Huyu mjamzito amenyanyaswa na wahudumu wa mwendokasi hapa Mbezi Mwisho mpaka akazimia

Yaani ulivoandika utafikiri wewe sio mtanzania. Mtanzania anashindwa kusimamia haki yake ndio ataweza kujitoa kwa ajili ya haki ya mtu mwingine?
 
Watu wote hao mmeshindwa kutoa hata msaada?
Mwendokasi nao siyo usafiri salama tena.
 
Duh!
 
Duh! 🤔🙄
 
Watu wa dar bhana kulalamika tu mitandaoni
 
Mimi,kuna kitu sijaelewa. Siku hizi, staff wa mwendokasi wanakuwa ndani!? Nijuavyo,ticket hutolewa kabla hata ya kuingia kwenye eneo la kusubilia gari. Huko si ndo walitakiwa wamalizane,kama mtoto analipiwa au anapewa msaada! Hiyo purukushani ya anapanda,hapandi, kwenye gari imefikafikaje huko!

Ila,binadamu pia tuwe waelewa upande mwingine. Ndo maana makonda wa daladala,japo wehu,lakini wana point. Huyo mtoto,ni mtu. Ikiulizwa gari ilikuwa na watu wangapi, na yeye anahesabika. Ikitokea ajari,familia yake itadai fidia kama amekufa,au matibabu kama kaumia. Lakini watu wengi utakuta ameobgozana na watoto,kisa nauli hawalipi. Siyo poa.

Kwenye kuzimia,hatujui ni kweli au si kweli. Lakini,mhudumu kakosa utu, na gari zima akakosekana mwenye 200? Af mtu anapiga picha tu! Anaona fahari?!
 
Kitu kimoja bado kinaleta utata: nauli za mwendokasi siku hizi,zinalipiwa mlangoni kwenye gari? Zinapopatikana tiketi,si ndo huko huko hili jambo lingeishia?
 
Hivi hii roho mbaya ya staff wa mwendokasi chanzo chake ni nini hasa? Kwanini wanakosa utu kabisa?!
 
Nauli anaanza lipia mtoto wa la kwanza.

Miaka 7 mtu hutakiwa kuanza la kwanza.

Miaka 5 au 6 kuanza la kwanza hii ni trend imevamiwa na wamama wa siku hizi.
Issue si umri,mtoto yeyote ni mtu. Mtoto anaetembea,anatakiwa alipe. Mwenye gari akipotezea,poa. Ila akichachamaa,ana hahi. Kuna nchi moja jirani,japo hawana namna wanapakiza,piki piki inabeba tu watu wawili,na bima yake ni watu 2. Sasa,tatizo linakujaga kwa wamama wenye watoto mgongoni. Ukimbeba,hilo ni kosa. Kwenye ajari,zinakuwepo,mahakamani bima haisimamii. Hapo nani mwenye kosa? Japo ni mtoto wa miezi! Mwendokasi nako au daladala,mtoto huyo anaongeza uzito na ulaji wa mafuta. Chochote lazima achangie sasa.
 
Ujinga mtupu yani wote hapo mlishindwa kumlipia au kumsaidia huyo Mama Tsh 200/= sasa hao wahudumu wana hela au tiketi za bure jamani mbona kama mnataka kuwaonea tuu? Hivi kundi lote hilo hamna mwenye akili hata mmoja? Kwenye hili nawatetea hao wahudumu!
 
Kwa uelewa wako ilipaswa apande nn
Ni swali ambalo nimekuuliza. Basi alipaswa akupande wewe. Yaani nyie madogo hamfikirii kabisa. Unashangaa mjamzito kupanda Udart. Unataka apande punda au ndege? Mtu ambaye ameshindwa mlipia mtoto wake tsh 200?nyie madogo miaka hii ndo maana mnabakwa sana na kulawitiwa. Hamna akili.
 
Wengi wanamlaumu mleta mada ila angeleta habari bila picha angesakamwa sana. Binadamu hawana jema.


Ni mpumbavu mwenzako, hatuna shida na picha zake au report, ila Je alisaidia chochote? Yani kaleta habari ina ukubwa kama Bwawa la nyerere wakati solution ilikuwa mikononi mwake, Jinga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…