Jakaya Kikwete aliwezaje kufanya mambo makubwa kwa wakati mmoja?

Jakaya Kikwete aliwezaje kufanya mambo makubwa kwa wakati mmoja?

Acha upotoshaji wewe kwani kipindi cha magufuli watu hawali rushwa nani kakudanganya?
 
Hakuna binadamu aliyekamilika lakini JK alijitahidi sana uongo mbaya
Ukiwa kiongozi huwezi kufurahisha wote

Unaweza kuamini Nyerere mwenye heshima zake kuna watu hawamkubali?
 
Sasa hizo ambazo kwa sasa haziibiwi zipo wapi,na ukumbuke deni la Taifa lime shoot Mara 2 ya alipoliacha Kikwete.
Kabisa mkuu yaani deni linakuwa kwa kasi kiasi kwamba wachina hii nchi watainunua sass
 
Ukiwa kiongozi huwezi kufurahisha wote

Unaweza kuamini Nyerere mwenye heshima zake kuna watu hawamkubali?
Mmojawapo ni huyu aliepo sasa hivi ashajivika cheo cha baba wa taifa tayari hata nyerere wanaona hafai tena mpaka wanafikiria kumpa atawale milele
 
Kweli Kikwete ashukuriwe sana, kipindi chake tulikuwa tukipiga hela kinoma. Ukiiba hakuna wa kufuatilia, ilikuwa kweli CCM. CHUKUA CHAKO MAPEMA, lakini leo thubutu kuvamia banki au kuteka magari tu barabarani usiku, utakiona cha mtema kuni.
 
Yaaah mkuu sema watu walishalemaa na yale maisha ya kupatikana kwa hela kirahisi.

Mfano biashara ya madawa ya kulevya ina pigwa vita Duniani kwa sababu inaua uchumi kwa kufanya wauzaji wawe na pesa ndefu sana. Mtu anaingia bar alafu anakodisha bar yote kwa mda, just imagine kiburi cha pesa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Pia enzi hizo kuna misemo ilizuka " NTAKUPIGA .NTAKUUMIZA, ALAFU NTAKUTIBU". LAKI SI PESA. Kwahiyo hii inaleta negative impact kwenye uchumi
 
Mmojawapo ni huyu aliepo sasa hivi ashajivika cheo cha baba wa taifa tayari hata nyerere wanaona hafai tena mpaka wanafikiria kumpa atawale milele
[emoji23][emoji23]
 
Mmojawapo ni huyu aliepo sasa hivi ashajivika cheo cha baba wa taifa tayari hata nyerere wanaona hafai tena mpaka wanafikiria kumpa atawale milele
Tuvumiliane mkuu, Jk nae tukizungumza kama taifa alikuwa na shida zake
Kufanya nchi kuwa shamba la bibi halikuwa jambo lenye siha kwa taifa
 
JOESKY umesahau kuwa na ufisadi ulishamiri pia freedom of express ilikuwepo na hatukuona mapungufu Zaidi watu tulifurahia maisha ,ila awamu hii tunaweza kujiuliza izo ela zinaenda wapi? Na Tushafika uchumi mdogo wa Kati.
Ajira hamna.
Mishahara haingozeki,
Semina na posho zimefutwa ,
Lakini ngoja tusubiri JNHP , SGR, ujenzi wa vituo vya afya, shule, viwanja vya ndege viishe hafu tuone itakuaje,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
KWA KIFUPI,WAKATI WA UTAWALA WA KIKWETE FEDHA NYINGI ZILIZOKUWA ZIINGIE KWENYE HAZINA YA SERIKALI,ZILIINGIA MIFUKONI MWA WATU BINAFSI NA TAASISI BINAFSI KUPITIA UFISADI WA VIONGOZI NA WAFANYABIADHARA WACHACHE WAKUBWA..Unanikumbusha enzi za EPA,IPTL,MEREMETA,ISUE YA UMEME ILIYOKATISHA UWAZIRI MKUU WA LOWASA n.k.Tender nyingi za Serikali zilichukuliwa na WAKUBWA na watoto wao na WAFANYABIAshara WAKUBWA ambao Ni marafiki zao,HUKU WAKILIPA KODI KIDOGO SERIKALINI.Wananchi tulikuwa tunaliShwa makombo TU KUPITIA KUFANYA vibarua kwenye maduka yao makubwa,na vibarua kwenye miradi yao ya ujenzi wa mahekalu yao.Tender nyingi za Barabara na madaraja vilijengwa CHINI ya viwango.Barabara zilizojengwa enzi hizo lami yake leo Ni mashimo tupu,madaraja yao Karibu yote yalishazombwa na mvua za kawaida TU za masika.Kupitia tender "fake na miradi fake" HAZINA YA TAIFA ILIKAUSHWA.Wananchi wenzangu tuvumilie kidogo,matunda ya juhudi za RAIS Magufuli mtayaona baadaye.Chakula ndo kipo Jikoni Kinapikwa,Subirini kitaiva.KWA KWELI,RAIS MAGUFULI MUNGU AMUJALIE AFYA NA MAISHA NAREFU NA MIAKA MINGINE YA YA KUITAWALA TANZANIA HADI ATAKAPOFIKISHA UMRI WA KAMA RAIS JOE BIDEN NA AU UMRI WA The Late Maalum Sharifu Hamadi,NDIPO AACHE URAIS.
 
