Jaji Warioba: Dkt. Bashiru ajibiwe kwa hoja, hajafanya kosa lolote acheni kumshambulia

Jaji Warioba: Dkt. Bashiru ajibiwe kwa hoja, hajafanya kosa lolote acheni kumshambulia

Mzee maisha yamempiga, anahaha tu kutafuta ajira kupitia wapiga debe wa katiba mpya.

Huyu alikaa na Nyerere kwa miongo kadhaa, hakumshauri kuhusu katiba, na aliiacha nchi imefilisika, kwa Sasa hivi hana la kutushauri, ni mtu wa hovyo tu, na pia alikula Hela katika kashfa ya meremeta.

Matapeli wa kisiasa waliobaki
Mkuu utakuwa na lako Jambo. Yaani unasema mzee Warioba maisha yamempiga? Hujui huyu anapokea mapene na masurufu mengine sawa na Kasimu Majaliwa (80%)?

Hufahamu kuwa huyu mzee ni zaidi malaika kwa usafi na uadilifu?
 
Kauli ya Bashiru ni fursa kwa wapuuzi wenzake kama yule mwizi wa vyeti Kingwalagwala, midume mizima inawaza tuu namna ya kurudi kwenye siasa ipate vyeo, rudini sekta binafsi muanze kulipa kodi kama wengine
 
Mkuu utakuwa na lako Jambo. Yaani unasema mzee Warioba maisha yamempiga? Hujui huyu anapokea mapene na masurufu mengine sawa na Kasimu Majaliwa (80%)?

Hufahamu kuwa huyu mzee ni zaidi malaika kwa usafi na uadilifu?
Huyo taahira anajua kuropoka tu! Waziri mkuu mustaafu analipwa mshahara 80% ya mshahara wa waziti mkuu!
 
Mzee maisha yamempiga, anahaha tu kutafuta ajira kupitia wapiga debe wa katiba mpya.

Huyu alikaa na Nyerere kwa miongo kadhaa, hakumshauri kuhusu katiba, na aliiacha nchi imefilisika, kwa Sasa hivi hana la kutushauri, ni mtu wa hovyo tu, na pia alikula Hela katika kashfa ya meremeta.

Matapeli wa kisiasa waliobaki
Ungejibu Hoja yake kwanza ,kabla ya kuanza kumshambulia yeye binafsi.
 
Majibu aliyopewa Mjinha Bashiru mpaka sasa ndio hasa yanamfaa. Kwamba alichifanya yeye awamu ya tano ndio hicho hicho kinafanyika awamu hii so atulie au atoke. Warioba nae atulie hana ladha tena.
 
RAIS SAMIA SULUHU HASAAN ANAENDESHA NCHI KWA WELEDI MKUBWA NA UBORA WA HALI YA YA JUU KULIKO MTANGULIZI WAKE HUU NDIO UKWELI WENYEWE, (ANAUPIGA MWINGI HASA)
"wanaoumia juu ya hili ni wengi kweli"
Tunatarajia wengi zaidi watajitokeza.
 
Mzee maisha yamempiga, anahaha tu kutafuta ajira kupitia wapiga debe wa katiba mpya.

Huyu alikaa na Nyerere kwa miongo kadhaa, hakumshauri kuhusu katiba, na aliiacha nchi imefilisika, kwa Sasa hivi hana la kutushauri, ni mtu wa hovyo tu, na pia alikula Hela katika kashfa ya meremeta.

Matapeli wa kisiasa waliobaki
Hoja ya Bashiru uliielewa, na je hii ya jaji Waryoba? Jibuni hoja, acheni viroja, enyi ukoo wa panya!
 
Siasa za Tanzania ni za njaa kila mtu ni full kujikomba hasa wale wenye ugali ili waendelee kulamba
 
Nilitarajia ungejibu hoja ya Dr Bashiri lakini kwa mshangao mkubwa sioni tofauti yako wewe na Msukuma.Ujinga umekujaa
Wapinzania nchi hii watapata shida sana sasa wana trend na Bashiru wameshamsahau Majaliwa. Nimjibu wa nini kwa hoja ipi? hakuna sehemu nimesema alishosema sio sawa shida ni unafiki maana yeye ndio alianzisha hii system ya mapambio wakati yeye ni katibu mkuu wa CCM sasa nini kipya leo? zaidi huwezi kuwa sehemu ya serikali halafu ukajiengue mimi naanza kuamini kuna shida kubwa na watu kanda ya ziwa bado hawaja move on Mungu aliwakatia ndoto yao. CCM watamjibu sio mimi
 
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Sinde Warioba, ameeleza kuwa Balozi Bashiru Ally, hajafanya kosa lolote hakustahili kushambuliwa. Amesema, watu wajibu hoja badala ya kumshambulia yeye binafsi.

