Mungu hayupo.

Kwa sababu, angekuwepo, asingeumba mtu mjinga kama wewe.
 
Mungu ndiye atoaye na kuuchukua uhai wa mwanadamu...

Ayubu 1
21 akasema, Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu nili uchi, nami nitarudi tena huko uchi vilevile; Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe.
So mungu ndo anaua?
 
Ukisoma Yohana 1: 1 - 18

Utaona inatoa majibu ya kwamba wakati wa uumbaji wa ulimwengu na vitu vyake, utaona ulimwengu ulifanywa na Mungu baba na mwana, huyu mwana katajwa kama Nuru au Neno aliyekuja kufanyika mwili (Yesu Kristo)...
Unaongeza ukakasi zaidi.
 
Biblia ipo kiroho zaidi. Huwezi elewa baadhi ya maandiko mpaka umaanishe kumfuata Kristo.
“ili wakitazama watazame, wasione; Na wakisikia wasikie, wasielewe; Wasije wakaongoka, na kusamehewa.

— Marko 4:12

Kwa kukusaidia machache:
1. Tumfanye mtu kwa sura na mfano wetu: kumbe yupo Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu

3. Hapo kwa wazaliwa wa kwanza, kibinadamu ni wazaliwa wa kwanza ndiyo, lakini Mungu alikuwa anashughulikia miungu ya Wamisri inayompa kiburi farao. Hapo ilikuwa vita ya Mungu na miungu. Kumbuka Waisraeli walikuwa ni wazaliwa wa kwanza kwa Mungu kabla ya mataifa mengine yote.

4. Hapo kwa Joshua, kumbuka huko nyuma aliangamiza wanadamu wote na kubaki Nuhu tu sababu ya maovu mengi ya wanadamu. Kumbuka Sodoma na Gomora. Kumbuka Ninawi. Toka Adam atende dhambi, ndiyo mwanzo wa mauaji, mwanzo wa kuondoka amani duniani. Biblia inasema hakuna amani kwa wabaya. Na Yesu hakuja kuleta amani duniani bali upanga ili mtu achukiane na ndugu yake. Halafu akaleta amani yake ya kipekee tofauti na hizi amani za kidunia. Joshua aliwaua wote waliokataa kufanya shirika na Israel, na waisrael walikatazwa kuoana na watu wa maraifa mengine kwani wangewafanya Israel waabudu miungu mingine. Hata sasa tunaishi duniani Mungu akiwa na huruma lakini huruma ya Mungu haipo kwa wafu. Aliyekufa katika dhambi hakuna msamaha tena, ukomo wa huruma ya Mungu.

5. Kuhusu Ayubu. Kwani kwanin Mungu kamwacha shetani kwa muda. Hapo mwanzo Shetani alitaka kuabudiwa kwa kushawishi malaika wenzake kuwa Mungu ni dikteta. Mungu akamwacha ili kudhihirisha je, madai ya Shetani ni kweli au uongo. Akamwacha kila malaika na kila mwanadamu afanye machaguzi aidha ya kusimama na Mungu au kumwamini Shetani. Leo watu wote tunaoana Shetani ni mwongo. Tafuta kitabu cha Yashari (the book of jashar) na kitabu cha henoko (The book of enock). Utaona mengi humo
Itoshe kusema umeandika upumbavu mtupu.
 
Angalau kwa biblia ila Kuna kitabu hiko Kuna Aya hadi leo inanifikirisha sana na sielewi kwanini wafuasi wake wanakaza shingo kukiamini

Qu'ran 2:97
Sema: Aliye kuwa ni adui wa Jibril, basi huyo ndiye aliye iteremsha Qur'ani moyoni mwako kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inayo thibitisha yaliyo kuwa kabla yake, na ni uwongofu na bishara njema kwa Waumini.

Nani ni adui wa Jibril? Jibu ni shetani
Kwanini shetani ateremshe Quran na tunaambiwa kuran ni tukufu?

Hili swali haitatakea nikapata jibu la kuridhika
Kama kweli unataka kujua ilitakiwa umtafute anayejua akufundishe

Quran imeletwa Kwa lugha ya kiarabu na kiswahili ni mtoto wa lugha ya kiarabu Yani 95% ya misamiati ya kiswahili ni kiarabu hivyo kiswahili akina uwezo wa kutafsiri Kwa ufasaha lugha ya kiarabu

Ila maana halisi ya hiyo Aya ni hii yapa

Sema:Anayemfanyia uadui Jibrail(anajisumbua),hakika yeye(Jibrail) ameiteremsha (Qur’an) moyoni mwako,kwa idhni ya Mwenyeezi Mungu,inayosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake,na ni uongofu na bishara ya waumini”.


Lakini pia kama kweli unataka kujua nani aliyekuwa anamletea mtume Muhammad hiyo Quran mbona Aya nyingine zipo nyingi tu ambazo hazina lugha ngumu Kwa Nini usizisome hizo



Quran 16:102 -
Sema: Ameiteremsha hii Roho takatifu kutokana na Mola wako Mlezi kwa haki, ili awathibitishe wale walio amini, na kuwa ni uwongofu, na ni bishara kwa Waislamu.
 
Ndugu nimepitia andiko lako,ila kwa uelewa mdogo nilionao juu ya biblia ni mkusanyiko wa nyaraka zilizoandikwa na wanadamu,kila waraka ulielekezwa kwa jamii fulani.Nadhani nyaraka hizi kwakuwa waandishi ni binadamu basi zina mapungufu mengi na inawezekana baadhi zimetungwa tu.
Umemaliza.

Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu mkuu mkuu nimekuita mara tatu bibilia siyo kitabu cha ukweli (siyo cha Mungu) ndani ya bibilia kuna vitabu havijulikani muandishi ni nani na kama hio haitoshi bibilia ni maneno (utashi) wa Paulo,
3;15 wagalatia ,
Matendo ya mitume 11:25-26 , kubatizwa napo story zake ni utata mtupu, kifo cha yesu napo hvo hvo , kufufuka napo kila mtume anasema lake yaani kitabu kimejaa utata kila kona, atakaye bisha alete point according to bibilia only
Biblia, Koran na vijarida vingine vyote ni mawazp ta binadamu waliolenga kuwatawala kifikra binadamu wenzao (wasio na ufahamu)
Ukitoka nje ya box ykasoma hivyo vitabu utagundua makosa mengi mno na utashangaa inakuwaje watu wazima wanaviheshimu kiasi cha kuwa tayari kumchinja anayevikosoa!

Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom