IGP Sirro: CHADEMA wanamuona Mbowe Malaika hawezi kosea, ushahidi tunao

IGP Sirro: CHADEMA wanamuona Mbowe Malaika hawezi kosea, ushahidi tunao

Labdakama hukumsikiliza amesema maandamano ya amani ambayo yanaruhusiwa kisheria sasa achunge nini Kwani kwenye nchi za demokrasia kuandamana sasa limekuwa kosa la jinai nani amewahi kufungwa kwa kosa la kuandamana hebu tusifanywe wajinga.
Kuandamana mahakamani. ...???basi tangulia mbele uongoze wengine wakufuate
 
We wachuuze tu wenzio wakati wewe utakuwepo mahakamani kwa kutmia mitandao wenzio wakapondwe pondwe wavunjwe miguu keshoyake uje tena kuwapa pole na kulaumu polisi sana
Kwani sheria gani ya nchi hii inayosema kwamba watu wakiandamana adhabu ni kupigwa na police?

Au mmezoea tu kuvunja sheria?

Halafu tangu lini maandamano ya amani yakawa uvunjifu wa sheria? Mbona katiba imeweka wazi haki ya kuandamana?
 
We wachuuze tu wenzio wakati wewe utakuwepo mahakamani kwa kutmia mitandao wenzio wakapondwe pondwe wavunjwe miguu keshoyake uje tena kuwapa pole na kulaumu polisi sana
Mimi sio mwanachama wa chama wa chama chochote cha siasa ila sipendi uonevu kwa raia.

Pia wapo watu waliokuwa wakiongea jeuri wakiwa madarakani wakiamini jeshi lao lipo imara kuwashughulikia raia pasipo makosa ila raia walipochoka kilichofuata hao hao viongozi wa juu walitoroka wakiwa wamevalia mabaibui kukwepa kisasi kutoka kwa wananchi waliochafukwa.
 
Kitu pekee Polisi wa kitanzania hawajawahi kudanganya ni wakisema watakupiga mpaka uchakae.Hakika utachakaa
 
Ahsante sana IGP kwa maelezo na makatazo, wenye akili tumekuelewa vizuri sana.

Tuache kufuata upepo kamwe tusiburuzwe, tuheshimu sheria pamoja na vyombo vinavyo simamia sheria.

Katibu Mkuu wa Chadema Mnyika na Mrema naamini wamepata ujumbe na watautekeleza.
Naomba kueleweshwa kwa mujibu wa sheria ni wapi kuandamana kumepewa jina la uvunjifu wa amani?

Naomba kifungu cha sheria kinachotaja maandamano kama uvunjifu wa sheria.Nijuavyo maandamano ni haki ya raia kueleza masahibu au uungaji mkono jambo fulani.
 
Kwamba Mbowe alipanga kufanya Ugaidi bila kumshirikisha kiongozi yeyote wa Chadema?
 
Hili jeshi naona wamekosa kazi ya kufanya tangu kuisha kwa kagera war

Kama wanajiona wanajimudu kiuwezo, yaani wana mafunzo ya kutosha si angalau hata waende hapo Cabo Delgado au Somalia, wakapimane nguvu na wenye silaha wenzao, sisi CDM hatuna hata panga
 
Hii ndio Tanzania
IMG_20210731_105235.jpg
 
Wewe Siro kama kweli unamjua Yesu tuambie nani alimpiga Lissu risasi na ni kweli askari wako walisimamia haki ktk uchaguzi ulopita?

Kama Mbowe ni gaidi basi we ni gaidi mara alf moja ya Mbowe kwa yale unayoyasimamia.

Huna haki ya kulitaja jina la Yesu katika mambo yako ya kishetani...

Na ushindwee, kwa jina la Yesu.

Mwachieni Mbowe nyie waovu.
 
Na najiuliza hivi uchaguzi mkuu uko mbele au? Mbona hakuna visima vilivyolipuliwa na wakati uchaguzi umeshaisha?

Ni nini kilimzuia asitimize azma yake? Na nyie kujua mtu ana nia kama hiyo mmuache uraiani toka mwaka jana hadi leo? Kwelii?

Mwachieni Mbowe nyie waovu...
 
Wewe Siro kama kweli unamjua Yesu tuambie nani alimpiga Lissu risasi na ni kweli askari wako walisimamia haki ktk uchaguzi ulopita?

Kama Mbowe ni gaidi basi we ni gaidi mara alf moja ya Mbowe kwa yale unayoyasimamia.

Huna haki ya kulitaja jina la Yesu katika mambo yako ya kishetani...

Na ushindwee, kwa jina la Yesuuu...

