Huyu mhalifu wa Selander alipaswa kukamatwa, siyo kuuawa
Haya ni maoni yako ila tambua kuwa huyo jamaa alikuwa mobile siyo kuwa alikuwa kasimama tu. Ni lazima atakuwa na weledi mkubwa wa kutumia silaha hivyo lazima atakuwa na ana mafunzo kiasi ya kijeshi
Hakuna kitu kama hii, huyo jamaa alikuwa anaranda barabarani na kitambi chake. Polisi walifyatua risasi ovyo yani yeye asiye na mafunzo kaua wanne alafu wao wanazubaa nusu saa nzima
 
Tukio 1 tu limegeuza matukio mazuri maelfu na maelfu kuwa hakuna kitu na Askari kuonekana hawana maana.

Wapumzisheni Askari wetu jamani, siasa zenu za kipumbavu zisiwatoe hata ufahamu wa kuvukia barabara.
Wewe hata ufahamu wa kuvukia barabara nadhani huna. Kilichoandikwa kingine umeleta hoja mfu nyingine. Very stupidity at its best.
 
Halafu kuna taarifa za mashuhuda kuwa alijisalimisha still polisi wakampiga risasi.

Polisi wetu ni debe tupu kichwani kwa sababu Tanzania haijawahi kuwa na polisi wa wananchi tofauti na hawa polisi wa kuitumikia CCM ambao wamezoea mabavu ya kuiweka CCM madarakani na kuilinda isiangushwe kwa nguvu za uma.
 
Jamaa hana mafunzo makubwa. Askari wanaonekana kukosa weledi na woga kupita kiasi.

Jamaa alikuwa open wamepiga risasi zaidi ya 20 wakimkosa kihasara jamaa ambaye yupo open na polisi wapo zaidi ya 10. Wanakimbia kimbia tu.

Ni udhaifu yeye ambaye hana mafunzo makubwa kuwapora askari smg na kuendelea kuwatandika kuua wanne. Mtu mmoja wamejibishana naye kwa nusu saa nzima. Wangekuwa watatu na wenye uwezo mkubwa?

Kwa woga wa polisi walishindwa hata kum netraulize wampate akiwa hai kwa mahojiano. Wamempiga risasi kaangua badala ya kufanya utaratibu wa kumpata hai wanaendelea kumpiga risasi mtu ambaye tayari isnt a threat. Ni woga. Woga wa hali ya juu.

Inaonekana waliendelea hata kuimiminia risasi maiti huko mbele wakiwa hawaamini kama jamaa amefariki.

Huyu alipaswa akamatwe mzima. Angepigwa risasi miguuni au sehemu ambayo isingemlazimisha kufa. Then wange mchukua kumtibu na kuja mhoji awaeleze kisa na mkasa.

Polisi acheni kuwa mnaonea tu raia wasio na silaha. Huyu jamaa ndo alikuwa kipimo chenu tosha.
Keyboard expert.
 
usijitoe ufahamu kwani hao askari hawajaenda shule ? wanajua kila mbinu za kushambulia na kuuwa pale ilikuwa sio kuuwa ni kuhakikisha anapatikana akiwa hai labda iwe haiwezekani kupatikana hivyo. je kwa mazingira yale kulikuwa hakuna uwezekano wa kumkamata mzima? kwani walikuwepo askari wangapi kwenye tukio ? na je maadui walikuwa wangapi? lkn adui alikuwa mmoja na ameweza kuuwa watu wa4 na baadae akawa anatamba njia yote tena kweupeeeeee bila miwani... askari walikuwa wanaweza kwa asilimia 1000 kumkamata bila kumuuwa.
WAME
usijitoe ufahamu kwani hao askari hawajaenda shule ? wanajua kila mbinu za kushambulia na kuuwa pale ilikuwa sio kuuwa ni kuhakikisha anapatikana akiwa hai labda iwe haiwezekani kupatikana hivyo. je kwa mazingira yale kulikuwa hakuna uwezekano wa kumkamata mzima? kwani walikuwepo askari wangapi kwenye tukio ? na je maadui walikuwa wangapi? lkn adui alikuwa mmoja na ameweza kuuwa watu wa4 na baadae akawa anatamba njia yote tena kweupeeeeee bila miwani... askari walikuwa wanaweza kwa asilimia 1000 kumkamata bila kumuuwa.
WAMEPOTEZA USHAHIDI NA KESI ITABAKIA KUSUMBUA TU FAMILIA YA HUYO KIJANA MUUWAJI.
Mh ndugu taratibu.
Unatakiwa uangalie je Tz ni nchi ilopitia matokea haya mara ngapi na imezoelekaje mazingira yake?
Tz imezoeleka nchi ya amani ndugu na ndio maana hata tukio km la jana limesumbua kwasababu jeshi letu lime relax kulingana na hali ilokuwepo nchini.
Jiulize mbn USA walishindwa kumkamata Farah Somalia na wao walikua na jeshi kubwa well equiped?
 
