Iran ni nchi ya maajabu sana

Iran ni nchi ya maajabu sana

Mwenye akili na mfuatiliaji kuhusu Iran anajua kwanini anachungwa sana na kuzuiwa kufanya mengi na hata vikwazo vingi kuwekewa

Iran ana wataalamu wengi sana na ni akili kubwa
Amejiwekeza kwenye maendeleo na kutengeneza silaha mwenyewe kama wazungu wanavyofanya kwa nchi zao

Woga wa wazungu uliwafanya watafute nchi itakayopigana na Iran kwa kuwa tu wanaogopa ipo siku ataishika Saudia
Na Saudia ni kibaraka wa wazungu huku akiwauzia mafuta na wao wakijenga nchi za GCC kwa kupata ukandarasi wote

Hapo wakamshawishi Iraq aingie vita ya bila kichwa wala miguu kwenye mto wa Shat Al Arab ambapo kwa bahati nilikuwa huko na kushuhudia vita zote mbili, hiyo ya 1980 na uvamizi tena wa Iraq huko Kuwait 1990

Iran wana wataalamu wengi sana wa masuala ya utengenezaji wa silaha na mengine mengi ila wanaogopwa sana eti kwa usalama wa ME lakini ukweli ni kuwa wanaemlinda ni Israel


Bora na sisi tuanze kununua silaha za Iran kama Rifles zao za Fajr
Wako vizuri kwa nyanja nyingi na wanatengeneza silaha nyingi sana za maangamizi ambapo kuna wengi humu watashangaa na hata kupinga kuwa jamaa yuko vizuri sana

List ya silaha anayotengeneza Iran ni ndefu sana yaani kama ningekuwa na uwezo wa kupata hata tenda ya kuanza na military uniforms tu halafu taratibu nikaanza kuuwauzia silaha hata bunduki 1000 tu kwa kuanzia

Kuna fursa duniani ila tumekazana za [emoji631] na [emoji636] tu huu ni utumwa na hautaisha
Tuna safari ndefu sana
Asante mkuu kwa haya uliyoyaandika.
Wakati sisi tunaandika mambo yenye uhalisia, wengine wanaleta story za kwenye vitabu vya dini, huku wakisahau kuwa hata huyo msaudia na nchi zingine za falme za kiarabu ni waislamu lkn ni maadui wakubwa wa huyu jemedari wa vita na silaha.
 
Tukiuweka uislamu pembeni wairan ni waajemi na kama umesoma Biblia kwenye kitabu Cha Danieli Hawa Jamaa Tangu zamani ni watu Wenye akili nyingi (mf Mfalme Nebukadreza)ni Watu ambao maswala ya Sayansi na Teknolojia ilishakwepo kwao kabla hata ya kuja Kwa Yesu

Hivyo sizani hivo vikwazo uchwara vya watu magharibi kama vinaweza kukwamisha Maendeleo ya hao watu
Mimi siongelei mambo ya dini, bali uwezo wa kijeshi wa nchi ambayo iliwekewa vikwazo vya kijeshi miaka zaidi ya 50, lkn bado ni tishio kwa waliomuwekea vikwazo hivyo.
 
Wakuu vipi, kwema.

Wakuu Iran ni mmoja kati ya nchi ambazo ziliwekewa vikwazo vikali na nchi za magharibi toka mnamo mwa miaka ya 70s huko hadi leo hii na siku zijazo.

Vikwazo hivyo ni vya kiuchumi, kijeshi nk, tena vimekuwa vikiongezwa siku hadi siku.

Tofauti na ilivyo kwa nchi nyingine kama vile Cuba, Venezuela nk zilizowekewa vikwazo pengine na marekan tu, au baadhi ya nchi za magharibi. vikwazo vya Iran vimewekwa na nchi za magharibi kama zote wakishirikiana na makampuni ya nchi hizo.

Lakini cha kushangaza Iran imeweza kuwa na uwezo hasa wa kijeshi sawa au pengine zaidi ya ule wa nchi ambazo hazijawahi kuwekewa vikwazo na nchi hizo.

