Hofu hii inasababishwa na nini na kwanini haikuwapo wakati wa kupigania uhuru?

Hofu hii inasababishwa na nini na kwanini haikuwapo wakati wa kupigania uhuru?

Pacbig,
Uislam ulikuwa na nguvu katika TANU.
Lakini si kuwa wapigania uhuru wote walikuwa Waislam.

Nini nafaidika ni kuwa historia ilipokuja kuandikwa mchango wa Waislam ukafutwa.

Hii ilikuwa kufutwa kwa historia ya wazee wangu na takriban historia ya miaka inayokaribia karne moja au na zaidi.

Faida niliyopata ni huku kuandika historia hiyo na sasa ni sehemu muhimu katika historia ya Tanganyika na Afrika.

Kleist Sykes na wanae wamo katika Dictionary of African Biography ingawa hawamo katika kitabu cha historia ya TANU kilichoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni.
Mzee baba kwani mtu alizaliwa Mwafrika au alizaliwa muislamu. Kwanini dini imekuwa kigezo kwako. Wakati dini zote hizi tumelewewa na wafanya biashara haramu za utumwa(wZungu na Waarabu)
 
Hv kugombania dini ya mtu fulani itatusaidia ni i Waafrika. Au dini Inaumuhimu hmgani kwetu?
Ed ...
Tatizo lililopo Tanzania ni hofu iliyopo juu ya Uislam.

Mkwawa Museum ndiyo wanaeleza kuwa Mkwawa alikuwa Muislam.

Watu wanapinga.

Songea Mbano jina lake Abdulrauf Songea Mbano.

Inapingwa.
Mkomanile jina lake Khadija Mkomanile.

Inapingwa.

Africa Association iliasisiwa na watu tisa saba ni Waislam na sababu wamishionari wakiwakataza waumini wao kujiingiza katika siasa.

Hili halitakiwi lisemwe.

Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika alikuwa anauza kadi za TANU msikitini.

Baraza la Wazee wa TANU liliundwa na wajumbe 120 wote Waislam hili halitakiwi liwe katika historia ya TANU.

Halitakiwi hili lisemwe nk.nk. nk.

Mradi ni Uislam ni mwiko kuwa sehemu ya historia ya Tanganyika.

Matokeo yake Chuo Cha CCM Kivukoni ikaandika historia ya TANU ikimlenga Nyerere peke yake.

Lakini Nyerere kaja Dar es Salaam mwaka wa 1952 harakati zimeanza 1929 kapokelewa na Abdul Sykes.

Abdul Sykes kadi yake ya TANU na 3 ya ndugu yake No. 2 ya Nyerere kama TAA Territorial President ni No. 1 na hizo kadi za TANU kazichapa Ally Sykes Printpak wachapaji wa gazeti la Tanganyika Standard.

Na hiyo kadi ya Nyerere, Mwalimu kaandikiwa na Ally Sykes.

Historia hii haitakiwi.
Tatizo liko hapo.

Huwezi kufuta historia za watu.
Huu ni muhali mkubwa.

Wenyewe hawatakubali.

Ndiyo leo mko hapa mnasoneshwa historia ambayo hamkupata kuijua, kuisoma wala kuisikia popote.

Mnaonyeshwa picha hamkupata kuziona hata siku moja.

Kujikinga na dhoruba hii mnakimbilia hoja ya "Udini."

Kuwa hii historia ilihujumiwa hili halipiti katika fikra zenu.

Laiti lingepita mngefahamu kuwa hawa waliokula njama kufuta historia ya kweli ya TANU walifanya hivyo katika kujaribu kuhami imani zao.
 
Invisible...
Ngoja nikuambie kitu.
Haiba ambayo Allah kaniumba nayo ni kuwa siwezi kumtisha mtu yeyote.
Hii mosi.

Pili hutanijua hadi umekaa na mimi kwa muda mrefu.
Sawa Bw. Moh'med... kwenye fasihi andishi unachoandika kinaweza leta mtizamo tofauti kwenye jamii na pia kwa mambo mengine madogo madogo ni ya kumalizia tumboni sababu vichwa vyetu wanaume vina mambo mengi zaidi kwa kadiri ya maagizo ya Allah.! Lingine hata kama ni Verified Member, bado watu hawawezi kuona jina wakakujua ni wewe sababu majina ya Mohamed Saidi ni mengi sana otherwise ungeambatanisha na picha (sema hapo umekuwa mjanja Shehe😀) kwa hiyo hata ikitokea mtu ka-reply kwa kejeli au dharau ni vigumu sana kujua mtu aliyejibiwa hivyo direct ni wewe otherwise umuambie mtu physically... kingine Amaizing, mimi pia ni Mohamed Said ingawa Said ni jina la Katikati, la mwisho sisemi😀
 
