IGP Simon Sirro afanya mabadiliko madogo kwa Makamanda wa Polisi

IGP Simon Sirro afanya mabadiliko madogo kwa Makamanda wa Polisi

Mkuu Kilwa94 nimeuliza hivyo ili nijue ni nani hasa anaepanga wa kuu wa vituo hivya chini ndani ya wilaya.

Kuna mkuu wa kituo cha Mtibwa ni mpemba "mla urojo" aliletwa kituo hiki akitokea Zanzibar. Alibadilishana vituo na mkuu wa awali aitwae Zayumba.

Sasa tangu afike kituo hiki hakuna mabadiliko yoyote uharifu mtaani umerudi upya, vijana wetu wanaporwa pikipiki na kuuawa kikatiri, rushwa pale kituoni imekithiri mahabusu hawapati haki zao za msingi.
Mtu unakamatwa na kuswekwa rumande wiki nzima bila hata chukuliwa maelezo.
Kesi za vibaka ndo za kupelekwa mahakamani.

Ukiombwa rushwa ukatoa haraka dau linapanda hata mara tatu make unaonekana una hela nyingi.
Wafugaji wavaa mashuka ndo wahanga wakuu wa rushwa.

Tunaomba mamlaka za uteuzi na wanaopanga wakifumue kituo cha mtibwa.
Pale kuna polisi wawili Baraka na Dulla waondolewe haraka sana ndo wamemshika mkuu kwa hela ya rushwa.
Pale kituoni kwa wk wachukua rushwa hata zaidi ya mil30! Imagine hizo hela zinatoka kwa wakulima watu kipato cha chini.
Rushwa 30M kwa wik ?? Duh kweli noma
 
Just Google hivyo vyeo vipo tu But RCO (Regional Crimes Officer) kimsingi angepaswa kuwa na cheo cha kipolisi (rank) ya Assistant Commissioner of Police (ACP) then RPC (Regional Commander) at least angekuwa na cheo cha SACP ( Senior Assistant Commissioner of Police).

SSP ni Senior Superintendent of Police anakuwa na lishilingi mabegani Hawa wanakuwaga OCD wa wilaya nyingi ambazo hazina changamoto ya kipolisi.

Sasa SSP ambaye anapewa kuongoza wilaya kama OCD (Officer Commander of District) kiukweli kuwa sawa na RCO ambaye hawana tofauti sana na RPC sema sababu ya Chain of Command inabidi RPC ndio awe na Rank kubwa ya Usenior kamishna huwezi kumfananisha kwa rank wawe sawa na OCD.

Kama ndio hivyo, je staff officer atakuwa na rank gani? Polisi wananyima vyeo sana bila sababu. Mtu anapewa mkoa mzima unamuacha awaongoze SSP wenzie heshima ya kijeshi including proper chain of command inatoka wapi?

Yani ni sawa na RPC awe rank moja na RCO au Staff officer [emoji1745] hapo hakuna wa kumbabaisha mwenzake.

Note: RPC, RCO, OCD, OCS hizi ni administrative posts ambazo zinaongozwa na police wenye rank mbalimbali za kupishana kulingana na majukumu na chain of command.
Sasa mkuu si Kuna vyeo na utawala huyo OCD na RCO wakiwa cheo kimoja si bado bado RCO anakua juu ya OCD kutokana na nguvu ya utawala aliopewa na anaweza kutoa amri ambayo OCD akaitekeleza au wakiwa cheo kimoja huko polis hakuna kuheshimiana hta kma mmoja ndo mtawala? Nisaidie hapo maana bado natoka kapa sijaelewa
 
Sasa mkuu si Kuna vyeo na utawala huyo OCD na RCO wakiwa cheo kimoja si bado bado RCO anakua juu ya OCD kutokana na nguvu ya utawala aliopewa na anaweza kutoa amri ambayo OCD akaitekeleza au wakiwa cheo kimoja huko polis hakuna kuheshimiana hta kma mmoja ndo mtawala? Nisaidie hapo maana bado natoka kapa sijaelewa
Kwa jeshini sababu kila kitu ni amri, Cheo Cha kiutawala kinapaswa kuendana na rank ya juu pia.

Ni sawa ujiite baba lakini mkeo ndio anakulisha sijui utampa amri gani, I hope umenielewa.
 
