Japhet Maganga wa CWT akamatwa kwa kufanya fujo

Japhet Maganga wa CWT akamatwa kwa kufanya fujo

Wajaluo kwao ni Kenya,tena Kisumu...specifically, usilazimishe! Huyo jamaa yako Otieno ni mkenya... Arudi kwao tu, mbona Kenya kuna Polisi pia?
Nani kakuambia hata Sudan wako wajaluo,na huko ndiko chumbiko lao
Nigeria pua wa luo wapo

Ova
 
Huu ni mjadala mpana ambao tena ni wa kitaifa na bado umenajisiwa kwa muda mrefu, badala ya kuhoji ametanguliza matusi... Niambie kama Verified member hapataswi kujibu mapigo?.
Mkuu unless uwe unamfahamu Kwa undani zaid ila Martin Otieno ni jina la kijaluo na wajaluo ni wenyeji wa wilaya ya rorya hasa shirati,utegi na maeneo mengine ya rorya. Ebu justify hapa hayo madai yako.
 
So we acha tu uhamiaji wafanye kazi yao.
Otieno ni jina au ubini wa wajaluo ambao wanapatikana Kisumu zaidi lakini kusini magharibi mwa Kenya. Ushahidi ulioutoa kwa mifano kwa watu uliowahisi kuwa warundi hauna tofauti na kumhoji Otieno aliyepo Tanzania kwa kuwa kuna County nchini kenya inayofahamika kama eneo lenye idadi kubwa ya wajaluo tena wenye ardhi na urithi wao, kuwepo Tanzania au Uganda bado hakuhalalishi kuwa watanzania mpaka point iliyopo hapo juu itekelezwe.
 
Otieno ni jina au ubini wa wajaluo ambao wanapatikana Kisumu zaidi lakini kusini magharibi mwa Kenya. Ushahidi ulioutoa kwa mifano kwa watu uliowahisi kuwa warundi hauna tofauti na kumhoji Otieno aliyepo Tanzania kwa kuwa kuna Count nchini kenya inayofahamika kama eneo lenye idadi kubwa ya wajaluo tena wenye ardhi na urithi wao, kuwepo Tanzania au Uganda bado hakuhalalishi kuwa watanzania mpaka point iliyopo hapo juu itekelezwe.
Kwahiyo wewe ni afisa wa uhamiaji mpaka useme Otieno arudi kwao Kenya?
 
Ukikosolewa kubali. Ulibugi stepu pale uliposema kwa sababu ana jina la Otieno basi ni mkenya. Hukufikiria sawasawa. Jina haliwezi kuonyesha utaifa wa mtu. Tuna watanzania wanaoitwa Mackenzie na siyo watu wa Ulaya. Otieno Tanzania wapo wengi.
Huu ni mjadala ambao unajadiliwa mara kwa mara humu na una dalili za ndimi mbili. vigezo vya majina na ubini ndivyo vinavyotumiwa na Jeshi letu la uhamiaji kuwanyanyasa watu wa mipakani hasa mikoa ya Kigoma na Kagera. Majina ya Otieno asili yake ni Kisumu Kenya, Kwa nini mtu anaanzisha matusi humu badala ya kujadili hoja? Kwa nini kuwe na double standards huku raia wa mipaka na Kenya, Mbeya,Ruvuma, au Zanzibar wasiguswe?
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga, na wenzake 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya fujo kwenye mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho wakati wakipitisha bajeti ya mwaka.

Tukio hilo lilitokea baada ya baraza hilo kuazimia kumsimamisha kazi Maganga kutokana na kupoteza sifa baada ya kufukuzwa kazi na mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, amethibitisha kukumatwa kwa kiongozi huyo pamoja na wenzake wakati wa mkutano huo.

“Tulipata taarifa kuwa kuna watu wanafanya fujo tukaenda kudhibiti kabla hayajatokea madhara. Kwenye mkutano huo sisi hatufahamu ilikuwaje zikatokea fujo. Ukitaka kufahamu zaidi waulizwe CWT wenyewe,” amesema Kamanda Otieno.

Source - Nipashe
Hawa watu wa ccm na madaraka ni kama wamelogwa.

Imagine mtu kama huyu kafukuzwa Mchana kweup na bado anang'angania.

Je huyu akiwa Rais atakuwa tofauti na Magufuli?

Inaonekana ni mtu jeuri na mkatili sana
 
Kwahiyo wewe ni afisa wa uhamiaji mpaka useme Otieno arudi kwao Kenya?
Hilo nimemjibu aliyeanza kunitusi kwa kuhoji tu kuwa : Otieno si majina ya Kenya haya?... Hivi kulikuwa na sababu ya kuhamaki zaidi ya kujadili kwa hoja? Mimi sio afisa uhamiaji lakini naona na kusikia kauli kama niliyoitoa ikitolewa na watu humu, ikiwalenga watu wa Kigoma zaidi.
 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga, na wenzake 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa tuhuma za kufanya fujo kwenye mkutano wa Baraza Kuu la chama hicho wakati wakipitisha bajeti ya mwaka.

Tukio hilo lilitokea baada ya baraza hilo kuazimia kumsimamisha kazi Maganga kutokana na kupoteza sifa baada ya kufukuzwa kazi na mwajiri wake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Martin Otieno, amethibitisha kukumatwa kwa kiongozi huyo pamoja na wenzake wakati wa mkutano huo.

“Tulipata taarifa kuwa kuna watu wanafanya fujo tukaenda kudhibiti kabla hayajatokea madhara. Kwenye mkutano huo sisi hatufahamu ilikuwaje zikatokea fujo. Ukitaka kufahamu zaidi waulizwe CWT wenyewe,” amesema Kamanda Otieno.

Source - Nipashe
Ukishajambiana na CCM wewe kaza wala usirudi nyuma.

Ukigeuka nyuma unageuka jiwe la chumvi na utarambwa ukose wa kukutetea
 
Back
Top Bottom