James Rugemalira aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka

James Rugemalira aachiwa huru, DPP hana nia ya kuendelea na mashtaka

Salaam Wakuu,

Leo nimepita maeneo ya Mahakama ya Kisutu, Nikakuta Mkurugenzi wa kampuni ya VIP na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL, James Rugemalira anatabasamu akiwa na ndugu zake wakipeana hugs na kuchumiana. Inaashilia kuna dalili nzuri leo Mzee wa Henken akaliona jua. Langu Dua.

_MG_0435.JPG
James Rugemalila(Kulia) na mmiliki wa Kampuni ya IPTL, Harbinder Seth Sigh(Kushoto), wakiwa chini ya ulinzi wa Polisi kabla ya kupanda kizimbani Mahakamani Kisutu Jijini Dar.

Tarehe 19 Jun, 2017 TAKUKURU wawafikisha mahakamani Seth Na Rugemalila kwa uhujumi uchumi. walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu wakishtakiwa kwa makosa sita ya uhujumu uchumi, likiwamo la kuisababisha Serikali hasara ya jumla ya takriban Sh358 bilioni.

Wakili wa Serikali, Paul Kadushi aliyataja mashtaka mengine yanayowakabili wawili hao kuwa ni kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu na kuisababishia hasara Serikali.

Zaidi Soma:

1). TAKUKURU yawafikisha mahakamani Harbinder Sethi na James Rugemalira kwa kosa la Uhujumu uchumi

UPDATE:

Rugemalila yupo huru!

Mashtaka yake yameondolewa chini ya kifungu cha 91(1) cha Mwanendo wa Makosa ya Jinai


Ushahidi tosha ya udhalimu wa Mwendakuzimu na udhaifu wa mfumo wa kusimamia haki nchini ni huu hapa.

Yaani ng’ombe mmoja aliyetokea Chato aliweza kuvifanya vyombo vyetu vitende kila alichokitaka yeye bila kujali wapo sahihi au la!

Popote alipo huyo ng’ombe afe tena.
 
Wandugu

Huyu mzee Rugemalira leo hataweza kulala kwenye godoro. Kila akijaribu kulala atakuwa anaona kama anazama ndani ya godoro.

Hii hali ni kutokana kashazoea kulala kwenye kitu kigumu/sakafu kwa miaka minne. Hivyo basi mke na wanafamilia wasije huzunika kuona mzee wao anakataa kulala kwenye godoro, wajue hio ni hali ya kawaida.

Itachukua mda akili yake kujiadjust kupokea mazingira mapya.

Sijajua ukweli nachoweza kusema huyu mzee Rugemalira amekuwa mfano mzuri katika philosophy za Ustoic.

Misingi mikuu hii philosophy inafundisha ni juu ya kutambua mambo yaliyo ndani ya uwezo wetu na mambo yalio njee.

Mzee alitambua mapema kukubali au kukataa mashtaka yapo ndani ya uwezo wake na kufungwa, kuabishwa kupo nje ya uwezo wake, hali kadhalika watesi wake waliweza kumweka ndani na kushindwa kupata tubu yake.

Yapo mengi ya kujifunza na hakuna wa kulaumu katika hizi pande mbili kinzani kwani ubora wa Rugemalira unatokana pia na ubora katika kutenda hayo kinyume na haki kwa watesi wake.

Alamsiki
Hii Tz ina matabaka, wanasiasa hawakufungwa kabisa lkn luge na mwenzake wamesota balaa
 
Mkuu hi kesi wapinzan wakina Lissu nawenzie si ndio waliitolea macho na kushikilia kidete pale bungeni mpka kutoa maamuzi hayo Sasa Magu kosa lake ni lipi maana yet alitekeleza vile bunge lilivyotaka
Kina Lissu walitaka kesi iendeshwe na uamuzi wa mahakama upatikane kwa wote waliohusika. Sio kukamata watu wawili, watatu na kuwaweka ndani indefinitely. Kosa la Magufuli ni kutoruhusu mahakama ifanye kazi yake na, badala yake, kumtuma DPP kujadiliana plea bargain ili kujipatia mgao wa ufisadi jambo ambalo limeacha mafisadi kutochukuliwa hatua stahiki za kisheria.

Usifikiri akina Lissu walikuwa wanawaonea huruma kina Ruge na Singa. La. Walitaka ukweli ujulikane kupitia mahakama na wote waliohusika wachukuliwe hatua. Serikali za JK na Magu hazikuwa tayari kutokana na "unyeti" wa suala hilo kwao.
 
Haki imeshinda. Mara baada ya kuachiliwa huru, ameenda kanisani kusali na kumshukuru Mungu. Alimwachia kila kitu Mungu, akabaki na rozari yake shingoni and he would say it daily. Hata sasa Mungu amemsaidia.
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Kweli nchi ilikuwa inaendeshwa mjinga wa mihemko ya kijingajinga...
Yule mfu hata angekuwa anapumulia machine angelazimisha kesi iendelee na mahakama yake ya kipuuzi ya miaka ya 80 ya uhujumu uchumi
Karudisha nchi nyuma sana mpaka dunia imesahau kuna nchi inaitwa Tanzania....
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Kweli nchi ilikuwa inaendeshwa mjinga wa mihemko ya kijingajinga...
Yule mfu hata angekuwa anapumulia machine angelazimisha kesi iendelee na mahakama yake ya kipuuzi ya miaka ya 80 ya uhujumu uchumi
Karudisha nchi nyuma sana mpaka dunia imesahau kuna nchi inaitwa Tanzania....
Wewe inaonekana ni mtoto wa fisadi, ndio maana una chuki na Magufuri.Magufuri amewaenyesha Mpaka kiburi kikawaisha,zile zama za unanijua me nani alizikomesha, kipindi cha Magufuri Mafisadi wameionja joto ya jiwe,huyo Lugemarila wenu hawezi kurudia mchezo wake wa kuchora madili ya kuibia serikali tena.
 
