Huyu Wenje mbona anazidi kumuharibia Mbowe, kama amechangia 250M Mkutano Mkuu wa Taifa nani amechangia mikutano mikuu 64,000 ya misingi nchi nzima?

Huyu Wenje mbona anazidi kumuharibia Mbowe, kama amechangia 250M Mkutano Mkuu wa Taifa nani amechangia mikutano mikuu 64,000 ya misingi nchi nzima?

Bajeti ya mkutano mkuu ni zaidi ya milioni 700? Hawa ukiwapa nchi wataitafuna kuliko CCM.
 
Mafisadi muda wenu umewadia kutuliza wenge.
Mbowe kila akichangia anaandika ni mkopo ruzuku ikija analipwa, hajawahi ku hangia bure kwani hulipwa hadi riba
Madeni feki bandia huiba pesa za chama kisha kutakatisha pesa kwa kujidai alikopesha chama, Mbowe ni mwizi kama wezi wengine
 
Hicho unachoita mpango kazi sio kuwa ninakifahamu bali maisha yangu yote ya kazi kuandaa mpango kazi ni sehemu ya kazi yangu kwa hiyo ninafahamu kuliko wewe unayekariri. Mpango kazi unaendana na bajeti na kila ngazi ya uongozi ina majukumu yake na bajet yake na mpango kazi wake.

Katika ngazi ya tawi, jimbo, wilaya pesa inayihitajika siyo kubwa kwa sababu hakuna mjumbe anayelipwa pesa ya malazi; mjumbe anakuja na kurudi nyumbani kwake. Pili uongozi wa ngazi hizo ni jukumu lake kugharimia uendeshaji wa ofisi kwa ngazi hiyo hata kama sehemu ya bajeti yake inatoka hq.

Suala la kuchangia si la lazima kwa mwanachama kwa sababu kwanza linategemea uwezo wa mwanachama na inategemea anavyoguswa.

Hiyo idadi ya wanachama inaweza kuwa sio sahihi na ilikuzwa makusudi au hata kama ni sahihi ni historical sio updated. Mtu anaweza xkuwa mwanachama wa chama fulani kisha kuacha kimya kimya.

Busara ya kawaida kama kamati kuu nzima imepotoka kama Lissu na nyie mnaomshabikia blindly mnavyoamini basi ufumbuzi ni kujitenga na kuanzisha chama chenu ili sasa kiyafanye hayo yaliyo sahihi. Hao mnaodai wananchi watawafuata huko mtakakoenda.

Haitatokea kamati kuu ikae kujadili jambo kwa kufuata maoni ya mtandaoni tena ya watu wenye poor reasoning.
Unatumia nguvu sana mkuu,

Mikutano 64,000 inaweza kugharimu kiasi gani Cha pesa?

Tumia akili kidogo.
 
Bajeti ya mkutano mkuu ni zaidi ya milioni 700? Hawa ukiwapa nchi wataitafuna kuliko CCM.
Ni mbinu ya mbowe kuiba pesa za chama kisha kutakatisha kupitia hivyo visingizio ndiyo maana mbowe hataki mtu mwingine awe mwenyekiti kwa sasa akihofia kuibua madudu yake ya ufisadi pesa za chadema
 
Unatumia nguvu sana mkuu,

Mikutano 64,000 inaweza kugharimu kiasi gani Cha pesa?

