James Mbatia amtaka Majaliwa ajiuzulu Uwaziri Mkuu

James Mbatia amtaka Majaliwa ajiuzulu Uwaziri Mkuu

Nilifikiri anamtaka ajiuzulu kwa kuudanganya uuma wa watanzania na dunia kwa ujumla juu ya afya ya Rais hayati JPM
Angesimama kwenye angle hii ingekuwa ni poa zaidi, kuliko huko alikopuyanga!
Ifike mahali kiongozi kwa makusudi akawadanganya wananchi outomatic awe amepoteza sifa za kuendelea kuwa kiongozi.
Kama hakuna unachoficha huwezi danganya! Uongo ndugu yake ni "mwizi"
Baba wa uongo ni "shetani"
 
Mbatia vyema kujua tz haitaki wanafiki Kama yeye, akalale huko , watu wameamuka kabla yeye amelala , binfsi sio mungu but mbatia hu mnafiki na ujumbe huu ukufikie popote ulipo ,asema bwana
 
Hicho kifungu kinahusu kaimu Rais hataweza kufanya mabadiliko kwakuwa Rais bado yupo isipokuwa madaraka yake yanatekelezwa na mtu mwingine kwa muda.
Acha zako wewe. Ni wapi ilipoandikwa kwenye katiba hiyo kuwa kifungu kidogo cha (10) ni kwa ajili ya rais aliyepatikana kupitia kifungu cha (7) na cha (8) tu, na hakihusu rais aliyepatikana kwa vifungu vidogo vya (3), (4) na (5). Kifungu hicho kimeandika wazi kumhusu rais yeyeote anakayepatikana chini ya aya ya 37 Katiba, ambayo ina vifungu vidogo 11 vikiwemo hivyo vya (3), (4), (5) na hivyo vya (7) na (8) ambavyo ndivyo wewe unaangalia badala ya kuangalia aya yote!

Kilichopo hapa ni kuwa katiba hiyo haikuandikwa vizuri, lakini ndiyo katiba tunayotumia na ni lazima tuifuate kifungu-kwa-kifungu hadi pale tutakapoibadilisha!
 
Majaliwa hana kosa wala hana sababu za kukosa usingizi. Kama madame president hana guts za kumtumbua na kuvunja baraza, who is to blame? It is certenaly not Majaliwa’s business

Ndio maana Bashiru na Majaliwa wanasema madame has no clue. Yeye anachojua ni kususasusa tuu na kufunga mitandio tu😊. Probably akasusa na kuresign before 2025
Mkuu.., hayo maneno ya kuwa "madame has no clue" Bashiru na Majaliwa wameyasemea wapi?
 
Kuna utofauti kati ya kutoa ushauri na kumpangia Rais cha kufanya.

Ushauri- Rais anaweza kuufuata au hasiufuate.

Kumpangia Rais cha kufanya- hapa Rais analazimika kufanya kitu, ikiwezekana bila hata utashi wake.(Sidhani kuna Raia hapa Tanzania anaweza kufanya hiki kitu except watu waliokaribu na Rais nayo ni mara chache).


Labda kama unataka watu wapunguze kutoa ushauri.


Umemjibu vizuri sana maana naona jamaa amepanic sana!

Kimshauri mtu siyo kumpangia mtu!
 
Mbatia amatoa maoni yake Wala sio Katiba/Sheria. Hivyo usitumie maoni yake kama Katiba.
Labda umekosea kuni-quote mkuu,au hakika ume ni kiquote mimi?

Mimi pia naungana na wewe hayo ni mawazo ya Mbatia,sio sheria wala katiba.
Ila kwenye hili majibu yawe ya kisheria/katiba inasemaje?
 
Acha zako wewe. Ni wapi ilipoandikwa kwenye katiba hiyo kuwa kifungu kidogo cha (10) ni kwa ajili ya rais aliyepatikana kupitia kifungu cha (7) na cha (8) tu, na hakihusu rais aliyepatikana kwa vifungu vidogo vya (3), (4) na (5). Kifungu hicho kimeandika wazi kumhusu rais yeyeote anakayepatikana chini ya aya ya 37 Katiba, ambayo ina vifungu vidogo 11 vikiwemo hivyo vya (3), (4), (5) na hivyo vya (7) na (8) ambavyo ndivyo wewe unaangalia badala ya kuangalia aya yote!

Kilichopo hapa ni kuwa katiba hiyo haikuandikwa vizuri, lakini ndiyo katiba tunayotumia na ni lazima tuifuate kifungu-kwa-kifungu hadi pale tutakapoibadilisha!
Zangu zipi jadili hoja usiwe na mihemko tulia soma ibara hiyo yote utaelewa maudhui yake imeelezea watakao kaimu nafasi Rais na namna ya makamu kuwa Rais kwa tafsiri yako maana yake mh Rais Samia hawezi tengua uteuzi wa waziri yoyote mpaka amalize 2025 ? Inaingia akilini?
 
