Je, harusi ya Adam na Hawa ilifanyikia wapi, nani aliwafungisha ndoa?

Je, harusi ya Adam na Hawa ilifanyikia wapi, nani aliwafungisha ndoa?

Sababu tunakosea ba hatujakamilika mlango wa toba uko wazi muda wote.



kutokana na kauli hiyo uliyotoa. nikisema Mungu kakusudia kumuumba mtu ili akafanye makosa nitakuwa nakosea?



Si kweli hapa inabidi uthibitishe kauli yako, si uishie kusema tu.

Ndiyo maana tunaambiwa kila mwanadamu ni mkosani, na mbora ya wakosaji ni mwenye kutubia.

Mola amemuumba mja ili amuabudu. Hili lina ushahidi.



Soma kwa umakini unachokiandika na ujue wapi ulipoegemea.

Sasa ulitaka nisemaje ? Sasa wapi nimepinga kwamba mwanadamu hakosei ?
ukipitia vizuri hizo post tokea awali nilikwambia ya kwamba kitendo cha wewe kukiri kuwa binadamu anakosea kwavile hajakamilika kinathibitisha kuwa Mungu ameumba watu makusudi ili wakosee. Nasema hivyo kwasababu Mungu ni muweza wa vyote hivyo alikuwa anaweza kuumba watu wakiwa wakamilifu wasiofanya hata chembe ya kosa. Au unakataa kuwa Mungu angeshindwa kuumba watu waliokamilika ambao wasingeweza fanya makosa?
 
Sasa mbona unajikanganya mzee ? Nilichokiona ni kuwa hufikiri juu ya unachokiandika.

Kama unajua hilo mbona unaufanya utashi na akili ndiyo ukamilifu wenyewe ?

Embu onesha wapi nilipoandika utashi na akili ni ukamilifu.
 
hao wanaovuta hawakuwa na uwezo wa kuacha bangi na pombe kama wewe ulivyoacha ?
Wangekuwa na uwezo wangeshaacha. Kitendo cha mtu kuendelea kufanya jambo fulani maanake ameshindwa kuacha. Ukiona kaacha hiko kitendo ujue ameweza kuacha.
 
ukipitia vizuri hizo post tokea awali nilikwambia ya kwamba kitendo cha wewe kukiri kuwa binadamu anakosea kwavile hajakamilika kinathibitisha kuwa Mungu ameumba watu makusudi ili wakosee. Nasema hivyo kwasababu Mungu ni muweza wa vyote hivyo alikuwa anaweza kuumba watu wakiwa wakamilifu wasiofanya hata chembe ya kosa. Au unakataa kuwa Mungu angeshindwa kuumba watu waliokamilika ambao wasingeweza fanya makosa?
Ndiyo maana nikakutaka ushahidi ambao una onyesha ya kuwa Mola amemuumba mtu kwa makusudi ili akosee. Hili huna ushahidi nalo zaidi ya kulazimisha hitimisho ambalo si sahihi. Nilikwambia hapo kabla. Kisha nikakwambia ya kuwa Mola amemuumba mwanadamu ili amuabudu hili ndiyo lengo. Lakini sababu Mola ni muweza wa yote na amemfanya mwanadamu kuwa huru, akaumba uovu na wema ili mwanadamu akikosea atubu na akifanya wema humlipa thawabu.

Kwahiyo kukosea na kupatia ni jambo dogo sana ambalo limewekewa majibi yake na suluhisho lake, na haliwezi kuwa lengo balo no njia katika kulifikia lengo.

Ndiyo maana nahitimisha ya kuwa, unachokikana hukijui,hili ni tatizo kubwa.

Mola angetaka angeumba hivyo, ila amemuumba mwanadamu ambaye si mkamilifu na akamuwekea ala na nyenzo za kumfanya afikir ukamilifu na lengo kuu la kumuumba.
 