Bureau de change zilifanya jukumu lake ipasavyo,boss Majaji na Yanga vilikuwa imara kwelikweli,Mazao ya biashara mfano Korosho,ufuta,mtama vililipa kinoma na zaidi mtaani miradi ya ujenzi,biashara na mzunguko wa pesa uliendelea vzr,mikopo na benki kama yote!
 
Unasema fedha zote ziliishia mifukoni mwa watu binafsi lakini mleta mada anasema kila mwaka mishahara ilikuwa ikipanda je ndio ilikuwa ikilipwa na hao watu binafsi? Unazungumzia habari ya tenda je unaweza kutuambia tenda ya kujenga uwanja wa ndege Chato ilifanyika vipi au bajeti ya kwanza ya ununuzi wa ndege ilipitishwa na chombo gani zaidi ya maagizo na amri tu ambazo hazitakiwi kuhojiwa zaidi ya kusifu na kuabudu tu na hayo mabarabara unayodai yalijengwa chini ya usimamizi wa nani kama sio waziri husika na Tanroad ambao mpaka leo hao wahusika ni marafiki wa kufa na kuzikana ebu fikiria wao ndio wajenzi wa hizo barabara mbovu na bado wameshikana kama pete na chanda huku wakiendelea kupiga dili za huku wakipeana zawadi ya majina ya madaraja,vipi ununuzi wa ile boti ya mwendo kasi iliyotakiwa kupiga ruti za Dar to Bagamoyo ambayo haikuwa kupiga hata ruti moja mnunuzi unamjua na ndio huyo unayemsifia lakini unadai wakati huo watu walikuwa wanafanya vibarua tu kwenye maduka ya hao unaowaita mafisadi je leo ajira zipo? Leo hii kila mtu anatamani kuwa machinga ambao yeye anajifanya kuwatetea sana lakini ukiangalia kiundani ni anachonganisha watu kwa sababu huwezi kuwaambia hao machinga eti wafanye biashara kokote hata ikiwa kwenye baraza ya mtu bila idhini ya muhusika leo huko Kariakoo na maeneo mengine kote kumekuwa vurugu kuanzia magari hadi wapita njia kwa mguu kupita kwa tabu na wao ndio wababe yeye ametulia kimya anaangalia kama haoni kama sio uchonganishi ni nini? Haya ukiangalia barabara za mwendo kasi zilizongwa wakati wa Kikwete hadi zipo imara angalau hilo walilolianza wao kabla halijaanza kutumika limeanza kumong'onyoka huu sio ufisadi wa wazi kabisa? Kwa ufupi huyo unayempia debe amefeli kabisa.
Maelezo yamejitosheleza kabisa mkuu. Hongera kwa ufafanuzi
 
JOESKY umesahau kuwa na ufisadi ulishamiri pia freedom of express ilikuwepo na hatukuona mapungufu Zaidi watu tulifurahia maisha ,ila awamu hii tunaweza kujiuliza izo ela zinaenda wapi? Na Tushafika uchumi mdogo wa Kati.
Ajira hamna.
Mishahara haingozeki,
Semina na posho zimefutwa ,
Lakini ngoja tusubiri JNHP , SGR, ujenzi wa vituo vya afya, shule, viwanja vya ndege viishe hafu tuone itakuaje,

Sent using Jamii Forums mobile app
Awamu hii sijaona lolote jipya mkuu uingo mbaya mimi Rais wangu bado ni jk
 
Back
Top Bottom