Wewe inaonekana ni mtoto wa fisadi, ndio maana una chuki na Magufuri.Magufuri amewaenyesha Mpaka kiburi kikawaisha,zile zama za unanijua me nani alizikomesha, kipindi cha Magufuri Mafisadi wameionja joto ya jiwe,huyo Lugemarila wenu hawezi kurudia mchezo wake wa kuchora madili ya kuibia serikali tena.
Ndio sisi mafisadi tumeshirikiana mabeberu kumchapa na covid...
Ameshakufa huyo hafufuki....
Kwisha habari yake.....
 
Ndio sisi mafisadi tumeshirikiana mabeberu kumchapa na covid...
Ameshakufa huyo hafufuki....
Kwisha habari yake.....
Hata Wewe nawe siku yako ya kufa itafika,tena utakufa kifo kibaya, akuna mtu atakeyetamani kuona maiti yako
 
Mafisadi wanazidi kujikusanya na kufufua team yao chini ya mama samia the killer one
Tafuta pesa, wivu wa kimasikini utakufanya uishi maisha ya kifukara huku ukilialia na kumuita kila aliyefanikiwa fisadi. Upumbavu na wivu wa kishamba wa Jiwe umfuate huko huko kaburini kwake. Narudia tena, tafuta pesa.
 
Mafisadi wanazidi kujikusanya na kufufua team yao chini ya mama samia the killer one
Huwezi kumfunga Lugemalila ukamuacha Kikwete , ile ilikuwa uonevu , yeye alikuwa mwakilishi wa VIP , nani aliyeleta IPTL , kwanini aliachwa ?
 
Wewe inaonekana ni mtoto wa fisadi, ndio maana una chuki na Magufuri.Magufuri amewaenyesha Mpaka kiburi kikawaisha,zile zama za unanijua me nani alizikomesha, kipindi cha Magufuri Mafisadi wameionja joto ya jiwe,huyo Lugemarila wenu hawezi kurudia mchezo wake wa kuchora madili ya kuibia serikali tena.
Kipindi cha Jiwe 'unajua mie nani' ndipo ilikithiri kutoka kwa 'wasiojulikana', sasa raia at least wanapumua na Rugemalira yuko huru na biashara zake zitaendelea kama ilivyokuwa awali. Wenye vijiba vya roho shauri zao.
 
Kuna watu walikufa kwa kukosa madawa hospital,wamama walikosa vitanda vya kujifungulia wakati mke wake akijifungulia Marekani, watoto walikosa madawati,wakati wakwakwe akipeleka Ulaya,acha akomeshwe, sasahivi awezi rudia dili zake za kuibia serikali
Wale wanasiasa walioshirikiana nae kupiga Mbona hawajakomeshwa Sasa
Itatuchukua miaka mia 100 kupevuka kiakili. Afungwe asifungwe si jambo linalonihangaisha mimi sana. Kwangu ni kuona haki inatendeka na mahakama ndio chombo kinachotoa haki. Chombo hiki kikijikita na kuendeshwa kisiasa tumekwisha. Tukaweka ushabiki mbele kwa kitu tusichokijua ni akili ya ujima.

Maamuzi ni yetu, kama tumeridhika baada ya miaka 60 kuishi hivi tunavyoishi au kuwawinda wanaochelewesha maendeleo yetu.
Ukiambiwa katiba mpya ccm hamtaki. Mnataka hii ya kimagumashi inayoruhusu dpp kumfunga ama kumuachia mtu vile anavyojisikia
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Imagine, angefanya alivofanya Harbinder watu wangesema haki imetendeka ila sasa wanajua kuwa nchi hii unaweza kaa gerezani muda wwt visivo halali. Maana hata ile ya ku.kamata na kumfunglia shitaka upya, wamegwaya. Ndo ujue DPP anaposema wanatenda "Haki", wanachomaanisha ndo hicho! Miaka 4 "Upelelezi Haujakamilika", lakini lipa utoke, halafu yanaishia hapo - bila kujali ikiwa atadai fidia italipwa na nani, Za kodi au za mfukoni! Wanachezea maisha ya watu kutokana na madaraka yao, hawajali. Kila kitu kina mwisho
Jambo la kheri, yeye aligoma kabisa kukiri kosa na kulipa fidia?
 
JK alituambia zile hela ni mali ya IPTL tukamuoma mjinga na kumnanga kila kona...

Ni ngumu sana kuwaelewa watanzania na Tanzania juu ya haya yanayotokea, nafikiri hata dunia kuna mahala inatuona ni species tofauti..

tulipiga sana kelele JK alipoacha kuchukua hatua juu ya Ruge na Singasinga, tukamuita dhaifu na zihaka nyingi sana...Wanasiasa wetu tunaowashabikia wakashupaza shingo bungeni,, Hatimaye JPM akasikia kilio na kuwatia mkononi Singa na Ruge, Watanzania walewale wakamuita JPM dikteta na leo wanashangilia Ruge kuachiwa na kumdhiki marehemu JPM...

Kwa akili hizi ni bora CCM ikaendelea kutawala miaka mingine 300 labda kitakuja kizazi kinachojielewa...
 
Mama akileta Tozo tuache kulialia..maana hawa wote wanaotoka wanaweza kuishitaki serikali na kudai mabilioni ya fidia...Serikali itabidi itukamue kufidia hizo fidia....
 
Back
Top Bottom