Hotuba nyingi za viongozi wa Afrika kwenye mkutano wa UN zimejaa malalamiko

Hotuba nyingi za viongozi wa Afrika kwenye mkutano wa UN zimejaa malalamiko

Viongozi wa nchi zote za dunia wanakutana Marekani kwenye mkutano mkuu wa Baraza la usalama la umoja wa mataifa (General Assembly of United Nations). Hotuba nyingi za viongozi kutoka Afrika ni za malalamiko kuhusu nchi za Magharibi na Marekani kama chanzo Chao kikuu Cha matatizo kwenye nchi zao. Hotuba nyingi za viongozi wetu ni kuhusu wazungu kutotimiza ahadi zao za kutoa mapesa kwa nchi za Afrika kugharimia miradi Yao, madeni makubwa wanayodaiwa na ukosefu wa masoko na technology.

Bahati mbaya sijamsikia kiongozi wetu hata mmoja akizungumzia shida wanazozisababisha wao wenyewe kama vile:
1. Kuiba kura kwenye chaguzi
2. Kung'ang'ania madarakani
3. Wizi wa mali za wananchi wao na ubadhilifu.
4. Matumizi mabaya ya mikopo wanayopewa.
5. Kushindwa kukusanya kodi
6. Rushwa kwenye nchi zao.
7. Viongozi kujiwekea kinga za kutokushitakiwa.

Bahati mbaya nchi za Magharibi wanayajua madhaifu yote ya viongozi wa Afrika, ndio maana wakati wa hotuba za viongozi kutoka Afrika Wazungu wengi wanapuuza na wanatoka nje.

Afrika hawana mshipa hata mmoja wa aibu, kazi Yao ni kuwanyooshea vidole nchi za Western na kusahau udhaifu wao kwanza.

Mfano, nani anawazuia nchi za Afrika kuuziana bidhaa wao kwa wao kwa kutumia fedha zao. Nani kawazuia waafrika kuondoa VISA kati ya nchi na nchi ili watu Waafrika wawe huru kwenda na kutoka nchi nyingine ya ya Africa kufanya kazi au biashara? Nani kawazuia waafrika wasilime chakula Chao? Nani kawazuia kukusanya kodi?

Watakwambia eti afrika ina demokrasia yake sio lazima ifanane na ya magharibi,upuuzi mtupu majizi yanataka kuendelea kunyonya wananchi wao huku yakijineemesha yenyewe viongozi wa afrika ni laana.
 
Viongozi wa nchi zote za dunia wanakutana Marekani kwenye mkutano mkuu wa Baraza la usalama la umoja wa mataifa (General Assembly of United Nations). Hotuba nyingi za viongozi kutoka Afrika ni za malalamiko kuhusu nchi za Magharibi na Marekani kama chanzo Chao kikuu Cha matatizo kwenye nchi zao. Hotuba nyingi za viongozi wetu ni kuhusu wazungu kutotimiza ahadi zao za kutoa mapesa kwa nchi za Afrika kugharimia miradi Yao, madeni makubwa wanayodaiwa na ukosefu wa masoko na technology.

Bahati mbaya sijamsikia kiongozi wetu hata mmoja akizungumzia shida wanazozisababisha wao wenyewe kama vile:
1. Kuiba kura kwenye chaguzi
2. Kung'ang'ania madarakani
3. Wizi wa mali za wananchi wao na ubadhilifu.
4. Matumizi mabaya ya mikopo wanayopewa.
5. Kushindwa kukusanya kodi
6. Rushwa kwenye nchi zao.
7. Viongozi kujiwekea kinga za kutokushitakiwa.

Bahati mbaya nchi za Magharibi wanayajua madhaifu yote ya viongozi wa Afrika, ndio maana wakati wa hotuba za viongozi kutoka Afrika Wazungu wengi wanapuuza na wanatoka nje.

Afrika hawana mshipa hata mmoja wa aibu, kazi Yao ni kuwanyooshea vidole nchi za Western na kusahau udhaifu wao kwanza.

