Je, kweli ni bora kuamini Mungu yupo halafu siku ya mwisho usimkute, kuliko kutoamini halafu ukamkuta?

Je, kweli ni bora kuamini Mungu yupo halafu siku ya mwisho usimkute, kuliko kutoamini halafu ukamkuta?

Scars
Kiranga
min -me
Infropreneur

Mmekua mnapinga uwepo wa Mungu kila siku kwa kuuliza maswali yale yale bila kuja na kitu kipya
Sasa naomba niwaulize kama mmeweza kujua kuwa hakuna Mungu, pia kuna uwezekano mmeshajua Chanzo cha huu uliwengu na viumbe vyake
Naomba mje kutueleza chanzo cha huu ulimwengu na viumbe vyake ni nini?

Nafkiri sisi tuona Amini uwepo wa Mungu tuanze kuwa challenge hawa Atheist kwa kuwahoji maswali fikirishi sio kila kubishana Mungu yupo au hayupo
Kabla ya kujibu swali lako kwanza nijibu langu, chanzo cha Mungu ni kipi?
 
Kujua ni bora zaidi kuliko kuamini.

Kwa nini huyo Mungu ajifiche na aachie watu wakisie uwepo wake ilhali angeweza tu kujitokeza na wote tukamjua?

Kujificha kuna maana nani ? Au nani amekwambia Mungu amejificha ? Kwahiyo kila ambacho hakionekani kimejificha ?

Kingine watu hawakisii juu ya uwepo wa Mungu, bali ni hakika. Tena yeye Allah ndio aliwachagua miongoni mwa waja wake akawafanya kuwa mitume na manabii.

Unatofautisha vipi kujua na kuamini ? Shida naiona ni kwamba mna ufahamu mdogo sana juu ya tamko Imani na kuamini.
 
Makala hii nitaiweka kwa vipande kuepusha kero ya usomaji.

Moja ya hoja maarufu kutoka kwa watu wanaoamini Mungu (Theists).

Ni hoja ambayo imelenga kuweka matumaini ya mwelekeo katika maisha ili kuwafanya watu waone kuamini Mungu yupo ndio uchaguzi bora zaidi (rational) kwasababu haitakupa matokeo mabaya mwishoni.

Hii ni Analogy iliyopata sana umaarufu miaka ya 1640s na muazilishi aitwaye Pascal Wager.

Huyu jamaa alihoji kuwa ni vyema ukaamini kuwa Mungu yupo ukafa na usimkute kuliko kutokuamini halafu ukafa ukamkuta.

Pascal analaani kuwa kuamini kuwepo kwa Mungu ni tendo la busara zaidi kuliko kutokuamini kuwepo kwake, hata kama hatuna uhakika kuhusu kuwepo kwake. Hii ni kwasababu zifuatazo.

  1. Kama Mungu yupo na tutamwabudu, tutapata thawabu ya milele (kama ushindi mkubwa).
  2. Lakini kama Mungu hayupo na hatumwamini, hatutapata chochote (kama hasara ndogo).
  3. Kwa upande mwingine, kama Mungu yupo na hatumwamini, tutapata adhabu ya milele (hasara kubwa).
  4. Lakini kama Mungu hayupo na hatumwamini, hatutapata chochote (ushindi mdogo).

Hivyo, Pascal anasema kwamba kuamini kuwepo kwa Mungu ni tendo la busara zaidi, kwasababu unaweza kupata thawabu ya milele na kuepuka adhabu ya milele, hata kama hatuna uhakika kuhusu kuwepo kwake.

Swali: Je Atheists hawatuogopi siku ya mwisho kukutana na hukumu ya Mungu na kutupwa kwenye moto wa milele?

Hatuogopi kubaini kuwa hadithi za mitume zinazosimuliwa kuhusu Yesu na Muhammad kuwa ni za kweli na kwamba tumepoteza nafasi ya kuishi maisha ya milele peponi kwa kutoamini?

