Je, Baba askofu wa Kanisa Katoliki anaweza kugombea Ubunge?

Je, Baba askofu wa Kanisa Katoliki anaweza kugombea Ubunge?

Mh askofu Ni cheo Cha juu zaidi ya ubunge
Ukitaka kujua mtafute askofu mstaafu
Na mbunge Alie pigwa chini
Pili askofu Ni mtuu anaandaliwa muda mrefu na anapimwa toka mtoto
Ubunge Ni kazi ya urafiki na watu zaidi
Ikitokea akagombea atakuwa ameshusha
huu uongo uliambiwa na nani?
 
Nauliza tu wadau kama baba askofu wa Kanisa Katoliki anaweza kugombea ubunge.

Kwa mfano baba askofu Ruwaich anaweza kugombea ubunge jimbo la Ilala?

Maendeleo hayana vyama!
It is Impossible....kanisa katolik Lina misingi na kanuni zake...yaani uamuzi hauwezi kufanywa na yeye Bali mpaka aombe kibali kutoka Vatican kwa Pope...ni kazi ngumu mno...
 
Mh askofu Ni cheo Cha juu zaidi ya ubunge
Ukitaka kujua mtafute askofu mstaafu
Na mbunge Alie pigwa chini
Pili askofu Ni mtuu anaandaliwa muda mrefu na anapimwa toka mtoto
Ubunge Ni kazi ya urafiki na watu zaidi
Ikitokea akagombea atakuwa ameshusha
Hakuna mtu anayeandaliwa kuwa Askofu bali anaandaliwa kuwa Padre. Na Padre yeyote anaweza kuwa Askofu. Kitu msichokijua ni kwamba hata Pope Francis hana tofauti na padre yeyote bali kile ni cheo kilichowekwa na kanisa. Kuna siku vijana waliobadili dini kutoka uislamu kwenda Ukatoliki walimuuliza padre mmoja anaitwa Padre Peter Morgan, ni paroko wa parokia mmoja Liverpool, kwamba nini tofauti ya yeye na Francis Papa. Akawaambia kwanza wote ni mapadre ila mmoja ni kiongozi wa ngazi ya juu. Hivyo hilo swala la kwamba wanaandaliwa wakiwa wadogo kuwa maaskofu ni uongo wa hali ya juu na uliotukuka.

Maaskofu wanapendekezwa na kwa tabia zao, majina matatu yanapelekwa kwa Pope yeye analichagua moja na kurudisha kwa waliolipeleka na hivyo kuwa Askofu Mteule kabla hajawekwa wakfu. Askofu Filbert Mhasi kwa mfano wa jimbo la Masasi, nilikua naye Seminarini kabla sijaacha na alikua nyuma yangu madarasa manne na nilikua kiranja wake na mpaka anateuliwa hakujua kabisa kama angekuwa Askofu. Hata alipopigiwa simu na mjumbe wa Baba mtakatifu hakujua kwanini alipigiwa simu.

Jaribuni kuandika vitu mnavyovijua ama fanyeni utafiti kabla hamujawadanganya watu hapa kwenye Forums
 
mkitaka kujua kwanini mapadre na maaskofu wakatoliki hawajishughulishi na shughuli za kisiasa na serikali jaribuni kupitia sheria zao kasomeni: Canon 285 Code3 ya 1983 ambayo inajulikana pia kama 1983 CIC (codex luris canonic) ama Johanno-Pauline Code kwa maana ilipitishwa wakati wa Pope John Paul wa Pili January 25 mwaka 1983 na 1917 code of canon law ijulikanayo pia kama Pio-Benedictine Code
 
Marehemu lwakatare alikuwa askofu mchungaji wa mlima wa moto hivyo hata gwajima na wengine wanaweza kuwa
 
Sababu iliyomtoa uaskofu padre Mtega ni kushiriki siasa kwa kukumsaidia Slaa kuingia ikulu 2010
Licha ya kushika madaraka hawaruhusiwi kushiriki siasa kwa lengo la kunufaika binafsi na huyo kiongozi au hiyo kampeni
 
Kwanza askofu wa Kanisa Katoliki akigombea ubunge anakuwa amejishusha sana, ni sawa na rais agombee udiwani. Pili Kanisa haliruhusu maaskofu na mapadre kuchukua nafasi za kisiasa labda kwa ruhusa maalumu ya Papa. Kuna askofu Amerika ya Kusini aliruhusiwa na Papa kuwa rais wa nchi kwa rukra maalumu na katika mazingira maalumu. Nafikiri ilikuwa kipindi cha mpito tu. Mara nyingi njaa ndio zinazowapeleka watu kugombea nafasi za siasa. Wahudumu wa Kanisa Katoliki hawana njaa hizo.
COVID-19 imeyumbisha sadaka na miujiza ya misukule hailipi tena.
 
