Je, inawezekana Jakaya Kikwete ndiye Nyerere wa leo?

Je, inawezekana Jakaya Kikwete ndiye Nyerere wa leo?

Wakuu kwanza nianze kwa kujihami mimi ni layman kwenye upande wa political science! Pia si mkereketwa kbs wa siasa lakini kwa kuwa maisha ya binadamu wa leo ni ngumu sana kuyatenga na politics by default najikuta tu niko uwanjani.

Nimejaribu kufuatilia safari ya maisha ya JK ya kisiasa influence yake ndani na nje ya nchi, namna viongozi wanavyokimbilia kwake kuomba ushauri, inanipa nafasi ya kufikiri kwa uchache wake.

Je, inawezekana yeye ndo Nyerere wa Tanzania ya leo?! (Remote from Msoga).
Pumba,auwe wenzie kwa hila kisha ajivike Unyerere?, pathetic wewe na yeye
 
Nani "mwanajumuishi"? Unamaanisha nini kwa "jumuishi"?
Mkuu Faiza fox Mwanamajumui ni Panafricanism na hii jumuishi haipo kwenye vocabulary za wapigania uhuru.
kifupi huwezi kumwelezea Nyerere bila umajumui wa Africa ndio alitumia muda mwingi kupambana na ukoloni kwenye mataifa mengine ya africa hivyo kudumaza juhudi
za kujitafutia maendeleo ndani ya nchi.
 
Wakuu kwanza nianze kwa kujihami mimi ni layman kwenye upande wa political science! Pia si mkereketwa kbs wa siasa lakini kwa kuwa maisha ya binadamu wa leo ni ngumu sana kuyatenga na politics by default najikuta tu niko uwanjani.

Nimejaribu kufuatilia safari ya maisha ya JK ya kisiasa influence yake ndani na nje ya nchi, namna viongozi wanavyokimbilia kwake kuomba ushauri, inanipa nafasi ya kufikiri kwa uchache wake.

Je, inawezekana yeye ndo Nyerere wa Tanzania ya leo?! (Remote from Msoga).
Kikwete ni zaidi ya Nyerere. Nyerere alikuwa mnafiki sana mdini kupita maelezo akipendelea kanisa katoliki kuliko wengine hasa waislamu. Aliunga mkona Biafra kujitenga na Nigeria huku akipigia chapuo umoja wa Africa na akinza na muungano wa tanganyika na Zenj. UNAFKI HUU.
Alikuwa mdini kwa kuifungia jumuia ya kiislamu ya maendeleo ya Africa Mashariki EAMS huku akiliahidi kanisa kulipa a better chance. Rejea padre John Sivalon.
Alienda kusapoti Biafra kwa kuwa kule wengi ni wakatoliki ili wajitenge na influence ya nothern Nigeria ambayo ina waislamu wengi.
KIKWETE NI BORA SAAAAANA KULIKO NYERERE. KIKWETE NI MLIMA KILIMANJARO WAKATI NYERERE NI KICHUGUU.
 
Mkuu Faiza fox Mwanamajumui ni Panafricanism na hii jumuishi haipo kwenye vocabulary za wapigania uhuru.
kifupi huwezi kumwelezea Nyerere bila umajumui wa Africa ndio alitumia muda mwingi kupambana na ukoloni kwenye mataifa mengine ya africa hivyo kudumaza juhudi
za kujitafutia maendeleo ndani ya nchi.
"Mwanamajumui" aliyefanya kila njia Nigeria igawanyike? Akashindwa.

Unalijuwa hilo?
 
"Mwanamajumui" aliyefanya kila njia Nigeria igawanyike? Akashindwa.

Unalijuwa hilo?
Watu wana haki ya kujitawala na kuamua aina ya Uongozi wanaoutaka.
Waigbo wa Nigeria walikuwa wanauuliwa Kaskazini na Fulani
Hivyo wengi kurudi eneo lao na kutaka kuanzisha nchi ya Biafra kuna tatizo?