Exactly

Kuna desturi ya kijeshi kuwa junior anapopanda cheo zaidi ya senior senior inatakiwa astaafu

Waitara alikuwa sahihi japo sina na uhakika na zile fununu kuwa alikataa kuongezewa muda
Hii chai hiiii
 
Huko mikoani weka viongozi ambao ni senior kwa wenzao ili akitoa amri hairusiwi Mara mbili watu wanatafutaga kama kuku Ila ukiweka wanaofanana vyeo wataanza kuangalia nani aliapishwa kabla ya mwenzake na hii ndio shida.

Maofisa wanaheshimiana pale makao makuu pekee sababu anayevaa kofia ni IGP pekee wengine wote walifika wanavua kofia ili kuondoa saluti kila wakati.
Jkt tuliambiwa anae vaa kofia ndo anapiga salute kwahiyo unamaanisha IGP ndo anakua anawapigia hao makamishna salute huku hao makamishna wakiwa hawapigi salute wanabana mikono tu? Sasa mbona inakua siyo adabu kwa mkulu wao? Au na ww uliskia?
 
Jkt tuliambiwa anae vaa kofia ndo anapiga salute kwahiyo unamaanisha IGP ndo anakua anawapigia hao makamishna salute huku hao makamishna wakiwa hawapigi salute wanabana mikono tu? Sasa mbona inakua siyo adabu kwa mkulu wao? Au na ww uliskia?
Mbona nimeandika kitu kunaeleweka tu. IGP husalimiwa kwa ujumla. Akiwa anatoka kiongozi aliye na cheo cha juu kwanaskari waliopo eneo analopita IGP yeye hutoa ishara kwamba mkuu anapita na kuweka askari wote sawa na yeye pekee atamsalimia mkuu then anatendelea na ishu zake.

Mfano, askari mmekaa au mnafanya mambo yenu na ikawa IGP anapita, fahamu lazima officer wa zamu anakuwepo pale makao kuhakikisha ulinzi na mambo mengine yanaendelea, atakapoona mkuu anatoka yeye atawajibika kusema kwa sauti "wote sawa" then wote mnakauka yeye lazima awe kwenye full uniform atampigia salute then akijibiwa kama hakuna maelekezo atawajambia "mwili legeza" then mnaendelea na ishu zenu.



Kumbuka IGP hazururi kwenye makorido kama askari wa chini kutumwa kila saa na kuzunguka katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku.

Hata hivyo ili kuepuka salute wao huvua kofia ili ukikutana na boss unakauka tu, kumbuka nae hawezi kukujibu kwa salute hata kama amevaa kofia sababu wewe anayekujibu haipo kwenye uniform kamili ya kupigiwa salute ya mkono Bali ya kukauka tu.

IGP anaweza kuingia ofisini akatoka Mara moja tu.
 
Exactly

Kuna desturi ya kijeshi kuwa junior anapopanda cheo zaidi ya senior senior inatakiwa astaafu

Waitara alikuwa sahihi japo sina na uhakika na zile fununu kuwa alikataa kuongezewa muda
Its ok, lakini kwenye level ya Mkoa huwa RPCs ndio Boss wa RCO.
 
Naunga mkono hoja. MaRCO wako chini ya DCI ambaye ni presidential appointment na mzigo mkubwa wa kazi za kipolisi ni kwenye makosa ya jinai hivyo sababu RCO kuwa chini ya RPC. Wawe kwenye level moja pamoja na rank.
Na ndio inatakiwa hivyo, ili kuwe na uwazi katika utendaji, na kuepusha miingiliano katika majukumu.
 
Just Google hivyo vyeo vipo tu But RCO (Regional Crimes Officer) kimsingi angepaswa kuwa na cheo cha kipolisi (rank) ya Assistant Commissioner of Police (ACP) then RPC (Regional Commander) at least angekuwa na cheo cha SACP ( Senior Assistant Commissioner of Police).

SSP ni Senior Superintendent of Police anakuwa na lishilingi mabegani Hawa wanakuwaga OCD wa wilaya nyingi ambazo hazina changamoto ya kipolisi.

Sasa SSP ambaye anapewa kuongoza wilaya kama OCD (Officer Commander of District) kiukweli kuwa sawa na RCO ambaye hawana tofauti sana na RPC sema sababu ya Chain of Command inabidi RPC ndio awe na Rank kubwa ya Usenior kamishna huwezi kumfananisha kwa rank wawe sawa na OCD.

Kama ndio hivyo, je staff officer atakuwa na rank gani? Polisi wananyima vyeo sana bila sababu. Mtu anapewa mkoa mzima unamuacha awaongoze SSP wenzie heshima ya kijeshi including proper chain of command inatoka wapi?

