Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Je, ulifika Third floor(30s) bila kuwa na familia? Hali ilikuwaje?

Hakunaga maisha ambayo yatakutaa kabisa ukose mfumo wa kuishi na kujenga familia. Tatizo katika mahusiano ya miaka hii na hawa wanawake wa kizazi cha kuanzia 1985 kuja huku mbele ujuaji ni mwingi.

Mwanamke hataki kuanzia chini anataka kuanzia level ambayo inawataka muwe na kipato cha kuanzia milioni 3 kwa mwezi huku yeye haweki hata buku mezani na anaishia kukwambia wewe si ni mwanaume.

Kuna brother m'moja nimejifunza kwake. Alianza na mkewe walifunga ndoa huyo bro akiwa anakaa kwao yaani vyumba vya uwani. Wakakaa miezi michache wakaenda kupanga sehemu hapo vyumba vya 30,000 viwili yaani chumba na sebule. Na hiyo sehemu ni bondeni mvua ikinyesha unacheza twist na tope na madimbwi ya maji hadi ukome mixer vyura wanakutumbuiza hadi alfajiri, ila ndipo walipoanzia.

Leo wana nyumba nne moja ndio wanaishi tatu wamepangisha, wana magari mawili mke analake mume ana lake. Wana watoto 4.

Kimsingi maisha yanataka utulivu na projection nzuri ya mnaelekea wapi pamoja. Hizo fujo za nataka mwanaume mrefu, awe ana akaunti yenye seven figures, awe na gari na nyumba nzuri ya kupanga kuanzia vyumba vitatu iwe ndani ya fensi. Haya maisha ya ndoto za mchana huwa yanawagharimu sana mabinti wa kisasa na tamaa zao.

Mwanaume ukute amejiimarisha hivyo halafu awe anakungoja wewe tu utokee akushobokee? So wewe ni nani aisee.
Hoja nzuri hii
 
Habari ya weekend great thinkers?

Maisha yananipa experience tofauti, Sikuwahi kufikiria kama ningefika third floor bila kuwa na familia wala watoto, kuna muda nahisi kupanic nahofia watoto wasije kuniita bibi badala ya mama, au kukosa kabisa sababu ya umri mkubwa🤔

Enzi hizo nilikua nashangaa mtu hasa mdada unafikaje hadi 30s huna familia, aisee kumbe ni kweli now ni mimi mwenyewe.

Mlioanza familia mkiwa 30s je ni kweli au mnaona dalili za watoto wenu kuwaita bibi au babu? Vipi changamoto za uzazi sababu ya umri mkubwa?😔

Nipo tayari kwa comments zote.

Happy valentine's day in advance 👏🥰
Bora kuchelewa Sana kuliko kuwa single mother bora uolewe hata na Mzee
 
Hii suala ya umri isikuwazishe
Swali:Je unaliishi kusudi lako kikamilifu??
Maybe ni nje ya mada, nimedoscover channel flani inaonyesha sana masuala ya uaminifu katika mahusiano youtube. Inaitwa comrades flavour, aisee humu ndo kuna mambo katika hii dunia sio rahisi kuimagine.

Watu (couples) wanakuwa challenged kubadilishana simu. Ni kenya by the way. Kuna stereotype ilishajengeka katika jamii kuwa wanaume wengi si waaminifu. Jamani jamani, ukiangalia hiki kipindi utagundua wanawake tumeongoza ligi. Aisee tuko njema. Unakuta boy na girl wanampa simu host wa kipindi. Mwanaume anacome out clean mwanamke anadakwa. Either ex, baba mtoto halisi, ama side guy. Na dada hata mshipa hashtuki. Kuna episode nikaiona, yule dada ana mwanaume na ndo baba mtoto halisi. Kuulizwa na jamaa as in guy wake anakataa kabisa anasema ni wa kwake, yule jamaa akaondoka kwa hasira, host kumuuliza yule dada ndo kusema nilimbambikia kwa sabbu yuko responsible. Huyu baby daddy hayuko serious na maisha. Jamaa kakasirika kinoma huku analia.

