Je, Membe kosa lake kubwa ni kutaka kuwa Rais wakati yeye ni jasusi?

Je, Membe kosa lake kubwa ni kutaka kuwa Rais wakati yeye ni jasusi?

Mh jasusi hawezi kuwa raisi ? Eti kuwa raisi lazima uwe jasusi ?

Tanzania my coyntry a long way to go , asante Maxence Melo kwa kutupa hili jamvi hakika tunafurahi maana kila ashibae anakuja kupumzisha shibe haba jamvini .

Nenda Bernad , hii ni njia yetu sote .[emoji24]
 
2015 Membe mwenyewe alikuwa akiitaka ile nafasi, bahati mbaya ushindani ulioibuka ndani ya chumba cha mkutano baada ya jina la Lowassa kukatwa, ukasababishwa Membe nae akatwe ili kutuliza hali ya mambo.

Hizo sifa nyingi ulizompa hapo juu sioni kiuhalisia kama alikuwa nazo, kwangu alikuwa anasubiri kubebwa na rafiki yake Kikwete awe Rais wa JMT, lakini yeye binafsi sikuwahi kumuona kama mwanasiasa mwenye ushawishi wa aina yoyote ili kufanikisha hiyo ndoto yake.

Kwa hali hiyo, naona ungemlaumu zaidi yule aliyetaka Membe awe Rais wakati akijua alikuwa jasusi, Membe ni kama alishawishiwa tu achukue fomu agombee akiaminishwa atakuwa, lakini bahati mbaya mambo yakaenda sivyo.
Kumekuchaaaaaaah!!!
 
Huwezi kuwa Rais bila kuwa jasusi mkuu!!

System haiwezi muweka mtu ambaye gajaiva kwenye ujasusi ndani ya nchi!!

Lazima kwanza upate mafunzo kivitendo ndani ya Tiss ndio unakua !

Jua hivyo!
Huna ujualo, Magufuli hajawahi kuwa JASUSI zaidi ya kwenda JKT kwa mujibu wa Sheria kama ilivyo kwa vijana wanaomaliza elimu ya kidato cha 6 sasa hivi.
 
Membe alisaidia Sana harakati za kuondoa Rais dicteta nchi hii na kuvunja mfumo wake wote aliokuwa anautengeneza kutawala Tanzania milele.

[emoji848]
Leo wanatajana wazi wazi wenyewee, tusubiri wanasema nyama ziko chinii.
 
Kwani BWM hakuwa mtu wa kitengo?
Kama ni ndiyo ilikuwaje yeye ikawezekana kuwa Rais?
Kama siyo, je kuna madhara gani Mtu wa kitengo kuwa Rais?
Urusi ya Vladimir Putin na Benjamin Netanyahu ni Majasusi na ni viongozi wa kuu kwenye nchi zao na wako Very smart, Tanzania kuwa na Rais Spy imekatazwa kwenye katiba?
 
George Bush Sr aliwahi kuwa Mkuu wa CIA kabla ya kuja kuwa Rais. Ile CIA ambayo hakukuwa na Intelligence Community juu yake. Sasa cha ajabu kwa Tanzania nini? Mahiga alikaimu ukuu wa Idara, 2015 alichukua fomu.
 
Mh jasusi hawezi kuwa raisi ? Eti kuwa raisi lazima uwe jasusi ?

Tanzania my coyntry a long way to go , asante Maxence Melo kwa kutupa hili jamvi hakika tunafurahi maana kila ashibae anakuja kupumzisha shibe haba jamvini .

Nenda Bernad , hii ni njia yetu sote .[emoji24]
Visungura vinatusumbua kaka mkubwa
 
Back
Top Bottom