Tumia akili kidogo.
Chawa wa mbowe awali hawakuzoea haya ya sasa walizoea mbowe anapita bila kupingwa, safari hii wamepagawa sana
 
Madeni feki bandia huiba pesa za chama kisha kutakatisha pesa kwa kujidai alikopesha chama, Mbowe ni mwizi kama wezi wengine
Kambo baya zaidi, akipewa pesa na wafadhili akileta kqenye chama anajifanya amewapa mkopo.
Huyu ni dalali zaidi ya Wenje.
Sasa safu ya kifisadi imejipanga.
1. Mbowe
2. Makamu dalali Wenje
 
Mtasubiri sana meli huko Dodoma!
Mbowe ataiba kura atafanya uchakachuaji atapora ushindi wa Lisu na kuwa mwenyekiti haramu lakini atambue kuwa chadema inaenda kuwa kama NCCR TLP na CUF ya Lipumba, vinginevyo wampigie magoti lisu wamuombe msamaha awe mpole
 
View attachment 3189332
Kamanda Wenje mbona unazidi kumuanika na kumuharibia kabisa kamanda Mbowe,

Umesema CHADEMA hatuna pesa ni kweli hatuna lakini kwanini hatuna pesa?Jibu wahisani hawamwamini tena Mbowe.

Naomba unijubu maswali haya,

1. Je, mikutano mikuu yote ya misingi zaidi ya 64,274 nchi nzima ni Mbowe katoa pesa zake?

2. Je, mikutano mikuu yote ya matawi zaidi 16,602 ni Mbowe ametoa pesa zake?

3. Je, mikutano mikuu yote ya kata zaidi ya 3,956 ni Mbowe katoa Pesa zake?

4. Je, mikutano mikuu ya majimbo yote 264 katoa pesa Mbowe?

5. Je, mikutano mikuu ya Mikoa yote 31 ni Mbowe katoa Pesa zake?

6. Je, mikutano mikuu yote 10 ya Kanda za Chama ni Mbowe katoa Pesa zake?

7. Sasa Wenje, kama hawa wanachama waliogharamia mikutano mikuu yao yote tangu misingi mpaka Kanda wanashindwaje kujigharamia kwenye mkutano Mkuu wao huu maalum mmoja tu wa Taifa?

Mwisho, Mkutano Mkuu wa mwaka 2019 Mbowe aliichangia kiasi gani mbona hujasema??!!

Mbowe kwanini hakuchangia 2019 achangie 2024?!!

Hii TZS250M ni rushwa toka CCM


Hakuna namna Mbowe ataendelea kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA lazima apishe akili mpya za kutafuta pesa sio kuchangisha wajumbe wa Kamati Kuu kwani hilo sio jukumu la mjumbe wa Kamati Kuu.


Chadema inavuja aisee
 
Kambo baya zaidi, akipewa pesa na wafadhili akileta kqenye chama anajifanya amewapa mkopo.
Huyu ni dalali zaidi ya Wenje.
Sasa safu ya kifisadi imejipanga.
1. Mbowe
2. Makamu dalali Wenje
Hahaha hao wawili ni kikundi cha kigaidi ni mchwa ni watu waroho wachoyo wabinafsi na hata wakipora ushindi wa Lisu wakaingia kwenye Uongozi watagombana wenyewe kwa wenyewe kwani Mbowe ni mchoyo na wenje ni mrafi njaa Dalali, asipopewa pesa na mbowe watagombana au atafanya udalali mali za chama
 
Ccm wanahusila hapa niliangalia ukaribu wa nchimbi na lisu kuna jambo
 
Mbowe anautaka uenyekiti kwa gharama yeyote yupo tayari kuuza hata figo yake ili mradi awe mwenyekiti na lengo kuu ni kuficha ufisadi madudu yote aliyofanya ikiwemo Rushwa za ngono upendeleo viti maalumu, na mambo mengi ya hovyo, Mbowe anaishi kwa hofu kubwa sana, hakuzoea hii pressure kama ya sasa alikuwa akipita bila kupingwa chaguzi zote
 
Matokeo ya January yataonesha Either CDM kizidi kuwa chama kikuu cha Upinzani ama kigeuke kuwa NCCR-Mageuzi!
Endapo Mbowe atampora ushindi Lisu kwa njia haramu lazima chadema itadhoofika sana na kuwa kama vyama Dhoofu vya akina cheyo na wenzao
 
Back
Top Bottom