Je, unajua kuwa Roho huwa ina kawaida ya kutoka tulalapo?

Je, unajua kuwa Roho huwa ina kawaida ya kutoka tulalapo?

Sio sawa kwamba tutafufuliwa na miili hii yetu ya udongo, miili iliyoumbwa kwa ajili ya maisha ya hapa duniani.

Angalia hzi aya za Qur'an zinavyosema:-

Sisi tumewawekeeni kati yenu mauti, Na sisi hatuwezi kushindwa kuzibadili sura zenu na kukuinueni na sura MSIZOZITAMBUA

Qur'an 56:60-61

Hizo aya zinasema tukifufuliwa tutakuwa na sura/umbo tusilolitambua, sasa utasemaje tutakuwa na miili hii yetu ya duniani??.

Tutafufuliwa tukiwa na maumbo/sura tofauti na hizi tulizonazo na roho ndiyo itakayohukumiwa, hivyo ninaposema roho itafufuliwa kutoka Barzakh kuingia ahera maana yake hiyo roho itakuwa ndani ya sura/umbo/mwili mwingine tusioujua.

Raha zote za peponi zilizotajwa ni mfano tu kwani mtume Mtukufu Muhammad (saw) alipata kusema hakuna jicho limeshashuhudia mambo ya huko peponi.

Juu ya adhabu ya moto huko jehanam pia moto si kama moto huu tunaopikia majumbani bali moto inawakilisha mfano wa adhabu kali ya huko jehanamu, Allah atulinde na adhabu hiyo.
Umbo lingine ndio kama Hilo la ujana na Katu hakuna kuzeeka,kwani Mtume Muhammad rehma na Amani ziwe juu yake ndio alitufahamisha natambua unajua kuna mambo mengine yametafsiriwa vizur na mtukufu WA daraja


Umesema roho itahukumiwa,je itayopata adhabu ni roho pasina mwili au na mwili?
 
Umbo lingine ndio kama Hilo la ujana na Katu hakuna kuzeeka,kwani Mtume Muhammad rehma na Amani ziwe juu yake ndio alitufahamisha natambua unajua kuna mambo mengine yametafsiriwa vizur na mtukufu WA daraja


Umesema roho itahukumiwa,je itayopata adhabu ni roho pasina mwili au na mwili?


Allah anasema sura tusiyoijua, sasa kwanini wewe tayari umeishaijua??

Tuaposema roho itahukumiwa ni sababu yenyewe ndio mbeba taarifa za matendo ya mtu, mfano wa Roho ni kama black box kwenye ndege, na ndio maana mfano muuaji watu wanaweza kumuita mtu mwenye roho mbaya kwasababu ni roho yake ndiyo inabeba taarifa za maovu yake.

Unauliza inayoadhibiwa na kuhukumiwa ni roho na mwili au??, inayohukumiwa na kuadhibiwa ni roho mwili ni kama chombo tu cha kubeba huo mwili na ndio maana Allah kauita huo mwili umbo tusilolijua. Roho ndani ya huo mwili ni sawa na dumu la mafuta ya taa ndani ya nyumba, ukipiga kiberiti dumu ndilo litashika moto na mafuta yakiisha moto utazimika, hapo sasa utaona kwamba mafuta ndio dhambi, dumu ndio roho na nyumba ndio huo mwili tusioujua na moto ndio afhabu ya jehanamu, huo ni mfano tu waila الله يعلم.
 
Yote mnayo jadili hapa myth sio kweli hakuna kitu kama hicho

Huyo ni michezo ya ubongo tu unapokua umelala ndo maana huewezi kumbuka ata siku moja ndoto yako ilivyoanza.


Rejea wavuta bangi wanapo kuwa high. Nao huona hivyo hivyo


Msidangayike.
 
Hivi umeshawahi lala usiku halafu ukajikuta kama unaota hivi lakini fahamu zako zinakuonyesha kabisa upo macho na unajiona mwepesi Sana pasipo kawaida na saa nyingine huenda ukahisi kama upo hewani hivi

Au

Unaweza kwenda sehemu Fulani ambayo hujawahi fika lakini kuna kumbukumbu Fulani inakujia kana kwamba hiyo sehemu unaijua au ushawahi fika hivi.

Kifupi ni kwamba roho zetu huwa zinatoka katika viwili viwili vyetu na kwenda kupiga misele sehemu mbali mbali na mara nyingine hukutana na roho nyingine za ndugu zetu,ndio maana utasikia mtu atakwambia Jana nilimuota babu ananiambia moja mbili tatu na mara nyingi watu hao walikuwa Wacha Mungu.

Anyways sasa ni hivi, Kwa kawaida tunapo lala basi roho zetu huenda Kwa Mwenyezi Mungu kila siku ya Maisha yetu hapa duniani,sasa huenda zinaporudi ndio hukutana na roho nyingine na kukutana na matukio mbali mbali.

Kwa mujibu wa Qur'an inasema hivi Mwenyezi Mungu huzipokea roho zinazo kufa Kwa maana roho ambazo watu wameaga dunia,na roho ambazo watu wanakuwa wamelala,zile roho ambazo Mda wa kufa umefika huzizua na kubaki nazo,ndio hapa utasikia Fulani bwana kafa usingizini ujue roho yake haikurudi tena usiku huo na wale ambao mdao WA kufa bado basi Mwenyezi Mungu huziachia zile na kurudi katika miili yetu.

