Hussein Bashe anastahili pongezi kwa namna anavyochapa kazi katika Wizara ya Kilimo na kutekeleza maelekezo ya Rais Samia

Hussein Bashe anastahili pongezi kwa namna anavyochapa kazi katika Wizara ya Kilimo na kutekeleza maelekezo ya Rais Samia

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Hussein Bashe hata kabla ya kuingia na kuteuliwa katika wizara hii alikuwa akisimama bungeni kuchangia katika wizara hii. Kila mtanzania alitamani na kuomba apewe uwaziri wa kilimo ili atekeleze kwa matendo yale azungumzayo. Hatimaye akaaminiwa na kupewa wizara. Kiukweli tangu amepewa tumeona namna wizara ilivyobadilika kiutendaji.

Ni mfuatiliaji mzuri juu ya kinachoendelea wizarani kwake na hata akisimama kuzungumza unajua na kuona kuwa anazo taarifa zote za wizara na anafuatilia utendaji kazi wizarani. Naona namna yeye na mama yetu Mh. Rais wanavyopambana kuhakikisha mwaka huu mbolea inapatikana kwa bei rafiki kwa kutoa ruzuku huku mkulima akiuza mazao yake kwa bei nzuri.

Hongera Sana Mh. Hussein Bashe, vijana tunakutegemea uendeleee kuchapa kazi ili kilimo kitunufaishe. Maana kilimo ni ajira na pumzi yetu, kilimo ndio usalama wa nchi, hivyo simamia vyema kulinda usalama wetu wa chakula na uchumi wetu. Maana kilimo ndio uti wa mgongo wa nchi yetu.

Asante, kazi iendeleeee! Baba yangu anasema wewe ni kama mzee Paul Kimiti alivyoitendea haki wizara hiyo.
 
Tumefuatilia bei hizo za mbolea kwa mkulima kweli ni nzuri, lakini ili mbolea ifike kwa mkulima zinapita kwa walioleta na kuziweka kwa mifuko;

1. Kuna mawakala mikoani
2. Kuna maduka ya pembejeo wilayani hadi vijijini

Je, wao watakuwa na bei za kununulia ili mkulima auziwe kwa bei hiyo elekezi?.
 
Tumefuatilia bei hizo za mbole kwa mkulima kwelu ni nzuri.lakini ili mbolea ifike kwa mkulima zinapita kwa walioleta na kuziweka kwa mifuko...
Naamini utaratibu utawekwa vizuri kwa kuwa sina mashaka na Mh. Hussein Bashe. Kama ulivyosikia Mh. Rais wetu akitoa maagizo katika kilele cha Nane Nane mkoani Mbeya kuwa kuanzia tar 15 mwez huu Wizara ya Fedha ihakikishe Inamaliza taratibu ili fedha za ruzuku zitolewe ili mkulima afanye maandalizi ya msimu mpya wa kilimo mapema zaidi.
 
Ni maagizo ama ni initiative zake mwenyewe !! Jamaa anafanya vizuri sababu kwa asili si mbatu ngozi nyeusi kama sisi - uchawa unatumaliza.
Maagizo ya Mh Rais wetu anayatekeleza vizuri lakini pia nimbunifu na mfuatiliaji mzuri, kwani huoni wengine Hadi Inafika wakati mh mama yetu kipenzi anatamka hadharani kuwa natoa maagizo kwa Mara ya mwisho ikimaanisha kuwa anakuwa alishatoa maagizo lakini hayajatekelezwa na wahusika, Tuendelee pia kumuunga mkono Waziri wetu na kumtia moyo na kwa sisi tusio na nafasi serikalini Basi tumshauri kupitia jukwaa Hili pale panapostahili, kazi iendelee.
 
Mapropaganda haya....

bashe is a useless guy....kujipromoti tu...na maneno kibaoo...he is not what he is claiming to be

I know sh1t when i see one!
Tusipende kuwakatisha Tamaa watu wanaojituma na kufanya kazi kwa bidii Kama mh Hussein Bashe, wewe kweli huwezi ukaona kazi kubwa anazofanya kweli.

Hapana ukweli lazima usemwe kuwa mh Hussein Bashe Ni mchapa kazi Sana, Tumtie moyo na kumpa faraja badala ya kumkatisha Tamaaa kwa kazi nzuri afanyazo wizarani, wamepita wengi hapo lakini mh Bashe viatu vya Wizara hiyo vimemtosha barabara.
 
Kongole kwake Sana. Huyu wazir kwakweli anajitahidi Sana na anatupa matumaini WANANCHI wake
 
Kongole kwake Sana. Huyu wazir kwakweli anajitahidi Sana na anatupa matumaini WANANCHI wake
Kabisaa mkuu, mh anafanya Sana kazi katika wizara hii, Hakika ni mchapa kazi Sana, Mtulivu, Anajuwa kujenga hoja vizuri, muungwana na mnyenyekevu Sana, Angalia alivyowaomba msamaha wakulima wa parachichi mkoani Mbeya, hivyo huyu ni kiongozi anayejishusha bila kujali cheo chake.
 
Tusipende kuwakatisha Tamaa watu wanaojituma na kufanya kazi kwa bidii Kama mh Hussein Bashe, wewe kweli huwezi ukaona kazi kubwa anazofanya kweli, Hapana ukweli lazima usemwe kuwa mh Hussein Bashe Ni mchapa kazi Sana, Tumtie moyo na kumpa faraja badala ya kumkatisha Tamaaa kwa kazi nzuri afanyazo wizarani, wamepita wengi hapo lakini mh Bashe viatu vya Wizara hiyo vimemtosha barabara.
Wewe umeona anachapa kazi well and good

Kuna mimi naona ni mavi matupu,well and good

Shida ni pale wewe unapolazimisha watu wafate unavyoona wewe...eti "tumpongeze"....mpongeze wewe!