Iran ni miongoni mwa nchi zenye eneo kubwa na watu wengi barani Asia, so pamoja na vikwazo vya kiuchumi walivyowekewa takriban miaka 50 na zaidi, lkn wameweza kuwa na mifumo mizuri ya kudhibiti hali ya umasikini nchini mwao, tofauti na nchi kama Venezuela ambazo vikwazo vya miaka miwili au mitatu vimesababisha mamilioni ya raia waishi maisha ya shida na ya umasikini kupita maelezo.

Pamoja na vikwazo vikali vya magharibi hasa kwa upande wa mambo ya ulinzi, lkn bado nchi hiyo imeweza kuonesha kuwa haipo chini au nyuma kijeshi hata siku moja. Wengi tuliona jinsi wa Iran walivyoziangamiza ndege zisizo na ruban zilizokuwa zinatumiwa na Marekan kupima upepo katika eneo lao, wengi tuliona jinsi Iran ilivyozilipua meli ambazo zilikuwa zinabeba wapelelezi mbali mbali wa magharibi karibu na eneo lake, wengi tuliona jinsi Iran ilivyoshambulia kambi kadhaa za Marekani kule Iraq na kusababisha maafa na uharibifu mkubwa katika kambi hizo baada ya Mmarekani kumuuwa mmoja wa maofisa wakubwa wa Iran kule Iraq, tena kabla ya kufanya mashambulizi hayo wa Iran walitoa taarifa mapema kuwa watalipiza kisasi kupitia kambi za wamarekan kule Iraq, so marekan ikajiandaa kuzuia shambulizi lkn mwisho wa siku shambulizi likashindikana kuzuilika na kuleta maafa kwa jeshi la nchi hiyo kubwa duniani.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyotoa msaada wa silaha kwa kundi la hezbullah ambalo liliichachafya Israel inayopata msaada mkubwa wa fedha kutoka Marekani kwa ajili ya ulinzi wao. Hiyo ilikuwa mwaka 2006 hadi jumuiya ya kimataifa ikaingilia kati na kuomba ipatekane suluhu ya kudumu baina ya Israeli na hezbullah.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyosimama na kumlinda Asad wa Syria katika vita vyake, hadi kupelekea mipango ya Marekani na nchi za magharibi kumng'oa imeshindikana.

Wengi tunashuhudia sasa jinsi silaha kidogo tu za ndege zisikuwa na rubani za Iran zinavyofanya uharibifu mkubwa, na kusababisha maafa makubwa na zaidi ya yale yaliokuwa yanafanywa na Russia kupitia silaha zake mwenyewe (Russia) huko Ukraine.
Mpaka Marekani na nchi zingine za magharibi zinapiga kelele, maana silaha zinazotumika sio zile za Russia ambazo zilikuwa zinampa jeuri raisi wa Ukraine kuona kwamba sasa vita vimekwisha.

Hata zile himars za Marekani sasa hivi zinaonekana hazifanyi kazi mbele ya maangamizi ya ndege hizi za Iran.

Sasa tujiulize, kama nchi iliyowekewa vikwazo na mataifa makubwa duniani kwa zaidi ya miaka 50 bado ina uwezo iliyo nao leo, sasa je kama isingewekewa vikwazo kwa miaka yote hiyo 50 leo ni nchi gani ambayo ingeitisha pale Asia na hata duniani kwa ujumla.

Hizo nilizosema hapa ni zile silaha ilizotoa kuwawezesha hao niliwataja washinde mapambano yao, hapo hatujazungumzia silaha zake mwenyewe alizoweka kwa lengo la kujilinda ambazo kwa sheria za kijeshi duniani huwa zinafanywa siri kubwa ili adui asizione.

Mpaka sasa Marekani na nchi za magharibi zinashindwa kujua ni njia gani nyingine ya kumdhibiti huyu mtemi, maana wamarekani waliwahi kumtumia msaudi mwaka jana, hapo hapo Iran hakuchelewesha akaangamiza mitungi yake mikubwa ya kuwekea mafuta mpaka saudia na dunia ikapiga kelele.

