Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Mkuu ni wapi ulisikia watoto wa adammu walizaa na dada zao?. Adamu alipata watoto watatu tu wote wa kiume inamaanisha kulikuwa na jamii nyingine tofauti na mwanzo wa uzao wa adamu.
Mkuu Hilo nalo itabidi liangaliwe
 
Just chukulia wewe ndo ungekuwa huyo mtoto halafu ukaambiwa hiyo ni sheria ya Mola,je kweli utampenda huyo Mola?
Mkuu unajua wanaokubali Sheria za Mungu ni Wale wanao mjua Mungu

Kwa mfano Kwa mafundisho ya Uislamu pale Ibrahim alipomwambia mwanae Ismail kuwa nimeota ndoto Nataka nikuchinje na ndoto za Manabii ni maono

Ismail kwakuwa anamjua Mola wake akasema "Baba maadam Hilo ni agizo la Mungu basi hakuna tatizo"

Ninachotaka kusema hapa amjuaye Mungu ataelewa tu
 
Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.
Hii hapa imekaaje? Sasa hapo huyo mtoto hatoolewa Ama ?
 
Mmekaa kikandamizi sana,ona lawama zote mnamsukumizia mwanamke…Hata katika mahusiano ya mapenzi kawaida nani huwa initiator kama sio mwanaume? Sasa mwanamke anakujaje hapo?ok sawa na je waliobakwa? Wao ndo wamesababisha?
Tembea kila kona nchi hii nani anae jiuza kila kona wako uchi
 
Mkuu Hilo nalo itabidi liangaliwe
Tuachane na kizazi cha kwanza cha adamu tuje kwa adamu wa tatu ambaye ni Ibrahim aliye tuletea imani mbili ya Isaka na Ismail, Iweje imani ya Ismail umbague na kumkandamiza mtoto wa nje ya ndoa kiasi hicho ilihali muasisi wake alizaliwa nje ya ndoa?. Kwanini isingetoa room ya kurekebisha na kupewa haki kama watoto waliozaliwa ndani ya ndoa.
 
Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.
Hii imekaaje?
kwani hiyo imani yako inasemaje? kuhusu mke ulio jitwalia bila hizi ya wazazi wake kwa sababu tunapo ongelea ndoa ni kitendo cha kukabidhiwa mke na wazazi wake wakiume hiyo bdio ndoa labda wewe ujui nini maana ya neno ndoa

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Sasa kama ni wazazi wake wa kiume na hai wazazi ndio hawatambuliki ina maana huyo mtoto hatoolewa?
 
Unyanyasaji huo….Nyie ndo chanzo cha watoto wa mitaani
Chanzo cha watoto wa mitaani ni uzinzi ambao nyinyi hapa mpo mna utetea.
Dawa ya kuhepusha watoto wa namna hiyo ni kutulia na wake zetu tuache uzinzi na kama huna mke oa na sio kuchezea chezea watoto wa watu hovyo na kuwapa mimba kwa kigezo cha kuwa utalea mtoto.

Hakika ni ukatiri mkubwa kumpa mimba binti wa wawatu wakati huna mipango ya kumuoa hata kama utatunza huyo mtoto.
 
Tatizo mtazamo wako hauwezi kubadilisha ukweli.
Kuna watu hawa kubaliani na utawala wa Samia lakini hilo haliondoi ukweli kuwa ndo kiongozi wa nchi hii.
Kitu chochote kinacho patikana nje ya utaratibu ulio wekwa na mungu aliye kuumba ni haramu.
Awe haramu kwa Mungu, lakini kwangu ni mtoto wangu halali. Na atapata haki kama wapatavyo watoto wangu wengine.
 
Inafikrisha. Kwaiyo wanawake hawatakuwa na adhabu ya uzinzi kwa muumba ? Maana ya kwao kameisha imaliza au watakuwa nayo nyingine tena ?
Mtoto kwa mwanamke sio hadhabu bali ni zawadi kwa sababu huyo mtoto akikuwa mama ana haki zote za kula matunda ya huyo mtoto ,wakati ww baba hutakuwa na haki ya kudai chochote kutoka kwa huyo mtoto hata kama atapata hela kama billget.

Mfano baba yake na Diamond alikuwa ana lalamika eti mtoto hamjali ila kidini domo yuko sawa huyo baba yake hana haki ya kudai chochote kutoka kwa domo lakini mama yake ana haki ya kula matunda ya mafanikio ya mwanae.
 
Tatizo mtazamo wako hauwezi kubadilisha ukweli.
Kuna watu hawa kubaliani na utawala wa Samia lakini hilo haliondoi ukweli kuwa ndo kiongozi wa nchi hii.
Kitu chochote kinacho patikana nje ya utaratibu ulio wekwa na mungu aliye kuumba ni haramu.
Ni vile sijazaa nje ya ndoa ila ingetokea ningempa jina langu mara mbili mbili. Yaani Tsh TSH TSH Na huyo mungu unayemuongelea hapa angemtambua.
 
Awe haramu kwa Mungu, lakini kwangu ni mtoto wangu halali. Na atapata haki kama wapatavyo watoto wangu wengine.
Na ndio maana unashauliwa kama ni kumpa huyo mtoto mali mpe kabla hujafa.
 
