Je, inawezekana Jakaya Kikwete ndiye Nyerere wa leo?

Je, inawezekana Jakaya Kikwete ndiye Nyerere wa leo?

Acha dharau unawezaje kumfananisha Nyerere na kikwete

Nyerere alikuwa mbali Sana kuliko akina kikwete ,na maraisi wengine kiufupi sioni wa kufananisha na Nyerere
Tuache porojo twende na Facts

Mimi nasimama na Jakaya wewe simama na Nyerere halafu tuanze kutaja mafanikio na madhaifu ya kila mmoja
 
Msoga was one of the best Leader existed as Butiama was one best president existed in different era

Msoga = the extreme corruption
Butiama = the extreme dictator with fake Constitution.
 
Wakuu kwanza nianze kwa kujihami mimi ni layman kwenye upande wa political science! Pia si mkereketwa kbs wa siasa lakini kwa kuwa maisha ya binadamu wa leo ni ngumu sana kuyatenga na politics by default najikuta tu niko uwanjani.

Nimejaribu kufuatilia safari ya maisha ya JK ya kisiasa influence yake ndani na nje ya nchi, namna viongozi wanavyokimbilia kwake kuomba ushauri, inanipa nafasi ya kufikiri kwa uchache wake.

Je, inawezekana yeye ndo Nyerere wa Tanzania ya leo?! (Remote from Msoga).
kweli kabisaaaa. mimi nampenda sana kikwete na kusema ukweli kamzidi nyerere mara 70x70.
Kikwete kajenga secondari za kata nchi nzima na kuwaokoa vijana wengi kurudia rudia darasa la sana!
Kikwete kajenga high schools kila wilaya nchi nzima na kufanya elimu ya secondari na high school kuwa haki ya raia
Kikwete huyo huyo kajenga UDOM na kupeleka wanafunzi wengi chuo kikuu kupita nchi zote kusini mwa jangwa la sahala!
kikwete alifanyia kazi matatizo ya mwananchi mtanzania katika elimu hapo alikomboa wanyonge.
 
Kikwete ni zaidi ya Nyerere. Nyerere alikuwa mnafiki sana mdini kupita maelezo akipendelea kanisa katoliki kuliko wengine hasa waislamu. Aliunga mkona Biafra kujitenga na Nigeria huku akipigia chapuo umoja wa Africa na akinza na muungano wa tanganyika na Zenj. UNAFKI HUU.
Alikuwa mdini kwa kuifungia jumuia ya kiislamu ya maendeleo ya Africa Mashariki EAMS huku akiliahidi kanisa kulipa a better chance. Rejea padre John Sivalon.
Alienda kusapoti Biafra kwa kuwa kule wengi ni wakatoliki ili wajitenge na influence ya nothern Nigeria ambayo ina waislamu wengi.
KIKWETE NI BORA SAAAAANA KULIKO NYERERE. KIKWETE NI MLIMA KILIMANJARO WAKATI NYERERE NI KICHUGUU.

Huna unachoelewa, umekalilishwa vitu masijid/madirasa! Biafra alikowatetea walikuwa wanakaa wakristo? Wakati anavunja mahusiano na Israeli kwa sbb ya mateso ya Wapalestina, hao waparestina ni wakatoriki? Ufia dini ni uchizi uliopitiliza aisee
 
Wakuu kwanza nianze kwa kujihami mimi ni layman kwenye upande wa political science! Pia si mkereketwa kbs wa siasa lakini kwa kuwa maisha ya binadamu wa leo ni ngumu sana kuyatenga na politics by default najikuta tu niko uwanjani.

Nimejaribu kufuatilia safari ya maisha ya JK ya kisiasa influence yake ndani na nje ya nchi, namna viongozi wanavyokimbilia kwake kuomba ushauri, inanipa nafasi ya kufikiri kwa uchache wake.

Je, inawezekana yeye ndo Nyerere wa Tanzania ya leo?! (Remote from Msoga).
Wala hakuna kitu kama hicho. Jibu ni kuwa ndiye rais mstafu ambaye anaishi kwa sasa. Mwinyi ameshazeeka hawezi kushauri chochote
 
Hapana, haiwezwkani. Jakaya yupo juu sana ya Nyerere kiuongozi.

Magu ndiye unaweza kumfananisha na Nyerere, wote hao walikuwa hawaambiliki, wakurupukaji na walitumia nguvu nyingi kuliko akili katika uongozi.
Napenda kukupinga, huyo Jakaya ni mwanafunzi wa Nyerere aliyekuzwa nae kiuongozi. Nyerere alihakikisha anaacha kizazi cha viongozi wenye umri mdogo waje walifae taifa siku za baadae.

Na ndio hawa kina Jakaya, Lowassa, Mkuchika, Ole Sendeka, Lukuvi na wengine wa umri huo.
 
Napenda kukupinga, huyo Jakaya ni mwanafunzi wa Nyerere aliyekuzwa nae kiuongozi. Nyerere alihakikisha anaacha kizazi cha viongozi wenye umri mdogo waje walifae taifa siku za baadae.

