Huna Wajibu wa kumtunza au kumhudumia Mzazi wako akiwa chini ya miaka 60 kama haumwi

Kusaidia ni moyo kama huna utatumia visingizio vingi kama mleta uzi
 
Vita dhidi ya umasikini siyo nyepesi, inafaa wazazi na watoto kuungana bila kurudishana nyuma wala kutegeana kuupiga teke umasikini
 

Ungekuja na hoja Mkuu.
Hivi kwa nini Watanzania wengi mnashindwa kutetea hoja za upande mliopo?
 
Mkuu Robert,

Umri wa mzazi aliye chini ya miaka 60 hapaswi kuhudumiwa hiyo ni kwa mujibu wa sheria?

Na kuhusu miaka 18 mtoto anakuwa mtu mzima anaweza kujitegemea, ni kweli wazazi huwa wanawaacha? Ni watoto wangapi huanza kujitegemea katika umri huo haswa mjini?
 
Jambo la hekima hili
Ukisubiria hawa watoto uje uwategemee Kwa Kila kitu tegemea kugombana nao na wakati mwingine hata kuwatolea maneno ya laana.

Me najipanga ili nisije kuwa mzigo Kwa watoto.

Nataka niwe na viakiba vyangu ili hata ikitokea naumwa na nalazimika kwenda India/South Africa basi nisiwasumbue watoto zaidi ya kuwaomba sapoti ya wao kunipeleka lakini sio msaada wa Kiuchumi.
 
Mkuu Robert,

Umri wa mzazi aliye chini ya miaka 60 hapaswi kuhudumiwa hiyo ni kwa mujibu wa sheria?
Sheria za dunia na nchi haisemi popote kuwa unatakiwa umhudumie mzazi wako. Kumaanisha sio wajibu wa mtoto kumhudumia mzazi wake.
Kwenye dini hasa dini kongwe kama ukristo na Uyahudi. Hakuna sheria ya kumhudumia mzazi hata moja. Bali mzazi ndiye katika umri huo anatakiwa kutoa urithi kwa watoto.

Kiafrika, watoto ni watumwa wa wazazi. Kabla ya ujio wa wageni mtoto ni mtumwa wa mzazi wake.

Na kuhusu miaka 18 mtoto anakuwa mtu mzima anaweza kujitegemea, ni kweli wazazi huwa wanawaacha? Ni watoto wangapi huanza kujitegemea katika umri huo haswa mjini?

Mantiki ya andiko ni kuwa Wazee ndio UNAOWAJIBU wa kuwatunza na kuwahudumia.
Na watoto wadogo.
 
Ila maisha bhana, utakuta watu kama mtoa mada ukweni hata wakikohowa tu msaada ashafikisha haraka Sana ila Kwa wazazi wake mpaka awasimange kwanza
 

Na hiyo ndio Haki na Mungu anavyotaka ufanye.
Huna huwezi wa kumlaani yeyote kisa hakuhudumii na upo umri wa kujitegemea.
Biblia inasema amelaaniwa amtegemeaye mwanadamu. Tena mtoto wake.
 
Kuhudumia wazaz siyo hiari bwana ni wajibu wa mtoto km ilivyokuwa wajibu kwake ukiwa mdogo.
Twende kisheria mzazi asipo muhudumia mtotowake anashitakiwa sio! Je mzazi anaweza kumshitaki mtoto kwa kutomuhudumia?
 
Badilisha rangi uwe mzungu kama kila kitu cha kiuafrika unakiponda na nimeshakuona kwenye nyuzi nyingi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…