Je isingekuwa vyema Atheists kuwa upande salama wa kumuamini Yesu, Muhammad na Mungu kama backup just in case?
Imani ya Mola haitaki kubahatisha, hata ukiamini kwa lengo la kwamba ukimkuta iwe kheri kwako, hapa Imani yako sio sahihi na utaenda motoni tu. Bali Imani ya Mola inataka elimu, mazingatio na uhakika usilo kuwa na shaka kabisa, kwa ufupi ni mchakato wa muda mrefu wenye kuambatana na utiifu na kumpwekesha yeye katika ibada.

Ndio maana Allah anataka watu wenye kutafakari kwa kina na wenye mazingatio.
 
Kujificha kuna maana nani ? Au nani amekwambia Mungu amejificha ? Kwahiyo kila ambacho hakionekani kimejificha ?

Kingine watu hawakisii juu ya uwepo wa Mungu, bali ni hakika. Tena yeye Allah ndio aliwachagua miongoni mwa waja wake akawafanya kuwa mitume na manabii.

Unatofautisha vipi kujua na kuamini ? Shida naiona ni kwamba mna ufahamu mdogo sana juu ya tamko Imani na kuamini.
Imani ni nini?
 
Kabla ya kujibu swali lako kwanza nijibu langu, chanzo cha Mungu ni kipi?
Mkuu hoja kuwa huamini uwepo wa Mungu mimi nimekuacha nayo, nimeomba kuanzisha hoja nyingine kwenu nyie msio amini uwepo wa Mungu, mtuambie kwa kuthibitisha chanzo cha huu ulimwengu na viumbe vyake ni nini?
Ukishindwa kujibu hili basi ujijue bado we ni mweupe sana
 
Ni rahisi wewe kuona mimi nai praise sana Sayansi na kuchukulia kitu hicho kama cha kijinga kutokana na msingi wako wa maisha ulilenga kujikita zaidi kwenye madrasa.

Ni kama ambavyo tumezoea kuona jamii nyingi za waislamu wamekuwa wakipuuza elimu dunia halafu ikifika siku ya Iddi wanaanza kuisumbua serikali iwanunulie binocular ya kisayansi kwa ajili ya kutazama mwezi.
Duh! We jamaa naona hatuelewani kabisa una tatizo la kushindwa kuelewa unachosoma.

Nachokupinga ni hizo kauliza za kusema sayansi inakubali kukosolewa mara sayansi inasema, unafanya sayansi ni kama mtu hivi kitu ambacho naona unakosea kuelezea hivyo. Mimi sipingi sayansi wala kuidharau sayansi.
 
Sasa ushajua hatima inayokusubiri ikiwa hautaamini hizi habari. Je tayari ushaanza kuwa muumini wa Anubis?

Kitu ambacho hamkijui ni kuwa, Imani nayo uhakikiwa.

Kwanza lazima tuzohakiki habari hizi zinazowa husu Wamisri na Imani yao hii. Wapi chimbuko la Imani hii ?
 
Mkuu hoja kuwa huamini uwepo wa Mungu mimi nimekuacha nayo, nimeomba kuanzisha hoja nyingine kwenu nyie msio amini uwepo wa Mungu, mtuambie chanzo cha huu ulimwengu na viumbe vyake ni nini?
Ukishindwa kujibu hili basi ujijue bado we ni mweupe sana
Sijui kama umenielewa lakini🤔 kwani nilazima kila kitu kiwe na chanzo?
 
Kujua kipo ndani ya Imani. Lazima kwanza ujue hakika ya jambo fulani kisha unaliweka moyoni na kulisadiki na kulifanyia kazi jambo husika.
Unachokifanya wewe ni kulazimisha jibu ambalo sio sahihi liwe sahihi . Ni kwamba hujui tofauti ya kujua na kuamini kweli?
 