Na ndio hawa kina Jakaya, Lowassa, Mkuchika, Ole Sendeka, Lukuvi na wengine wa umri huo.
Hivi ulikuwa huelewi kuwa mwanafunzi siku zote huwa zaidi ya aliyemfundisha? Fikiri.
 
Ukiwapanga marais wanne bora kidemokrasia nchini
Namba 1 ni JKN
2. Mzee Ruksah
3. Ni JMK
4. Samia (huyu mpaka amalize kipindi chake akiendelea hiv, akawapuuza wahafidhina) kuna uwezekano akawa namba 2)
5. Mkapa
6. Hakuna
Mimi kwangu ni:
1.Mkapa Benjamin
2.Nyerere Julius
3.Kikwete Jakaya
4.Magufuri John
5.Ali Hassan Mwinyi
6.Samiah Suluhu.
 
Hapana mkuu mimi sio bavicha! Huu ni mtazamo wangu huru!Pia nakuheshimu sana kwa unguli wako kwny jukwaa la siasa either post yako iwe hasi au chanya! Ndivyo demokrasia inavyotaka!Mwalimu na JK wamelitumikia Taifa hili kwa nyakati tofauti!Ndo maana nimetumia neno this era si kwamba nimeshusha hadhi ya Baba wa Taifa.
Hata hivyo mwalimu ni binadamu kama wengine wala si haramu kumlinganisha na wengine kwani kipaji alichopewa yeye pia Mungu anaweza kumjaalia mtu mwingine kama alivyomjaalia yeye na hakumfanya kuwa binadamu wa kipekee ndiyo maana hata kwenye uongozi wake kuna makosa kadhaa aliyafanya na mengine ndiyo yamesababisha umasikini wetu hadi leo hii.
 
Huna unachoelewa, umekalilishwa vitu masijid/madirasa! Biafra alikowatetea walikuwa wanakaa wakristo? Wakati anavunja mahusiano na Israeli kwa sbb ya mateso ya Wapalestina, hao waparestina ni wakatoriki? Ufia dini ni uchizi uliopitiliza aisee
Kwa hiyo Nyerere kuimasikinisha nchi kwa kujiingiza ktk ma vita ya kusini mwa Africa yasiyokuwa na tija na ile ya Uganda kumtetea mkatoliki mwenzake Milton Obote wewe unaona ni sawa? Wewe kweli kilaza na umekunywa maji ya bendera.
 
Alijenga kanisa la parokia ipi?, Au alimsomesha padre yupi?, Au alijenga seminari gani?
Tatizo la kutumia maneno ya vijiwe bila kuwa na fikra tunduizi( critical thinking) ndio haya.
Nyerere katika maisha yake ya siasa na elimu alisaidiwa na kanisa ndio sababu ya ukaribu na hao jamaa.
Issue ya wakristo wengi kuwa viongozi ilitengenezwa na suala la elimu. Waislamu wengi hawakusoma elimu ya kikoloni ambayo ilikuwa ndilo hitaji la uongozi.
SASA utampaje mtu uongozi wa Katibu mkuu wa wizara au mkurugenzi wa idara fulani na wakati ameishia darasa la nne na hajui chochote kuhusiana na hiyo wizara au idara?
KIFUPI: Hakukuwepo upendeleo ila upande wa pili walikuwa hawana elimu iliyohitajika.
Waislamu walikuwa wana elimu ya dini ambayo inasisitiza uongozi apewe muislamu mwenzao na siyo vinginevyo ( Nyerere alifanya kazi ya kuondoa mawazo ya aina hii, Ndio maana anachukiwa na upande huo).
Angekuwa mdini uongozi wa URAISI angemkabidhi MKRISTO mwenzake lakini hakufanya hivyo. Kwahiyo, Nyerere analaumiwa kwa kutengeneza jamii yenye usawa ( Kwasababu, wale waliotarajia kupendelewa, hawakupendelewa).
Soma reference zenye akili kisha ndo uje kuandika. Wajerumani walipofika tanganyika walikuta wasomi wakiwa waislamu ambao waliandika kila kitu kwa hati ya kiarabu.
Taasisi ya EAST AFRICA MUSLIM WELFARE SOCIETY iliyojenga mashule kibao Tanganyika kwa ajili ya waislamu Nyerere aliipiga ban mwaka 1968.
Kama ni mtu wa usawa kwa nini hakupiga marufuku mashirika ya kikristo yaliyomiliki shule mbalimbali ili kufanya usawa?
Sasa nakusaidia. Kasome Kitabu cha Padre Dr John Sivalon na Kitabu cha Mohamed Said humo utapata kumjua Nyerere ni nani hasa na utaacha porojo zako ulizodesa kutoka magazeti ya uhuru na mzalendo. Utaelewa kwa nini wakati wa kuandika historia ya Tanganyika na uhuru wake walipewa hiyo kazi watu 2 :
1. Dr Wilbert Kleruu
2. Abdulwaheed Sykes
Baadaye Abdulwaheed akaondolewa na akaandika Dr Kleruu peke yake.
SOMA KIJANA ACHA POVU.
 
Back
Top Bottom