Nauliza tu wadau kama baba askofu wa Kanisa Katoliki anaweza kugombea ubunge.

Kwa mfano baba askofu Ruwaich anaweza kugombea ubunge jimbo la Ilala?

Maendeleo hayana vyama!
Hiyo itakua ni kumshushia hadhi na pia Catholic Wana Mambo Yao hapa Duniani..ni mhimili uliojichimbia Chini zaidi kwenye mataifa mengi.
 
Hata mapadre kwa sasa hawawezi zamani Dodoma alikuwepo mbunge Nakumbuka pdr Disuza
 
Canon Law No 285(3): "Clerics (bishops, priests and deacons) are forbidden to assume public office whenever it means sharing in the exercise of civil power."

Does the same law allow clerics to engage themselves in politics or be partisan to a political party?
 
Kama kuna tungo tata, hii ni mojawapo. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema (kwa fasili ya Kiingereza ambayo ndiyo fasili rasmi: Ibara ya 1(3): The Republic is a secular...state..." Ina maana Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 'haina dini rasmi' (kama ilivyo kwa baadhi ya nchi kwa mfano, dini ya nchi ya Uingereza ni 'Anglicanism', Poland ni Roman 'Catholicism', Morocco ni Sunni Islam, Israel ni 'Judaism', Cambodia ni 'Buddhism' etc.

Kama nchi haina dini rasmi haina maana wananchi wake hawana dini rasmi. Ina maana kila mwananchi wa Tanzania anaamini au haamini katika dini fulani. Na kila mwanachi ni mwanasiasa, lakini siyo kila mwanasiasa ni muumini wa dini fulani. Kwa hiyo, muumini au kiongozi wa dini akisema kitu fulani kinachohusiana na siasa, kwa vile yeye pia ni mwananichi, mpiga kura na mlipa kodi, akiona kuna sehemu mambo hayaendi, akisema 'mambo hayaendi...' siyo kwamba amechanganya dini na siasa. Anayechanganya dini na siasa ni kwa mfano anayempigia debe mtia nia wa cheo fulani katika nchi au chama cha siasa. Siasa maana yake ni the art of governance of its country and people'. Na kila muumini ni mwanadamu (yaani mwanasiasa). Kwa hiyo, kila mwanadini ni mwanasiasa, ila siyo kila mwanasiasa ni mwanadini/muumini wa dini fulani. Mfano, huwa tunawasikia viongozi wetu wakisema "viongozi wa dini mna mchango mkubwa sana kwenye jamii. Mtusaidie kuwaasa vijana wawe waadilifu, kutokomeza maambukizi ya virusi vya ukwimwi etc."Je, ni kuchanganya dini na siasa? Lakini kuna viongozi wa dini pia huwa wanasema: "wanasiasa wanapaswa kutenda haki ili tuwe na jamii inayojali utu, utawala wa sheria na uwajibikaji..." Je, kiongozi wa dini akisema hivi anachanganya dini na siasa? Kwa wa upande wangu, akisema hivyo ametimiza wajibu wake kama Mtanzania na pia kama kiongozi wa dini anayewaongoza waumi wake ambao kati yao ni wanasiasa pia kwa sababu kama hakuna siasa yenye tija nchini hata dini haifuatwi vizuri. Na kama wanasiasa wanaosali kama hawataambiwa hivyo, kiongozi wa dini anayewaongoza anakuwa hajatimiza wajibu wake.
Uko sahihi.

Kwa maana rahisi [japo haiko halisi] serikali ni watu, na sio viongozi walioko madarakani, ambao tunawaita "watawala".

Dini [kwa tafsiri rahisi] ni imani na kuabudu kwa vitu/Mungu/miungu iliyo zaidi ya binadamu (sisi).

Siasa [tafsiri binafsi na rahisi] maana yake inahusishwa na uongozi/utawala wa watu au eneo kwa "mtazamo/mlengo fulani".

Serikali haina dini, ikiwa na maana watu wa nchi au eneo husika wana "imani" tofauti [ikiwa wana imani moja wanaweza kutamka/kuwa na dini].

Dini haina siasa maana yake, Dini haina "mtazamo au mlengo wa kitawala" isipokuwa msingi wa dini ni "imani" na maandiko matakatifu ya dini husika.

Hivi havichangamani, hata ikiwa kiongozi wa kisiasa atazungumza jambo la kisiasa kwenye uwanja wa dini, haimaanishi amechanganya dini na siasa.

Hata ikiwa kiongozi wa dini atazungumza jambo la kisiasa kwenye uwanja wa dini, haina maana kachanganya vitu hivi viwili.

Cha msingi ni maudhui ya kinachozungumzwa kwa wakati huo, na athari ya kinachozungumzwa...je kina madhara nje ya wigo wa eneo lake la kiuongozi au la!!
 