Mfano, nani anawazuia nchi za Afrika kuuziana bidhaa wao kwa wao kwa kutumia fedha zao. Nani kawazuia waafrika kuondoa VISA kati ya nchi na nchi ili watu Waafrika wawe huru kwenda na kutoka nchi nyingine ya ya Africa kufanya kazi au biashara? Nani kawazuia waafrika wasilime chakula Chao? Nani kawazuia kukusanya kodi?
Inafikirisha sana kwa wenye Akili na wanaojali !! 🙏🙏
 
Suluhisho liko Afrika kwenyewe braza. Sasa hivi ni rahisi kwa mtanzania kuingia Uingereza kuliko kuingia Nigeria au Msumbiji na Angola. Kwanini wafrika watumie sarafu za wazungu kununua bidhaa kutoka nchi za Afrika? Kwanini kiongozi aibe kura ili asababishe watu kuzozana na kupigana wenyewe kwa wenyewe, kwanini kiongozi aende akajenge mahekalu yake binafsi kwa fedha za wananchi au za mikopo? Wazungu wanahusikaje na haya?
Na yote hayo uliyoyaeleza Wazungu wanayajua yanafanyika sana Afrika !!
Tukiwalalamikia wanatuzoom tu kisha wanacheeeeka !!
 
Ni kweli, lakini ndio tushindwe kabisa hata kusafisha mitaro yetu mitaani? ndio tushindwe kupangana kwenye maeneo tunakojenga makazi? Ndio tuwapatie kinga ya kutoshitakiwa viongozi wote wenye uwezo wa kutuibia rasilimali zetu? Ndio tushindwe kuwasimamia watu wetu kuvuna maji yanayopotea kwenye mapaa ya nyumba zao? Ndiyo tushindwe kuwalisha watu wetu?. Haya nayo yanahitaji pesa za kigeni?
Hata wakilalama vipi Wazungu wanawatazama tu maana Wazungu wanayajua yote yanayofanywa na hao wanaolalamika !!
 
Wazungu ndio chanzo cha matatizo bila kuwachukua utumwa babu zetu na kuchukua mali zetu Africa tulikuwa huru na tunajitegemea.
Wazungu ndio wanawapambania hao viongozi wabovu waendelee kukuaa madarakani na kusainishana nao mikataba ya kinyonyaji.
Angalia viongozi bora kutoka Africa waliishia wapi kama sio jela na kuuawa?
Viongozi wengi wanaingia madarakani kwa nia njema lakini wanatolewa relini na ukoloni mambo leo.

Wala wazungu si chanzo cha matatizo 100%.
Utumwa ilipata nguvu maana sisi waafrika tuliuzana wenyewe kwa wenyewe.
watawala wengi wa kiafrika walipewa zawadi na vitu. Mbali mbali na mtu mweupe ili kuwauza wenzao, tena wengine walisaidia kuwakamata waafrika wenzao.

Hili mpaka leo linaendelea, viongozi wa kiafrika wanaongeka, kupenda pesa za mtu mweupe na kutoa sadaka rasilimali za nchi

Mpaka hapo mtu mweusi atakapo gundua chanzo cha matatixo yake ni yeye mwenyewe, hakuna litalobadilika
 
Kagame ana akili nyingi sana kulko viongozi wengi wa Afrika, Rwanda iko kama Ulaya. Ona inavyofanya branding ya nchi yake duniani. Anadhamini hadi timu za ligi kuu ya Ulaya.
Jamaa kweli anajitahidi sana tena sana !!
 
Lawama zitabaki palepale kwa nchi za kibeberu, hawa jamaa huwa hawataki kiongozi wa Africa anayejielewa, ukiingia madarakani ukawa na msimamo mkali wa kizalendo watakuletea zengwe tu! Hasa wakiona unaleta maproject makubwa ya ukombozi wa Kiuchumi ujue kabisa roho yako umeiweka rehani au nchi yako itadhoofishwa na makundi ya kigaidi, au kuwekewa vikwazo vya kijinga kijinga tu. Kama unataka ku-transform nchi Yako jitoe sadaka kwaajili ya Nchi yako.

Ni sisi waafrika tumekosa msimamo tokea zamani. Viongozi wa hovyo tunao wapata ninsababu sisi wenyewe tunawaruhusu kwa jina la siasa.

Mtu mweupe anapata nguvu pale kiongozi wa nchi husika anapokuwa mtu wa tamaa ya mali na pesa. Wazungu kuonga kwao ni ishu ndogo

Walitokea akina sankara, lumumba wana harakati wa kweli. Nani aliwaua kama sio watu wao wa karibu ambao ni waafrika wenzetu?
 
