Iringa: Polisi yakana madai ya kada wa CHADEMA, Vitus Nkuna kushambuliwa na wasiojulikana barabarani, yasema alisababisha ajali kutokana na ulevi

Iringa: Polisi yakana madai ya kada wa CHADEMA, Vitus Nkuna kushambuliwa na wasiojulikana barabarani, yasema alisababisha ajali kutokana na ulevi

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938

Jeshi la Polisi mkoani Iringa limemkamata kada wa Chadema, Vitus Nkuna kwa kusababisha ajali mnamo Septemba 30, 2024. Kamanda wa Polisi, SACP Allan Bukumbi, ameeleza kuwa Nkuna alikuwa anaendesha gari akiwa na kiwango kikubwa cha ulevi, hali iliyosababisha kugonga gari la kampuni ya KINGS.

Hata hivyo, kupitia ukurasa wake wa Twitter siku ya Jumatatu, Nkuna alidai kushambuliwa na watu wasiojulikana. "Nimeshambuliwa na watu wasiojulikana nikiwa barabarani hapa Iringa," aliandika.

Aliongeza kuwa baada ya kufika kituo cha polisi, viongozi wa Chadema walifika kumuunga mkono.

“Tunatoka Kituo Kikuu cha Polisi Iringa na naelekea kwangu. Kesho tutajua nani alikuwa wanataka kunikamata barabarani usiku huu kwa kunizuia mbele na nyuma. Tutaujuza umma kwa kila hatua”, alisisitiza Nkuna katika chapisho lingine.

Jeshi la Polisi limekanusha madai hayo, likieleza kuwa hakukuwa na shambulio, na tukio hilo lilitokana na ajali iliyosababishwa na Nkuna mwenyewe akiwa amelewa.

Nkuna1.jpg

Nkuna2.jpg
 
Dah aisee kazi sana, yaani sasa hivi mtu hata akijikwaa anaseme Serikali inataka kumuua
 
Ccm wanahitaji mtu jasiri kama Netanyahu awatoe kamasi, miaka 60 na...... Bado watu wanakunywa maji na mifugo? Sasa Ester Luxury vipi? Mafisadi Kila Mahali!
 
Dah aisee kazi sana, yaani sasa hivi mtu hata akijikwaa anaseme Serikali inataka kumuua
Mbowe alianguka kwenye ngazi akiwa ameyatutika akasingizia kuwa wasiojulikana walikuwa wanataka kumfanyizia. Bahati nzuri waliokuwepo wakatibua dili la kuudanganya umma kwa kusema ukweli kwamba jamaa nyagi lilizidi.
 
Jeshi la Polisi mkoani Iringa limemkamata kada wa Chadema, Vitus Nkuna kwa kusababisha ajali mnamo Septemba 30, 2024. Kamanda wa Polisi, SACP Allan Bukumbi, ameeleza kuwa Nkuna alikuwa anaendesha gari akiwa na kiwango kikubwa cha ulevi, hali iliyosababisha kugonga gari la kampuni ya KINGS.

Hata hivyo, kupitia ukurasa wake wa Twitter siku ya Jumatatu, Nkuna alidai kushambuliwa na watu wasiojulikana. "Nimeshambuliwa na watu wasiojulikana nikiwa barabarani hapa Iringa," aliandika.

Aliongeza kuwa baada ya kufika kituo cha polisi, viongozi wa Chadema walifika kumuunga mkono.

“Tunatoka Kituo Kikuu cha Polisi Iringa na naelekea kwangu. Kesho tutajua nani alikuwa wanataka kunikamata barabarani usiku huu kwa kunizuia mbele na nyuma. Tutaujuza umma kwa kila hatua”, alisisitiza Nkuna katika chapisho lingine.

Jeshi la Polisi limekanusha madai hayo, likieleza kuwa hakukuwa na shambulio, na tukio hilo lilitokana na ajali iliyosababishwa na Nkuna mwenyewe akiwa amelewa.
walevi bana,
akipigwa ngumi kali ya uso, anasingizia kapigwa na tofaulia au na kitu kizito..

sasa jamaa kagonga kari la watu halafu anasingizia kazuiwa mbele na nyuma 🤣

Pombe sio chai ndrugo zango, kunywa kistaarabu 🐒

ukweli ni kitu muhimu sana aise
 
Back
Top Bottom