Mwachieni Mbowe nyie waovu...
nyinyi mlimjaza misifa kisha akavimba akajiona kweli yeye ni mwamba sasa ona matokeo yake ameangamia kwa matendo yake.
 
Mara Nyingine mimi huwa namlaumu Mchonga kwa kuliua Jeshi la Polisi tuliolirithi kutoka kwa Waingereza na kulitengeneza hili jeshi la Polisi ambalo lilifanywa kuwa la TANU na hata baada ya CCM kuzaliwa limekuwa la CCM

Tukiongelea kulivunja watu wanadhani nimetumwa na Mabeberu aisee!! ona sasa Wakoloni weusi wanavyotutesa.
 
Labda kama hukumsikiliza amesema maandamano ya amani ambayo yanaruhusiwa kisheria sasa achunge nini Kwani kwenye nchi za demokrasia kuandamana sasa limekuwa kosa la jinai nani amewahi kufungwa kwa kosa la kuandamana hebu tusifanywe wajinga.
wewe nenda ukaandamane na familia yako utaonekana jasiri sana.
 
View attachment 1877322
IGP Simon Sirro leo Agosti 2, 2021 akizungumza kukamatwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe


IGP Simon Sirro leo Agost 2,2021 amefanya mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amezungumza mbalimbali kuhusu kukamatwa na Mwenyekiti wa Chadema pamoja na vuguvugu la kutaka kufanya maandamano. Akiwa katika mkutano huo SIrro alisema yafuatayo:

“CHADEMA wanaona Mwenyekiti wao (Mbowe) ameonewa na wanasema hawezi kuwa hivyo wanamuona ni Malaika hawezi kufanya kosa”

“Kabla ya Uchaguzi nilisema kuna Watu wamepanga kuhakikisha Uchaguzi haufanyiki, nilisema kuna baadhi ya Watu wamepanga kulipua visima vya mafuta na kufanya mauaji ya Viongozi na nilisema tutawakamata kabla hawajafanya hivyo”

“Tuliwakamata kabla, hayo ya Mwenyekiti wao (Mbowe) sitaki kuzungumzia sana lipo Mahakama ila wajue yeye ni Binadamu kama Binadamu wengine na anaweza kufanya kosa tumempeleka Mahakamani tuache Mahakama itimize wajibu wake”

“Kama kweli ni mkweli Mwenyekiti wao (Mbowe) na anamuamini Mungu waende wamuulize habari hiyo, kuna mambo unaweza kuyafanya kwamba ni siri lakini ndio mana Vyombo vya Habari vipo, niwaombe Watanzania wenzangu usilolijua ni kama usiku wa giza usiingie kwenye mtego ambao hujui aliyeutega ana jambo gani”

“Waende wamuulize huyo Mtu tuliyempeleka Mahakamani (Mbowe) kwamba hili jambo unalijua na kama ni ukweli ana Dini yake na anamjua Yesu Kristo aende aaambiwe, tunamuonea kwa lipi ?, tupate nini?, tuna ushahidi wa kutosha tuache Mahakama iamue, kafanya Yes hakufanya Yes lakini habari ya kikundi cha Watu kusema tunataka kuandamana wewe ni nani Bro!? hiyo nafasi hauna”

Awaonya Wanaotaka kuandamana
“Niwaombe Watanzania tuache wale Watu wachache ambao wanataka kupambana na Serikali wapambane nayo labda wana sababu zake lakini Mtu wenye hekima na busara anielewe, lakini kikubwa kama wameandaa kwenda Canada au Marekani wajiandae ila hatuwezi kuruhusu Watu wachache wavuruge Nchi kwasababu wamekosa madaraka”

“Habari ya kusema mnataka kuandamana mnavunja sheria na ukivunja sheria usilaumu Jeshi, ukivunja sheria umeingia kwenye uhalifu, Sirro hatokuacha na Polisi hawatokuacha na ndio maana wanafanya siasa kwa sababu amani na utulivu upo, Sisi hatufanyi Siasa”

“Niwaombe Watanzania ambao wameambiwa mkusanyike kutoka Mara kutoka wapi sijui na muelewe Mahakamana ni kituo nyeti ni kama Kituo cha Polisi ukitaka kuvamia utakung’utwa kwa mujibu wa sheria sababu umetaka sasa kama kuna Mtu maisha yamemshinda aje ila asije kulalamika, hii kesi iko Mahakamani tuiachie Mahakama iamue”
Katiba mpya tunaitaka,Mbowe MUACHIENI ,tarehe tano lazima nikatimeze takwa langu la kikatiba,maandamano ya amani, mh IGP ni haki YENU kulinda maandamano ya amani,
 
Back
Top Bottom