Je, ni halali kumpiga makofi mama mkwe anayekukera kila siku?

Je, ni halali kumpiga makofi mama mkwe anayekukera kila siku?

Aache upuuzi.Kama mumewe hana shida yeye anajikasirisha nini?Au mayai alikaangia chipsi?Kama anaona anaweza kutatua hilo jambo si azae mtoto?Mambo mengine hayataki ujuaji.Anatakiwa aishi kwa akili hata jamii itamtetea bila kujali kasoro iko wapi.Utulivu!
Yeah,indeed! Ilibidi avunge TU kimtindo
 
Huyo mama si ajabu hata usiku wakilala anaenda kusikilizia kwa mlango kama wanachakatana [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Ni tukio limetokea jana jioni hapa uyole....Ndoa ina miaka mitatu mke hajabahatika kushika ujauzito....Sasa mama mtu alikuwa anapiga kelele juu ya hilo ....Nataka mjukuu nataka mjukuu, mnataka nife sijaona wajukuu na kadhalika.

Ni mama mkwe ivo binti akawa hana la kusema zaidi ya tutapata mama na mume kumwambia mama yake kuwa na subra.....Nadhani huyu mama aliona kelele za mbali hazifanyi kazi, akamwomba mwanae amtumie nauli aje awasalimie ivo akasafiri na tangu mwez wa 6 yupo pale nadhani alikuwa anataka ashuhudie tumbo likinyanyuka akiwa pale pale.....

Sasa kisa cha ugomvi ni nini?....Unaambiwa tangu afike ni kelele hizohizo, sasa jana binti kamfuma mama anamwambia mwanae " Au uoe mke mwingine mwanangu?" Binti hakutaka kupepesa akamrukia mama na kumpa mabanzi ya mashavu ya maana...Mama kizunguzungu chali...

Mwenye mama kaghadhibika kamrukia mke ...Kwanini unanipigia mama yangu wakati mimi nakuvumilia na maneno mengi mengi....Ndo ivo ugomvi ukawa ugomvi mpaka majirani kwenda kuamria.
Kama yupo Arusha aje nimpeleka sehemu mmoja HV kwa bib mmoja Yuko ngaramtoni ndani wa mwezi tu tumbo Hilo aje hkun garama kubwa Zaid San elf 70 mpk 60
Mungu atamjalia atapa uajauzito wake vzr Sana bib yule ashindwi hata akitaka mapacha atapata tu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Nahisi mama alikuwa na mamlaka zaidi kwenye maamuzi ya mwanae
Hata mimi nimeona hilo

Mimi nilipooa nilikaa na mama yangu mzazi nikamshauri kuhusu uvukwaji wa mipaka ya ndoa yangu. Sikuwahi kuona bibi akija kumzingua kwa baba yangu

Leo naishi ninavyoishi kwa sababu mipaka iliheshimiwa
 
Namsifu huyo mdada hata kama ataachika atakumbukwa milele na mama mkwe.. Saa nyingine wanazidi sana dada ana stress zake za kutopata mtoto ongeza na mikelele ya siku nyingi. halafu anasikia anaaambiwa aachwe piga vibao tuu.
 
Kwani yeye anaitaka ndoa ya hovyo namna hiyo? NI kwamba kamaliza kazi anafungasha mwenyewe, jamaa Kama bado anampenda mkewe atamfuata kwa muda wake, kaa mbali na wana ndoa huwezi amini wanaweza kurudiana na wakaishi kwa FURAHA tu ila.mama mke ndio hakanyagi tena pale watamtumia pesa ya matumizi akitaka apokee hataki aache [emoji3][emoji3][emoji3]

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
Kabsa. Mapenzi ya mtu usiingilie mazima
 
Hata mimi nimeona hilo

Mimi nilipooa nilikaa na mama yangu mzazi nikamshauri kuhusu uvukwaji wa mipaka ya ndoa yangu. Sikuwahi kuona bibi akija kumzingua kwa baba yangu

Leo naishi ninavyoishi kwa sababu mipaka iliheshimiwa
Yeah,Bora ulimwambia mapema
 
Namsifu huyo mdada hata kama ataachika atakumbukwa milele na mama mkwe.. Saa nyingine wanazidi sana dada ana stress zake za kutopata mtoto ongeza na mikelele ya siku nyingi. halafu anasikia anaaambiwa aachwe piga vibao tuu.
🤣🤣🤣🤣Watu mmechoka khaa 🙌
 
Katika vitu nimeapa kuvalia njuga na sitaki masihara ni mzazi wangu au wa upande mwingine kuingilia mahusiano yangu,hili ni pepo baya sana linaloteketeza ndoa nyingi
 
Naomba nitoe elimu kuhusu wanadoa kuchelewa kupata ujauzito, sababu zifuatazo. Kwa sababu ilimtokea rafiki yangu wa tangu school.
Ipo hivi kuna sababu nyingi za kuchelewa kupata mtoto na zimegawanyika katika makundi,
Kundi A,
1. ulaji wa vyakula_ hapa tunazungunzia aina ya chakula ambacho yamkni husababisha mwanaume kuwa na bengu isiyoweza kurutubisha yai,
2.Mtindo wa maisha, _Mtindo wa maisha ni pale wakati unasex na mtu wako mda ule unatoa mbegu badara uachiemo kwa mda wa kama dakika 5 hivi wewe unachomoa uume au mwanamke anajipindua ,
Mtundo wa maisha hata utumiaji wa uzizi wa mpango kwa mda mrefu husababisha kizazi au damu kusogea nakutokwa tayari katika kupokea mtoto, hasa mwanamke kutumia uzazi wa mpango tangu akiwa mdogo kipindi cha school, Hili somo ni pana acha niishie hapa

Kundi B,
1.magonwa ya kurithi,_ hapa utakuta mtu anarithi ugumba kutoka kwenye ukoo ikiwa kati yao alikuwepo mtu mwenye tatizo hili

2.Group la damu, kama nyo mpo katika group moja la damu mfano grop O,
Aisee kupata mtoto huwa ni bahati sana,
Hiyo ni kwa uchache sana naomba niishie hapa
Ila rafiki angu alikaa kwa mda wa miaka 6 bila kupata mtoto mwaka wa 7 akapata mtoto wa kiume sasa hivi anao watoto 3, asingekuwa na roho ya uvumilivu basi angekuwa ashaachana na mke wake, ingawa ilifika pahara akataka kuchepuka ila tulimshauri sana madhara ya kuwa na mtoto nje ya ndoa
 
Back
Top Bottom