Mtoto kwa mwanamke sio hadhabu bali ni zawadi kwa sababu huyo mtoto akikuwa mama ana haki zote za kula matunda ya huyo mtoto ,wakati ww baba hutakuwa na haki ya kudai chochote kutoka kwa huyo mtoto hata kama atapata hela kama billget.

Mfano baba yake na Diamond alikuwa ana lalamika eti mtoto hamjali ila kidini domo yuko sawa huyo baba yake hana haki ya kudai chochote kutoka kwa domo lakini mama yake ana haki ya kula matunda ya mafanikio ya mwanae.
Sizani kama umenijibu swali langu nililouliza kulingana na nilichokuwa nimequote
 
Hizi dini za kuletewa hizi zinavioja Sana. Mungu mlikutana nae wapi akayasema yote hayo? Au utashi wa binadamu ndio umepelekea kuyaandika hayo? Labda tuwaulize Ismail ni mtoto wa nani? Maana Abraham alimpata nje ya ndoa.

Masuala ya kusema ndoa ya kanisani au msikitini ni halali na nje ya hapo ni haramu yanaudhi Sana. Yaani mwanangu asirithi Mali au asitumie jina langu kisa dini! Basi Bora niachane na hiyo dini kuliko kupoteza uhusiano wa damu baina yangu na mtoto.
Yaani dini zilizoletwa na majahazi zinampangia binadam jina la kumpa mwanae
 
Kwa mujibu wa imani ya kiislamu mtoto ambaye amezaliwa nje ya ndoa hatambuliki Kwa mujibu wa Sheria kama mtoto wa Baba husika.

Kwasababu kizazi au uzao WA familia unatakiwa upatikane ndani ya ndoa ya kisheria au ndoa iliyofungwa Kwa misingi ya Dini,na nje ya hapo huyo ni mtoto wa zinaa ambaye kisheria anatambulika kama mtoto wa mama aliye mzaa Tu.

Ingawa kikawaida atafahamika kama mtoto wa Baba Fulani lkn kidini huyo Baba hatambuliki na hivyo kuna haki Fulani ambazo Baba hawezi kumfanyia mtoto wake.

Moja wapo ni huyo mtoto hafai kuitwa Jina la ubini WA Baba yake,Hilo Jambo ni haramu Sana na Mungu ameshalikemea tayari, ingawa Kwa bahati mbaya Sana Kwa kutojua wengi wamewapa majina ya ubini wao hao watoto wa nje ya ndoa.

Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.

Lingine huyo mtoto hawezi kumrithi Baba yake kwasababu kisheria huyo mtoto sio WA huyo Baba,Bali Baba anaweza kumpa sehemu ya Mali huyo mtoto,lkn mara Tu huyo Baba anapokufa basi huyo mtoto Hana haki ya Kurithi chochote.

Lakini sio vibaya huyo Baba kumhudumia huyo kijana Kwa malezi na mahitaji mbali mbali maadam Tu yeye ndiye sababu ya kuja Hicho kiumbe hapa duniani.

Na mtoto ambaye Hana Baba kisheria anaweza kuitwa Kwa jina la mama yake, Kwa mfano ETUGRUL BEY ASHA au Kwa jina la ubini Kwa upande wa mama yake.

Kubwa ni kutambua uzao mzuri ambao hata kizazi chako kinaweza pata haki stahiki ni kizazi ambacho kinatokana na ndoa takatifu ambayo IPO Kwa mujibu wa Sheria.

Na hata wale ambao wanafunga ndoa za kiserikali basi watambue kidini Hicho kizazi Chao hakitambuliki na Sheria za Dini Kwa maana Baba Hana watoto hapo Ila watoto ni WA mama.

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
Nurain
adriz
professional Driver
baby zu
Nikisahihishe kidogo, ni kweli ndoa ya msingi ya dini inapendelewa zaidi ila katika uislamu ndoa zilizofungwa kwa imani nyengine zinatambuliwa pia, yani mtu akifunga ndoa kanisani huko ama uhinduni huko hiyo ndoa inatambulika

Ndio maana wanaondoa wa imani tofauti wakiingia uislamu hawana haja ya kufunga ndoa upya
 
Chanzo cha watoto wa mitaani ni uzinzi ambao nyinyi hapa mpo mna utetea.
Dawa ya kuhepusha watoto wa namna hiyo ni kutulia na wake zetu tuache uzinzi na kama huna mke oa na sio kuchezea chezea watoto wa watu hovyo na kuwapa mimba kwa kigezo cha kuwa utalea mtoto.

Hakika ni ukatiri mkubwa kumpa mimba binti wa wawatu wakati huna mipango ya kumuoa hata kama utatunza huyo mtoto.
Chanzo cha watoto wa mitaani ni janja janja mingi za kutaka kumtumia binti na kumkimbia, Woga na udhaifu wa kushindwa kubeba majukumu kama mwanaume.

SIMAMA TETEA DAMU YAKO HATA MBELE YA MUNGU KAMA ANA HASIRA SANA AKUUE UKITETEA ZAWADI YA MAISHA ALIYOILETA DUNIANI KUPITIA WEWE.
 
Back
Top Bottom