Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Je, Mtoto aliyezaliwa nje ya Ndoa anafaa kuitwa Jina la ubini la Baba yake?

Hizi dini bwana.
Ommy dimpos kawa tajiri baba na ndugu wanajipendekeza kumjua mtoto wao mlikuwa wapi na dini zenu.

Domo leo ni tajiri kila ndugu na masheik mnajazana kwake mlikuwa wapi pindi maskini.
Na hapo ndio ujue haijalishi ulizaliwa ndani ya ndoa au nje Mungu anaweza kumjalia yeyote kati yao.

Na hapo ndio ujue pia Mungu hajasema hicho kilicholetwa na mleta mada,ni mambo yaliyopangwa na wana wa adamu tu kwa kuwabagua wengine ambao pia ni viumbe kwa maslahi wanayoyajua wenyewe
 
Usizae nje ya ndoa
Ndo tunafundishwa ivo kua ni vibaya
Kuzaa hovyo kunapoteza uwezo wa mzazi kutoa huduma, hii ndo sababu yenye maana ya katazo la usizae nje ya ndoa, nyingine zote ni ubatili.
 
Ngoja nikuelimishe kidogo kila unachokiona duniani kiko chini ya under control hata ww uko chini ya under control.

Mwenyezi mungu kaumba binadamu na kamuwekea na taratibu maalumu ni namna gani aendeshe maisha yake na sio ilimradi tu anaishi.

Mfano leo ww utatafuta pesa kwa nguvu zako utanunua gari lakini hiyo gari huwezi kuiendesha barabarani mpaka upitie utaratibu fulani licha ya kwamba hakuna aliye kusaidia kununua hilo gari.

Au ukitaka kufungua biashara utatakiwa ufuate utaratibu maalumu licha ya sio kufungua kiholela holela.

Hivyo hivyo kwa mungu alikuumba akasema nendeni mkaijaze dunia lakini kaweka utaratibu wa kuzaliana na sio kuzaliana kiholela holela.

Dawa ya kuhepusha haya sio kuukimbia ukweli bali ni sisi kuacha uzinzi wa kiholela, hakika ni ukatiri na ubinafisi mkubwa kwa mwanaume kumpa binti wa watu mimba hali ya kuwa huna mipango ya kumuoa.
Hivi wakati Mungu ananiumba alinijua kuwa nitakuwa mzinzi?
 
Watu wa dini wanatakiwa kuelewa kuwa hakuna mtoto halamu,lakini wazazi waliomzaa ndio halamu.

Mtoto hajachagua kuzaliwa nje ya ndoa,lakini wazazi ndio walifanya mapenzi.

Na kwa kusema haya natangaza kuwa dini zenu zina upotofu kwa kuwatenga watoto wasio na hatia
 
Sasa mtoto anakuaje hana baba aisee. Na vipi mtoto akipatikana kabla ya ndoa na mkaoana mkiwa na huyo mtoto bado atakua hana baba??
 
Kwa mujibu wa imani ya kiislamu mtoto ambaye amezaliwa nje ya ndoa hatambuliki Kwa mujibu wa Sheria kama mtoto wa Baba husika.

Kwasababu kizazi au uzao WA familia unatakiwa upatikane ndani ya ndoa ya kisheria au ndoa iliyofungwa Kwa misingi ya Dini,na nje ya hapo huyo ni mtoto wa zinaa ambaye kisheria anatambulika kama mtoto wa mama aliye mzaa Tu.

Ingawa kikawaida atafahamika kama mtoto wa Baba Fulani lkn kidini huyo Baba hatambuliki na hivyo kuna haki Fulani ambazo Baba hawezi kumfanyia mtoto wake.

Moja wapo ni huyo mtoto hafai kuitwa Jina la ubini WA Baba yake,Hilo Jambo ni haramu Sana na Mungu ameshalikemea tayari, ingawa Kwa bahati mbaya Sana Kwa kutojua wengi wamewapa majina ya ubini wao hao watoto wa nje ya ndoa.

Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.

Lingine huyo mtoto hawezi kumrithi Baba yake kwasababu kisheria huyo mtoto sio WA huyo Baba,Bali Baba anaweza kumpa sehemu ya Mali huyo mtoto,lkn mara Tu huyo Baba anapokufa basi huyo mtoto Hana haki ya Kurithi chochote.

Lakini sio vibaya huyo Baba kumhudumia huyo kijana Kwa malezi na mahitaji mbali mbali maadam Tu yeye ndiye sababu ya kuja Hicho kiumbe hapa duniani.

Na mtoto ambaye Hana Baba kisheria anaweza kuitwa Kwa jina la mama yake, Kwa mfano ETUGRUL BEY ASHA au Kwa jina la ubini Kwa upande wa mama yake.

Kubwa ni kutambua uzao mzuri ambao hata kizazi chako kinaweza pata haki stahiki ni kizazi ambacho kinatokana na ndoa takatifu ambayo IPO Kwa mujibu wa Sheria.

Na hata wale ambao wanafunga ndoa za kiserikali basi watambue kidini Hicho kizazi Chao hakitambuliki na Sheria za Dini Kwa maana Baba Hana watoto hapo Ila watoto ni WA mama.