Najaribu kusema nini...umri usikubabaishe. Just pray uliishi kusudi kwanza ili mume,mke akukute ndani katika nafasi yako. Then mpursue purpose pamoja. Lakin eti kuangalia miaka, muda, itakuharakisha somewhere ambapo hukutegemea tena ukaja jilaani. Though kuna wewe ambae Mungu ameshakupaga spouse mzuri earlier na ukamkataa kwa sabbu ya chura, hela etc. Sijui tukusaidieje hapo....
 
😂😂😂 Sasa chief ukisema swala la haipiti huo ni uzinzi. Sababu wazinzi kokote wenyewe inapita hata kwa watoto..!
Sasa mwanamke aliyekuzidi 10yrs unataka kuoa mama zako wadogo??
Mama mdogo vipi na hajazaliwa na mama yangu.

Mie msiniambie masuala yenu, muhimu ipenye tu,
Japo mie na vitoto vidogo ni TOFAUTI kabisaaa, akinizidi miaka kadhaa au tukiwa sawa kidoogo hapo naiENJOY, 🤣😂
Sio mie nichukue mdogo wangu wa miaka zaidi ya mi5 huko hapana kwa kweli 😂
Ila wanaochukua wadogo zao siwadharau pia, kipendacho roho.
 
A ha ha huyo ndio size yangu, nyie wa 90S wenzetu mna gubu sana, halafu mmeshaona mambo mengi, nahakuna mwanaume anataka mwanamke alieona mengi 😃
Sema mnatafuta pa kuficha madhaifu yenu 😂
Sisi wa 90s wenzenu mnatuogopa tushajipata kuwazidi so mnakuwa hamna cha kutupanga
 
Mama mdogo vipi na hajazaliwa na mama yangu.

Mie msiniambie masuala yenu, muhimu ipenye tu,
Japo mie na vitoto vidogo ni TOFAUTI kabisaaa, akinizidi miaka kadhaa au tukiwa sawa kidoogo hapo naiENJOY, 🤣😂
Sio mie nichukue mdogo wangu wa miaka zaidi ya mi5 huko hapana kwa kweli 😂
Ila wanaochukua wadogo zao siwadharau pia, kipendacho roho.
Ww ndio tunaenda sawa sasa, chukua agemate wenzio. Hao wa vibinti vidogo achana nao kuna kitu wanaogopa wanakimbilia huko kuficha madhaifu yao..!!
Mentali leo umeongea kitu cha maana sana.
Hao wanaokimbilia vitoto ni mafataki 😂
 
Ww ndio tunaenda sawa sasa, chukua agemate wenzio. Hao wa vibinti vidogo achana nao kuna kitu wanaogopa wanakimbilia huko kuficha madhaifu yao..!!
Mentali leo umeongea kitu cha maana sana.
Hao wanaokimbilia vitoto ni mafataki 😂
Sisemi ni mafataki, ni kioendacho roho, naheshimu machaguzi yao, ila nabaki najiuliza tu inakuwaje kuwaje, wanaanzaje na wanaishi vip! 😂🤣
Kiukweli vitoto siviwezi, yaani mtu namzidi miaka 5,10.. Haya mahusiano siyawezi
 
Tatizo jingine mabinti wa siku hizi wengi wenu, mnamatarajio makubwa ya kiuchumi kupitia ndoa na ndio maana hata standards zenu mnazo set kipindi mkiwa hot zinakuwa sio halisi. Ila jua likizama ndipo unakuja kujua vyote mlivyokuwa mkivitaka ni batili. Mnamahitaji mengi sana ambayo si ya msingi Mf vikoba viwili viwili,mchezo majina matatu,unataka simu kali tena latest,nguo zinazo trend,nyumba kali,usafiri nk wakati shughuli ya kumuingizia kipata hana.