Ni kweli Rais huwa harithi watu..hawa wote waliapa kiapo cha utii mbele ya Rais ambaye ni Marehemu,

Sasa wanatakiwa kuapa kiapo cha utii mbele ya Mama Samia.

Huwezi kufanya kazi na mtu mwenye kiapo kingine protocol inagoma hapo!!

Cha msingi ni ajiuźulu ama asipojiongeza basi mama avunje balaza lote aanze na Mwanasheria Mkuu!!

Tatizo CCM hawataafiki hoja hii...wazoefu wa kuvunja katiba na Protocol.
Mwishowe tutasema avunje na bunge uchaguzu ufanyike, Ili pia wabunge walio teuliwa naraisi aliyepita waachwe
 
Zangu zipi jadili hoja usiwe na mihemko tulia soma ibara hiyo yote utaelewa maudhui yake imeelezea watakao kaimu nafasi Rais na namna ya makamu kuwa Rais kwa tafsiri yako maana yake mh Rais Samia hawezi tengua uteuzi wa waziri yoyote mpaka amalize 2025 ? Inaingia akilini?
Katiba haileweki au Watanzania hatuelewi?
 
Rais Mpya atatushangaza Watanzania na dunia kwa ujumla iwapo ataendelea kufanya kazi na Baraza la Mawaziri ambalo hakuliapisha yeye kama Rais!
Ma DED, DC ,DAS, RAS, RC the list goes on...nao aache kufanya nao kazi kisa hakuwateua yeye na kuwaapisha yeye? Shida sio kuliapisha yeye , shida ni kwamba kuna ombwe kwenye Katiba
 
Sio vichwa vigumu bali ni wajuaji. Ndio maana ili utawale vyema ni muhimu kuwaziba midomo wapuuzi maana watakuyumbisha katika mission yako! Hiki ndio alikifanya Magufuli akaonekana katili ila dhamira ilikua njema kabisa.

Yani kuongoza Tanzania ni sawa na kufundisha darasa la wanafunzi 200 ukitarajia kutakuwa na hali ya utulivu na ustaarabu katika kuuliza maswali na majibu ila badala yake kila mtu ananong'ona na kuropoka ovyo bila utaratibu halafu kuadhibiwa hawataki.

Wana expect wafanyiwe ustaarabu ambao wao hawana, hao ndio watanzania bana.[emoji16]
Natamani kukupa likes 100 mkuu, Safi sana. Kuongoza hii nchi sio kazi rahisi, ujuaji na unafiki kuanzia juu hadi chini...
 
Majaliwa anatakiwa aonyeshe njia, anapaswa kujiuzuru ili kumpa nafasi mama Samia kuunda baraza lake la mawaziri.

Kitendo cha Majaliwa kung'ang'ania madaraka ni kitendo cha aibu kwa taifa na kinaweza kutoa ishara kuwa huenda Majaliwa ni mmoja ya wahusika wa lile genge lililohisiwa kuwa linataka kumpora mama madaraka ya kiti cha urais.

Majaliwa onyesha njia sasa.
Jiuzuru haraka iwezekanavyo.
Nimecheka Sana,aisee...
 
lichowekea rangi, kuwa mtu atakayechukua madaraka ya urais ama kwa kurithi kutokana na kifungu kidogo cha (3) (yaani rais kuondolewa madarakani na baraza la mawaziri) hadi kifungu kidogo cha (5) (yaani rais akifariki), hana madaraka ya kuvunja Bunge au Baraza la mawaziri au kutengua teuzi za rais aliyekuwapo.
Nafikiri ungesoma tena na kurudia tena na tena. Katiba ipo wazi kabisa ila wewe umeelewa vibaya. Kipengere namba 10 kinahusu mtu tu anayeweza tekeleza kazi za rais kwa kukahimishwa na si vinginevyo.
Swali, je wakati Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassani alipokuwa ni makamu wa Rais alikuwa na maamlaka kamili ya Urais? Jibu ni Hapana. Ila baada ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT anakuwa na mamlaka yote ya Urais.
Sasa ukija kwa Waziri Mkuu, kifung namba 51 ya katiba yetu kinasema hivi;

(1) Kutakuwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais kwa kufuata masharti ya ibara hii na ambaye kabla ya kushika madaraka yake ataapa mbele ya Rais kwa kiapo kinachohusika na kiti cha Waziri Mkuu kitakachowekwa na Bunge.