Wala wazungu si chanzo cha matatizo 100%.
Utumwa ilipata nguvu maana sisi waafrika tuliuzana wenyewe kwa wenyewe.
watawala wengi wa kiafrika walipewa zawadi na vitu. Mbali mbali na mtu mweupe ili kuwauza wenzao, tena wengine walisaidia kuwakamata waafrika wenzao.

Hili mpaka leo linaendelea, viongozi wa kiafrika wanaongeka, kupenda pesa za mtu mweupe na kutoa sadaka rasilimali za nchi

Mpaka hapo mtu mweusi atakapo gundua chanzo cha matatixo yake ni yeye mwenyewe, hakuna litalobadilika
Nashangaa ninapomsikia mtu anasingizia umasikini wa Africa eti ni sababu ya utumwa ! Kwani huo utumwa ndio umewafunza watu ukwapuaji na ubadhirifu kwenye mali za Afrika. ??!!
Maisha ya fahari tunayoishi ni kwa sababu ya Utumwa ?!
 
Ni sisi waafrika tumekosa msimamo tokea zamani. Viongozi wa hovyo tunao wapata ninsababu sisi wenyewe tunawaruhusu kwa jina la siasa.

Mtu mweupe anapata nguvu pale kiongozi wa nchi husika anapokuwa mtu wa tamaa ya mali na pesa. Wazungu kuonga kwao ni ishu ndogo

Walitokea akina sankara, lumumba wana harakati wa kweli. Nani aliwaua kama sio watu wao wa karibu ambao ni waafrika wenzetu?
Kabisa !!
 
Ni kweli, lakini ndio tushindwe kabisa hata kusafisha mitaro yetu mitaani? ndio tushindwe kupangana kwenye maeneo tunakojenga makazi? Ndio tuwapatie kinga ya kutoshitakiwa viongozi wote wenye uwezo wa kutuibia rasilimali zetu? Ndio tushindwe kuwasimamia watu wetu kuvuna maji yanayopotea kwenye mapaa ya nyumba zao? Ndiyo tushindwe kuwalisha watu wetu?. Haya nayo yanahitaji pesa za kigeni?
Tutawasingizia sana wazungu mkuu wakati shida ni sisi wenyewe.
 
Nimeona Hadi hao wanajeshi kina doumbia wa guinea anasema democracy imekuwa msamiati kwao ,kwmab Africa swla la democracy haliwezekani analazimisha kuaminisha kuwa waafrica wanapazwa kuchagua njia Yao ya kujitawal na siyo hyo democracy ambayo imekuwa Ni utamaduni wa kimagharibi
Ndugu, hili neno ni la kweli kwa 100%, Democrats ni utamaduni wa kwao, ndiyo maana walipoiingiza kwenye nchi za kiarabu ambazo wao utamaduni wao wanaoongoza nchi zao kiimla na hawakua na shida yoyote, walipomezeshwa neno democrats wakapigana vibaya

Rejea pale Libya, walisukwa watu wachache na kulipwa pesa,kuhusu kumkataa Gaddafi kwamba ameongoza miaka mingi,kwamba wanatakiwa kudai demokrasia, walipojichanganya tu, mpaka leo wanajuta

Mtu awaye yote akitaka kujua demokrasia ni ngumu aende akai- apply nyumbani kwake akae ki-demokrasia na mke wake na watoto wake aone kitakacho tokea

Afrika ilitakiwa kua na taratibu zake zisizo ingiliwa maana haya mambo ya kuiga yamefeli pakubwa, we unafanya siasa watu wanagawana mapesa mengi kuendesha siasa ktk nchi ambazo hazina maji, madawa, umeme, barabara.. hamuoni kama huu ni ujinga mkubwa? Pesa za kuchimba maji watu wanaenda kununua magari wafanyie siasa, na lengo kubwa la kufanya hivi ni mzungu anajaribu kama Kuna watu wa chama fulani wako madarakani na wamewanyima dhahabu zao, Almasi zao, na baadhi ya wanacho taka kupora, basi wanaingia ku- support chama kingine ili kikifanikiwa wapitie hicho kukidhi matakwa yao, Democrats ni mtego mbaya na WA kishenzi sana hapa Africa.
 