Yani ni sawa na RPC awe rank moja na RCO au Staff officer 🤷 hapo hakuna wa kumbabaisha mwenzake.

Note: RPC, RCO, OCD, OCS hizi ni administrative posts ambazo zinaongozwa na police wenye rank mbalimbali za kupishana kulingana na majukumu na chain of command.
Kuna watu mmebobea aisee, Hongera zenu.
Nadhan nahitaji kukusoma mara mbili mbili nikuelewe zaidi
 
Kuna watu mmebobea aisee, Hongera zenu.
Nadhan nahitaji kukusoma mara mbili mbili nikuelewe zaidi
Staff officer ndiye hasa nayatakiwa kuwa sawa kicheo na RPC, au ampite cheo kimoja.
 
Mbona nimeandika kitu kunaeleweka tu. IGP husalimiwa kwa ujumla. Akiwa anatoka kiongozi aliye na cheo cha juu kwanaskari waliopo eneo analopita IGP yeye hutoa ishara kwamba mkuu anapita na kuweka askari wote sawa na yeye pekee atamsalimia mkuu then anatendelea na ishu zake.

Mfano, askari mmekaa au mnafanya mambo yenu na ikawa IGP anapita, fahamu lazima officer wa zamu anakuwepo pale makao kuhakikisha ulinzi na mambo mengine yanaendelea, atakapoona mkuu anatoka yeye atawajibika kusema kwa sauti "wote sawa" then wote mnakauka yeye lazima awe kwenye full uniform atampigia salute then akijibiwa kama hakuna maelekezo atawajambia "mwili legeza" then mnaendelea na ishu zenu.



Kumbuka IGP hazururi kwenye makorido kama askari wa chini kutumwa kila saa na kuzunguka katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku.

Hata hivyo ili kuepuka salute wao huvua kofia ili ukikutana na boss unakauka tu, kumbuka nae hawezi kukujibu kwa salute hata kama amevaa kofia sababu wewe anayekujibu haipo kwenye uniform kamili ya kupigiwa salute ya mkono Bali ya kukauka tu.

IGP anaweza kuingia ofisini akatoka Mara moja tu.
Mkuu askari hata awe na cheo Cha CDF akikutana na askari alie vaa kiraia na akambania mikono yule CDF ikiwa anamtambua yule alie bana mikono ni askar na anauhakika kuwa ni askari Kama CDF yupo kweny full unform itambidi apige salute huku askar akiwa kabana mikono hata akiwa ni private hana cheo chochote
Hiyo ndo sheria ya salute ilivyo na siyo kweli kuwa IGP akiwa kwenye full unform hatapiga salute akiwa anasalimiwa na mtu ambae hyupo kwenye full unform kwanza askari ukivaa unform mbele ya mkubwa wako huruhusiwi kukaa bila kuvaa kofia ukimuona tu ni lazima uvae kofia hata kama ulikua umevua
Ukipitia JKT hiv vtu utavijua tu huwa wanaelekeza
 
Mkuu askari hata awe na cheo Cha CDF akikutana na askari alie vaa kiraia na akambania mikono yule CDF ikiwa anamtambua yule alie bana mikono ni askar na anauhakika kuwa ni askari Kama CDF yupo kweny full unform itambidi apige salute huku askar akiwa kabana mikono hata akiwa ni private hana cheo chochote
Hiyo ndo sheria ya salute ilivyo na siyo kweli kuwa IGP akiwa kwenye full unform hatapiga salute akiwa anasalimiwa na mtu ambae hyupo kwenye full unform kwanza askari ukivaa unform mbele ya mkubwa wako huruhusiwi kukaa bila kuvaa kofia ukimuona tu ni lazima uvae kofia hata kama ulikua umevua
Ukipitia JKT hiv vtu utavijua tu huwa wanaelekeza
Unazidi kuongelea JKT sisi tupo makazini tunakueleza yanayofanyika achana na nadharia.

Ukikaa makao makuu utaelewa ni utaratibu unaoeleweka sasa we sababu unataka kuleta JKT yako basi sawa.

Tuliofanya kazi muda mrefu wanaelewa. Yani siku nzima hautafanya kazi sababu ya nadharia zako utaishia kupiga saluti maana pale wakubwa kila Idara, utadhangaa wanakuambia askari relax.

Wakikuona unaleta ujkt wako watakusaidia kulainisha maisha yako ili ufanye kazi.