Mwanamajumui ni angali mpaka sasa kwa sababau alisikia manyanyaso na mateso ya waafrika wenzie
Ni kama Sudan kinachotokea Sudan kati ya Watu wa West Nile na Darful kutaka kujitenga sisi kama binadamu tutsapoti ziwe nchi huru? au tutaacha waendelee kuchinjwa na janjawee?
 
Wakuu kwanza nianze kwa kujihami mimi ni layman kwenye upande wa political science! Pia si mkereketwa kbs wa siasa lakini kwa kuwa maisha ya binadamu wa leo ni ngumu sana kuyatenga na politics by default najikuta tu niko uwanjani.

Nimejaribu kufuatilia safari ya maisha ya JK ya kisiasa influence yake ndani na nje ya nchi, namna viongozi wanavyokimbilia kwake kuomba ushauri, inanipa nafasi ya kufikiri kwa uchache wake.

Je, inawezekana yeye ndo Nyerere wa Tanzania ya leo?! (Remote from Msoga).
Kama alivyokuwa kipindi cha utawala wa Magufuri Rais mstaafu Mwinyi alikuwa Nyerere kwake na leo inawezekana kabisa Kikwete kuwa Nyerere,kuimba kupokezana.
 
Hapana, haiwezwkani. Jakaya yupo juu sana ya Nyerere kiuongozi.

Magu ndiye unaweza kumfananisha na Nyerere, wote hao walikuwa hawaambiliki, wakurupukaji na walitumia nguvu nyingi kuliko akili katika uongozi.
Nadhani hujaelewa hoja ya mhusika.
Hoja ya mchangiaji ipo katika kufananisha, " Alichokuwa anafanya Nyerere kwa RAIS aliyekuwepo madarakani kipindi yupo hai" ni sawa na anachofanya Kikwete kwa RAIS ambaye yupo madarakani kipindi hiki.( Hoja ya ulinganisho ndio ilikuwa hapo).
NB
URAISI ni kazi ngumu sana, katika uongozi huwezi kuwa unakubali kila kitu, ukifanya hivyo utaruhusu mambo ya ajabu sana kwa kigezo cha demokrasia( Hivyo, Udikteta katika baadhi ya mambo ni MUHIMU. Hasa yale yanayolinda maslahi ya nchi).
Kashfa za rushwa, wizi, matumizi mabaya ya madaraka, uuzaji wa rasilimali za nchi, nk. Nyerere hakuwa nazo, Hivyo aliondoka na mikono safi( Hii inaonesha kuwa alikuwa ana nia njema).
Hao waliokuwa wanamshauri walikuwa wana mtazamo wa chini na walikuwa wanatumika na maadui wa nchi. Ndio maana Nyerere alikataa ushauri wao.
 
Wakuu kwanza nianze kwa kujihami mimi ni layman kwenye upande wa political science! Pia si mkereketwa kbs wa siasa lakini kwa kuwa maisha ya binadamu wa leo ni ngumu sana kuyatenga na politics by default najikuta tu niko uwanjani.

Nimejaribu kufuatilia safari ya maisha ya JK ya kisiasa influence yake ndani na nje ya nchi, namna viongozi wanavyokimbilia kwake kuomba ushauri, inanipa nafasi ya kufikiri kwa uchache wake.

Je, inawezekana yeye ndo Nyerere wa Tanzania ya leo?! (Remote from Msoga).
Akili mtu wangu.., hata kama hujihusishi na Siasa huwezi linganisha Mwalimu na huyo jamaa yenu yaani huwez hata kwa ndoto.
 
Nadhani hujaelewa hoja ya mhusika.
Hoja ya mchangiaji ipo katika kufananisha, " Alichokuwa anafanya Nyerere kwa RAIS aliyekuwepo madarakani kipindi yupo hai" ni sawa na anachofanya Kikwete kwa RAIS ambaye yupo madarakani kipindi hiki.( Hoja ya ulinganisho ndio ilikuwa hapo).
NB
URAISI ni kazi ngumu sana, katika uongozi huwezi kuwa unakubali kila kitu, ukifanya hivyo ukakaruhusu mambo ya ajabu sana kwa kigezo cha demokrasia( Hivyo, Udikteta katika baadhi ya mambo ni MUHIMU. Hasa yale yanayolinda maslahi ya nchi).
Kashfa za rushwa, wizi, matumizi mabaya ya madaraka, uuzaji wa rasilimali za nchi, nk. Nyerere hakuwa nazo, Hivyo aliondoka na mikono safi( Hii inaonesha kuwa alikuwa ana nia njema).
Hao waliokuwa wanamshauri walikuwa wana mtazamo wa chini na walikuwa wanatumika na maadui wa nchi. Ndio maana Nyerere alikataa ushauri wao.
Kila Rais wa zamani ni mshauri wa Rais aliyopo madarakani.

