Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Acheni kumpa moyo kinafiki, mwambieni ukweli hasa ninyi wanawake wenzie.

Iko hivi;

Mara zote maisha ya mwanamke huwa yanakuja na expire date kinyume na kwa mwanaume. Muda ambao binti unakuwa unapigiwa miruzi mingi, kijana wa kiume kwa muda huo ni sifuri kabisa ila ikifika muda sasa kila mtu anajitenga na wewe ndipo kijana huyu wa kiume unaelingana nae kiumri ndipo anaanza kuhesabu namba zake.


Nachokiona kwako ni ile kawaida yenu ya nyodo kupitiliza uliyokuwa nayo kwa waliokuwa wakikufuata. Kuchagua halijawahi kuwa tatizo kwangu ila hapo kwenye nyodo hapo ndipo panapokujaga kuwasurubu wengi wenu
Hakuna mwanamke ambaye ana haki ya kusema yeye hana bahati ya mahusiano kiukweli ni uongo. Wanawake wengi ule umri wa kuwa mabinti na kuwa na mvuto wao huwa wanautumia kuleta maringo na kuruka na wanaume tofauti wakiamini hakuna kuzeeka.

Mwanamke ana miaka 10 tu ya kucheza karata zake na kuwa na uhakika wa kushinda nje ya hapo ni kubet na maisha yake.

Binti ana advantage ya kufanikiwa kimahusiano akiwa kati ya umri wa miaka 16 hadi 25. Kuanzia 26 hadi 30 huo ni umri wa nenda kwa tahadhari au lala salama.

Akivuka tu hizi stage mbili ndio basi. Huko mbele ni kubahatisha kwenda mbele.
 
Kwa mwanamke kufika 30s si nzuri though sio umri ulioenda saana.

Usiogope,AMUA.
Hata mimi nipo tayari niishi nawe,natakupenda nitakujali nitakuheshimu. Na tupate watoto wetu 2 wazuri wa interval ya miaka 2.
 
Vikapuku vitakukatisha tamaa nia yao uishi kwa masononeko kama wao, usiwajali

Ushauri wangu ni kucalm down endelea na your daily life mtu sahihi atakuja kwako mtafunga ndoa na utazaa watoto wengi upendavyo, ila ukweli ni kwamba ukifika 36 uzazi unaweza kukusumbua sana....mambo mengine yatakua vile vile zaidi utakua umepevuka kiakili.
Mmmmmmhmn. Unajua mtu mzima kumdanganya mtu mzima mwenzake kama mtoto mdogo sio uungwana. Hivi mtu yupo 30,watoto wengi wanatokea wapi labda kama ata adopt wengine.

Hebu tazama, mtoto anabebwa tumboni miezi 9. Kumlea hadi kuwa tayari kumuachisha kunyonya ili usim'bemende yaani uzazi na malezi ya mtoto mchanga ni miaka si chini ya mitatu, so ukijumlisha na ile miezi tisa ya kubeba tifanye ni mwaka kabisa so ni miaka minne hiyo imekwenda. Miaka 30 + 4 ni miaka 34. Akiongeza mtoto wa pili bila kupumzika ni 38 hiyo wa tatu mfululizo itakuwaje sasa?

Kimsingi ni mtego mbaya sana wa kujiingiza mwenyewe. Hapo pia uombe MUNGU sasa awe na experience nzuri ya malezi ya watoto ama kama sivyo anaweza pata kichaa maana kudeal na watoto wadogo umri ukiwa mkubwa nayo inataka utulivu na ujuzi kuwalisha,kuwatrain,kuwafunza tabia,etc sio kazi ya dakika tano plus mtoto wako ni jukumu lako 100% bila kusaidiwa, bado maisha yanakusubiri, huku mume ambaye hamjuani maana m'mekutana mkiwa wakubwa umri umeenda so una struggle kubalance ndoa, familia, uchumi,malezi na afya yako ya akili na mwili. Hii ni kujipa kazi ambayo ungeanza mapema at 20s ungekuwa salama zaidi.

Kitu sipendi ni kumshauri mtu kinadharia bila kuzingatia uhalisia wa maisha yanakwendaje. Mwanamke suala na mahusiano na uzazi na ujenzi wa familia anatakiwa kulichulia serious kuliko kitu chochote hapa duniani maana lina limit ya muda na haliwezi kusubiria.

Shule unaweza soma hata ukiwa na 30 utaenda kusoma, ila ukifika 30 unakuwa na mitihani mingi sana kuanzisha familia kama mwanamke wa kawaida na kujenga mahusiano mazuri na mwanaume maana wanaume wengi utakaokutana nao huko ni reject au complicated.
 
