Hussein Bashe, zuia mahindi kutoka nje kwanza nchi ijitosheleze

Hussein Bashe, zuia mahindi kutoka nje kwanza nchi ijitosheleze

Kwa nini sasa iwe lazima mkulima apangiwe wa kumuuzia mazao yake?
Mimi naona Serikali ingeruhusu soko huria kwa pande zote mbili! Yaani kwa wakulima wa ndani kuuza mazao yao nje ya nchi kwa bei nzuri!

Lakini pia wafanyabiashara wetu nao wangeruhusiwa kuingiza chakula chenye ubora ndani ya nchi, na kukiuza kwa bei nafuu.
 
Kama una familia ya kulisha nenda kalime. Usitegemee wengine wakulimie na wakuuzie wewe kwa bei unayotaka, nenda kalime na uuzie familia yako kwa bei unayotaka ama uwape bure.

Ulivyo taahira unataka mimi nilime kwa gharama zangu halafu wewe uje ununue kwa bei ndogo ukalishe familia yako, kalime uwalishe mwenyewe.

Nimelima mwenyewe kwa gharama zangu na nitauza mahala napotaka.

Familia yako inanihusu nini mimi? Walale njaa, wafe njaa mimi nahusikaje? Walikuja kunisaidia kupalilia?

Wakulima wauze wanapotaka kwa bei wanayotaka.
Ukweli mtupu.. Hawa wajinga ndio wanafanya kilimo kionekane cha watu masikini... Tunataka mahindi yote yatoke nje tupate hela turudi shamba... Sisi wakulima tunataka hilo
 
Ukweli mtupu.. Hawa wajinga ndio wanafanya kilimo kionekane cha watu masikini... Tunataka mahindi yote yatoke nje tupate hela turudi shamba... Sisi wakulima tunataka hilo
Hakuna shida hizo faida na makusanyo yanayopatikana kwenye kilimo zitumike kugharamia hizo sector pia na madeni yake serikali inayokopa.

Hela za watu wa mjini zitumike kutengeneza utajiri wa mijini pia kuna vijana wengi hayo mabillioni yanayoenda vijijini wangefaidika kama zingewekezwa kwenye viwanda wapate ajira; hiko chakula wakimudu.

Yaani wakulima wao wanajua kupokea tu, ubaya tunawalaumu watu wasiofaidika isipokuwa madalali wa chakula.
 
Unajua mahusiano yaliyopo kati ya hazina ya CHAKULA nchini na USALAMA wa Nchi?

Kama Kweli wakulima wanatosheleza soko la ndani, mbona hatuoni competition itayoleta unafuu wa Bei masokoni na ubora wa bidhaa Kutoka masokoni?
Bei ni nafuu mno wewe ndio huna hela... Haiwezekani Bia ununue ths 3000/= kwa chupa halafu kilo ya Unga unataka ununue kwa tsh900/=
Sisi wakulima tunataka watu waheshimu kilimo... Tunataka bei kubwa ya mazao bila kujali nani atakufa ndio interest yetu...
 
So uache uongeleee mambo mengine,au unaonea wivu wakulima,Kama unaumua mwambie mwenyekiti wako akupe muongozo Basi, jamaniiii,tuacheni tuu, wakulima
 
Ushauri wangu kwenu ni huu hapa; kama serikali inaruhusu wakulima/wafanyabiadhara kuuza chakula nje ya nchi kwa bei nzuri, basi iruhusu pia wafanyabiashara wengine kuingiza chakula nchini na kukiuza kwa bei nafuu.

Au unaonaje. Maana hakuna sababu ya haya malalamiko! Lakini pia kulazimisha Watanzania wote kuwa wakulima.

Hutaki kulazimishwa kulima sasa kwa nini unataka kulazimisha mkulima apangiwe pa kuuza?
 
Mimi naona Serikali ingeruhusu soko huria kwa pande zote mbili! Yaani kwa wakulima wa ndani kuuza mazao yao nje ya nchi kwa bei nzuri!

Lakini pia wafanyabiashara wetu nao wangeruhusiwa kuingiza chakula chenye ubora ndani ya nchi, na kukiuza kwa bei nafuu.

Sawa muhimu hapo mkulima hajapangiwa pa kuuza
 
Hutaki kulazimishwa kulima sasa kwa nini unataka kulazimisha mkulima apangiwe pa kuuza?
Mimi sijalazimisha mkulima kupangiwa pa kuuza. Mimi natamani kuona bei ya chakula ikiwa rafiki kwa mlaji. Hivyo naunga mkono wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi kwa bei nzuri.

Ila wakati huo huo Serikali iruhusu chakula kutoka nje, kuingizwa nchini na kuuzwa kwa bei nafuu na hivyo kupunguza mfumuko wa bei ya chakula nchini.
 
Muwe waelewa pia pale Serikali itakapofungua mipaka yake kuruhusu chakula kutoka nje, kuuzwa nchini. Maana na sisi ambao siyo wakulima, tunachoka kununua chakula kwa bei isiyo na uhalisia.
Wewe husiye lima unadhani bei yenye uhalisia ni kama bei gani
 
Tatizo akili zenu ni takataka unadhani mkenya akinunua 120k ndio uchumi wa mkulima unakuwa? Yaani ni kuhamisha tatizo unalitoa kwa mkulima mwezi huu kesho unalirudisha ... mkulima anauza 120k baada ya miezi mitatu mahindi yanarudi shamba kwa 150k kwa gunia umefanya nini kama sio akili matope.
Bro nenda kalime acha ujinga aisee...
 
Kwenye population ya 60 million Tanzanians. 30% sio wakulima na wanaishi mijini.

Hayo mazao ya shambani mengi yanauzwa magengeni hakuna cha VAT huko serikali aipati makusanyo ya hivyo.

Ilhali mpaka sasa huyo kichaa Bashe ameshapewa zaidi ya trillion moja kufanya upuuzi wake huko kwenye kilimo. Hiyo 30% ni sawa na 18 million people wakubwa na vichanga kwa wastani kila mtu kachangia tsh 55 elfu, hao wakulima waweze pata mbolea za ruzuku, Bashe afanye experiment za kipumbavu za kilimo.

Bado ujaweka mchango wa watu mijini kwenye kujenga hizo barabara zinazoenda mpaka kijijini na kuwafungulia masoko hao wakulima, mchango wao kufikishiwa umeme vijijini na mambo luluki.

Wanastahili zote kuangaliwa kwenye bei himilivu ya chakula; hizo hela zinazoenda huko azitoki mfukoni kwa baba yake Bashe ni kodi za watu wa mjini; bila ya wao hakuna mkulima wala watu wakwenda kununua hayo mazao.

Mkulima hana mchango wowote kwenye kodi ni kupe anaetegemea hela za walipa kodi mjini ili aishi; halafu mnasema watu wa majini hawana mchango kwa mkulima. Hizo sijui akili za wapi.
Huu ujinga ulimezeshwa na nani ndugu..
 
Mimi sijalazimisha mkulima kupangiwa pa kuuza. Mimi natamani kuona bei ya chakula ikiwa rafiki kwa mlaji. Hivyo naunga mkono wakulima kuuza mazao yao nje ya nchi kwa bei nzuri.

Ila wakati huo huo Serikali iruhusu chakula kutoka nje, kuingizwa nchini na kuuzwa kwa bei nafuu na hivyo kupunguza mfumuko wa bei ya chakula nchini.

Wa kuangalia maslahi ya wazo lako ni serikali na sio mkulima/wakulima mkuu
 
Back
Top Bottom