Hili taifa ni la maajabu sana, japo lina maadui wengi lililotengenezewa na nchi za magharibi na halipati msaada wa kifedha kutoka kwa nchi yoyote lkn bado linajiamini kupita maelezo.

Mti wenye matunda ndio hurushiwa mawe, namaanisha ukiona nchi za magharibi na vibaraka wao wanapambana kwa hali na mali dhidi ya uchumi na ulinzi wa kijeshi wa nchi moja, basi jua kwamba wamagharibi hao wameshagundua kwamba nchi hiyo ni hatari maradufu kwa mustakabali wa uchumi wao pamoja na ulinzi wao.
Jibu ni moja Wana akili za uvumbuzi kama tuu Koreans zote..

Hiki ni kipawa kama vipawa vingine..

Na bado wanatoa misaada na kukopesha Nchi zingine ikiwemo Tanzania 👇
 

Attachments

  • FWWvd0BWYAAm2L4.jpg
    FWWvd0BWYAAm2L4.jpg
    63.9 KB · Views: 8
Wewe ndie msomi unayeandika "ilani"... "hawana"...hehehehe makubwa haya

Lakini nakusahisha bwana Msomi mtoa mada hajasema 'ilani' iko top zaidi ya hizo nchi ulizotaja bali ameshangazwa na kugangamala kwake licha ya kuwekewa vikwazo kwa zaidi ya miaka 50 lakini hajatetereka ukilinganisha na Nchi zingine akatoa mfano wa Venezuela,

Kusoma ni kuelewa sio ukariri tu.
Mkuu agiza supu ya njiwa nakuja kulipa. Jamaa anajifanaya ana elimu kuhusu mamb haya tunayojadili.

Lakini cha kushangaza ameshindwa kuonesha elimu yake hata namna ya kuandika nchi husika 😂😂😂
 
Wewe nae unajitia mjuaji kumbe huna lolote,muwe mnasoma thd na kuzielewa kwanza kuliko kukurupuka tu kama chafya,ni wapi mleta mada amesema Iran ina nguvu kuliko mataifa mengine kama Marekani,China na Russia? mleta mada anasema licha ya Iran kuwekewa vikwazo kwa miaka kibao ila wapo vizuri kwenye kutengeneza silaha zao wao wenyewe,

Halafu na wewe eti unajiita ni msomi na kujiona ni bora zaidi kuliko mleta mada!
Mkuu huyu jamaa ukimsoma kwa makini utagundua kuwa ni wale vijana wenye mihamko fulan ambayo haina ulazima wa kuitaja.

Ila kiuhalisia hawana fact yoyote ya kuandika hapa.
 
Kuna akili inanambia tz nasisi tungewekewa vikwazo tangu Uhuru tungekua Kama Iran.
Bila kuwa na asili ya akili kubwa kama Iran kamwe hamuwezi kutoboa.

Angalia wenzenu Cuba, Venezuela, Libya na nyinginezo nyingi zilivyoomba poo kwa vikwazo vya miaka michache tu, tena vikwazo vya kiuchumi na sio silaha.
 
Baki na propaganda zako ulizolishwa na magharibi mkuu.
Ukiona mtu anakimbilia kumwambia mwenzake amelishwa propaganda na upande flani basi jua fika kwamba hana uelewa na issue anayoiongelea. Mbona wewe hujaambiwa uliyoandika ni propaganda?
 
Ukiona mtu anakimbilia kumwambia mwenzake amelishwa propaganda na upande flani basi jua fika kwamba hana uelewa na issue anayoiongelea. Mbona wewe hujaambiwa uliyoandika ni propaganda?
Mfano huu ulioutoa pia uelekeze kwa Israel. Ukiona Israel inapiga kelele kuwa Iran iendelee kuwekewa vikwazo vya kiuchumi na kijeshi, jua yenyewe haijiamini, inahofia Iran ikiachwa huru itamuacha mbali kisilaha na kiuchumi?