TZ tuko wapumbavu wengi sana.

Askari wetu wale 14 waliofia vitani Sudan ktk kulinda amani walitukanwa mwanzo mwisho.

Polisi wa3 waliofia kwenye msafara wa viongozi kusini mwa TZ hivi karibuni waliogeshwa matusi mwanzo mwisho.

TRA wa5 waliofariki hivi karibuni halikadhalika walitukanwa kuwa ni waovu hata shetani anawaogopa.

TZ tupimwe akili maana siasa uchwara za mitandaoni zimetufanya tumekuwa wajinga hata hatuna mshikamano ktk mambo ya kitaifa.
Kuna tatizo kubwa sana kwenye vichwa vya Wabongo. Msongo wa mawazo ni tatizo kubwa na sehemu kama hizi hutumika kupunguza msongo.
 
Sijui ingekuaje Kama angeamua kudhuru na raia wa kawaida pale yangekua maafa yasiyomithilika hata kidogo...ila sisi watz wengi tu wajinga Sana.
 
Mh ndugu taratibu.
Unatakiwa uangalie je Tz ni nchi ilopitia matokea haya mara ngapi na imezoelekaje mazingira yake?
Tz imezoeleka nchi ya amani ndugu na ndio maana hata tukio km la jana limesumbua kwasababu jeshi letu lime relax kulingana na hali ilokuwepo nchini.
Jiulize mbn USA walishindwa kumkamata Farah Somalia na wao walikua na jeshi kubwa well equiped?
Kila mtu nyuma ya keyborad ni warrior,expert na kujua kila kitu.
 
Hivi police hawana masnaper mpaka wanalazimika kupambana na msomali kindezi ndezi namna ile
 
Hii ni taaluma ambayo sii yangu ila ningetegemea lengo kuu la police liwe kumweka chini ya ulinzi na sio kuuwa. Faida za arrest ni kubwa kuliko kuua. Alipojitokeza hadharani ilikuwa dalili za kutaka suluhu wangetumia weledi wao kumfanya asiwe madhara zaidi kwao na kumweka chini ya ulinzi. Wange mwambia weka silaha chini through vipaaza sauti sijui kama vilikuwepo hii ni mkujaribu kuweka mawasiliano. Wameuwa na kupiga maiti risasi za kutosha.
 
Wewe hata ufahamu wa kuvukia barabara nadhani huna. Kilichoandikwa kingine umeleta hoja mfu nyingine. Very stupidity at its best.
Kwa upumbavu wako unadhani ukiandika lugha ya utumwa ndiyo utaonekana una akili za kuvukia barabara?

Ungakaa kimya pia ungeonekana una hekima sababu ujuaji mwingi mbele giza.
 
TZ tuko wapumbavu wengi sana.

Askari wetu wale 14 waliofia vitani Sudan ktk kulinda amani walitukanwa mwanzo mwisho.

Polisi wa3 waliofia kwenye msafara wa viongozi kusini mwa TZ hivi karibuni waliogeshwa matusi mwanzo mwisho.

TRA wa5 waliofariki hivi karibuni halikadhalika walitukanwa kuwa ni waovu hata shetani anawaogopa.

TZ tupimwe akili maana siasa uchwara za mitandaoni zimetufanya tumekuwa wajinga hata hatuna mshikamano ktk mambo ya kitaifa.
Huwezi kupanda maharagwe ukatarajia kuvuna mahindi. Kama ungekuwa na akili ungejiuliza kwa umakini mkubwa zaidi chanzo cha chuki hiyo ni nini badala ya kubwabwaja tu kuwa watu ni 'wapumbavu'.
 
Kufa kwake inawezekana kabisa ni faida kubwa kwa wengine...marehemu always hana haki....
Kwa sasa kilichopo ni kusubiri kelele za mitandaoni zipoe na pengine inaweza kuundwa tume ya kiaina itakayokuja na mapendekezo kadha namna ya kuboresha utendaji wa jeshi letu!
Umeona eenhh??!! .Mimi nilifikiri ingekuwa busara km wangemjeruhi tu halafu awe chini ya ulinzi ili ahojiwe tuweze kupata undani wa Nini kilisababisha achukue uamuzi huo.
 