Kila kitu kinafaida na hasara
Trust me huyo ata make a very good wife and mother, Kwa umri wake...
Kapitia mengi..
Kayajua mengi...
Anajua ninini anahitaji...
Na uwezokano wa kuwa na ndoto mpya mdogo...
So ata stick...na kukishikilia vizuri alichonacho.
Wapi sasa?
 
Okay wacha tuone. Kinachowafelisha wengi ni kutafta perfect match.
Humu watu wanatoa ushauri utadhani mtu anataka kununua kiwanja kumbe mtu anataka kujenga mahusiano ili aanzishe familia masikini.

Mimi nawaonea huruma sana mabinti wa kizazi hiki maana jamii imewaachia uhuru fulani hivi wa kucheza na maisha yao wakidhania huko mbeleni wanadhamana ya kutoboa kifamilia na kimahusiano. Huwa nawaonea huruma sana nikiwa natafakari future zao.
 
Kwa wanaume ukiwa senior bachelor basi ukimpata binti kwa gia ya kumuoa unakuwa na test ya kumshawishi tena aamini hujawahi kuoa na ukisema huna hata mtoto basi ujieleze tena kwa nini huna![emoji16]
Mimi huo muda siwezi kuwa nao. Kwa mtu mwenye akili timamu atajua ukiona mtu anakuuliza maswali ya kipuuzi jua hatumii akili anatumia hisia
 
Cha ajabu unaweza kuja kumuoa binti yangu[emoji23][emoji23][emoji23]. Wanaume mna raha kweli
Unasema hivi kuna mdada tulicheza sote utotoni huko. Mdogo wake wa mwisho mimi siwezi kudate nae kwa sasa maana ameshakuwa mama, mtoto wake huyo dada mzaliwa wa mwaka 2000 akiniona anaona mimi chaguo lake.[emoji23][emoji23][emoji23]

Ni vile tu wengine maadili yametushika ningeweza mtembezea moto dada mtu mdogo wake na mtoto wao pia.
 
You are right. Lakini msizipuuze love language zetu 🤣🤣
Mkuu ubaya nyie wanawake mpo kama maboss wakihindi, huwa mnajaribu kuingiza kidole kidogo kidogo ili muone reaction, mkiona mtu katulia mnataka muingize chote, kwahio haitakiwi mpewe nafasi hio hata yakuwaza kujaribu. Mimi napenda nifanye kitu bila kuombwa, yaani nijisikie, lakini ukianza niambia nahisi Iko siku utavuka mipaka. Kwahio siruhusu hicho kitu.
 
Now Maisha yamechange Sana, sio kama zaman
Watu wengi wa zaman kuanzisha family ilikuwa easy Tu ndio maana walikuwa wanazaa Sana

Mtoto anaweza Kula hata Kwa Jirani, unaweza kusafiri mwez mzima na watoto ukawaacha Kwa rafiki yako,

Kwa sasa hayo mambo hamna, watoto hawachezei tena udongo wanachezea tablet haha

So before ujapanga kuwa na family kwanza jiangalie mwenyewe na jifanyie tathimin je Una uwezo wa kulea familia?

Ela unayo bank?

Una kazi mzuri?
Hakunaga maisha ambayo yatakutaa kabisa ukose mfumo wa kuishi na kujenga familia. Tatizo katika mahusiano ya miaka hii na hawa wanawake wa kizazi cha kuanzia 1985 kuja huku mbele ujuaji ni mwingi.

Mwanamke hataki kuanzia chini anataka kuanzia level ambayo inawataka muwe na kipato cha kuanzia milioni 3 kwa mwezi huku yeye haweki hata buku mezani na anaishia kukwambia wewe si ni mwanaume.

Kuna brother m'moja nimejifunza kwake. Alianza na mkewe walifunga ndoa huyo bro akiwa anakaa kwao yaani vyumba vya uwani. Wakakaa miezi michache wakaenda kupanga sehemu hapo vyumba vya 30,000 viwili yaani chumba na sebule. Na hiyo sehemu ni bondeni mvua ikinyesha unacheza twist na tope na madimbwi ya maji hadi ukome mixer vyura wanakutumbuiza hadi alfajiri, ila ndipo walipoanzia.

Leo wana nyumba nne moja ndio wanaishi tatu wamepangisha, wana magari mawili mke analake mume ana lake. Wana watoto 4.

