Hizi sio mboga ni jaza tumbo

Hizi sio mboga ni jaza tumbo

Kisamvu kinafanyiwa make up ili kiwe mboga, kutwanga, karanga, kuchemsha n.k.
Sasa mkuu hata kuku anapitia process ngapi ili uweze kumla. Achinjwe, yachemshwe maji, anyonyolewe, na wale wataalamu, lazma wambanike kidogo ili waondoe manyoya madogo kwenye ngozi

Bado kuna kumpasua, kumtoa uchafu na kumkatakata

Bado tena umchemshe au umkaange then umuunge.. Hapo kuna tofauti gani na hivyo visamvu

Na kama unapenda shortcuts, hata hizo mboga za majani na maharage, ukipita migahawani wanauza vile ambavyo havijaungwa so kazi yako inakuwa ni kuunga tu unavyotaka.. Big deal ni nini mkuu 😁
 
Mengine hayo ni magugu, walioyagundua walikuwa wanajaribujaribu wakaona hawajafa wakayaita mboga za majani. Mfano mnavu na mchunga sijui unaitwa.

Mara ya kwanza kuonja mnavu nilikuwa shule, nikahisi supplier wa chakula kakosea mboga kaleta majani ya mbuzi. Nikasikia mchungu na hauna radha ya kustahili kuitwa chakula labda uitwe dawa, nikawaambia wadau leo supplier kapigwa wakulima wamemkusanyia malisho ya mbuzi. Washkaji wakanieleza eti hiyo ni mboga, haikuniingia akilini.
Ukizingatia utamu wa ugali ni mboga, iweje mboga ikawa chungu?
 
Majani ya maboga, my favourite 😍, kisamvu na mlenda sili..actually sijawahi kula mlenda.
Ni muda wa kupata kigori wa kinyamwezi ili akuonjeshe mboga za asili mkuu 😁😁😁
 
Nipeni hata jina moja la kiingereza ya mboga tajwa hapo juu? Hazifaahamiki na WHO. Usile nyasi kwani we ni mbuzi 🐐🐐🐐?
 
Back
Top Bottom