Salute sio kazi mzee, kazi ipo makao ni ofisi tupu mafaili yanazunguka na vikao tupu sasa salute zako zitakupotezea muda na watabaki wanakuangalia tu, acha nidhamu ya uoga wakubwa wanaangaliaga pia mazingira ukileta sana nidhamu za uoga utakuja kuishia kuwa RSM
 
Unazidi kuongelea JKT sisi tupo makazini tunakueleza yanayofanyika achana na nadharia.

Ukikaa makao makuu utaelewa ni utaratibu unaoeleweka sasa we sababu unataka kuleta JKT yako basi sawa.

Tuliofanya kazi muda mrefu wanaelewa. Yani siku nzima hautafanya kazi sababu ya nadharia zako utaishia kupiga saluti maana pale wakubwa kila Idara, utadhangaa wanakuambia askari relax.

Wakikuona unaleta ujkt wako watakusaidia kulainisha maisha yako ili ufanye kazi.

Salute sio kazi mzee, kazi ipo makao ni ofisi tupu mafaili yanazunguka na vikao tupu sasa salute zako zitakupotezea muda na watabaki wanakuangalia tu, acha nidhamu ya uoga wakubwa wanaangaliaga pia mazingira ukileta sana nidhamu za uoga utakuja kuishia kuwa RSM
Alafu huko jkt alikaa mwezi mmoja[emoji23]mara nyingine ni bora kukaa kimya na kujifunza tu.
 
Alafu huko jkt alikaa mwezi mmoja[emoji23]mara nyingine ni bora kukaa kimya na kujifunza tu.
Yani amekomaa na saluti as if ni ishu sana. Hili ni tatizo la mitaala ya kozi za kuruta wanaammbiwa saluti kila saa na smart area uwe mkakamavu wakati ukishakuwa askari smart area unakatiza tu sio ishu.

Yani kwa makao wanaopata shida ni walinzi getini na askari kiongozi wa zamu hao muda wote lazima kuwa na silaha na full uniform na Beret iwe kichwani.

Wengine sasa haipo kwenye Vita upo ofisini tu unaanza kuvaa kofia masaa yote aisee 😃😃😃😃 hajapata kukutana na ofisi za wakubwa achana na huko vituo vya polisi unakuta mwenye nyota ni mkuu wa kituo pekee au na msaidizi wengine ni NCO tu. Huko juu kukutana na manyota ni kawaida na yapo kibao maana ndio maeneo yao wasomi na watawala wa jeshini.

Kule kuna maofisa huku chini kuna askari. Maofisa hawanaga mambo mengi ya kinoko although wanaona mwenendo wa askari.
 
Its ok, lakini kwenye level ya Mkoa huwa RPCs ndio Boss wa RCO.
Ni dhahiri kwamba polisi kwa sasa wanapaswa kutenganishwa zaidi kama ilivyokuwa zamani kwenye kuendesha mashtaka mpaka walipoondolewa hiyo power.

Hii ya kuchunguza pia waondolewe iwe no Agency inayojitegemea ili haki itendeke.

Mtu anayekukamata ndio anakupeleleza hii sio sawa anaweza kuamua kukuwekea ushahidi wa kubambikia ilimradi akukomeshe tu.

Anayepeleleza jinai watoke kwa DCI na wasiingiliane kiutawala kabisa. Anayekamata alete ushahidi, anayechunguza adhibitishe kama kuna kosa na huo ushahidi ni wa kweli then wapeleke kwa DPP ili apeleke mahakamani.

Hapo kila mmoja atakuwa na sehemu yake ya utendaji na itakuwa rahisi sana kujua nani hafanyi kazi kwa haki.

Hapa karibuni kulikuwa na malalamiko mengi sana kwamba DPP hatendi haki Mahakamani jambo ambalo sio la kweli.

DPP huletewa ushahidi na polisi waliomkamata mtu wanayemtuhumu ni muhalifu. DPP kazi yake ni kwenda mahakamani kusimama kwa niaba ya Jamhuri Ila yeye hahusiki popote zaidi ya kuletewa malalamiko na mtuhumiwa aliyekamatwa na polisi.

Naelewa itatengeneza gharama katika kufungua ofisi za public investigation kila mkoa na wilaya Ila ili tuweze kutengeneza misingi ya haki ni bora kuwaachia wahalifu 100 kuliko kumfunga mwenye haki mmoja tu kwa uzembe .

Na wakifungua hizi ofisi za public investigation pia waruhusu private investigation ili kuwa na option ya upelelezi sio kutegemea polisi pekee ambao nao wanaweza kukwama kwa sababu mbalimbali.
 
Back
Top Bottom