(2) Mapema iwezekanavyo, na kwa vyovyote vile ndani ya siku kumi na nne, baada ya kushika madaraka yake, Rais atamteua Mbunge wa kuchaguliwa kutoka katika Jimbo la Uchaguzi anayetokana na chama cha siasa chenye Wabunge wengi zaidi Bungeni au kama hakuna chama cha siasa chenye Wabunge wengi zaidi, anayeelekea kuungwa mkono na Wabunge walio wengi kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano, naye hatashika madaraka hayo mpaka kwanza uteuzi wake uwe umethibitishwa na Bunge kwa azimio litakaloungwa mkono na kura za Wabunge walio wengi.

(3) Bila ya kuathiri masharti mengineyo ya Katiba hii, Waziri Mkuu atashika kiti cha Waziri Mkuu hadi-
(a) siku ambapo Rais mteule ataapa kushika kiti chake; au
(b) siku ambapo atafariki dunia akiwa katika madaraka; au
(c) siku atakapojiuzulu; au
(d) siku Rais atakapomteua Mbunge mwingine kuwa Waziri Mkuu; au
(e) atakapoacha kushika kiti cha Waziri Mkuu kwa mujibu wa masharti mengineyo ya Katiba hii.

Majibu yote yapo kwenye 51 - (2) na (3a) yaani Mwanzo na Ukomo wa Waziri Mkuu Kikatiba
 
Zangu zipi jadili hoja usiwe na mihemko tulia soma ibara hiyo yote utaelewa maudhui yake imeelezea watakao kaimu nafasi Rais na namna ya makamu kuwa Rais kwa tafsiri yako maana yake mh Rais Samia hawezi tengua uteuzi wa waziri yoyote mpaka amalize 2025 ? Inaingia akilini?
Hujasoma ibara hiyo; ina vifungu vidogo 11; umevisoma vyote? Nitajiaraibu kukufafanulia kama ifuatavyo.

Ibara ya 37 inahusu utejkelezaji wa kazi na shughuli za Rais aliyeko madarakani

Kifungu kidogo cha (1) kinasema rais halazaimishwi kufuata maoni ya washauri; hiyo ikiwa ni pampoja na baraza la mawaziri.

Kifungu kidogo cha (2) kinasema rais anaweza kuondolewa madarakani na baraza la mawaziri.

Kifungu kidogo cha (3) kinaweka utaratibu wa kumpata rais mwingine iwapo baraza la mawaziri litaamua kumuondoa madarakani rais aliyepo

Kifungu kidogo cha (4) kinaweka utaratibu wa kumpata rais mwingine iwapo baraza la mawaziri litaamua kumuondoa madarakani rais aliyepo ambaye hakidhi matakwa ya kifungu kidogo cha tatu.

Kifungu kidogo cha (5) kinaweka utaratibu wa kumpata rais mwingine iwapo kiti hicho kitakuwa wazi kutokana na rais aliyekuwapo kufariki, kupoteza sifa za uraisi na sababu nyinginezo.

Kifungu kidogo cha (6) kinazuia kumuondoa madarakani prematurely rais aliyepo madarakani

Kifungu kidogo cha (7) kinazuia kinaweka utaratibu wa rais kumteua mtu mwingine kukaimu nafasi ya urasi wakati rais mwenyewe hawezi kuyatekeleza

Kifungu kidogo cha (8) kinazuia kinaweka utaratibu wa rais kudelegate sehemu ya madaraka yake kwa waziri yoyote na jinsi ya utekelezaji wa madaraka hayo

Kifungu kidogo cha (8) kinazuia kinaweka utaratibu wa rais kudelegate sehemu ya madaraka yake kwa waziri yoyote na jinsi ya utekelezaji wa madaraka hayo

Kifungu kidogo cha (9)-hiki ni redundant- kinahalalisha maamuzi ya baraza la mawaziri kwenye kifungu kidogo cha (2) na vile vile kinasistiza kuwa kuwa kifungu kidogo cha (7) hakimwondoi madarakani rais aliyepo.

Kifungu kidogo cha (10) kinaweka ukomo wa mamlaka ya rais yeyote aliyepatikana kwa kupitia vifungu hivyo hapo juu kuhusu Bunge wateule walioachwa na rais aliyekuwapo. Hiki ndicho kina matatizo sana, kwani kimeandikwa kuonyesha kuwa kuwa rais akishafariki, basi hata Bunge halitavunjwa tena ambavyo ni kupingana na sehemu nyingine za katiba!! Lakini kwa sasa ndivyo katiba yetu ilivyo!

Kifungu kidogo cha (11) kinasema kuwa iwapo mbunge wa kuchaguliwa akipata madaraka ya urais kupitia aya hii ya 37 (yaani kifungu kidogo chochote kuanzia cha (1) hadi (10)) hatapoteza sifa za ubunge.

Hivyo ndivyo katiba yetu ilivyo. Sasa wewe nionyeshe ni kifungu gani kinachoweka ukomo wa matumizi ya hicho kifungu kidogo cha (10) cha katiba!
 
Back
Top Bottom