Kimsingi maisha yanataka utulivu na projection nzuri ya mnaelekea wapi pamoja. Hizo fujo za nataka mwanaume mrefu, awe ana akaunti yenye seven figures, awe na gari na nyumba nzuri ya kupanga kuanzia vyumba vitatu iwe ndani ya fensi. Haya maisha ya ndoto za mchana huwa yanawagharimu sana mabinti wa kisasa na tamaa zao.

Mwanaume ukute amejiimarisha hivyo halafu awe anakungoja wewe tu utokee akushobokee? So wewe ni nani aisee.
 
Yaani watu wanapenda kujipa presha na kujinyima raha kwenye maisha yao.......

Ukitaka uishi maisha ya tabu ,sonona na msongo wa mawazo hata kufa mapema basi wakabidhi walimwengu hizo funguo.......

Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kuwa asilimia 90 ya mambo yanayotokea maishani mwetu si kwa mipango yetu....ndio maana unapanga ufanye jambo fulani wakati fulani alafu ukajikuta hata hujafanya.......

Jikabidhi kwa Mungu ili upate furaha na amani ya moyo....yeye ndio anajua kusudio la maisha yako na yeye ndio anajua amekupangia nini.....

Wapo waliowahi kuzaa na watoto wote wakafariki......

Wapo waliowahi kuoa au kuolewa wakaambulia mateso mpaka wakazikimbia ndoa........

Kwa Mungu hakuna kuchelewa au kuwahi kwani kila kiumbe humrudhuku kwa wakati anaoona unafaa.......

Wapo watu ni wagumba kabisa na hawakuchagua kuwa hivyo lakini wanaishi maisha yao kwa raha na furaha......

Na wapo watu sio wagumba lakini Mungu anaamua kuwapa watoto uzeeni.....

Ulimwengu una mambo mengi sana

Acha kujipa stress....Acha kukusanya maoni na mitazamo ya watu juu ya maisha yako.....enenda katika njia ya Mungu kwani kila mtu kampa njia yake
Hapa bado unatoa faraja. Kidonda hakiponi kwa kupulizwa ndugu, kinatakiwa kusafishwa kwa dawa na kupakwa dawa ya kukausha kisizidi kuambukiza na kuoza.

Kusafisha kidonda si kazi ndogo aiseee maumivu huwa ni makali. Sasa wewe ni kama mtu anae mwambia mleta mada asikubali kusafishwa ataumia ila atulie wewe umpulize hata umia.

Sasa jiulize unamsaidia au unataka alale usingizi wa nusu kaputi huku anachelewa kuamka kutatua changamoto zake?

Wanaokupenda na kukujali wanakupa makavu live.
 
Hivi kwanini Mwanamke akifika miaka 25+ kama hana Mtoto wala Mume anachanganyikiwa alafu Mwanaume anaweza kua na 32+ hana Mtoto wala Mke alafu fresh tu hata hapagawi???
Wala siyo wao ni jamii ndio imewajengea wanawake hasa wa kiafrika hiyo mentality so wanakuwa hivyo kwa sababu wanaogopa jamii itawachukuliaje, laiti kama jamii ingeacha kuwasema vibaya wanawake wanaochelewa kuolewa au kuzaa kama kwa wenzetu wazungu basi mtashangaa wanafika hadi miaka 40 na hata hawashituki, kitu ambacho wanaume hamtaki ndio maana mnaendelea kuwasema na kutumia ndoa kama fimbo ya kuwachapia ili waolewe mapema iwe faida kwenu na wawe watumwa wenu
 
Hapa bado unatoa faraja. Kidonda hakiponi kwa kupulizwa ndugu, kinatakiwa kusafishwa kwa dawa na kupakwa dawa ya kukausha kisizidi kuambukiza na kuoza.

Kusafisha kidonda si kazi ndogo aiseee maumivu huwa ni makali. Sasa wewe ni kama mtu anae mwambia mleta mada asikubali kusafishwa ataumia ila atulie wewe umpulize hata umia.

Sasa jiulize unamsaidia au unataka alale usingizi wa nusu kaputi huku anachelewa kuamka kutatua changamoto zake?

Wanaokupenda na kukujali wanakupa makavu live.
Tumetofautiana kwa namna tunavyoyatazama mambo...... inawezekana upande uliotazama wewe sio niliotazama mimi hivyo nimeamua kuheshimu maoni yako.........

NB;
Huwezi kujua kuwa dunia ina mambo mpaka likukute jambo.......
 
Back
Top Bottom