Uchaguzi 2020 Itokee Lissu akashinda Urais, akakupa nafasi ya kutoa pendekezo, ni kitu gani alichofanya Magufuli utamwomba akiondoe mara moja?

Uchaguzi 2020 Itokee Lissu akashinda Urais, akakupa nafasi ya kutoa pendekezo, ni kitu gani alichofanya Magufuli utamwomba akiondoe mara moja?

Nini kitolewe na nini kifanyike vinashabihiana. KUna watu wanamchukia Magufuli kutokana na aliyotenda, ndio maana kuna element ya nini kikomeshwe. Kama kila aliyotenda yanakubalika, kwa nini wamchukie?
Kuhusu nn kifanyike. Sauti zetu ni ndogo sana hatuwezi kusikika. Tunaweza umiza vichwa hapa then hata maombi yetu yasisikike. Mi naona jamii forum ni sehemu ya kutolea hasira tu kwa mambo yaliyoko moyoni. Serikali yetu sidhani kama inaichukulia serious. Itachukulia serious endapo itaanza kuona impact.
 
Katiba mbovu,kuukuu ya kijima iliyo jaa viraka,jeshi la polisi la kikoloni lifumuliwe,mageuzi ya mfumo mzima wa elimu yetu toka wa kinadharia hadi wa kivitendo,wizara ya elimu iwekwe kikatiba ili wanasiasa wasiichezee,yapo mengi sana
Kama Katiba ni mbovu sio Magufuli alileta
 
Naona Lisu kaishiwa sasa anatafuta alishwe maneno ya kuongea kwenye kampeni za lala salama baada ya kugundua kuwa mikutano yote aliyofanya hajawagusa wananchi na kitu cha kueleweka

LISU ni mgombea pekee wa uraisi ambaye anamaliza ngwe yake bila kunadi sera za CHAMA CHAKE
Kama huna la kuongea zaidi ya ushabiki wa kipumbavu kaa kimya
 
Kuhusu nn kifanyike. Sauti zetu ni ndogo sana hatuwezi kusikika. Tunaweza umiza vichwa hapa then hata maombi yetu yasisikike. Mi naona jamii forum ni sehemu ya kutolea hasira tu kwa mambo yaliyoko moyoni. Serikali yetu sidhani kama inaichukulia serious. Itachukulia serious endapo itaanza kuona impact.
Usikate tamaa. KUna jume zinaenyeza na kupita kupitia Jamii Forum. KUmbuka kwamba Jamii Forum na kina Maxello wanafuatwa kila wakati kutokana na mambo yanayopostiwa hadi wamelazimishwa kupitia thread kabla ya kuzipost. Ina maana kuna watu wanasoma ndio aana wanawasumbua JF
 
..Nitamshauri aachane na ujenzi wa gharama kubwa wa ikulu ya kifahari dodoma.

..badala yake fedha zilizotengwa zikasaidie miradi ya maendeleo maeneo mbalimbali ya mkoa wa dodoma.
 
Wengi nasikia tu mnasema ooh Magufuli hajafanya lolote, ooh katupiga sana nk. Lakini pale ninapouliza baadhi ya watu kwamba ni kitu gani ambacho amefanya Magufuli ambacho unaona hakifai, wengi wanashindwa kutoa jibu la haraka.

Sasa leo ningependa kuwauliza katika mtandao wa JF, kwamba ikitokea Tundu Lissu anashinda kiti cha uraisi, na akakuambia toa pendekezo ni kitu gani ambacho Magufuli alikifanya nikiondoe au kukikomesha mara moja, utapendekeza nini?
Arudishe UHURU HAKI NA MAENDELEO YA WATU.
 
Wengi nasikia tu mnasema ooh Magufuli hajafanya lolote, ooh katupiga sana nk. Lakini pale ninapouliza baadhi ya watu kwamba ni kitu gani ambacho amefanya Magufuli ambacho unaona hakifai, wengi wanashindwa kutoa jibu la haraka.

