Huyu Wenje mbona anazidi kumuharibia Mbowe, kama amechangia 250M Mkutano Mkuu wa Taifa nani amechangia mikutano mikuu 64,000 ya misingi nchi nzima?

Huyu Wenje mbona anazidi kumuharibia Mbowe, kama amechangia 250M Mkutano Mkuu wa Taifa nani amechangia mikutano mikuu 64,000 ya misingi nchi nzima?

Wenje amemuonea sana Lisu, kunbuka chanzo ni Wenje kujipeleka nyumbani kwa lisu kwa nia mbaya ya kumdhoofisha kisiasa, lisu alipomshitukia wakaanza njama zinginezo za kumg’oa kwenye umakamu mwenyekiti, lakini kwa kuwa Lisu ana marafiki wengi ndani ya uongozi wa juu wakampa taarifa zote za njama za mbowe na Wenje, ndipo wakamshauri agombee uenyekiti kwa kuwa sasa mbowe na Wenje siyo watu wazuri kwake, ndipo Lisu akatangaza ghafra kwa kumshitukiza Mbowe kabla hajajipanga kumhujumu zaidi, baada ya kutangaza kuwania uenyekiti mbowe alipandwa na pressure kubwa hakupata usingizi akataka kufanya umafia kama aliomfanyia zito wangwe na sasa Heche lakini chawa wa mbowe ambao wana upendo wa moyoni na Lisu wakamtaarifu kila kitu ndipo Lisu akamwambia mbowe kuwa anajua kila kitu anachopanga juu yake Mbowe slammers, sasa anatumia pesa kuwanunua Wajumbe tu ili siku ya uchaguzi wamsaidie kupora ushindi wa lisu kwa njia za uchakachuaji tu
 
Wenje na mbowe wanakula pesa za chama kisha sasa wanajidai chama kinaomba michango ya nini? Pesa za chama zipo wapi?
 
Mbona Lissu amekuwa akichangiwa na mpaka naxCCM au hujui hata hela za kununua gari na za matibabu alichangiwa je ilikuwa rushwa?

Maamuzi ya kanati kuu unayaita maamuzi ya gizani inaonyesha huna uwezo wa kudadavua mambo ni ushabiki tu. Hivi baraza la mawaziri kwa mfano wakiamua au kujadili jambo huwa huku nje wananchi wanajua kilichozungumzwa. Basi nini maana ya vikao kama kila kinachozungumzwa katika kikao kiwe wazi kwa umma wote.

Hata Marekani wamemaliza uchaguzi majuzi mbona vyama vimechangiwa na matajiri? CCM wakitaka kufanya mkutano wao mkuu huea wanachangiwa na wafanyabiashara kwani hawana wanachama na vitegauchumi kibao.

Hujui namna ofisi zinavyoendeshwa shughuli ziinavyopangwa ambazo zinaweza kuwa katika horizon ya miaka 1, 5 au hata zaidi mfano dira ya taifa miaka 25.

Rudi jifunze namna ofisi zinavyoendeshwa. Wenzako sisi tumezeekea humo tukipanga kuanzia strategic plans, programme , projects,, budgets, action plans na kuchambua maandiko mbalimbali na kushauri .
HOJA #1: Yeye Tundu Lissu huchangiwa, Je, hiyo huwa ni rushwa...?

JIBU: Kwani wewe unaonaje? Si umesema huwa anachangiwa? Sasa inawezaje kuwa rushwa hiyo? Contrary na nyie mnaojiita "wajumbe wa kamati kuu", hizo mnazopangiana wewe Kigaila tafuta leta milioni 30, Yericko Nyerere 25, Mwenyekiti Freeman Mbowe leta milioni 250 nk nk. Kwani nyie mliomba wapi na lini hiyo michango? Kwanini kama ni michango huyu Freeman Mbowe hurudi na kuamuru arudishiwe zake kutoka kwenye pesa ya ruzuku au kwa kupora tu fedha za mapato mengine ya chama ikiwemo ya JOIN THE CHAIN..?

HOJA #2: Maamuzi ya Kamati kuu ya gizani? Naweza kuita uamuzi wa Baraza la mawaziri ni WA gizani?

JIBU: Absolutely, Yes.
Na nani kukuambia kuwa kamati kuu yenu yenye njaa ya pesa au Cabinet ktk serikali haiwezi ku - compromise na uchafu au rushwa na kisha kufanya maamuzi ya hovyo? Serikalini unakumbuka maamuzi ya mkataba wa bandari recently ambao nyie CHADEMA mliupinga? Kwanini mliupinga? Ni kwa sababu Kuna kila dalili kuwa watu wamehongwa kama ilivyo kwenye mikataba mingi mingine inayoleta shida hapa nchini sasa. Ndivyo ilivyo huko CHADEMA. Kiongozi wenu mkuu ameshanunuliwa kitambo na Mama Abdul na pesa hizo mnapewa huko..!

