Je, Tundu Lissu anazo sifa za kuwa Rais wa Tanzania?

Ndio ujanze Link kwenye nyusi za watu hv
 
UTU
 
Hebu upinzani wawe serious kidogo basii! Ni kweli mzee Slaa pamoja na yote anataka kurudi tena chadema?
 
Dah hatari sana, no way out tuendelee kuwalamba miguu tu.
 
Haya yote uliyoandika hapa ni ujinga, na situmii neno hilo kama tusi, ninalitumia kwa maana yake halisi.

Kama siyo ujinga, basi utakuwa unayaandika haya kwa kurudia rudia yale yaliyosemwa na wapotoshaji na wewe sasa unayaimba hapa kama kasuku tu, asiyejua anafanya nini.

Kwa mfano:

Huna uwezo wowote wa kuelezea "ubovu wa sera za ujamaa" zilizosababisha "uharibifu wa nchi, 'like forever'".

Kutokana na uandishi wako inaonyesha wewe ni hawa wa siku hizi msiokuwa na nyuma wala mbele katika kuelewa mswala ya kidunia.
Kama ujamaa wa Nyerere" umeweza kuharibu nchi, like forever", wewew hata katika hili tu huwezi kuona ubovu wa akili yako katika kuyang'ang'ania haya ya miaka chungu nzima iliyopita? Umeuona mfano upi wa nchi ya mfumo wa kibeberu (unakotoa jina lako), hapa Afrika na kwingieko ambako 'ujamaa wa Nyerere' haukuwagusa, na sasa ni mfano mzuri wa kuigwa?

Sitapoteza muda mwingi na kukujibu upuuzi mwingine ulioandika huko chini.

Niakupa ushauri tu, achana na tabia za kukaririshwa mambo. Umejaaliwa akili, zitumie kufikiri na kupata majibu sahihi ya maswala unayotakiwa kuyakariri kama kasuku.
 
Ana akili Sana kama za Nyerere.
Hakuna unishi kuwa akili anzo lakini ni za kuwa Rais wa nchi au TLS? Kuna wakati nashangaa watu wenye akili nyingi wanatetea watu wanaozidi kuzaana kwa Kasi na wanyama wanaozidi kuzaana kwa kasi waishi pamoja kwenye eneo ambalo haliongezeki ukubwa; mwisho wa watu na wanyama hao ungekuwaje? Watu wenye akili nuingi sana wanatetea wamachinga wanaozidi kuongezeka idadi Yao kila siku na kila mwaka waendelee kufanya biashara barabarani, mitaani, mwisho wake utakuaje? Wakati mwingine unaona professor anaongoza wizara vibaya kuliko asiye na PhD. Kuna wakati mwingine unamkuta mbunge wa darasa la sana anajenga nzuri kuliko mbunge mwenye PhD. Nadhani akili peke yake sio kigezo pekee Cha kuwa kiongozi bora.
 
Hana sifa, anafaa kuwa mwanaharakati, angalau awe mbunge kwaajili ya kuichachafya serikali. Hata uwaziri tu hana sifa.
 
Hebu upinzani wawe serious kidogo basii! Ni kweli mzee Slaa pamoja na yote anataka kurudi tena chadema?
Politics is a game of numbers, sio sababu wanamhitaji ila sababu wanajua ni anti CCM basi Wana take advantage kumtumia kuwaongezea political power and influence.
 
Mwambie huyu kaka ili aelewe. Mfano, Kenya ya Jomo, Malawi ya Kamuzu na DR Congo ya Mobutu hawakuwa na ujamaa hata kidogo, waliamua kuendelea na ujamaa wao, je, hizo nchi Zina afadhali gani Leo kuliko Tanzania? Ujamaa wa Nyerere ndio msingi wa umoja wetu unaouona Leo hii. Bila ujamaa ule wa Nyerere huenda Leo hii wazazi wako wasingekuwa na mahali pa kulima, huenda hata wewe usingekuwa umesoma shule. Ujamaa ule ndio uliowapokonya mabeberu (dini) shule zao na kuwapa watoto wa maskini wasome humo.
 
Politics is a game of numbers, sio sababu wanamhitaji ila sababu wanajua ni anti CCM basi Wana take advantage kumtumia kuwaongezea political power and influence.
Ni mpiga kura mjinga TU anaeweza kuzubaishwa mara zote siku zote kwa mara moja. Siku hizi ninawatizama usoni wagombea na records zao. Kuna wabunge ambao walijenga mahoteli badala ya kujenga Chama mashinani, na wengine wajumba, wengine mashamba makubwa, nk. Sikujua kama siasa ni ajira za watu kama ajira za watu wengine tu. Mwanzo nillikuwa nafahamu kuwa kazi ya siasa ni kazi ya umma kwa manufaa ya umma.
 
Naambiwa kuwa urais sio mtu bali ni taasisi, Sasa sijui ni Mama Samia, taasisi ya urais au CCM anayejenga hizi barabara zote ninazoziona zinajengwa, anaesambaza maji na umeme vijijini na mijini, anaejenga haya madarasa mapya ninayoyaona mashuleni, anaejenga viwanja vya ndege kule Msalato, anaemalizia kujenga Bwawa la umeme, madaraja na reli ya SGR, anaewapa vijana miradi ya kilimo. Ninahitaji mtu mwenye akili timamu anifahamishe polepole bila jazba kuhusu ubaya wa Mama Samia dhidi ya Marais wetu wengine waliopita. Mtu aje afafanue kuwa Samia hafanyi nini au anafanya nini pungufu au zaidi ya wenzake waliomtangulia.

Rais Samia ni muumini wa total football, JPM alikuwa muunini wa kwenda na vipandevipande. JPM alikuwa anasimamisha mambo mengine ili kufanikisha mambo mengine haraaka, lakini Mama Samia anafanikisha mambo yote kwa wakati mmoja polepole. Wakati wa JPM tuliona kuwa kipaumbele chake kilikuwa ni ujenzi, ujenzi, ujenzi, ujenzi, ujenzi na kusimamisha mambo mengine kwanza. Tuliona nchi kama vile imetekwa na jeshi, kila barabara kila mtaa, kila site ya ujenzi, kila lindo kulikuwa na wanajeshi/polisi. Polisi walikuwa anapita njia yoyote na upande wowote wa barabara bila kuzingatia alama za barabarani.

Bahati mbaya ujenzi ujenzi ujenzi huu ulifanywa zaidi katika mikoa 3 tu Tanzania ya Dar es Salaam, Dododoma na Mwanza/Geita/chato.
 
Akina Tinubu
 
Ungemweleza yule mkuu, 'kavulata', siyo mimi, kwa maana haya yote ninayafahamu na zaidi.
Wanachokosa kuelewa watu wengi hapa ni kuwa hakuna nchi yoyote duniani isiyokuwa na ujamaa ndani yake.

Hawa ambao ni kama wamewekewa 'software' ya kukariri maelezo ya kibepari wanafikiri huko nchi zinazojitangaza kuwa za kibepari hakuna ujamaa.
Hawa hawajishughulishi kabisa kujaribu kuelewa lengo lililokuwepo katika ujamaa wa Mwalimu Nyerere lilikuwa ni nini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…