---

Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema alichokisema Mbunge Dkt. Bashiru Ally hakikuwa na shida yoyote kwa kuwa alikuwa akitoa hoja yake, na kwamba viongozi wanapaswa kujibu hoja hiyo badala ya kumshambulia.

Akizungumza na chombo kimoja cha habari nchini, Jaji Warioba amesema ni kweli Serikali inafanya kazi nzuri lakini hiyo haimaanishi kila kitu kisifiwe, endapo kuna hoja ambayo itahitaji kujadiliwa iangaliwe.

“Hawa ni viongozi wa nchi, mimi nilifikiri watakuwa wanatetea wananchi zaidi. Naona kama wanatetea Serikali zaidi. Mimi nadhani kama wanatofauti zao huko wasizifanye ni tofauti za kitaifa. [..] Mimi sioni kama tunasaidia nchi kuanza kusema huyu awajibike kwa sababu ya mawazo aliyotoa, hivi mtu akitoa mawazo yake imekuwa ni kosa?” amehoji Warioba.

Aidha, Jaji Warioba amewakosoa wote wanaodharau nafasi yake ya ubunge kwa kuuita kuwa ni ubunge wa Ikulu, na kusema kuwa yeye ni mbunge kama wabunge wengine ambaye pia anatambulika kwenye katiba ya nchi, na kwamba hajateuliwa ili kuitetea Ikulu.

Dkt. Bashiru hivi karibuni alizungumza na wakulima wadogo katika warsha iliyoandaliwa na Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) akiwasihi kuacha tabia ya kushukuru na kusifu viongozi badala yake wadai haki zao kwa viongozi wao.
Mbona yeye hakuacha kusifu na kulitukuza jina la mtukufu wake nyakati zile za kiza, aache UNAFIKI WAKE.
 
..Dr.Bashiru ni fedhuli wa awamu ya 5 leo mnataka wahanga wa ufedhuli wake na Magufuli wajitokeze kumtetea?

..Dunia haiendi namna hiyo. Muache Dr.Bashiru atetewe na genge la mafedhuli wenzake kwani bado wapo serikalini na ktk chama.
Hisia hisia hisia....

Hata kama ni fedhuli, haki zake bado ziko pale pale, hata jambazi ana haki zake mpaka atakapokutwa na hatia mbele ya mahakama, hii pointi ndogo sijui kwanini inawasumbua sana kuielewa.

Siwezi kumuacha Dr. Bashiru ahangaike peke yake, kwasababu hiyo haki anayonyimwa, ndio wanayonyimwa wengine kama ambavyo tunaona hawaruhusiwi kufanya mikutano ya siasa japo ni haki yao..

Matokeo yake mnamuacha mwenye tatizo kama lenu ahangaike nalo peke yake huku mkimpongeza aliyemnyima haki yake, ajabu kesho tena nanyo mnarudi kwa yule mliyempongeza kumnyima mwingine haki yake kutaka awape nyie, hii ni double standard yenye vimelea vya ubinafsi
 
We

We ndo hujui watu, mtu ambaye ni waziri mkuu Mstaafu anakula 80percent ya mshahara wa waziri mkuu aliyeko madarakan, anahudumiwa na serikali kila kitu, Leo unasema Maisha yamempiga??ur kidding?
Tena atahudumiwa mpaka anaiaga dunia !! Kila kitu bwerere !! Hana shida Mzee. !
 
Mzee maisha yamempiga, anahaha tu kutafuta ajira kupitia wapiga debe wa katiba mpya.

Huyu alikaa na Nyerere kwa miongo kadhaa, hakumshauri kuhusu katiba, na aliiacha nchi imefilisika, kwa Sasa hivi hana la kutushauri, ni mtu wa hovyo tu, na pia alikula Hela katika kashfa ya meremeta.

Matapeli wa kisiasa waliobaki
Waziri mkuu mstaafu hupata 80% ya mshahara wa Waziri mkuu wa sasa
 


Mzee Warioba kasema kukosolewa kwa kiongozi siyo dhambi na pamoja na matatizo ya Wakulima lakini Wafugaji na Machinga pia wanakumbwa na matatizo ambayo wenye mamlaka yawapasa kuwasaidia.

NB: Bashiru siyo Ndugai.
 
Back
Top Bottom