Canon Law No 285(3): "Clerics (bishops, priests and deacons) are forbidden to assume public office whenever it means sharing in the exercise of civil power."
... baada ya Bible, Canon Law ndio document iliyosukwa zaidi.
 
Na ndiyo maana, maparokia mbalimbali yalishawahi kufiwa na maparoko wao, lakini maparokia hayo yapo vile vile... Lao hii mtazame Kakobe na kanisa lake...
... ha ha ha! Kanisa linazeeka kwa speed ile ile anayozeeka mwanzilishi wake! Tumwombee maisha marefu ili angalau kanisa liendelee kuwepo.
 
Uko sahihi.

Kwa maana rahisi [japo haiko halisi] serikali ni watu, na sio viongozi walioko madarakani, ambao tunawaita "watawala".

Dini [kwa tafsiri rahisi] ni imani na kuabudu kwa vitu/Mungu/miungu iliyo zaidi ya binadamu (sisi).

Siasa [tafsiri binafsi na rahisi] maana yake inahusishwa na uongozi/utawala wa watu au eneo kwa "mtazamo/mlengo fulani".

Serikali haina dini, ikiwa na maana watu wa nchi au eneo husika wana "imani" tofauti [ikiwa wana imani moja wanaweza kutamka/kuwa na dini].

Dini haina siasa maana yake, Dini haina "mtazamo au mlengo wa kitawala" isipokuwa msingi wa dini ni "imani" na maandiko matakatifu ya dini husika.

Hivi havichangamani, hata ikiwa kiongozi wa kisiasa atazungumza jambo la kisiasa kwenye uwanja wa dini, haimaanishi amechanganya dini na siasa.

Hata ikiwa kiongozi wa dini atazungumza jambo la kisiasa kwenye uwanja wa dini, haina maana kachanganya vitu hivi viwili.

Cha msingi ni maudhui ya kinachozungumzwa kwa wakati huo, na athari ya kinachozungumzwa...je kina madhara nje ya wigo wa eneo lake la kiuongozi au la!!
Uko sahihi. Lakini ukumbuke kuwa muumini wa dini anafungwa pia na sheria za nchi (au utaratibu wa utawala wa nchi na watu wake - ambao kwangu ndiyo siasa au tuseme ambao ni sehemu ya siasa). Kuna mwanasheria mmoja na mwalimu wa mambo ya jamii Paulo Freire anatoa mfano mzuri wa kuishi imani na siasa (in a cross-fertised way) kwa kulinganisha pande mbili za ngazi (ladder) - mhimili wa kushoto na kulia - moja kama imani na mwingine kama siasa). Kwamba ukitaka kupanda ngazi vizuri lazima ushike mihimili hii miwili kwa pamoja - i.e ukitaka uwe 'well-integrated' ni lazima imani yako ishirikiane na siasa kukufanya wewe uwe mtu mwema. Yaani, ni kwamba imani yako inachangamana na siasa na siasa inachangamana na imani (in a cross-fertised way). Maana yake ni nini? Maana yake ni kwamba mtu wa namna hiyo anaishi imani yake vizuri na wakati huohuo anaishi siasa yake vizuri tofauti na wale wakiwa nje ya nyumba ya ibada wanavua koti la imani na kuvaa koti la siasa na kinyume chake.

Watu wa namna hii kwa upande wangu ni 'opportunists' na katika maisha yao kuna 'dualism'. Mfano, kuna watu wanashiriki kuchoma moto vibaka mtaani kwa kuiba kuku, bata, TV set etc, lakini watu walewale wakiwa kwenye nyumba za ibada ndiyo wanaohubiri 'Mungu ni upendo na mwenye huruma na anataka na sisi tupendane na kusameheana'. Lakini 'well-integrated person' hawezi kumwua mtu mwenzake kwa kuiba bata, kuku, TV set etc kwa sababu anajua wazi kwamba licha ya kwamba Amri za Mungu zinakataza kuua, hata sheria za nchi pia zinakataza kujichukulia sheria mkononi maana kuna utaratibu wa kisheria wa kumpeleka mtuhumiwa wa wizi kwenye vyombo vya sheria na kuacha sheria ichukue mkondo wake. Hivyo, inategemea na uelewa wa mtu namna gani ana'practise' imani na siasa bila shida, ingawa wengine shida inaonekana waziwazi, mfano, mtumishi wa Mungu kuanza kuwanadi wagombea nafasi fulani za kisiasa madhahabuni au mwanasiasa kutumia madhahabu kunadi sera zake au kuwatumia waumini wake wamchague yeye kwa vile ni mwenzao na siyo kwa vile wanaona ana sifa za kuwa kiongozi bora etc.
 
Back
Top Bottom