Embu onesha wapi nilipoandika utashi na akili ni ukamilifu.
Kwanza sijasema umeandika sehemu ya kuwa viwili hivyo ndiyo ukamilifu, bali maana ya unachokiandika kinaonyesha umeufanya utashi na akili ndiyo ukamilifu. Kisha rejea post #188.
 
Ukishajua km walikuwa wazungu,waafrika au waarabu itakusaidia nini???.Muhimu hapo ni kumwamini Mungu na neno lake tu.
Usipokubali kufunguka utaishi kwenye mzunguko, mduara wa akili finyu. Huwazi nje ya box, ukiamini yote ni sababu ya Mungu! Mungu amekupa akili za nini?
 
Yaani unasema kabisa kuwa mtu hajakamilika halafu bado unakazana kusema umepewa utashi na akili. Je hiyo akili na utashi itasaidia nini wakati haujawa mkamilifu?
Kwanza sijasema umeandika sehemu ya kuwa viwili hivyo ndiyo ukamilifu, bali maana ya unachokiandika kinaonyesha umeufanya utashi na akili ndiyo ukamilifu. Kisha rejea post #188.
Post namba 188 inawezekana umesoma lakini hujaelewa point yangu. Unaweza kuniambia je Cha akili na utashi kutamfanya mtu atoke kwenye hii sifa ya kutokuwa mkamilifu? Point yangu yangu ni kwamba Kama hata uwe na akili na utashi wa namna gani hakuwezi kuondoa hali ya kukosa ukamilifu basi utashi na akili uliyopewa unakikomo
 
Mola angetaka angeumba hivyo, ila amemuumba mwanadamu ambaye si mkamilifu na akamuwekea ala na nyenzo za kumfanya afikir ukamilifu na lengo kuu la kumuumba.
Kwahiyo unakubali kuwa Mungu kapenda kwa maamuzi yake kuumba watu wasiowakamilifu japokuwa alikuwa anauwezo wa kuumba watu waliokuwa wakamilifu laiti kama angetaka?
 
Post namba 188 inawezekana umesoma lakini hujaelewa point yangu. Unaweza kuniambia je Cha akili na utashi kutamfanya mtu atoke kwenye hii sifa ya kutokuwa mkamilifu? Point yangu yangu ni kwamba Kama hata uwe na akili na utashi wa namna gani hakuwezi kuondoa hali ya kukosa ukamilifu basi utashi na akili uliyopewa unakikomo
Safi kabisa sasa kwanini umehitimisha ya kuwa mwanadamu ameumbwa makusudi kwa lengi la kukosea au akosee ?

Mwanadamu si mkamilifu ila amepewa nyenzo na ala za kufikia ukamilifu. Tulia katila nukta moja.
 
Kwahiyo unakubali kuwa Mungu kapenda kwa maamuzi yake kuumba watu wasiowakamilifu japokuwa alikuwa anauwezo wa kuumba watu waliokuwa wakamilifu laiti kama angetaka?
Bila shaka kabisa.

Sasa turudi katika hitimisho lako ambalo unatakiwa kuliwekea ithibati. Umejuaje ya kuwa Mola ameumba mwanadamu ili akosee ?
 
Bila shaka kabisa.

Sasa turudi katika hitimisho lako ambalo unatakiwa kuliwekea ithibati. Umejuaje ya kuwa Mola ameumba mwanadamu ili akosee ?
Kwasababu kaamua kumuumba mtu aliye na mapungufu ilihali uwezo wa kuumba mtu asiye na Mapungufu alikuwa nao.
 
Kwasababu kaamua kumuumba mtu aliye na mapungufu ilihali uwezo wa kuumba mtu asiye na Mapungufu alikuwa nao.
Sasa swali ni kuwa je alivyo muumba alimuacha hivi hivi au alimpa yale yote yakumfanya afikie lengo na ukamilifu tena kwa hiari yake ?

Sasa unachotaka wewe hapo ni nini au shida iko wapi ?
 