Sababu hizo ndio zina wafanya baadhi ya mabinti kudate na waume za watu na hata kuwazalia watoto sababu tu wana hela. Huku wakiwapiga vibuti vijana wenzao ambao walikuwa na nia thabiti ya kuwaoa.Ila siku wakiachwa baada ya umri kwenda na kuaanza kuchuja ndipo huja kugundua vyote ni batili. Mara nyingi mademu ambao huangukia kwenye kundi hili ni wale wanao jiona ni pisi kali.

Mara nyingi wanaume ambao huonyesha nia ya kweli ya kutaka kumuoa binti wakati akiwa ktk ubora wake, huwaga ktk kipindi fulani cha kujitafuta japo ana uwezo ya kutimiza mahitaji ya msingi na si hizi luxury ambazo baadhi ya mabinti mnaziendekeza ambazo hazina msingi. Anza nae hivyo hivyo kijana wa watu,kuna baadhi ya wazee ambao ndoa zao zimedumu, wamenza na vistuli na mkeka leo hii wametoboa.
 
Sisemi ni mafataki, ni kioendacho roho, naheshimu machaguzi yao, ila nabaki najiuliza tu inakuwaje kuwaje, wanaanzaje na wanaishi vip! 😂🤣
Kiukweli vitoto siviwezi, yaani mtu namzidi miaka 5,10.. Haya mahusiano siyawezi
Hata ukiachia shuzi mtoto anakusimanga eee we baba huoni aibu na umri huo unajamba hovyo..? 🤣🤣🤣
Wanapitia mengi sema wanajikaza wazee wenzio.!!
 
Hata ukiachia shuzi mtoto anakusimanga eee we baba huoni aibu na umri huo unajamba hovyo..? 🤣🤣🤣
Wanapitia mengi sema wanajikaza wazee wenzio.!!
Wazee wenzangu itakuwa waliruka stage, sasa hakuna namna inabidi waishi stage hiyo kwenye umri wa stage nyingine 😂
 
Yaani watu wanapenda kujipa presha na kujinyima raha kwenye maisha yao.......

Ukitaka uishi maisha ya tabu ,sonona na msongo wa mawazo hata kufa mapema basi wakabidhi walimwengu hizo funguo.......

Kitu ambacho watu wengi hawajui ni kuwa asilimia 90 ya mambo yanayotokea maishani mwetu si kwa mipango yetu....ndio maana unapanga ufanye jambo fulani wakati fulani alafu ukajikuta hata hujafanya.......

Jikabidhi kwa Mungu ili upate furaha na amani ya moyo....yeye ndio anajua kusudio la maisha yako na yeye ndio anajua amekupangia nini.....

Wapo waliowahi kuzaa na watoto wote wakafariki......

Wapo waliowahi kuoa au kuolewa wakaambulia mateso mpaka wakazikimbia ndoa........

Kwa Mungu hakuna kuchelewa au kuwahi kwani kila kiumbe humrudhuku kwa wakati anaoona unafaa.......

Wapo watu ni wagumba kabisa na hawakuchagua kuwa hivyo lakini wanaishi maisha yao kwa raha na furaha......

Na wapo watu sio wagumba lakini Mungu anaamua kuwapa watoto uzeeni.....

Ulimwengu una mambo mengi sana

Acha kujipa stress....Acha kukusanya maoni na mitazamo ya watu juu ya maisha yako.....enenda katika njia ya Mungu kwani kila mtu kampa njia yake
Upo sahihi kwa 100% kuna mahali Yesu alisema tuutafute kwanza ufalme wa Mungu na mengine tutazidishiwa.

Mungu anajua mahitaji yetu. Barikiwa sana mkuu.
 
Yatafanyika ila kwa kuchelewa.
Unarudije shule mfano ukiwa ktk ulezi? Katoto kana miezi mi3 ukaache urudi shule?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Si mshamaliza kusoma,

Incase unahitaji kusoma unamaliza swala la uzazi kisha unasoma tena.

Kupanga ni kuchagua
 
Back
Top Bottom