"MWENYEZI MUNGU huzipokea roho zinapo kufa. Na zile zisio kufa wakati wa kulala kwake, huzishika zilizo hukumiwa kufa, na huzirudisha nyengine mpaka ufike wakati uliowekwa. Hakika katika hayo bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri."
Azzumar : 42

Hayo ndio mambo ya Mwenyezi Mungu hakika mambo yake hakuna ayajuaye na hufanya katika namna atakavyo.

Ndio maana inatakiwa usiku Tulalapo basi tuombe msamaha na kuomba toba Kwa makosa yetu tuliyo fanya kutwa nzima kwani hatujui kama kesho tutaamka salama au laa!

Ni hayo Tu!

Kazakh destroyer
Msonjo
adriz
Nurain
Akhi
baby zu
Ntarudi
 
Allah anasema sura tusiyoijua, sasa kwanini wewe tayari umeishaijua??

Tuaposema roho itahukumiwa ni sababu yenyewe ndio mbeba taarifa za matendo ya mtu, mfano wa Roho ni kama black box kwenye ndege, na ndio maana mfano muuaji watu wanaweza kumuita mtu mwenye roho mbaya kwasababu ni roho yake ndiyo inabeba taarifa za maovu yake.

Unauliza inayoadhibiwa na kuhukumiwa ni roho na mwili au??, inayohukumiwa na kuadhibiwa ni roho mwili ni kama chombo tu cha kubeba huo mwili na ndio maana Allah kauita huo mwili umbo tusilolijua. Roho ndani ya huo mwili ni sawa na dumu la mafuta ya taa ndani ya nyumba, ukipiga kiberiti dumu ndilo litashika moto na mafuta yakiisha moto utazimika, hapo sasa utaona kwamba mafuta ndio dhambi, dumu ndio roho na nyumba ndio huo mwili tusioujua na moto ndio afhabu ya jehanamu, huo ni mfano tu waila الله يعلم.
Mkuu naona hapa unachanganya madesa.

Kwanza umeniuliza je imekuwaje Hilo umbo nimeshalijua nilikwambia kutokana na melezo ya Mtume.

Lakini pili, je unajua upi ni msingi WA hiyo Aya ya 56:60?

Msingi WA hiyo ni Aya ya 47 ya Sura hiyo hiyo


"Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?"
57:47

Allah anawazungumzia watu ambao wanaona ni vigumu baada ya kuoza na kubakia mifupa kuwa hataweza kufufuliwa, ndio inakuja hii aya


نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
56:60-62

Ukiangalia Aya hii Allah anajaribu kuwaeleza au kuwafahamisha kwamba hata Sisi tukifa au baada ya umauti wetu Kwa uwezo wake hashindwi kuleta viumbe wengine,maana wao walidhani ni vigumu kufufuliwa ndio anazidi kuwaambia kana kwamba sio kufufua Tu Bali hata viumbe wengine anaweza kuwaleta

Na

Amesema hashindwi kuleta kutuumba katika umbo tusilolijua,hapo inaonyesha kwamba ametoa mfano Tu lakini hajasema kuwa tutakuwa katika umbo tusilolijua na akaendelea katika ya 62 Kwa kusema bilashaka tulishajua umbo letu la awali alilotuumbia je ni kipi cha ajabu mpaka hatukumbuki uwezo wake?

Na Mimi kukuuliza wewe je inaadhibiwa roho na mwili au roho peke yake?

Ni kwamba Allah amesema ataujaza Moto WA jahanamu Kwa majini na watu, na hakusema atajaza huo Moto na roho.

Vile vile anaendelea katika Aya nyingine Kwa kusema kuwa kila mwanadamu atakapo kuwa anaungua basi atambadilishia ngozi nyingine ili machungu yaendelee ,na kwanini ngozi?

Kwasababu ngozi ndio organ ambayo inahusika na hisia za maumivu.

Natumaini umepata mwanga kidogo
 
Sio kutoka tu sometimes roho hufanya time traveling... Spiritual time traveling.

Ndio maana unaweza kufika sehemu for the first time ukawa unahisi sio mara yako ya kwanza. The truth ni kua roho yako ilianza kufika kabla ya physical body yako.

Ps. Miili yetu hua nalimit uwezo wa roho zetu.
Hii ilinitokea kama mara 2.
 
Sir, but sometimes it's just your brain playing with your tune! Meaning that you're just hallucinating and your Brain complying to show what you wanna see mental Illusion projection. Be careful.
Unaweza kuota upo na Mungu kabisa kumbe ni ubongo unafuata fikra zako.!
Fikra za Mtu si zinasababishwa na Brain itself Mkuu
 
Wakati Niko advance niliota niko chuo kikuu fulani....nimemaliza advance kweli nikapangwa hicho chuo[emoji848]
 
Niliposoma uzi wako akili iliwaza de javu nikaona niende kweny quran kusoma hyo aya ya juu yake na inayofwata kisha nikaenda kwenye tafsir ya ibn kathir , hakika quran haijaacha kitu na ni kitabu kisicho na shaka ndani mwake Allah Akbar,
Nimependa kuona comment leo za watu zimekubaliana na hili ila niwakumbushe mwisho wa aya hiyo
"hakika katika hayo bila shaka zipo ishara kwa wanao fikiri"
Na kumalizia dua ni muhimu sana kabla ya kulala , baada ya kukung'uta kitanda hata kama ni kisafi tauri basi dua hii ni muhimu
" In Your Name, O Lord, I lay down my side and in Your Name I raise it up; if You take my soul, have mercy on it, and if You send it back, protect it with that which You protect Your righteous servants.''
 
roho yangu jana nimeota eti nimemnyakua pande la samaki makamu wa rais maana alikua anakula bila kuniita hivi inawezekana
 
Back
Top Bottom