Sijui kama umenielewa lakini🤔 kwani nilazima kila kitu kiwe na chanzo?
Wewe unataka kunirudisha kwenye maswali yenu ya kila siku, Mimi nakutoa huko nimekuuliza swali dogo unaruka ruka
 
Na kwa hilo unapaswa kufuata mafundisho yote yaliyoandikwa katika Quran tukufu, kwa kufanya hivyo utakuwa umeepuka moto na kuzawadiwa bikra 72 peponi.

Tunasema kuhakiki hiki unachokiandika, hizi habari za kuwa Kuna kuzawadiwa mabikra 72, umezipata wapi ? Umezisikia tu pasi na kulifanyia uchunguzi au unazijua kwa kulifatilia na kuzihakiki ?
 
Unachokifanya wewe ni kulazimisha jibu ambalo sio sahihi liwe sahihi . Ni kwamba hujui tofauti ya kujua na kuamini kweli?

Unatakiwa ukosoe nilicho kiandika kwa wewe kuandika kilicho sahihi.

Najua tofauti ya kujua na kuamini ndio maana nimeandika hayo.

Kwetu sisi Waislamu huanza kwanza elimu kisha kauli na vitendo.

Sasa jadili jambo kielimu.
 
Wewe unataka kunirudisha kwenye maswali yenu ya kila siku, Mimi nakutoa huko nimekuuliza swali dogo unaruka ruka
Ukisha thibitisha uwepo wa Mungu hakuna swali litakalo jirudia , yani hata huu mjadala hautakuwepo ni sawa natuanze kuuliza je mama samia yupo?
 
Wanasema Mungu ni roho yupo kila sehemu ila haonekani kwasababu hana mwili.

Ila ukumbuke huyo huyo Mungu anayetajwa kuwa hana mwili ana jinsia ya kiume na ukifanya mocking kwa kumuita mwanamke utakumbana na ghadhabu za waumini kuwa umemdhalilisha Mungu wao.

Huyo huyo Mungu ambaye hana material body ana makazi yake huko juu yanaitwa Mbinguni, and just in case ukumbuke kuwa huko juu sio kama amesimama wima hapana maandiko yanasema ameketi kwenye kiti cha enzi kwa ajili ya kutu-monitor sisi. That means he's got a butt too.

But when it comes to evidence he disappears like poof.

Mungu hayupo kila mahali, hii ni Imani potofu.

Mungu ana umbile na Wala Mungu sio Roho, yeye ndio ameumbwa hizi roho.
 
Unatakiwa ukosoe nilicho kuandika kwa wewe kuandika kilicho sahihi.

Najua tofauti ya kujua na kuamini ndio maana nimeandika hayo.

Kwetu sisi Waislamu huanza kwanza elimu kisha kauli na vitendo.

Sasa jadili jambo kielimu.
Wewe unahubiri tu kila siku wala haujawahi thibitisha uwepo wa Mungu , unachokifanya unataka niamini mahubiri yako ,wakati mimi sitaki kuamini nataka nijue sijui kama unaelewa🤔
 
Ukisha thibitisha uwepo wa Mungu hakuna swali litakalo jirudia , yani hata huu mjadala hautakuwepo ni sawa natuanze kuuliza je mama samia yupo?
Umeshindwa kujibu, kwa maana hiyo hujui chochote kuhusu huu ulimwengu, Atheist ni watu ambao wamekosa majibu ya maswali fikirishi kuhusu chanzo cha huu ulimwengu wakakimbilia kwenye conclusion bila kutaka kujifunza maarifa mapya
 
Umeshindwa kujibu, kwa maana hiyo hujui chochote kuhusu huu ulimwengu, Atheist ni watu ambao wamekosa majibu ya maswali fikirishi kuhusu chanzo cha huu ulimwengu wakakimbilia kwenye conclusion bila kutaka kujifunza maarifa mapya
Hivi umesoma vizuri nilichokiandika ? Kwanini kwanza unahisi lazima kuwe na chanzo?
 
Back
Top Bottom