Huyu mjamzito amenyanyaswa na wahudumu wa mwendokasi hapa Mbezi Mwisho mpaka akazimia

Endelea kupuyanga
 
Hamna mtu mpumbavu kama wewe uliyepiga picha badala ya kutoa 200/= kulipa nauli.

Wewe ndio sababu wanaume wengi tunaonekana hatujitambui.

Kwa hiyo umeleta huku upate sifa au umaarufu?

Hujitambui kabisa wewe
 
Shosti povu lako halimsaidii chochote huyo mjamzito. Keyboards warrior. Nyoo hujakazwa asubuh unaniletea hasira ya kukosa bao la kutokea mpuuzi kweli wewe
Ni mpumbavu mwenzako, hatuna shida na picha zake au report, ila Je alisaidia chochote? Yani kaleta habari ina ukubwa kama Bwawa la nyerere wakati solution ilikuwa mikononi mwake, Jinga
 
Hata kama maisha magumu Wazee, hata shilingi 300 ya kumlipia huyo Mtoto nauli mlishindwa kumlipia?

Kuna Siku nilimlipia nauli, Kijana mmoja aliyetakiwa kushushwa Pale Mikumi National park Kwa kuwa na nauli nusu.

Alikuwa anaelekea DSM kubahatisha kazi/vibarua.

Imagine Konda amekomaa kabisa kumshusha Hifadhini bila kujalia Usalama wa abiria wake maana pale Mikumi, Wanyama wakali ni nje nje 🙌

Wababa tuzaeni watoto ambao tutaweza kuwatunza na kuwahudumia.

Mke wako ni Mjamzito yupo na mtoto mdogo, umeshindwa hata kuwalipia Uber/bolt wasafiri Kwa uhakika?
 
Mwendokasi walikuwa sahihi kimaamuzi ila wangejaribu kumuomea huruma. Umaskini ni fedheha sana kwa kweli nimeangalia hizo picha
Wamuonee huruma halafu mje kulaumu kuwa Kuna ufisadi shirika halipati faida?
 
Ni sawa anaweza kukosa, je hao mapunguani walosimama wakimuangalia na huyu alowahi kupiga picha ili alete umbea humu alishindwa kumsaidia huyo mama?
Hapo waliosimama wote pembeni hawajitambui na wanafiki nauli ya mtoto ni 200/= tu.
Wote hawana?
Na huyu mpiga picha ndiye punguani namba moja
 
Wewe hujitambui acha kujitetea hapo usisingizie huduma mvivu.
Huo mradi unajiendesha yanatakiwa mafuta, service na pesa za kulipa wafanyakazi we unadhani wakisema msaada watu wangapi wanahitaji kusaidiwa?

Yaani mtu kudai nauli na kuzuia mtu kusafiri bila malipo unasema huduma mbovu.

Nyinyi mlioshindwa kumlipia hiyo nauli ndio wajinga na hamjitambui
 
Mdada wa watu mpaka anazimia mnamtazama tu...

Itoshe tu kusema nimewatukana wanaume wote mliokuwa ndani ya mwendokasi.
 
Imejidhihiirisha kiasi gani huyu jamaa ni mpumbavu angemlipia huyo dogo yote haya yasingetokea.
Anakimbilia kuchukua umbea na kuleta huku hizi tabia hata wanawake hawana sikuhizi.
Ndio maana wanasema sikuhizi wanaume tumewazidi wanawake kwa umbea sababu ya tabia za watu kama hawa
 
Pole kwake
Siku nyingine ingilia kati hata watu wachache tu.
 
Yaani ulivoandika utafikiri wewe sio mtanzania. Mtanzania anashindwa kusimamia haki yake ndio ataweza kujitoa kwa ajili ya haki ya mtu mwingine?
Kupanda gari Bure sio haki.
Angemlipia huyo dogo hiyo miatano
 
Hii nchi wajinga ni wengi badala ya kumlipia mtoto nauli kaenda kupiga picha.
Zaidi ya kuwadhalilisha unadhani Ina msaada gani?
Mleta maada zaidi ya umbea hana utu ni bora angekaa kimya tu
 
Naunga mkono hoja
 
Hapo ili kufupisha mambo alitakiwa atoke mtu amlipie
Nauli hyo mtoto,maana wakati mwingine hapo udart kuna wafanyakazi wendawazi wana eoho mbaya makatili,wpmbv kabisa

Ova
 
Baadhi ya watu wamekuwa wajinga sana! Badala ya kuchukua hatua unapiga picha, ili iweje? Huyo konda wa mwendokasi amewashinda nini midume mizima?

Pumbavu mpiga picha!
duuuh konda wa mwendokasi tena au hii ni mwendokasi za mikoani?
 
Nchi ipo mikononi mwa wanyama wasio na utu.

Roho hiyo imeambukiza hadi watendaji huku chini.

Siku kikilipuka ndo watagundua uzito wa neno TOO LATE
 
Amenishangaza sana huyu dogo. Alidhani tutamsifia kwa kukimbilia kupost huku. Angeonesha ana akili kama angemlipia huyo dogo na kumwepusha huyo dada ma fadhaa. Kisha angetoa taarifa. Kama hana pesa angalau angekuja hapa kupost akielezea jinsi ambavyo amemtia vibao huyo mhudumu wa udart kwa huo ujinga aliofanya
 
Kwenye ndege mtoto wa kuanzia umri gani analipia nauli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…