Una hoja nzuri sana mkuu, ukweli ni kuwa hili bara linapuuzwa sana kwenye kila kitu, limegeuzwa eneo la majaribio ya chanjo na kuvunia rasilimali tu tena kwa bei sawa na bure.
Hakuna kitu kibaya kama kuwa tegemezi kwa mtu. Kama Afrika hatutaacha mentality ya kuwa bila kupewa msaada hatuwezi hatutoboi. Ni bora ya mkopo kuliko msaada.
 
Kwakweli hili jambo la kung'ang'ania kupima viwanja kwa ajili ya makazi tu ni miongoni mwa jambo linalonisikitisha sana. Kunasehemu nilinunua ekari kumi miaka Saba iliyopita na ilikuwa nje mji kabisa na hata Sasa ndio mji unasogea na bado hakujakuwa na watu wengi kivile. Cha kunishangaza wamekuja watu wa ardhi kwa ajili ya kurasimisha ardhi kwa wananchi ila wanachonikomalia ni kwamba hapo nilipo hawawezi kunipimia ardhi yote kama eneo la ufugali Wala kilimo na wanadai ni lazima nipime viwanja coz Hilo eneo sio rasmi kwa kilimo Wala ufugali Bali ni eneo la makazi. Kwakweli sijawaelewa naendelea kufuatilia kuujua ukweli na kiukweli wananishangaza sana.
Mitaala yetu ya elimu Ina kasoro nyingi sana. Wakoloni waliondoa SoMo la critical thinking kwenye mitaala waliyotuandikia. Elimu hii na jinsi ya kufikiria kwa kina ni muhimu sana. Mtoto wa kizungu wa darasa la 1 kama ukimpa pipi atakuuliza Kwanini unanipa "mimi", unataka nini kwangu. Ukimpa lift kwenye gari ataikataa mazima kama hakujui, akisikia sauti asiyoielewa anakimbia mbali na tukio. Hii ni kinyume na watoto wetu, watu wetu na hata viongozi wetu.
 
Ndugu, hili neno ni la kweli kwa 100%, Democrats ni utamaduni wa kwao, ndiyo maana walipoiingiza kwenye nchi za kiarabu ambazo wao utamaduni wao wanaoongoza nchi zao kiimla na hawakua na shida yoyote, walipomezeshwa neno democrats wakapigana vibaya

Rejea pale Libya, walisukwa watu wachache na kulipwa pesa,kuhusu kumkataa Gaddafi kwamba ameongoza miaka mingi,kwamba wanatakiwa kudai demokrasia, walipojichanganya tu, mpaka leo wanajuta

Mtu awaye yote akitaka kujua demokrasia ni ngumu aende akai- apply nyumbani kwake akae ki-demokrasia na mke wake na watoto wake aone kitakacho tokea

Afrika ilitakiwa kua na taratibu zake zisizo ingiliwa maana haya mambo ya kuiga yamefeli pakubwa, we unafanya siasa watu wanagawana mapesa mengi kuendesha siasa ktk nchi ambazo hazina maji, madawa, umeme, barabara.. hamuoni kama huu ni ujinga mkubwa? Pesa za kuchimba maji watu wanaenda kununua magari wafanyie siasa, na lengo kubwa la kufanya hivi ni mzungu anajaribu kama Kuna watu wa chama fulani wako madarakani na wamewanyima dhahabu zao, Almasi zao, na baadhi ya wanacho taka kupora, basi wanaingia ku- support chama kingine ili kikifanikiwa wapitie hicho kukidhi matakwa yao, Democrats ni mtego mbaya na WA kishenzi sana hapa Africa.
Afrika hatuna utamaduni wa demokrasia, hata malezi yetu hayana demokrasia, mtoto utalazimishwa kula, kunyamaza, kulala, kuswali, kwenda kanisani, kucheza mbali na wakubwa, kuvaa nguo inayokubalika kwenye familia, nk. Mama anachapwa na mtoto anachapwa. Demokrasia haiko majumbani haiwezi kuweko mitaani na kwenye taasisi.

Hebu ona kule mashuleni na vyuoni wasomi wetu wanakotoka je, Kuna demokrasia? Demokrasia haiwezi kuzuka TU ghafla kwenye Katiba ya nchi kwakuwa malezi ya viongozi wetu hayakuwa ya kidemokrasia.
 
Back
Top Bottom