Pia jiulize mbona Iran haijawahi kuomba au kulalamika kuwa Israel iwekewe vikwazo vya kijeshi, uchumi nk?
 
ni nchi ambayo iliweka misingi imala ya UONGOZI
Asikwambie mtu DEMOCRASIA inadumaza

ukitaka nchi yako ifanikiwe na ipige HATUA achana na DEMOCRASIA
DEMOCRASIA ni mtego mbaya wa WESTERN
ili kuendelea kukutawala na kukididimiza
CHINA ingekuwa imefuata huo upuuzi isingefika pele ilipo same na IRAN pia


hata ULAYA na AMERICA iliichukua mamia ya miaka mpk kuja kuwa na SERA ya DEMOCRASIA baada kuwa imejengeka na wamekuwa IMARA

Ndio maana hatahapa NCHINI kwetu tunahitaji RAISI mwenye kariba ya HAYATI MAGUFURI Ili kusonga mbele
DEMOCRASIA kwangu mimi ni ADUI mkubwa kwa MATAIFA yanayoendelea kama hapa NCHIN kwetu
Unazijua Nordic countries? Norway, Sweden, Denmark and Finland? Wana democracy ya kutosha na maendeleo makubwa. Ndiyo nchi zinaongoza kwa raia wake kuwa na furaha. Nchi yoyote inayoongozwa kidikteta tambua hilo linafanyika kwa faida ya watawala. Na ukikuta raia anashadidia utawala wa kidikteta basi tambua huyo raia hana hata uwezo wa kujiendesha yeye mwenyewe na pia kuiendesha familia yake. Ni raia ambaye kwanza haamini kabisa kwamba yeye kama yeye anauwezo wa kuwa na mchango kwenye jamii anayoishi, yaani maisha yake yoooteee huwa anategemea msaada wa mamlaka au mtu mwingine. Hasara ya raia wa aina hii ni pamoja na UCHAWA PRO MAX, majungu na kufuatilia maisha ya wengine, wivu mkubwa na chuki kwa waliofanikiwa na mwisho hawezi kuwa na ubunifu au mchango wowote kwa jamii na familia yake kwa sababu huamini kuwa huo uwezo hana.
 
Ni hawa hawa Iran wenye uwezo wa kuifuta Isreal kwenye uso wa dunia kwa maneno ya mdomoni, usifanye mchezo na taifa la kiyahudi, level yao ni juu mara mia zaidi ya binadamu mwingine yoyote anayeishi duniani....Israel is blessed.
Acha kutuletea hekaya za Abunuwasi wewe! Israel inaendelea kuwepo kutokana na sapoti kubwa kutoka Marekani na nchi za Ulaya ambako Jewish Lobby is very powerful. Without American support Israel is a paper tiger fit only to frighten the cowards.
 
Umeizungumzia Israel kwa mwonekano bila kugusia misingi ya nchi ya Israel kuanzishwa kwake na uimara wake,sijafahamu Imani ya dini yako,lakini kama ni Mkristo basi soma Biblia kitabu cha Mwanzo na kutoka utafahamu mengi na hata haya uliyoyaandika,kufanywa utumwa,kutawanyika kwao Dunian,kukusanyika kwao na kuundwa kwa hili Taifa utayapata...kifupi Israel ndio wenye nguvu kuliko hayo mataifa ya Ulaya na Marekani uliyosema,Iran alisha tamka kulifuta hilo Taifa lakini hatakaa aweze.
Jiulize Israel anazungukwa na maadui kote lkn bado anatoboa unafikiri ni rahisi?hilo ni Taifa teule japo wengi hawapendi kusikia likiitwa teule,lakini ndio ukweli mchungu.

Hili Taifa limepitia misukosuko mingi sana,hiyo uliyaandika hapo ni michache mno,rudi kwenye Biblia kalisome hili Taifa ndipo utalifahamu vizuri,huwezi pigana na Israel ukashinda maana mkono wa Mungu uko na hilo Taifa,kwa wale Wakristo wanasoma Biblia wanafahamu ninachozungumzia,lkn kama hausomi Biblia huwezi elewa haya.
Hili Taifa unalolisifu Mungu aliwalaani siku nyingi na wengine aliwageuza manyani kutokana na kufuru zao kubwa. Hawa ni watu washenzi wasiomheshimu Mungu na binadamu wenzao. Hawa ndio kwa imani yenu walimkamata Yesu wakamsulubu na kumuua. Hawa hawamuamini Yesu wala Injili. Watu washenzi wa kiwango hiki wanawezaje kuwa Taifa teule.
 