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
Nurain
adriz
professional Driver
baby zu
Upo sahihi hata huku kwa wakristo ni hivyo hivyo .. Nilisoma kitabu cha Esta kwenye biblia kuna stori yake ilinivutia ikabidi niende deep kujua historia na namna walivyokuwa wanaishi wakati ule ... kwa wakati huo (ancient time) kule kulikuwa kuna wanawake walikuwa wanaitwa MASURIA ambao siku hizi mnawaitwa nyumba ndogo a.k.a Mchepuko hawa kisheria toka enzi za wafalme walikuwa ni Low class wife kwa mfalme na endapo watazaa basi watoto na huyo mwanamke haki zao za urithi zinakuwa limited tofauti na wale ambao wamezaliwa na mke wa kwanza wa mfalme.
 
Kwa mujibu wa imani ya kiislamu mtoto ambaye amezaliwa nje ya ndoa hatambuliki Kwa mujibu wa Sheria kama mtoto wa Baba husika.

Kwasababu kizazi au uzao WA familia unatakiwa upatikane ndani ya ndoa ya kisheria au ndoa iliyofungwa Kwa misingi ya Dini,na nje ya hapo huyo ni mtoto wa zinaa ambaye kisheria anatambulika kama mtoto wa mama aliye mzaa Tu.

Ingawa kikawaida atafahamika kama mtoto wa Baba Fulani lkn kidini huyo Baba hatambuliki na hivyo kuna haki Fulani ambazo Baba hawezi kumfanyia mtoto wake.

Moja wapo ni huyo mtoto hafai kuitwa Jina la ubini WA Baba yake,Hilo Jambo ni haramu Sana na Mungu ameshalikemea tayari, ingawa Kwa bahati mbaya Sana Kwa kutojua wengi wamewapa majina ya ubini wao hao watoto wa nje ya ndoa.

Na lingine ni kumuozesha kwenye ndoa, Baba Hana haki ya kumuozesha binti yake WA nje ya ndoa Kwa mumewe kwani ndoa hiyo ni batili na haifai kabisa.

Lingine huyo mtoto hawezi kumrithi Baba yake kwasababu kisheria huyo mtoto sio WA huyo Baba,Bali Baba anaweza kumpa sehemu ya Mali huyo mtoto,lkn mara Tu huyo Baba anapokufa basi huyo mtoto Hana haki ya Kurithi chochote.

Lakini sio vibaya huyo Baba kumhudumia huyo kijana Kwa malezi na mahitaji mbali mbali maadam Tu yeye ndiye sababu ya kuja Hicho kiumbe hapa duniani.

Na mtoto ambaye Hana Baba kisheria anaweza kuitwa Kwa jina la mama yake, Kwa mfano ETUGRUL BEY ASHA au Kwa jina la ubini Kwa upande wa mama yake.

Kubwa ni kutambua uzao mzuri ambao hata kizazi chako kinaweza pata haki stahiki ni kizazi ambacho kinatokana na ndoa takatifu ambayo IPO Kwa mujibu wa Sheria.

Na hata wale ambao wanafunga ndoa za kiserikali basi watambue kidini Hicho kizazi Chao hakitambuliki na Sheria za Dini Kwa maana Baba Hana watoto hapo Ila watoto ni WA mama.

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
Nurain
adriz
professional Driver
baby zu
nimesoma title tu.Ukoo ni bloodline haijalishi ilizaaje au na nan na kivipi.
watoto wangu ni royal blood wanatumia majina yangu
 
Chanzo cha watoto wa mitaani ni janja janja mingi za kutaka kumtumia binti na kumkimbia, Woga na udhaifu wa kushindwa kubeba majukumu kama mwanaume.

SIMAMA TETEA DAMU YAKO HATA MBELE YA MUNGU KAMA ANA HASIRA SANA AKUUE UKITETEA ZAWADI YA MAISHA ALIYOILETA DUNIANI KUPITIA WEWE.
Kumpa mimba binti unaye jua huna mpango wa kumuowa ni moja wapo ya upumbavu na uzwazwa hata kama utajifanya kumlea huyo mtoto maana pamoja na kutoa matunzo lakini bado atakosa haki nyingi sana kutoka kwako ambazo wana zipata wenzake ambao umewazaa ndani ya ndoa.

Njia pekee ya kuzuia hilo ni kuacha uzinzi na mtulie ndani na wake zenu mnaharibu mabinti za watu kwa kisingizio cha akipata mimba nitalea.
Unaweza kumlea hujakatazwa unaweza kuwa unatoa matunzo lakini hutokuwa na haki wala amri yeyote mbele ya huyo mtoto bali mwenye mamlaka na huyo mtoto ni mama yake tu.
 
IPO kauli ya baadhi ya Ahlul ilmi ( Wanazuoni wa dino ya kiislamu) nafikiri mmojawapo ni Al-uthaimiin, kuwa mtoto wa nje ya ndoa anaweza kunasibishwa na baba Kwa masharti kadhaa, miongoni mwayo ni (I) Baba kumkubali mtoto kuwa ni wake (Ii) mwanamke aliyezaa na asiwe mke wa mtu (III) kusiwe na mtu mwingine anaedai pia kuwa mtoto husika ni wake.

Ninayoyakumbuka ni hayo juu, hivyo yakitimia hayo mtoto atapata haki zote apatazo mtoto aliyezaliwa ndani ya ndoa, Allah ni mjuzi zaidi.
 
Back
Top Bottom