HOJA #3: Marekani wamemaliza uchaguzi juzi, vyama vilichangiwa na matajiri?

JIBU: Yes, vilichangiwa Kwa mujibu wa sheria zao walizojiwekea kuratibu uchangiaji huo. Na wenzenu kila Kitu kipo wazi na wakichangia matajiri hao hawarudi kwa mlango wa nyuma tena kuomba kurudishiwa pesa zao. Nyie huko CHADEMA mna uwazi huo? Matajiri gani wamechangia kwa hiari? Si umesema mmepangiana nyie wajumbe wa kamati kuu? Hiyo ni hiari au lazima? Na kwanini Freeman Mbowe hurudi kwa mlango wa nyuma tena kudai pesa zake alizochangia na nyie chama kimlipa sometimes deni likiwa inflated..?

HOJA #4: Sijui shughuli za chama zinavyoendeshwa kwa sababu zinaweza kuwa ktk horizon za miaka 1, 5 na hata 25

JIBU: Mngekuwa na mipango ya namna hiyo ingekuwa wazi kwa wanachama wote na msingeweza kukosa pesa ya kugharamia kikao cha Baraza kuu kimoja kwa mwaka. Kama imefikia mnapanua mikono kwa MAMA ABDUL na mwanae ABDUL kukubali awannunue, ni wazi kuwa hamna ushawishi tena kwa wanachama, wapenzi na mashabiki kina sisi ambao ndiyo tuna pesa bukubulu, daladala kwa ajili ya kukiendesha chama. Solution ni kufanya "overhauling" ya uongozi chini ya Freeman Mbowe na kuweka uongozi mpya Ili kurudisha trust na hope kwa wanachama, wapenzi na mashabiki pamoja na wafadhili salama wa chama. Chama kwa Sasa chini ya Freeman Mbowe kimeoza, hakiaminiki tena na ndiyo kinaanza kuji - associate na pesa chafu toka CCM. Mnauzwa.........!!

HOJA #5: Nirudi nikajifunze kwa sababu wewe umezeekea chamani ukiwa ni strategic planner, programmer , projects master, budgets, action plans na kuchambua maandiko mbalimbali na kushauri

JIBU: Duuh, Master Planner wa uchafu wa kufanya Hezekiah Wenje dalali wa rushwa za Abdul na mama Abdul a.ka Bi Samia Suluhu Hassan Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi? Really?

Kweli wewe Master Planner, Strategist na mshauri matata wa uangamivu wa chama chako...

Kwa heri usiku mwema...
 
Lissu ana madeni mengi anataka kutumia ruzuku ya chama kulipa madeni na kujinufaisha
 
View attachment 3189332
Kamanda Wenje mbona unazidi kumuanika na kumuharibia kabisa kamanda Mbowe,

Umesema CHADEMA hatuna pesa ni kweli hatuna lakini kwanini hatuna pesa?Jibu wahisani hawamwamini tena Mbowe.

Naomba unijubu maswali haya,

1. Je, mikutano mikuu yote ya misingi zaidi ya 64,274 nchi nzima ni Mbowe katoa pesa zake?

2. Je, mikutano mikuu yote ya matawi zaidi 16,602 ni Mbowe ametoa pesa zake?

3. Je, mikutano mikuu yote ya kata zaidi ya 3,956 ni Mbowe katoa Pesa zake?

4. Je, mikutano mikuu ya majimbo yote 264 katoa pesa Mbowe?

5. Je, mikutano mikuu ya Mikoa yote 31 ni Mbowe katoa Pesa zake?

6. Je, mikutano mikuu yote 10 ya Kanda za Chama ni Mbowe katoa Pesa zake?

7. Sasa Wenje, kama hawa wanachama waliogharamia mikutano mikuu yao yote tangu misingi mpaka Kanda wanashindwaje kujigharamia kwenye mkutano Mkuu wao huu maalum mmoja tu wa Taifa?

Mwisho, Mkutano Mkuu wa mwaka 2019 Mbowe aliichangia kiasi gani mbona hujasema??!!

Mbowe kwanini hakuchangia 2019 achangie 2024?!!

Hii TZS250M ni rushwa toka CCM


Hakuna namna Mbowe ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA lazima apishe akili mpya za kutafuta pesa sio kuchangisha wajumbe wa Kamati Kuu kwani hilo sio jukumu la mjumbe wa Kamati Kuu.


Mbowe kwani hana aibu?
 
Back
Top Bottom