Sawa Bw. Moh'med... kwenye fasihi andishi unachoandika kinaweza leta mtizamo tofauti kwenye jamii na pia kwa mambo mengine madogo madogo ni ya kumalizia tumboni sababu vichwa vyetu wanaume vina mambo mengi zaidi kwa kadiri ya maagizo ya Allah.! Lingine hata kama ni Verified Member, bado watu hawawezi kuona jina wakakujua ni wewe sababu majina ya Mohamed Saidi ni mengi sana otherwise ungeambatanisha na picha (sema hapo umekuwa mjanja Shehe😀) kwa hiyo hata ikitokea mtu ka-reply kwa kejeli au dharau ni vigumu sana kujua mtu aliyejibiwa hivyo direct ni wewe otherwise umuambie mtu physically... kingine Amaizing, mimi pia ni Mohamed Said ingawa Said ni jina la Katikati, la mwisho sisemi😀
Invisible...
Inaelekea wewe si mwenyeji hapa barzani.
Hakuna asiyenijua kwa picha na sauti yangu:

 
Invisible...
Inaelekea wewe si mwenyeji hapa barzani.
Hakuna asiyenijua kwa picha na sauti yangu:


Hapa ni sasa mzee wa miaka 70.
Hapo ni 1992:

1656907145006.jpeg
 
JK,
Nashughulikia tafsir ya barua hiyo ya Mtwa Abdallah Mkwawa aliyoandika kwa herufi za Kiarabu.

ندانه لالی این بحالی کی جلوس
اجلها راجو الي سواه وسد الماء والسلام
مد وسلطان الو سے عورت
۱۳ ارل کی سنت ہو میرا دو اور دے دوں
جم الحفر بار علمی ادات التريق
وم تشریح کر جون الى الانوار
ست فجر
BARUA YA CHIFU MKWAWA / LETTER WRITTERN BY CHIEF MKWAWA
Barua iliyoandikwa na "Mtwa" kwa maandishi ya Kiarabu ikilalamikia Watemi wenzake Begere [Kilosa, Morogoro] Merere [Usangu, Mbeya] Kiwanga [Njombe] na Chabruma [Ruvuma] wakimsaliti na barua hii alimwandikia Lt. Engelhard.
The letter which was written by Chief Mkwawa by using Arabic language to complain about the fellow Chiefs Begere, Merere, Kiwanga and Chabruma who betrayed him and was addressed to Col. Engelhard.

Ningependa pia kukufahamisha kuwa Hassan bin Omar Mkunganya kaacha nyaraka nyingi alizoandika kwa herufi za Kiarabu.

Nyaraka hizi zimehifadhiwa Ujerumani.

Ukijaaliwa kupita Berlin fika Zentrum Moderner Orient (ZMO) utakuta mengi hapo katika historia ya Tanganyika.
Mzee je kuandika Kiarabu ndio Uislamu
 
Science,
Huku kwetu ukiona mtu anaweza kusoma Qur'an hiyo lazima na narudia lazima atakuwa Muislam.
Si lazima Mzee wangu, tena nakuhakikishia wakristo watawa wapo wengi tu wenye uwezo mkubwa wa kusoma Qur'an na kuitafsiri tena wameihifadhi kichwani sijui kifuwani but huo ndio ukweli wenyewe.

Kwa hili umepotoka.
 
Soma asili ya Tanu iliasisiwa na waislamu kwanza kama movement kilipokuwa ndo wakaanza ingiza wasomi wengine mfano Mwalimu Nyerere, waislamu wa pwani ndio walioleta UHURU wa nchi hii wao waliamua kumpa Mwalimu Nyerere ikiwa na maana ni msomi Ili aweze kuwaongoza wakiwa na lengo la kumdhibiti Mwalimu ambapo ikawa kinyume chake maana Mwalimu akaamua kuviunganisha vyama vyote maana vilikuwa na lengo moja la kudai UHURU ndipo ikazaliwa Tanu.
Huwezi kuja na hoja ya kijinga kiasi hiki kusema Waislamu wa Pwani. Hao waliogombania uhuru ni Waafrika. Nikuulize unahisi tulitawaliwa kwasababu ya dini ya uislamu au lah, je Waarabu walipokuwa wanafanya biashara ya utumwa walikua wanachukua Waafrika kisa sio Waislamu au? Mambo ya dini watu weupe hata hawajali inapokuja kuvuruga Mwafrika ndio maana mpaka leo hapo Saudia na arabia yote bado wanawatesa na kuwaua waafrika
 
Abdallah ni jina kiisilamu lililoandikwa Kiarabu.