Safi kabisa sasa kwanini umehitimisha ya kuwa mwanadamu ameumbwa makusudi kwa lengi la kukosea au akosee ?

Mwanadamu si mkamilifu ila amepewa nyenzo na ala za kufikia ukamilifu. Tulia katila nukta moja.

Naomba nitajie binadamu kama ishirini hivi au kumi hivi katika kumbukumbu zako, binadamu yeyote yule iwe nabii au mitume au mtu wa kawaida waliowahi kufikia daraja la ukamilifu kwa kutumia hizo nyenzo na hizo ala.
 
Sasa swali ni kuwa je alivyo muumba alimuacha hivi hivi au alimpa yale yote yakumfanya afikie lengo na ukamilifu tena kwa hiari yake ?

Sasa unachotaka wewe hapo ni nini au shida iko wapi ?
Ukishapewa kitu cha kukufikisha kwenye ukamilifu hatuwezi kutumia tena neno "sio mkamilifu" bali wataitwa wakamilifu kwasababu wanakila kitu cha kuwafanya wawe wakamilifu. Twende kwenye rejeo lako lako unayoitumia inasemaje. Je binadamu kaumbwa mkamilifu au sio mkamilifu?
 
Ukishapewa kitu cha kukufikisha kwenye ukamilifu hatuwezi kutumia tena neno "sio mkamilifu"
Umetumia msingi gani wa lugha kuhitimisha hili.

Naona unalazimisha mambo. Hili mbona rahisi sana kulitambua mzee. Unakuwa si mkamilifu ila unapewa ala za kufikia ukamilifu. Kijaa jaribu kufikiria kwanza kabla ya kuandika.

Sasa vipi utakuwa mkamilifu wakati hujaufikia ukamilifu wala hujatenda kwa muda huo ?
bali wataitwa wakamilifu kwasababu wanakila kitu cha kuwafanya wawe wakamilifu.
Hawaitwi wakamilifu sababu ukamilifu si tu uwe na nyenzo bali uzifanyie kazi nyenzo husika. Huitwi mcheza mpira kisa unamiliki njumu (Viatu vya kuchezea mpira) shartu lazima uucheze siyo tu kuucheza bali uweze kuucheza na ukidhi vigezo vya kuitwa mchezaji. Hili lina mifano mingi sana na liko wazi mno, ajabu hili dogo unashindwa kuling'amua bila shaka hayo makubwa ni muhali kabisa.

Nyinyi huwa mnatupa kazi sana mpaka tunaweka wazi yale ambayo yako wazi, sababu hamfikirii kwa undani.
Twende kwenye rejeo lako lako unayoitumia inasemaje. Je binadamu kaumbwa mkamilifu au sio mkamilifu?
Kijana inakuwaje unarudia kuuliza jambo ambalo nimeshaliweka wazi zaidi ya mara moja ? Au ndiyo umeishiwa na hoja au labda uniambie nikwambie mara ngapi ya kuwa mwanadamu si mkamilifu ?
 
Naomba nitajie binadamu kama ishirini hivi au kumi hivi katika kumbukumbu zako, binadamu yeyote yule iwe nabii au mitume au mtu wa kawaida waliowahi kufikia daraja la ukamilifu kwa kutumia hizo nyenzo na hizo ala.
hili hukulijibu. Nasubiri ujibu na hili kisha nikujibu ulichoandika juu
 
Sasa hili mbona liko wazi. Sasa onyesha wapi kitabu kimejipinga kama si akili yako ni ndogo inashindwa kuelewa maandiko.

Malaika walitii amri ya Mola wao na kuja kuua, sasa hapo kujipinga ni wapi na kosa lao liko wapi. ?

Vijana acheni kuruka ruka.
Waliambiwa waue wote, wao wakabakiza mmoja, huko si kukaidi? Na kukaidi amri ya Mungu si dhambi? Na kama ni dhambi, huoni ile kauli ya malaika hawatendi dhambi si kweli? Na hivyo kitabu kimejipinga?
 
Back
Top Bottom