Je, kweli ni bora kuamini Mungu yupo halafu siku ya mwisho usimkute, kuliko kutoamini halafu ukamkuta?

Sijui kama umeelewa ulichoandika mwenyewe.

Mkuu hadi leo zipo dawa za asili ambazo tunajua faida zake na watu hutumia ila hakuna uthibitisho wa kisayansi na ndio hoja yangu hapa, na ndio maana nikatoa mfano hadi wa Dowsing ambayo imekuwa ikitumika sana na ina visa vikubwa tu ila inapingwa kwa sababu bado haijathibitika kisayansi hivyo si kwamba nataka ukubali vitu tu kuwa ni kweli ila suala la kupinga kitu kisa hakijathibitika kisayansi.
 
Sarakasi ni kwa ajiri ya maonyesho watu waone waburudike, sasa uchawi si kwa ajiri ya maonyesho kwa lengo la kuburudisha watu ndio maana nasema nazungumzia kitu ambacho kinahusu maisha ya watu. Mazingaombwe ndio kwa ajiri ya maonyesho kuburudisha watu.
 
We ulikuwa ni mmoja wao wa watu walioamini Kikombe cha babu kinatibu ukimwi?

Kujibu hoja yako....

Unaposema hakuna uthibitisho wa kisayansi kwenye dawa za asili, unakuwa unalenga uthibitisho unaohusu nini?

Kwamba sayansi inasema hakuna uthibitisho kuwa hizo dawa zinatibu??

Kama jibu lako ni ndio basi utakuwa unakosea.

Japo ni kweli usiopingika kuwa katika sayansi dawa za asili zipo limited sana. Lakini bado haiondoi maana kuwa Sayansi inatambua zipo dawa za asili zenye uwezo wa kutibu magonjwa.

Mwaka 2015 WHO waliipitisha rasmi dawa ya kiasili ya kichina inayoitwa Artemisinin kama dawa rasmi ya kutibu Malaria.

Kwa hiyo sio kweli kuwa Sayansi inasema dawa za asili hazina uthibitisho kisayansi. Japo kuwa zipo pia dawa ambazo zinadaiwa kutibu baadhi ya magonjwa ambayo Sayansi im

Sayansi inasema hakuna uthibitisho wa kisayansi kuhusiana na efficacy zake hivyo utumiaji wa dawa za asili unaweza kuleta athari zaidi kwa mtumiaji.

Pia kunaweza kuwepo na hatari ya muingiliano wa dawa zingine na kusababisha tatizo lingine kiafya.

Sababu nyingine ambayo sayansi imeweka angalizo ni kuhusiana na kipimo rasmi cha dozi kwenye dawa hizo za asili mara nyingi dozi ni vague.

Kipimo cha dawa alichokunywa baba ndio kipimo hicho hicho anachopewa mtoto.
 
Kama sarakasi ni kwa ajili ya maonesho basi ngoja nibadilishe mfano.

Vipi kuhusiana na ufanyaji ngono? Hii pia si tunakubaliana kuwa ni sehemu ya maisha ya watu??
 
huwa nasema siku zote, utausifia sana uumbaji kwa kuangalia milima,bahari, anga, mito , sayari,..n.k,...lakini ukiangalia maisha ya viumbe hapa Duniani, utaulaani uumbaji,.... hakuna muumbaji anayeweza kuumba maisha ya ajabu na hovyo kwa viumbe wake,.....
 
Mimi binafsi naamini uwepo wa Mungu kwa kutazama jinsi vitu mbalimbali vilivyoumbika,..sababu ya pili ni Kutokana na Imani ya Mungu kuhimiza na kuhamasisha juu ya kutenda mema kitu ambacho kinaenda sawa na akili na moyo wa kibinadamu (kufanyiana mema).

So, kimsingi sioni hasara ninayoipata kwa kuamini uwepo wa Mungu..,
 
Kinachopelekea watu waende misikitini na makanisani ni nini sasa mkuu?
Ni imani tu walizo karirishwa, kupumbazwa na kuaminishwa.

Watu wanaenda makanisani na misikitini kwa vile wameaminishwa kufanya hivyo.

Na wame jengewa hofu kwamba wasipofanya hivyo watapewa adhabu za milele Jehanam.

Sasa hizo hofu walizo jengewa na kupumbazwa ndio zinawafanya kwenda makanisani na misikitini daily.
 
Yeah sure mkuu.
 
Kwaiyo wimbo wa Taifa wa Tanzania, Mungu ibariki afrika na wenyewe ni pointless ama
 
Kwaiyo wimbo wa Taifa wa Tanzania, Mungu ibariki afrika na wenyewe ni pointless ama
Ndio ni pointless.

Maana huyo Mungu anayeimbiwa kila siku " ibariki Afrika, ibariki Tanzania, wabariki viongozi wake" Hajawahi kubariki chochote.

Waafrika wanazidi kuteseka kwa umaskini, kudhulumiwa na viongozi wao wa serikali, kodi zao zinatapanywa hovyo hovyo tu na hakuna baraka zozote zile zinazo saidia kitu.
 
Kushangaa lazima maana sio kawaida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…