Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

Jaji Warioba: Miaka yote watu wanaelewa kujaza fomu, lakini 2020 ghafla hawajui. Siasa inataka kuingia kwenye Dini

Jaji Warioba akichangia kwenye mkutano wa TCD leo Dodoma, amenena haya

Miaka yote watu wanaelewa na wanajaza fomu vizuri lakini Mwaka 2020, ghafla watu hawajui kujaza fomu (wanaenguliwa). Hapa lazima kuna namna

Msitazame Wajumbe wa Tume pekee, angalieni Mfumo mzima wa Uchaguzi. Wizi wa kura unaanzia mbali. Unaanzia kwenye Kuandikisha wapiga kura, wakati wa kupiga kura na kutangaza matokeo

Siasa inataka kuingia kwenye dini, zamani viongozi tulikuwa tunakwenda kwenye vyumba vya ibada kama waumini, unasikiliza neno la Mungu. Siku hizi viongozi wakienda wanaombwa kutoa salamu za kisiasa, hii inaweza iingiza siasa katika dini tukapata matatizo

Vyama vingi vimekuwa kama makabila, vinaanza kugawa wananchi. Wananchi walikuwa kama jumuiya lakini siku hizi mambo mengi ya kijamii tunaingiza siasa, mfano msiba ni wa jamii lakini baadhi ya misiba unakuta sare za vyama,"

Katika vyama jumuiya zetu nazo zinakuwa kama za uhasama, badala ya kutuleta pamoja. Hali tuliyo nayo sasa utamaduni umetikiswa kidogo na tunapozungumzia maridhiano, nia yake kuturudisha kwenye utamaduni tuliokuwa nao


Viongozi wa kisiasa wangehubiri amani kama walivyofanya viongozi wa dini miaka michache iliyopita, nchi isingekuwa na malalamiko yanayolalamikiwa hivi sasa “kama wangetenda kama viongozi wa dini, nadhani matatizo haya tunayozungumza tusingekuwa nayo.

Naunga mkono hoja ya mh.Jaji Warioba kuwa :-

1)Tukomeshe tabia za wanasiasa kutoa salamu za kisiasa/kuomba kura wakiwa katika mahali patakatifu katika nyumba za ibada....tabia hii imefurutu ADA hata kwa wanasiasa wa vyama vya upinzani.....

2)Tabia ya kwenda misibani huku tukiwa na sare za vyama vyetu si AFYA KWA JAMII

#Siempre JMT🙏
#Nchi Kwanza 🙏
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?

Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.
Umerudi kule kule. Mahakamani gani,inayoweza kuamua haki?. Hii hii ya Tz?
 
Mahakama mwaka 2020 ilishikwa akili na "You know who"
Sio hiyo ya mwaka 2020. Mahakama za Tz serikali ikitia mkono tu tayari imetepeta. Hakuna wenye msimamo kule. Mahakama utazikuta kenya,zina uwezo wa kupingana na serikali kabisa. Wana uwezo kufuta uchaguzi. Wana maamuzi ya kumkamata al-Bashir wa Sudan il-hali serikali haitaki
 
Kwanini hawakuenda mahakamani?

Kubaki unalialia umeonewa wakati hakuna kesi hata moja mahakamani ya kupinga uchaguzi ni upuuzi na kupoteza muda.

..MAHAKAMA hiihii ambayo imekuwa ikitumika na Ccm kuwafunga wapinzani kwa KESI ZA MICHONGO?
 
Warioba ana level ya kuwa baba wa taifa
 
Huyo Kinana hayo ameona hayakuwepo 2020 tu?

Sent from my SM-T295 using JamiiForums mobile app
Kipindi Cha Kinana CCM waliiba kura ila kwa aligorithm yaani Gap iwe 60-40% kuanzia Kata hadi Urais. Ila kwa JPM aisee hakuna Cha formula yeye alizoa kila kitu kuanzia vijiji hadi Urais 84%+

Yaani mpaka Pemba eti CCM ilishinda majimbo karibu yote!! Seriously?
 
Ila lizee lilikuwa na Roho mbaya sana, Limetesa na hata kuwauwa vijana wa watu waliokuwa TISS kwa kushukiwa tu walikuwa wanampinga
Alikuwa anaogopa kivuli chake mwenyewe, huwa wanasema mara nyingi mtu/kiumbe anayefoka sana na kujitutumua mbele ya kadamnasi mara nyingi huwa hajiamini na ni muoga namba moja! Ref. Nyoka Koboko, ni nyoka anayeongoza kwa uoga na ndiyo maana ishu ndogo tu anaattack, huwa hana kufikiri mara 2, hajui hata kutunza sumu yake kwa matumizi muhimu ya baadaye (Kusaka chakula)
 
Uchaguzi mkuu 2015 Kinana alikuwa katibu mkuu ccm. Demokrasia na haki vilikuwepo wakati huo?!
Kipindi Cha Kinana CCM waliiba kura ila kwa aligorithm yaani Gap iwe 60-40% kuanzia Kata hadi Urais. Ila kwa JPM aisee hakuna Cha formula yeye alizoa kila kitu kuanzia vijiji hadi Urais 90%+

Yaani mpaka Pemba eti CCM ilishinda majimbo karibu yote!! Seriously?

Then demokrasia haiishii tu kwenye uchaguzi, hata ushiriki wa wapinzani kwenye vyombo vya wawakilishi, free media, na uhuru wa maoni ikiwemo vyama vingi kufanya mikutano n.k, and more than other 11 principles of democracy walau hata 9 zilikuwepo. Ila kwa JPM hakukuwepo hata moja so unapo compare factor in Kila kitu sio chaguzi pekee.
 
Kipindi Cha Kinana CCM waliiba kura ila kwa aligorithm yaani Gap iwe 60-40% kuanzia Kata hadi Urais. Ila kwa JPM aisee hakuna Cha formula yeye alizoa kila kitu kuanzia vijiji hadi Urais 84%+

Yaani mpaka Pemba eti CCM ilishinda majimbo karibu yote!! Seriously?
Hahaha, jamaa alitia fora Chief, CDM kupata mbunge 1 nchi nzima!! Ule wizi utakuwa ulisimamiwa na wahuni akina Bashite/Musiba
 
Back
Top Bottom