Nina mashaka na uwezo wako wa uelewa.

Uwanja wa vita kama ule jamaa anakuja na kushoot askari anapora bunduki anaanza kupiga kelele anadeal na askari ulitaka askari amkaribie na kumwambia "Hamza weka silaha chini bby wangu Hamza kibonge"

Ile ilikuwa vita ya niue au nikuue basi na polisi walichofanya si kosa. Unamtetea kuwa alinyosha mikono juu kivipi wakati ametoka kwenye kibanda na silaha yake.

Ulitaka polisi wamkimbilie amwage bongo zao utangaziwe polisi 24 wamefariki ufurahi?
Wewe ndo low IQ,huna ujualo Zaid ya ujinga na upumbavu tu umekujaa kichwani
 
Jamaa hana mafunzo makubwa. Askari wanaonekana kukosa weledi na woga kupita kiasi.

Jamaa alikuwa open wamepiga risasi zaidi ya 20 wakimkosa kihasara jamaa ambaye yupo open na polisi wapo zaidi ya 10. Wanakimbia kimbia tu.

Ni udhaifu yeye ambaye hana mafunzo makubwa kuwapora askari smg na kuendelea kuwatandika kuua wanne. Mtu mmoja wamejibishana naye kwa nusu saa nzima. Wangekuwa watatu na wenye uwezo mkubwa?

Kwa woga wa polisi walishindwa hata kum netraulize wampate akiwa hai kwa mahojiano. Wamempiga risasi kaangua badala ya kufanya utaratibu wa kumpata hai wanaendelea kumpiga risasi mtu ambaye tayari isnt a threat. Ni woga. Woga wa hali ya juu.

Inaonekana waliendelea hata kuimiminia risasi maiti huko mbele wakiwa hawaamini kama jamaa amefariki.

Huyu alipaswa akamatwe mzima. Angepigwa risasi miguuni au sehemu ambayo isingemlazimisha kufa. Then wange mchukua kumtibu na kuja mhoji awaeleze kisa na mkasa.

Polisi acheni kuwa mnaonea tu raia wasio na silaha. Huyu jamaa ndo alikuwa kipimo chenu tosha.
Sasa wakute kisutu kwenye kesi ya mbowe unaweza kufikiria swat wa usa,kumbe wapumbavu tu mikwara mingi hamza kawakalisha
 
Kila mtu nyuma ya keyborad ni warrior,expert na kujua kila kitu.
Wabongo hawanaga akili kabisa.
Nawashangaa sana.
Badala ya kuangalia vya maana wanaanza kukosoa ujinga.
Wamesahau kuwa polisi hao hao ndio waliweka hali shwari Kibiti na mpkn mwa Mtwara.Wameshasahau polisi hao hao ndio walioleta hali ya utulivu nchini.
Wanashindwa kupima tukio limetokea kwa mazingira gani na nchi yetu imezoea hali gani.
Hapa ndipo naelewa kwann Tz tuna safari ndefu ya maendeleo.
 
Jamaa hana mafunzo makubwa. Askari wanaonekana kukosa weledi na woga kupita kiasi.

Jamaa alikuwa open wamepiga risasi zaidi ya 20 wakimkosa kihasara jamaa ambaye yupo open na polisi wapo zaidi ya 10. Wanakimbia kimbia tu.

Ni udhaifu yeye ambaye hana mafunzo makubwa kuwapora askari smg na kuendelea kuwatandika kuua wanne. Mtu mmoja wamejibishana naye kwa nusu saa nzima. Wangekuwa watatu na wenye uwezo mkubwa?

Kwa woga wa polisi walishindwa hata kum netraulize wampate akiwa hai kwa mahojiano. Wamempiga risasi kaangua badala ya kufanya utaratibu wa kumpata hai wanaendelea kumpiga risasi mtu ambaye tayari isnt a threat. Ni woga. Woga wa hali ya juu.

Inaonekana waliendelea hata kuimiminia risasi maiti huko mbele wakiwa hawaamini kama jamaa amefariki.

Huyu alipaswa akamatwe mzima. Angepigwa risasi miguuni au sehemu ambayo isingemlazimisha kufa. Then wange mchukua kumtibu na kuja mhoji awaeleze kisa na mkasa.

Polisi acheni kuwa mnaonea tu raia wasio na silaha. Huyu jamaa ndo alikuwa kipimo chenu tosha.

Jamaa kawachangamsha kidogo[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom