Humphrey Polepole aelezea sababu za Kibeberu ya nchi moja kufunga ubalozi

Humphrey Polepole aelezea sababu za Kibeberu ya nchi moja kufunga ubalozi

Sidhani kama Scandinavian countries ziko kwenye group la mabeberu...hawa jamaa wamekuwa washirika wetu wa maendeleo tangu enzi za Mwalimu.

Polepole na chama chake waangalie walikokosea, hali ikiendelea namna hii basi yajayo ni machungu.
Watu wanajiropokea tu bila hata kujua historia za nchi hizo na ushirikiano tuliokuwa na nchi hizo. Hili ndilo tatizo la JF, kila mtu anafyatuka kivyake tu kadri anavyojisikia!
 
Nimesikiliza mpaka mwisho,sijaona alipoelezea sababu za nchi moja kufunga ubalozi wake,nafikiri hiyo ni majumuisho ya mleta Uzi,zaidi ameelezea kuhusu mifumo ya uporaji wa rasilimali za afrika,na umuhimu wa TZ na DRC katika uchumi na jamii duniani.
Geopolitical and strategic importance of TZ na DRC,
Ameelezea Tena kwa undani, hujasikiliza vizuri, watanzania tuna matatizo ya uvivu wa kusoma Sasa hata listening skills inaanza kuwa tatizo
 
Denmark pamoja na nchi za Nordic zimefanya mengi hapa nchini kimaendeleo.

Na hazikuwahi kutawala nchi yoyote kama koloni.

Hivyo kuwaita mabeberu si tu ujinga wa kukosa elimu bali ukosefu wa hekima kiujumla.
Mkuu 'Jidu', unajua huyu Polepole ni nani?
Binafsi ningependa kujua 'background' yake ikoje.

Ni watu kama huyu ndio wanaoshikilia sehemu muhimu zinazoendesha nchi yetu.

Inafaa kujua ni watu wa namna gani wanaofanya maamuzi muhimu ya nchi yetu , maamuzi yanayotugusa sote moja kwa moja.
 
Polepole Humphrey kumbe naye anaamini kuwa rasilimali za nchi lazima zilete Maendeleo ya Watu .

Parallel State iliyoongozwa na watu dizaini ya watu kama kina Gwaji , Ole Sabaya , Mayanga Construction company , wateuliwa wa awamu ya 5 ndiyo ilikuwa wanufaika na nafasi yao ya kimkakati ilipotea na walilia sana kulipotokea msiba wa kiongozi aliyekuwa anaendesha serikali na parallel state ya watu 'wasiojulikana' .

Ujenzi wa reli ya SGR usiokuwa na manufaa, wakati reli ya mkoloni ipo ikikarabatiwa sehemu korofi ingefaa na kufanya kazi ya ileile usafirishaji ni mkakati wa parallel state kujinufaisha kwa kutaka kupeleka madini na makinikia pwani ya bahari , mbali ya kuingiza nchi katika hasara kubwa kupitia mradi huu usio na tija ya reli ya SGR genge hili la watu waliokuwa karibu na uongozi walifaidika na wanaendelea kujinufaisha. Polepole anadai kuna kiongozi hivi karibuni amepambana kama Mwalimu Julius Nyerere alivyopambana wakati wake kwa serikali kuhodhi mashirika ya huduma za jamii n.k

Polepole Humphrey anasema asingependa kusema sana kwa sababu yeye pia Humphrey ni bado sehemu ya uongozi.

Nguvu za 'kibeberu' anazosema Polepole ni kwa kuwepo chama cha CCM , utulivu siyo amani, uongozi wa kimabavu n.k pia unawezesha mazingira ya uporaji wa madini, kuwepo mikataba mibovu ya siri, Bunge la uchama kimoja lisilo na meno ya kuhoji serikali, kuhoji mikataba ya madini / SGR reli/ Ndege za cash n.k

Yanayoendelea huko DR Congo, Humphrey Polepole anasema ni sawa na yanayoendelea Tanzania ila katika hali tofauti yaani Congo wanapambana kugombania ulaji kwa kutumia silaha na vita huku Tanzania wanatumia kuunda Bunge la chama kimoja, vitisho kwa kukamata na kusweka watu dani, kukaba demokrasia na kuzuia Maendeleo ya Watu kwa kakikundi kidogo cha wanaCCM kujinufaisha na kujimilikisha keki ya taifa.
Mkuu 'Bagamoyo', haya uliyoandika hapa ni mawazo yako, au una'paraphrase' aliyoyasema Polepole?