Sasa leo ningependa kuwauliza katika mtandao wa JF, kwamba ikitokea Tundu Lissu anashinda kiti cha uraisi, na akakuambia toa pendekezo ni kitu gani ambacho Magufuli alikifanya nikiondoe au kukikomesha mara moja, utapendekeza nini?
Aanze upya kufufua shirika la ndege. Sio kununua ndege na kupark. bali aanzishe mpango mkakati utakaoliwez sha shirika kufanya kazi kwa faida.
 
umesahau, lazima pia waliochoma moto ofisi za chadema washuhulikiwe
- zile bil 8 pia za mbowe zirudishwe kwenye mzunguko
- wale wabunge waliofukuzwa kisa walienda bungeni wakati wa corona wapewe haki yao maana hawakufanya kosa lolote
- matusi yanayorushiwa kwa polisi, polisi wapewe haki ya kuwaadhibu wanaowatukana ni binadam pia
CHADEMA Ni SERIKALI? NAJUA CHADEMA NI CHAMA.KAMA WALIKUBALIANA ADHABU NI HIYO KWA WASALITI LAZIMA ITEKELEZWE, NI KAMA CCM WALIVYOMTOSA MBOBEZ MEMBE MAMBO YA VYAMA..
 
1. Afute mara moja sheria za kidikteta zinazoondoa uhuru wa maoni na uhuru wa vyombo vya habari

2. Wakurugenzi waliochaguliwa kwa sababu ya ukada wa CCM badala ya weledi, waondolewe mara moja

3. TISS iundwe upya na ifanye kazi yenye manufaa kwa Taifa badala ya kuteka na kupoteza watu wanaokosoa watawala

4. Waloteuliwa kwa sababu ya undugu, ukabila na ukanda badala ya merits, waondolewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria zote kandamizi zilizotungwa chini ya utawala wake
 
Magufuli anafanya vzr isipokuwa yako mambo kadhaa ya kurekebisha mfano :
(1) Makato kwa wanufaika wa mikopo ya elimu ya juu yabaki 8%.
(2) Mikopo ya halmashauri kwa wajasiriamali iongezwe ili kuchochea shughuli za uzalishaji mali.
(3)JKT wapewe fedha zaidi za kuanzisha viwanda vingi zaidi hasa ambavyo ni labour intensive kama vya nguo nk ili kuajiri vijana wengi zaidi.
(4) Mazingira ya ufanyaji biashara yaboreshwe zaidi ikiwa ni pamoja na kupunguza urasimu katika uombaji vibali/leseni.
(5)Kuchochea uhuru wa mawazo na hasa mijadala yenye tija ktk jamii juu ya demokrasia na maendeleo ya watu.
 
Wengi nasikia tu mnasema ooh Magufuli hajafanya lolote, ooh katupiga sana nk. Lakini pale ninapouliza baadhi ya watu kwamba ni kitu gani ambacho amefanya Magufuli ambacho unaona hakifai, wengi wanashindwa kutoa jibu la haraka.

Sasa leo ningependa kuwauliza katika mtandao wa JF, kwamba ikitokea Tundu Lissu anashinda kiti cha uraisi, na akakuambia toa pendekezo ni kitu gani ambacho Magufuli alikifanya nikiondoe au kukikomesha mara moja, utapendekeza nini?
Naona unalialia tu. Unaeza ondoa kovu?
 
Afanye haraka kurudisha hospitali ya mloganzila MUHAS tupate university hospital nchini
 
Wengi nasikia tu mnasema ooh Magufuli hajafanya lolote, ooh katupiga sana nk. Lakini pale ninapouliza baadhi ya watu kwamba ni kitu gani ambacho amefanya Magufuli ambacho unaona hakifai, wengi wanashindwa kutoa jibu la haraka.

Sasa leo ningependa kuwauliza katika mtandao wa JF, kwamba ikitokea Tundu Lissu anashinda kiti cha uraisi, na akakuambia toa pendekezo ni kitu gani ambacho Magufuli alikifanya nikiondoe au kukikomesha mara moja, utapendekeza nini?
zuio la bunge laive
 
Back
Top Bottom