Iran imekataa kutawaliwa na ukoloni mamboleo, na ni nchi inayosimamia raslimali yake kubwa ya mafuta na gesi kwa manufaa yake. Hilo ndiyo chanzo ya ugomvi na nchi za Magharibi.
Ni nchi mmojawapo ya Kiislamu inayo ongoza kuelimisha wanawake.
 
Wakuu vipi, kwema.

Wakuu Iran ni mmoja kati ya nchi ambazo ziliwekewa vikwazo vikali na nchi za magharibi toka mnamo mwa miaka ya 70s huko hadi leo hii na siku zijazo.

Vikwazo hivyo ni vya kiuchumi, kijeshi nk, tena vimekuwa vikiongezwa siku hadi siku.

Tofauti na ilivyo kwa nchi nyingine kama vile Cuba, Venezuela nk zilizowekewa vikwazo pengine na marekan tu, au baadhi ya nchi za magharibi. vikwazo vya Iran vimewekwa na nchi za magharibi kama zote wakishirikiana na makampuni ya nchi hizo.

Lakini cha kushangaza Iran imeweza kuwa na uwezo hasa wa kijeshi sawa au pengine zaidi ya ule wa nchi ambazo hazijawahi kuwekewa vikwazo na nchi hizo.

Iran ni miongoni mwa nchi zenye eneo kubwa na watu wengi barani Asia, so pamoja na vikwazo vya kiuchumi walivyowekewa takriban miaka 50 na zaidi, lkn wameweza kuwa na mifumo mizuri ya kudhibiti hali ya umasikini nchini mwao, tofauti na nchi kama Venezuela ambazo vikwazo vya miaka miwili au mitatu vimesababisha mamilioni ya raia waishi maisha ya shida na ya umasikini kupita maelezo.

Pamoja na vikwazo vikali vya magharibi hasa kwa upande wa mambo ya ulinzi, lkn bado nchi hiyo imeweza kuonesha kuwa haipo chini au nyuma kijeshi hata siku moja. Wengi tuliona jinsi wa Iran walivyoziangamiza ndege zisizo na ruban zilizokuwa zinatumiwa na Marekan kupima upepo katika eneo lao, wengi tuliona jinsi Iran ilivyozilipua meli ambazo zilikuwa zinabeba wapelelezi mbali mbali wa magharibi karibu na eneo lake, wengi tuliona jinsi Iran ilivyoshambulia kambi kadhaa za Marekani kule Iraq na kusababisha maafa na uharibifu mkubwa katika kambi hizo baada ya Mmarekani kumuuwa mmoja wa maofisa wakubwa wa Iran kule Iraq, tena kabla ya kufanya mashambulizi hayo wa Iran walitoa taarifa mapema kuwa watalipiza kisasi kupitia kambi za wamarekan kule Iraq, so marekan ikajiandaa kuzuia shambulizi lkn mwisho wa siku shambulizi likashindikana kuzuilika na kuleta maafa kwa jeshi la nchi hiyo kubwa duniani.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyotoa msaada wa silaha kwa kundi la hezbullah ambalo liliichachafya Israel inayopata msaada mkubwa wa fedha kutoka Marekani kwa ajili ya ulinzi wao. Hiyo ilikuwa mwaka 2006 hadi jumuiya ya kimataifa ikaingilia kati na kuomba ipatekane suluhu ya kudumu baina ya Israeli na hezbullah.

Wengi tulishuhudia jinsi Iran ilivyosimama na kumlinda Asad wa Syria katika vita vyake, hadi kupelekea mipango ya Marekani na nchi za magharibi kumng'oa imeshindikana.