Huwezi ukaitwa Abdallah ukawa Humuamini Allah.

Abd-Allah maana yake ni servant of Allah ama Mja wa Allah.
Hujui lolote kaa kimya, usidhani Mzee Mohamed Said hajaliona swali langu.
 
Mbona Hautumii jina lako la Ukoo
Sojo. ..
Sina kawaida hiyo natumia majina mawili.

Lakini naweza kwenda nyuma vizazi saba hadi Belgian Congo walipotoka babu na bibi zangu upande wa baba yangu.
 
Mohamed Said hua nasoma sana makala zako nikiri kwamba zimeongeza Jambo kwenye ubongo wangu hata nikipita baadhi ya sehemu hapa mjini hua navuta picha ya makala zako nikijurudisha enzi hizo. Nimefika Kalenga yule bwana mtoa historia ya Mtwa mkwawa mwenye jina refu kama treni alikuwepo. Mkwawa alikua ni Mwisilamu hilo sio hoja hata kidogo hata hiyo barua niliiona na tafsiri tulipewa. Na ni kweli Mkwawa alisilimishwa na Abushiri kama ulivosema hilo nakuunga mkono pasi na shaka wala hutakiwi kushupaza shingo kulitetea Mkwawa alikua ni mwisilamu na amefariki akiwa ndani ya uislamu. Pia hizi hoja ndogo ndogo ulitakiwa uzijibu bila kuzikwepa majina ni ya kiarabu na sio ya kiislamu ila dini ya kiislamu inatumia sana majina ya Kiarabu. Ukienda Iringa sio kila Issa unaekutana nae huko ni Mwislamu au sio kila Asha, Mudi, Said ni waislamu la hasha. Mimi ni mzaliwa wa Nyanda za juu kusini watu wanatoa tuu majina kwa sababu kalisikia yule anaitwa hivyo wala sio kwa sababu ni la kiislamu, labda siku hizi kidogo Uislamu umeingia sana kule. Na ni kweli asilimia kubwa ya wakazi wa mkoa wa Iringa na Njombe ni wa kristo lakini Mkwawa ali silimu hata ukoo wake mpaka leo ni Waislamu labda Mjerumani angechelewa kuingia kulikua na uwezekano mkubwa sana Uislamu kuenea kule. Kule wilayani kwangu hakujawahi kua na msikiti mpaka mwaka 2004 ndo msikiti wa kwanza ulijengwa tena na wafanyakazi wa Serikali wenye Imani ya Kiislamu ndo walijenga na Uislamu ukaannza kujulikana kule. Ndio maana nimesema hoja ya jina ulipaswa kujibu tu ni majina ya kiarabu kwa sababu ukiwaona wakristo waliopo mataifa ya uarabuni wakisali unaweza sema ni waislamu kwa sababu ya Lugha inayotumika. Kuhusu kuandika historia sijui ni nchi gani inayo andika histirua hiyo kwamba Nyerere alipigania uhuru wa Tanzania na alikua mkristo, au Nkuruma alipigania uhuru wa ghana na alikua mkristo,. Pia akaburi mengi kama sio yote kwa Iringa yale ya zamani yapo kama hili la mkwawa hata yale ya Njiani yaliyo kua yanazuia umeme kupita yanafanana na ya Kiislamu hivyo watu wanaweza wasielewe hoja kwa sababu hiyo. Lakini itoshe kusema mkwa ali Silimu lakini Jeshi lak hali kusilimu kwa kiasi hicho inawezekana wap waliobadili dini kutoka zile za asili kuja za ya Kiaramu kwa sababu Ukristo ulikua bado haujafika umekuja baada ya Mkwawa kuuwawa ndipo wamisionary wa kijerumani walipo jichia na mimi nilipozaliwa nikajikuta nipo kwenye Ukristo.
 
Si lazima Mzee wangu, tena nakuhakikishia wakristo watawa wapo wengi tu wenye uwezo mkubwa wa kusoma Qur'an na kuitafsiri tena wameihifadhi kichwani sijui kifuwani but huo ndio ukweli wenyewe.

Kwa hili umepotoka.
Matola
Kwa kawaida katika ujengaji wa hoja ili iwe hoja ya kukubalika katika mawanda ya kisomi unajenga hoja kutokana na "general rule," yaani lile la kawaida.