Kikwangu mimi,Bashe ni mtu wa kujionesha na maneno mengi na kujifanya anajua sana vitu of which for the longest he has been given chances with nothing to show off.

Tatizo anajua kujipromoti mno kuliko anachoweza kufanya...useless kabisa

Mineno miiingiiii,sifa nyiiiiingi....we know his IQ is as low as the rest of us....katuzidi domo kubwa tu!
 
Wewe umeona anachapa kazi well and good

Kuna mimi naona ni mavi matupu,well and good...
Basi wewe itakuwa unachuki binafsi tu kwa mh Hussein Bashe, lakini Waziri huyu Ni migongoni mwa mawaziri Bora kabisa walio wahi kupita na kuhudumu katika wizara hii mbali na akina paul kimiti na Steven wasira.

Ameitendea haki Wizara hii, anajibu hoja kwa wakati, anakwenda kisasa na kutaka kilimo kiwe Cha kisasa kitakachokuwa na Tija.

kwa mkulima, Anataka kuona mkulima anafaidika na jasho lake
 
Hussein Bashe hata kabla ya kuingia na kuteuliwa katika Wizara hii alikuwa akisimama bungeni kuchangia katika Wizara hii, kila Mtanzania alitamani na kuomba apewe Uwaziri wa Kilimo ili atekeleze kwa matendo yale azungumzayo, hatimaye akàaminiwa na kupewa Wizara, kiukweli Tangia amepewa tumeona namna Wizara ilivyobadilika kiutendaji.

Ni mfuatiliaji mzuri juu ya kinachoendelea wizarani kwake na hata akisimama kuzungumza unajuwa na kuona kuwa anazo taarifa zote za Wizara na anafuatilia utendaji kazi wizarani, naona namna yeye na mama yetu mh Rais wanavyopambana kuhakikisha mwaka huu mbolea inapatikana kwa bei rafiki kwa kutoa Ruzuku huku mkulima akiuza mazao yake kwa Bei nzuri.

Hongera Sana Mh Hussein Bashe, vijana tunakutegemea uendeleee kuchapa kazi ili kilimo kitunufaishe maana kilimo ni ajira na pumzi yetu, kilimo ndio usalama wa nchi, hivyo simamia vyema kulinda usalama wetu wa chakula na uchumi wetu maana kilimo ndio uti wa mgongo wa nchi yetu, Asante kazi iendeleeee, Baba yangu anasema wewe ni kama mzee Paul kimiti alivyoitendea Haki Wizara hiyo.
Wewe ni bashe mwenyewe 😆
 
Basi wewe itakuwa unachuki binafsi tu kwa mh Hussein Bashe, lakini Waziri huyu Ni migongoni mwa mawaziri Bora kabisa walio wahi kupita na kuhudumu katika wizara hii mbali na akina paul kimiti na Steven wasira.

Ameitendea haki Wizara hii, anajibu hoja kwa wakati, anakwenda kisasa na kutaka kilimo kiwe Cha kisasa kitakachokuwa na Tija.

kwa mkulima, Anataka kuona mkulima anafaidika na jasho lake
Huyo Waziri wako "anamsaidia" nini Mkulima au mfugaji?

Maana naona unatumia neno "kusaidia" kimakosa!

Waziri ambae hajawahi kugusa jembe,waziri ambae hajui lolote kuhusu nini maana ya kuuza mazao ya mtu,waziri asiejua lolote kuhusu kukopa na kununua mbolea,waziri asiejua lolote jinsi ya mtu kupata ardhi,etc

Leo eti waziri huyo anajitia eti ni mesiah kaja kuwakomboa wakulima?

Yaani leo Bashe ndio awafundishe wakulima jinsi ya kulima na kufanya biashara ya kilimo?

Bashe anawapa kitu gani chochote cha bure?Hatoi hela,hatoi vifaa,hatoi ardhi,hajui lolote kuhusu kulima.....

Huo "msaada" unaosemea ni upi,hebu utaje!

Wewe ni Bashe,msomali mwenye domo kubwa kuliko wote...na self promotion!
 
Kabisaa mkuu, mh anafanya Sana kazi katika wizara hii, Hakika Ni mchapa kazi Sana, Mtulivu, Anajuwa kujenga hoja vizuri, muungwana na mnyenyekevu Sana, Angalia alivyowaomba msamaha wakulima wa parachichi mkoani Mbeya, hivyo huyu Ni kiongozi anayejishusha bila kujali cheo chake
Kweli mkuu
 
Zile billion Saba za Kilillmo naona wanapewa Wana CCM tu kama mlivyofanya kwenye sensa
Hakuna kitu Kama hicho mbona kwenye sensa watu wengi wamepata bila kuangalia vyama vyao, nafas zilikuwa chache tusingeweza sote kupata, waliopata wamepata na tuliokosa maisha lazima ya songe huku tuliendelea kusubiri kuhesabiwa na kuhamasisha wengine wahesabiwe kwa maendeleo ya Taifa letu
 
Mimi ni mwananchi wa kawaida,kwani wewe husomi jina langu hapo au wewe umeona limeandikwaje hapo
Wewe ni Bashe au Chawa wake....

Nashangaa unamgeuza kama ni mtu anaetoa vitu kabeba bure kwa wakulima kumbe yeye ni mpiga domo na mkwamishaji wakulima wanaotaka kuuza nje

Useless kabisa

Eti "nawasaidia",akasaidie familia yake..no one falls for that nonsense...hakuna msaada wowote kutoka kwa mwanasiasa yeyote on anything
 
Back
Top Bottom