Wengi tunashuhudia sasa jinsi silaha kidogo tu za ndege zisikuwa na rubani za Iran zinavyofanya uharibifu mkubwa, na kusababisha maafa makubwa na zaidi ya yale yaliokuwa yanafanywa na Russia kupitia silaha zake mwenyewe (Russia) huko Ukraine.
Mpaka Marekani na nchi zingine za magharibi zinapiga kelele, maana silaha zinazotumika sio zile za Russia ambazo zilikuwa zinampa jeuri raisi wa Ukraine kuona kwamba sasa vita vimekwisha.

Hata zile himars za Marekani sasa hivi zinaonekana hazifanyi kazi mbele ya maangamizi ya ndege hizi za Iran.

Sasa tujiulize, kama nchi iliyowekewa vikwazo na mataifa makubwa duniani kwa zaidi ya miaka 50 bado ina uwezo iliyo nao leo, sasa je kama isingewekewa vikwazo kwa miaka yote hiyo 50 leo ni nchi gani ambayo ingeitisha pale Asia na hata duniani kwa ujumla.

Hizo nilizosema hapa ni zile silaha ilizotoa kuwawezesha hao niliwataja washinde mapambano yao, hapo hatujazungumzia silaha zake mwenyewe alizoweka kwa lengo la kujilinda ambazo kwa sheria za kijeshi duniani huwa zinafanywa siri kubwa ili adui asizione.

Mpaka sasa Marekani na nchi za magharibi zinashindwa kujua ni njia gani nyingine ya kumdhibiti huyu mtemi, maana wamarekani waliwahi kumtumia msaudi mwaka jana, hapo hapo Iran hakuchelewesha akaangamiza mitungi yake mikubwa ya kuwekea mafuta mpaka saudia na dunia ikapiga kelele.

Hili taifa ni la maajabu sana, japo lina maadui wengi lililotengenezewa na nchi za magharibi na halipati msaada wa kifedha kutoka kwa nchi yoyote lkn bado linajiamini kupita maelezo.

Mti wenye matunda ndio hurushiwa mawe, namaanisha ukiona nchi za magharibi na vibaraka wao wanapambana kwa hali na mali dhidi ya uchumi na ulinzi wa kijeshi wa nchi moja, basi jua kwamba wamagharibi hao wameshagundua kwamba nchi hiyo ni hatari maradufu kwa mustakabali wa uchumi wao pamoja na ulinzi wao.
Iran ni nchi imara tena tajiri wa mali na utamaduni.
Ila tatizo iran huenda ikajikanga kwa mafuta yake yenyewe kwa kujiwekea sera na itikadi isiyo na tija kiuchumi kwa wananchi wake.
Mapinduzi ya kidini yana faida gani? Badala ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi yenye kufaidisha umma wao wanaua hadi wanawake kwa kutovaa hijab. Polisi wa maadili wanahangaika kusimamia watu waingie misikitini kusali. Sasa wakishasali inasaidia nini kiuchumi.
Kiuchumi iran wanaendeleza uchumi wa kibepari wanasema uislamu unaruhusu kulimbikiza mali kibepari.
Kwa hivyo iran haina sera ya kuona usawa na haki kwenye mgawanyo wa keki ya taifa.
Kwa kuwalazimisha wananchi kusali na wanawake kuvaa hijab ni mambo hayana faida yoyote na uchumi wao.
Siku si nyingi tutazamie mapinduzi ya kidini kusambaratika iran na pengine kurithiwa na mapinduzi ya kiuchumi kwa wavuja jasho kuchukua hatamu ya dola ili kupata uhuru wa nafsi zao na uhuru kiuchumi.
 
Acha kutuletea hekaya za Abunuwasi wewe! Israel inaendelea kuwepo kutokana na sapoti kubwa kutoka Marekani na nchi za Ulaya ambako Jewish Lobby is very powerful. Without American support Israel is a paper tiger fit only to frighten the cowards.
Wewe unafikiri innovations zinazotumia akili kubwa huko marekani na ulaya zinafanywa na nani kama siyo waisreali wanaoishi huko, unafikiri wanawakumbatia kindezi............
 
Back
Top Bottom