Namba 1 kipindi cha Lissu- Deportivo la Corunia ilifanya yake
Namba mbili kipindi cha Lissu- Alijawa na huruma akaenda kumsalimia Lissu nairobi Mungu akampa Urais
Katibu Mkuu kiongozi kipindi cha Lissu- Huyu ndo anasimamia shughuli za Tiss nae deportivo la corunia ilifanya yake
Kipilimba na Musalika- DG na DDG TISS- hawa wote hawapo kwenye nafasi zao
Mambosasa- Huyu alizuia maombi juu ya Lissu sasa haijulikani kama kastaafu au la
Balozi sokoine- Huyu aliondolewa ubalozi ubelgiji baada ya kwenda hospitali kumsalimia Lissu. Leo ni Katibu Mkuu mambo ya nje cheo kikubwa kuliko balozi
Kalemani ambae inasemwa alikuwa jirani wa Lissu na alihusika kutoa cctv camera za tukio la Lissu nae sio waziri tena
Job Ndugai- Huyu alizuia pesa za matibabu za Lissu na kuzuia mshahara wa Lissu, Kwa yanayoendelea sasa CCM inaonekana hata mwezi machi hakanyagi akiwa Spika. Katiba inasema spika akipata uspika kutokana na kuwa mbunge akipoteza ubunge anapoteza uspika. Je, CCM watamvua uanachama hivyo kukosa ubunge na uspika? Tusubiri
Waliotenda wema kwa Lissu, Mungu kawabariki, waliotenda ubaya kawaadhibu! Sasa Je jaribio la kumuua Lissu lilimkasirisha sana Mungu?
Mwisho Naona Lissu akirejea Mama Samia atamteua kuwa Mbunge ili kumfuta machozi!