Uchaguzi 2020 Ikungi: Magufuli amuahidi Lissu kazi, amuambia aachane na Urais ambao hatashinda

Umepanik sana,JPM kawachapa panapostahili,kwani uongo?hata Tundu anajua anafanya masihara hayupo siriaz
 
Hapa tafakuri inahitajika kiwango Cha Lami, hiyo kauli yake inatafsiri Mengi mbele ya huu uchaguzi.
 
Hili ni tusi kwa wanaikungi na kwa wanasingida wote adhabu yake ni kumfundisha Magufuli kwa kupeleka kura kwa Lissu, kuonyesha dharau kwa Lissu ni kuwadharau wanaikungi na wanasingida kuwa Magufuli akishinda hawana hadhi ya kupewa kazi yoyote labda kazi inayolingana na wahudumu wa Ikulu.
 
Manyimbo ya uchumi wa kati hayatavutii sisi wa vijijini, kwanza hatuyaelewi wala hatujaona tofauti yoyote popote.

Baada ya kucheza muziki tangu alfajili bila kula, kule Dodoma alisema keshajenga viwanda elfu 60. Ingefaa watuonyeshe tuwahi ajira kwanza matumbo yauma wajameni.

Ili atakapoleta hiyo midege mingine mipya, itukute tumeshiba na tuna uwezo wa kuitumia hii iliyopo kwenda kwetu Igulumbilo na kurudi kwenye matamasha hata wakati wa mvua ya kifuku.
 
Matusi ya Lissu umeyasikia wapi?
 
SASA BASI
 
Hivi kamanda Tindo unategemea Tundu kuchaguliwa na Watanzania awe Rais?hata yeye mwenyewe anajua anazuga

Suala la yeye kuchaguliwa na watanzania kuwa rais hilo wala halina mjadala, labda uzungumzie idadi ya kura kutokutosha. Na kimsingi Lisu hana tatizo na kutopata kura za kura za kuwa rais, bali ana tatizo na kura za kubumba ili kutangaza mshindi kinyume na kura za wananchi.
 
Majengo zahanati,vituo vya afya, maji.. Eti Sikuwahi kuombwa maji.... Mtaturu miezi michache kaniomba maji... wengine walikuwa hawaombi ( Lissu).. Hivi miradi afya,maji ,barabara ni hisani ya mtawala!?
Huyu jamaa kajisahau kabisa. Anafikiri kodi tunazolipa kugharamia maendeleo yetu anazimilki yeye na ni za kwake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…