Sielewi kwanini iwe hoja ni hiyo.
 
Watu wana haki ya kujitawala na kuamua aina ya Uongozi wanaoutaka.
Waigbo wa Nigeria walikuwa wanauuliwa Kaskazini na Fulani
Hivyo wengi kurudi eneo lao na kutaka kuanzisha nchi ya Biafra kuna tatizo?

Mwanamajumui ni angali mpaka sasa kwa sababau alisikia manyanyaso na mateso ya waafrika wenzie
Ni kama Sudan kinachotokea Sudan kati ya Watu wa West Nile na Darful kutaka kujitenga sisi kama binadamu tutsapoti ziwe nchi huru? au tutaacha waendelee kuchinjwa na janjawee?
Hata Wazanzibari wanataka kujitawala, mbona tunawabania?

Double standard?
 
Nyerere hakushirikiana na WA magharibi kuiba maliasili za nchi yake - kikwete alifanya na anaendelea

Nyerere alipambana na wezi wa mali za umma - kikwete alishirikiana nao

Nyerere ni kioo cha uongozi katika taifa hili na asifananishwe na viongozi wasioendana nae.
 
Kikwete ni zaidi ya Nyerere. Nyerere alikuwa mnafiki sana mdini kupita maelezo akipendelea kanisa katoliki kuliko wengine hasa waislamu. Aliunga mkona Biafra kujitenga na Nigeria huku akipigia chapuo umoja wa Africa na akinza na muungano wa tanganyika na Zenj. UNAFKI HUU.
Alikuwa mdini kwa kuifungia jumuia ya kiislamu ya maendeleo ya Africa Mashariki EAMS huku akiliahidi kanisa kulipa a better chance. Rejea padre John Sivalon.
Alienda kusapoti Biafra kwa kuwa kule wengi ni wakatoliki ili wajitenge na influence ya nothern Nigeria ambayo ina waislamu wengi.
KIKWETE NI BORA SAAAAANA KULIKO NYERERE. KIKWETE NI MLIMA KILIMANJARO WAKATI NYERERE NI KICHUGUU.
Alijenga kanisa la parokia ipi?, Au alimsomesha padre yupi?, Au alijenga seminari gani?
Tatizo la kutumia maneno ya vijiwe bila kuwa na fikra tunduizi( critical thinking) ndio haya.
Nyerere katika maisha yake ya siasa na elimu alisaidiwa na kanisa ndio sababu ya ukaribu na hao jamaa.
Issue ya wakristo wengi kuwa viongozi ilitengenezwa na suala la elimu. Waislamu wengi hawakusoma elimu ya kikoloni ambayo ilikuwa ndilo hitaji la uongozi.
SASA utampaje mtu uongozi wa Katibu mkuu wa wizara au mkurugenzi wa idara fulani na wakati ameishia darasa la nne na hajui chochote kuhusiana na hiyo wizara au idara?
KIFUPI: Hakukuwepo upendeleo ila upande wa pili walikuwa hawana elimu iliyohitajika.
Waislamu walikuwa wana elimu ya dini ambayo inasisitiza uongozi apewe muislamu mwenzao na siyo vinginevyo ( Nyerere alifanya kazi ya kuondoa mawazo ya aina hii, Ndio maana anachukiwa na upande huo).
Angekuwa mdini uongozi wa URAISI angemkabidhi MKRISTO mwenzake lakini hakufanya hivyo. Kwahiyo, Nyerere analaumiwa kwa kutengeneza jamii yenye usawa ( Kwasababu, wale waliotarajia kupendelewa, hawakupendelewa).
 
Back
Top Bottom