Hoja ya kisomi haijengwi kwenye, "exceptions," yaani yale nje ya kawaida.
Huo ndiyo mlango wa kuwatoa nje watawa.
 
Huwezi kuja na hoja ya kijinga kiasi hiki kusema Waislamu wa Pwani. Hao waliogombania uhuru ni Waafrika. Nikuulize unahisi tulitawaliwa kwasababu ya dini ya uislamu au lah, je Waarabu walipokuwa wanafanya biashara ya utumwa walikua wanachukua Waafrika kisa sio Waislamu au? Mambo ya dini watu weupe hata hawajali inapokuja kuvuruga Mwafrika ndio maana mpaka leo hapo Saudia na arabia yote bado wanawatesa na kuwaua waafrika
Ungesoma kwa utulivu ungeelewa.Kwani chama cha TAA na Afro shiraz vilivyokuja zaa TANU vilianzishwa na wabara.
Ungetofautisha uislamu na uarabu. Waarabu wapo wema na wabaya like other race zote kama wanatesa waafrika, wapo pia wengi tu wanawaneemesha waafrika pia, usijifungie kusikia habari za upande mmoja tu.
 
Ukoo wa Mkwawa upo..na sio waislamu....Sasa itakuwaje Mkwawa awe muislamu?.....Iringa waislamu ni wachache sana...kumejaa makanisa na wakristo kila kona
Sio kweli usitafanye kama hatujafika kalenga hizo barua zipo zimewekwa hapo museleum hio inaitwa Museleum tofautisha na museum barua hizo zipo za Kiswahili lakin zimeandikwa kwa herufi za kiarabu

Kusilimu machifu sio ajabu maana waarabu walikuwa wanaingiliana sana na huenda walikuwa wanavutiwa na zile ustaarabu.

Familia ipo mtwa wa sasa abdul dada yke yupo pale kalenga nyunba yao ipo labda iwe kuna wengine sio waislam maana kitanzania sasa hivi unakuta familia nying zina ndugu wakristo kwa waislam
 
Tuliofika iringa na tukaenda kufatilia historia ya mkawa mbona tunajua hilo alikua muislam
Watu tumefika kote huko mlambalasi,kikongoma kitanzin kote.na ukifika inafahamika
 
Sio kweli.usitafanye kama hatujafika kalenga.hizo barua zipo.zimewekwa hapo museleum.hio inaitwa Museleum.tofautisha na museum.barua hizo zipo za kiswahili lakin zimeandikwa kwa herufi za kiarabu
Kusilimu machifu sio ajabu maana waarabu walikuwa wanaingiliana sana na huenda walikuwa wanavutiwa na zile ustaarabu.
Familia ipo mtwa wa sasa abdul .dada yke yupo pale kalenga nyunba yao ipo.labda iwe kuna wengine sio waislam maana kitanzania sasa hiv unakuta familia nying zina ndugu wakristo kwa waislam.
Julai...
Hii si mara yangu ya kwanza kufika Kalenga.
Nakuomba utazame hapo chini angalia hapo Kalenga panaitwaje.

Baada ya Chief Mkwawa kujiua watoto wa kiume kumi waliwekwa kizuizini detention Dar es Salaam na wengine wanane walipelekwa Bagamoyo.

Watoto wawili walichukuliwa na kupelekwa Pugu Mission na majina yao ni Pancras na Boniface.

Hawa walibatizwa na kuwa Wakristo.

Kuna watoto wawili walibakia Kalenga nao ni Mkonowazi na Wanzali walibakia Kalenga kwa kuwa umri wao ulikuwa mdogo.

1657029240625.png
 
..Naweza kukubaliana na hilo.

..Je, hukubaliani na mimi kwamba warithi wa kiti cha Mkwawa ni Waislamu?
Machief dini waliokua nayo ndo wanaowatawala lazima wafuate, zile ni kingdom kama ungefuatilia kingdom nyingi dini ya mfalme ndo dini ya watu anaowatawala huwez enda kinyume na dini ya mfalme
 
Abdallah ni jina kiisilamu lililoandikwa Kiarabu.

Huwezi ukaitwa Abdallah ukawa Humuamini Allah.

Abd-Allah maana yake ni servant of Allah ama Mja wa Allah.
Kuna mtu anaitwa juma na mwingine maulid lakin ni wakristo unavyosema huwez ni sheria ipi inazuia mtu kuitwa abdalah na hawez kuwa mkristo acha upotoshaji
 
Back
Top Bottom