Ni vigumu sana kuamini kwamba Polepole atakuwa amejichanganya kiasi chote hiki!
 
Denmark na nchi za Scandinavia tofauti na kuipa masaada tena ya muhimu nchi hii.... walikuwa wanapata nini kutoka bongo?! Polepole anaona kama watu wote ni wajinga?!
 
Uchumi gani tulionao kuwatisha Denmark?

Polepole bado anaishi kwenye ndoto ya awamu iliyopita, "Tanzania donor country" akija kuamka usingizini aambiwe yule bosi wake alishafariki, miradi yake mingi bado inaendelea kuwapasua watu vichwa serikalini hawajui waikamilishe vipi.
Vieite
 
Denmark pamoja na nchi za Nordic zimefanya mengi hapa nchini kimaendeleo.

Na hazikuwahi kutawala nchi yoyote kama koloni.

Hivyo kuwaita mabeberu si tu ujinga wa kukosa elimu bali ukosefu wa hekima kiujumla.
Upo sahihi sana, nchi hizo zina miradi mingi sana ya kimaendeleo Tanzania mfano Denmark wana DANIDA, Norway wana hii wanaita NORAD na Sweden wana hii inaitwa SIDA pia.

These guys wana roho ya kipekee sana. Unakuta mijinga fulani inaongea pumba bila hata kujua lolote.
 
Ujinga mkubwa tulionao ni kuzani kuwa misaada wanayotoa hao jamaa ni free na wao hawana chochote cha kunufaika.
Mojawapo ya "Kunufaika" ni kuona misaada inayotolewa ikitoa manufaa yaliyolengwa kwa wanufaika. Kama ni kusomesha wataalamu katika nyanja fulani, wataalam hao wanapatikana na kulitumikia taifa lao.

Denmark na nchi za eneo lao huko haya yalikuwa malengo makubwa zaidi ya kunufaika na kuchota raslimali za Tanzania.

Kama wewe unajua manufaa waliyolenga Denmark katika kutoa misaada kwetu (Tanzania), tueleze nasi tujue.
 
wakati wa vita baridi. nchi zote za magharibi ziliisusa tanzania isipokuwa Denmark, waliendelea kuisaidia tz katika sekta mbalimbali hasa elimu na watu wakasoma bure. NI aibu kubwa serikali kupoteza mdau kama Denmark kisha mijitu mifala inakuja na analogy za kimalaya malaya
 
Hiyo ni nchi yenye wananchi wenye raha na furaha duniani
Hawana njaa
Pia wanaondoka China na Ofisi nyingine Spain
 
Huwezi ukawa na "misimamo ya kitaifa" halafu ukabaki kuwa ndani ya CCM iliyopo sasa! Huo ni unafiki usio na kifani.
Kama kwenye chama chako hawapo watu wenye mawazo huru usilazimishe na kwingine wasiwepo

Ccm wapo wengi sana, kuanzia kina mzee Warioba hadi kina Polepole.
 
Nimemsikiliza Humphrey Polepole, nimegundua ni kijana makini sana nchi yetu imewahi kumpata,

Ni msomi anayezingatia misingi, sio msomi njaa

Natamani aje kua Kiongozi mkubwa hapa nchini, atasaidia.
 
Mimi namfahamu nimeongea nae mara nyingi, hii ni hazina na naamini Rais Samia unasumbuka roho kama anafahamu uongozi kwa kutomtumia kama mwenezi wa CCM.
 
Back
Top Bottom